Kipindi gani unakikumbuka kutoka Radio Free Africa (RFA) ya wakati huo

Wakuu nimekaa nikakumbuka miaka hiyo kipindi cha SITOSAHAU cha RFA. Ilikuwa ikifika hiyo mida ni kukaa karibu na redio mfano wakati wa simulizi ya Gamboshi 😂 asee?

Wahenga kipindi kipi mnakumbuka? Au ulikuwa ukikipenda?
Wandugu. Msisahau na RTD yetu club raha leo na Marehemu Julius Nyaisanga. Japo Uzi ni kuhusu RFA. Hapo RFA lilikuwa na mwamba mmoja Zuberi Msabaha akijiita volts laki moja,, na kipindi chake cha miziki ya Zaire-DRC.
 
Wandugu. Msisahau na RTD yetu club raha leo na Marehemu Julius Nyaisanga. Japo Uzi ni kuhusu RFA. Hapo RFA lilikuwa na mwamba mmoja Zuberi Msabaha akijiita volts laki moja,, na kipindi chake cha miziki ya Zaire-DRC.
Hahah ndio huyo huyo Laki Sita Volt Zuberi Msabaha.

Anapiga kikongo kuliko wakongo wenydwe
 
Kipo, kuna siku nilikisikiliza kinaendeshwa na jamaa mmoja anajiita mlevi mwenye busara.
Sasa hivi hakuna mtu anayesikiliza hicho kipindi zaidi a ya mtangazaji anakiendesha mwenyewe (anajisikiliza)

Bogus kweli kweli.
Duu jamani, sijui nitakumbuka siku moja nikiwepo nyumbani huwa saangapi! 😀😀😀
 
Kumbe mimi ni mzee sana aisee nitoke nyumbani sasa. Legend habari za mchana
 
Wakuu nimekaa nikakumbuka miaka hiyo kipindi cha SITOSAHAU cha RFA. Ilikuwa ikifika hiyo mida ni kukaa karibu na redio mfano wakati wa simulizi ya Gamboshi 😂 asee?

Wahenga kipindi kipi mnakumbuka? Au ulikuwa ukikipenda?
Bolingo time,
Msabaha akigonga lingala hatari!
 
Kumbe mimi ni mzee sana aisee nitoke nyumbani sasa. Legend habari za mchana
Hahahahaha usiogope..... wengine tumeanza sikiliza vitu toka tukiwa primary huko.... 35 yenyewe bado sana ingawa tayari 3rd floor
 
Bila shaka ilikuwa ni African Beats hiyo.​
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…