Kipi ni bora - Useja au kuoa/kuolewa?

Kipi ni bora - Useja au kuoa/kuolewa?

Kikubwa tafuta kujua ni nini mapenzi ya Mungu kwako. Muombe Mungu akufunulie ni kwanini alikuleta duniani., maana hakuna mtu aliyejileta nwenyewe duniani. Tumekuja duniani kwa mapenzi ya Mungu, hivyo hatuna budi kutafuta kuyajua ili tuyaishi.

Ndoa ni kitu kizuri kwa kuwa ni Mungu mwenyewe aliyeanzisha ndoa pale kwenye bustani ya Edeni., Adui shetani ndiye aliyekuja kuharibu taasisi hii nyeti na kufanya ndoa ionekane kuwa kitu kisichofaa.



YESU KRISTO NI BWANA NA MWOKOZI
Kwahiyo kwako wewe unachagua ndoa kuliko useja? Mimi Kwangu kuwa mseja ni maisha yaliyo bora sana Kwangu.
 
Mathayo 19 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁰ Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.
¹¹ Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.
¹² Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee.
Kwa hiyo unashauri nini kupitia hizo hadithi za kwenye kitabu cha Biblia ?🤔
 
Useja unachosha jumlisha upweke.
Hapa tu nishachoka upweke sasa sijui kukaa maisha yote kiseja kama nitaweza.
Mi nishajua tu kukaa kiseja siwezi ila ndio hivo sasa bahati mbaya ndoa zinanipitia kushoto.
Sio ndoa zinakupita kushoto, ni nyie mna masharti magumu. Kila mwanamke anayetafuta mume anataka wa kuanzia Miaka 35, in reality Mwanaume wa umri huo kumpata Ni nadra sababu karibu wote wapo kwenye ndoa
Lower your standards, tafuta wa kuanzia Miaka 25
 
Tafuta mdada mpole zaa nae alafu iba mtoto kamlee, mama yake mtafutie kibiashara au kama ana pesa mteme.

Ukishapata mtoto tafta single mother kama wawili wenye maisha, anzisha urafiki kwa ajili ya shoo tu. usiponenepa nitafute unifunge.
 
*USEJA - hii ni ile hali ya mtu kuishi bila ndoa.

Swali: Kwa dunia ya Sasa na maisha ya sasa yalivyo kipi ni bora kuishi maisha ya useja au kukubali kuoa/kuolewa?

- Kwangu Mimi maisha yaliyo bora ni kuishi kwenye useja.

- Vipi kwenu nyie wanajamii majibu yenu ni yapi [ useja au kuoa/kuolewa ].
Kwani Mungu alifanya nini pale Eden?
 
*USEJA - hii ni ile hali ya mtu kuishi bila ndoa.

Swali: Kwa dunia ya Sasa na maisha ya sasa yalivyo kipi ni bora kuishi maisha ya useja au kukubali kuoa/kuolewa?

- Kwangu Mimi maisha yaliyo bora ni kuishi kwenye useja.

- Vipi kwenu nyie wanajamii majibu yenu ni yapi [ useja au kuoa/kuolewa ].

1 Kor 7:1-9​

Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke.
Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe. Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.
Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe. Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.
Lakini nasema hayo, kwa kutoa idhini yangu, si kwa amri. Ila nipendalo ni kwamba watu wote wawe kama mimi nilivyo; walakini kila mtu ana karama yake mwenyewe itokayo kwa Mungu, huyu hivi, na huyu hivi. Lakini nawaambia wale wasiooa bado, na wajane, Ni heri wakae kama mimi nilivyo. Lakini ikiwa hawawezi kujizuia, na waoe; maana ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa.
 
Back
Top Bottom