Kipandikizi kinamtesa mke wangu, tumbo linamuuma na haoni siku zake

Akakitoe kimemkataa in short Hakuna njia salama ya uzazi wa mpango cha msingi tumieni condoms au withdraw ni Nzuri na mtakuwa na uhakika wa kupata mimba ingine pindi mtakapohitaji
Ukitaka kunitesa kwenye ndoa niambie kuwa nitumie withdraw method!🙂🙂🙂
 

Umefanya vibaya mno kutubagua sisi Wanaume wenzio katika hili Mkuu kwani kuna wengine tunajua tatizo na tiba stahiki kwa Shemeji yetu ila kwakuwa Wewe humu JF umewaona tu akina Dada na Mama ukiamini kuwa watakusaidia basi ngoja na sisi Wanaume tuuchune ili uzidi kumpoteza Mpenzi wako na pengine unaweza sasa ukatushirikisha sisi Wanaume wenzio humu JF kuja kumchimbia Kaburi na kumbebea Jeneza lake na kumuhifadhi Kazi ambayo naamini akina Dada na Mama hao hawatathubutu kuifanya / kuikabili.

Siku nyingine mnapokuwa na tatizo la msingi acheni kubagua utoaji wa maoni yake kwani unaweza ukajikuta unawakwaza Watu na ukakosa msaada mkubwa tena wa bure tu ambao hata hukuwaza hata siku moja kuja kuupata. au umetubagua hivi kwakuwa sisi hatublidi na hatununui pedi labda? Nakutakia uuguzaji mwema wa Mpenzi wako Mkuu.
 
Tumsamee
 
Mwambie arudi clinic alikowekewa km kinamdhuru atatolewa na kushauriwa njia nyingine
 
Duh mkuu una maneno makali mno
 
TATIZO NI KWAMBA NYIE MMESHAJIHUKUMU!MIMI NIMEONYESHA TOKEA MWANZO KUWA WANAWAKE NDIYO WAATHIRIKA WAKUBWA WA NJIA HIZO.NA HUO NI UKWELI AMBAO WANAUME WENYE BUSARA LAZIMA TUKUBALI
 

Awasubiri hao hao akina Dada na Mama aliowataka yeye Mkuu kwani sisi wengine tukimjibu tutakuwa kama vile tunajipendekeza kama siyo hata kujikomba Kwake. Wewe unaumwa au una tatizo fulani kubwa halafu unabagua watoaji ushauri na tiba. Na bahati mbaya hadi hivi katika wote waliomjibu hakuna ambaye kampa jibu au tiba sahihi ya tatizo la Mkewe na nimuhakikishie tu kuwa Mimi najua Demu wake amekumbwa na nini na najua dawa gani tena ya Miti Shamba tu ambayo nikimwelekeza Mti au Jani lipi akachume na ampe anapona mara moja na anaanza kublidi kama kawaida na hatokuja kuugua tena. Sipendi Mtu anayebagua Watu wakati ana shida ya Kutukuka. Na Mimi nauchuna / naunyuti tu sasa japo najua atadanganywa na atapoteza Hela nyingi mno wakati hili ambalo ningemwambia kama akitumia Hela nyingi basi ni Tsh 800/ tu au 1,000/. Akitaka nimsaidie abadili Headline yake haraka sana ili tulioachiwa Mikoba na akina Bibi na Babu zetu tuweze kutiririka sasa hivi na kumsaidia.
 
Mkuu hilo wengi tunalo usihukum wewe tupe notes bwana
 
Duh mkuu una maneno makali mno

Nimeumbwa kunyoosha maneno na si kuvunga au kuwa mnafiki au kumwonea Mtu huruma na hivyo ndivyo nilivyo na sitokuja kubadilika hadi naondoka hapa duniani.
 
Mkuu hilo wengi tunalo usihukum wewe tupe notes bwana

Wangojeni akina Dada na Mama zenu watawajibia kwani sisi wengine hatublidi wala hatutumii pedi sasa ya nini tushoboke wakati tumeshatengwa kama si kubaguliwa na headline?
 
Nashukuru kwa ushauri,ila ninaomba mnielimishe nyie upande wenu ilikuwaje?Maana mimi ni mgeni wa mambo haya!!!!
Sio wote wanaotumia hizi njia za uzazi wa mpango,.ww fata ushauri tuu na mpeleke akatolewe hivo vitu bwana,.tumieni njia zingine salama.
 
Ushauri kwa uzoefu au wa kitiba?
Mbona unawaita kina dada/mama peke yao?
Hujui madaktari bingwa wa matatizo ya kinamama wanaume tumebobea ktk hilo?
Unataka kupata mtoto wa pili kwa njia hizo hizo za vichochoroni?
FANYA UOWE MKUU
NENDA HOSPITAL NA MWANAMKE WAKO AKATOLEWE HIVYO VIPANDIKIZI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…