Kipi kiliwahi kukutokea ukajikuta unaanza kuongea peke yako?

Kipi kiliwahi kukutokea ukajikuta unaanza kuongea peke yako?

Jana nimekutana na mwamba mmoja kavaa fresh tu na ukimtazamaunajua huyu anaelekea katika ofisi flani yenye hadhi au labda ni mtu mwenye mishe zake za kuelewekwa, lakini ajabu nikaona anaongea peke yake.

Awali wakati namkaribua sikutilia shaka sana hilo niliamini labda kuna kitu kaaa sikioni, si unajua tena siku hizi teknologia ipo juu, lakini haikuwa hivyo, alikuwa hajavaa kifaa chochote na tulipokaribiana nikiwa nimemtolea macho kwa ukaribu, akajishtukia akaacha kuongea.

Ni kama vile mwaba alikuwa kwenu kikao cha kwake mwenyewe kichwani.

Hii sio mara ya kwanza kutokea hali hiyo, hata mimi huwa inanitokea, hivi ni changamoto ya Afya ya Akili au maisha tu yanatupeleka puta.
Binafsi sioni tatizo kama mhusika hatoongea mwenyewe mbele ya watu,
Au atanyamaza baada ya kukutana na watu, kama ingekua ni tatizo la Afya ya akili....basi hata wanaojiangalia sana kwenye kioo na kujipiga sana picha kila wakati nao wamo kwenye hilo tatizo.
 
Kuna siku nilikuwa na father akiendesha gari hapa nilikuwa na age ya 10y. Namuona mzee anaongea peke yake mpaka akaanza kuugonga usukani🤣. Hapa ilibidi nimuulize mzee vipi tena baba mbona unaongea peke yako na unapika usukani?. Mzee aliniangalia na kutabasamu tu.

Hapa nilipo nafanya kama mzee sasa alivyofanya kuna siku najua mwanangu ataniuliza swali kama nililo muuliza father. Maisha hayana utani😂
Duh
 
Jaman hii ipo na ni moja kati ya aina ya communication inaitwa "intra-personal communication" kwaiyo hakuna Cha ajabu hapo na hii hali inamtokea Kila binadamu mwenye uhai kama unabisha jiulize nafsi yako toka umezaliwa ujawahi ongea mwenyewe hii ipo na inatambulika duniani na katika ngazi za elimu na ndo maana inafundishwa katika Kila taasisi za elimu
 
Kwa mujibu wa Likudd wa Jamii Forums, kuna faida kubwa sana kwenye ubongo wa mtu pale mtu anapo ongea peke yake. Likudd wa Jamii Forums amesema hayo kupitia Ukurasa wake wa Facebook swali lililoulizwa kwenye page ya Facebook ya jamiiforums kuhusu sababu gani kuwafanya watu kuongea peke yao.
Faida zipo Sana, mm nmeweza kujifunza lugha ya kijerumani kwa kuongea peke yangu na wajerumani wanashangaa nmejifunzaje Mana Niko fluent Kama vile nmeishi huko Munich.

Sent from my TECNO KD7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom