TANZIA Kipa wa zamani wa Simba, Yanga na Songea auawa kwa kuchomwa moto na Wananchi wenye hasira kali

Pumzika kwa Amani!
Ulikuwa mtu wa stori sana na vichekesho!
 
Inasikitisha sana watu kujichukulia sheria mikononi ,juzi juzi naona kuna DJ rasta naye walimuua.
 
Unaamka mzima wa Afya njema, Baadae binadamu wanakuua bila kosa

Inauma sana
 
Maisha haya bwana, kunantime ukiwaza sana kama uwezekano na uwezo upo, bora uishi umeiitenga mbali na watu
 
Dah, kujichukulua sheria mkononi napo jau sana, japo napo ukishakuwa uneoitia machungu ya kuibiwa inahitaji imani kubwa sana kusikia mwizi halafu uvunge.
 
Ni Mkwe wangu kabisa huyu kwani Kazaa Mtoto mmoja na Mwanangu (Mtoto wa Marehemu Kaka John) aitwae Buzo aishie Kibamba Dar es Salaam.

Kwahiyo ndiyo kusema kuwa Mwanangu Buzo kazaa na Mwizi / Paranja au?

RIP Mkwe wangu Kipa Doyi Moki.

Cc: bullar
 
WAKATI watani wa jadi wa soka la Bongo, Simba na Yanga, wakitarajiwa kushuka dimbani katika dabi inayonadiwa kwa kaulimbiu ya HAINA KIPENGELE, kuna taarifa mbaya na ya huzuni kwa nyota wa zamani wa timu hizo mbili. Huyu ni Mabruki Doyi Moke, kipa wa zamani wa Simba na Yanga aliyeishi kwenye mitaa ya Kariakoo kuanzia 1999 hadi 2003.

Moke, raia wa DRC kutoka Bukavu ameripotiwa kuuawa asubuhi ya Machi 6, mwaka huu huko kwao Bukavu.
Sababu za kifo chake zinatajwa ni kuchomwa moto na wananchi waliojichukulia sheria mkokoni wakidhani ni mhalifu. Katika siku za hivi karibuni matukio ya wananchi kujichukulia sheria mkononi huko Bukavu nchini DRC yamekuwa mengi sana.

Sababu kubwa inatajwa kuwa ni kupambana na wimbi la uhalifu kufuatia wafungwa wote kutolewa jela na waasi wa M23 baada ya kuliteka eneo hilo.

Wafungwa hao sasa wamegeuka kuwa wahalifu mitaani na wananchi hawana namna zaidi ya kuwakamata na kuwachoma moto.

Kwa hiyo wananchi walimkamata Doyi Moke kimakosa wakidhani mhalifu na kumchoma moto. Hii ni habari ya kuhunisha sana.

Chanzo: MwanaSpoti
 
daah hili kosi kitambo sana golini doy anacheza kafunga usongo wake kichwani kitasa anamaliza mayai tembele chibe chibindu kule pembeni pale kati mwanamtwa kihwelo na mahadhi wanakimbiza winga zinazibitiwa na vibelenge lunyalunya na saidi maulid senta fowadi mnyamwezi mwenyewe idi moshi.

r.i.p nyanda wa boli doy😭
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…