Kipindi gani unakikumbuka kutoka Radio Free Africa (RFA) ya wakati huo

Kipindi gani unakikumbuka kutoka Radio Free Africa (RFA) ya wakati huo

Show Time, J3,J5 na Ijumaa na Sindano tano za moto na Fred Waah kila Jumamosi asubuhi!
Jumapili tukitoka kanisani tunawahi kusikiliza Sitasahau!
Pia ilikuwepo Search Line!
Search line,
walikuwa wanatafutwa watu waliopotea.
 
Nilikuwa na sikiliza kipindi cha mambo mambo pamoja na Bolongo time (Ngoma Kali za kikongo). Halafu nasikia Yule jamaa aliyekuwa anaendesha kipindi cha Bolongo time amefariki.
 
Wakuu nimekaa nikakumbuka miaka hiyo kipindi cha SITOSAHAU cha RFA. Ilikuwa ikifika hiyo mida ni kukaa karibu na redio mfano wakati wa simulizi ya Gamboshi [emoji23] asee?

Wahenga kipindi kipi mnakumbuka? Au ulikuwa ukikipenda?
Weekend Fever
 
1. Je, huu ni uungwana la hasha huu si uungwana na Fredwaaaa.

2. Usiku wa mahaba na Erick Maganga na ile sauti yake iliyotulia usiku wacha kabisa

3. Sitasahau
 
1. Je, huu ni uungwana la hasha huu si uungwana na Fredwaaaa.

2. Usiku wa mahaba na Erick Maganga na ile sauti yake iliyotulia usiku wacha kabisa

3. Sitasahau
Ile jingle ya Deokaji Makomba kwenye kipindi cha michezo Kila jumapili asubuhi "ni katika michezo na burudani"
 
Hiki cha "sitasahau" watu walikua wanasimama barabarani kusikiliza kama njia moja ya kupumzika maana boda ya zamani ni miguu
Hiki kipindi kilinifanya nigombane sana na maza kuhusu mambo ya kanisani, zile story za zablon na yule jamaa wa south zilikuwa hot
Kule kiss kuna mc carter, dj D7, kuna american top 40 na Ryan Seacrest jumapili hiyo life was so fun
 
RFA ilikuwa vizuri Kila angle kuanzia habari, burudani na michezo, kuwasaidia wenye shida (kipindi cha ushauri wako).
Nakumbuka walikuwa wanajiunga na idhaa ya Kiswahili ya BBC sasa Kila siku ya juma mosi na juma pili BBC hutuletea mtanange wa EPL huku mtangazaji akiwa Charles Hilary na Salim kikeke, nilikuwa sibanduki karibu na redio kwani Charles Hilary alikuwa akikutangazia soka Una feel kama uko uwanjani.

Aise!
 
Wazee wa hip hop Mtakumbuka kipindi cha Weekend fever kikiongozwa na Uncle Sam....jamaa alivumbua vipaji vingi vya hip hop hakuna kipindi cha redio cha hip hop kama kile.

Halafu kuna RFA bonanza alikuwa anatangaza huyu jamaa Sky walker wa simulizi na sauti alikuwa anauwa sana.

Vodacom Burudani zaidi
Ndani yake kulikuwa na session ya sindano 5 za moto chini ya Marehem Freduwah.

Sitosahau- hichi kipindi kiliwateka watu wengi sana,mimi ile stori ya jamaa wa Gamboshi pamoja na Rojaz aliyezamia SA lakini hakutoboa akarudi bongo na kufungua Saluni.

Duniani wiki hii-kipindi kilichokuwa kina kusanya matukio yaliyotokea duniani kwa wiki Nzima~ Mtangazaji alikuwa kama Rahab Fred kama sijakosea.

Bolingo time chini ya Marehem u Zuberi Msabaha.
Show time ya kina kidbway Glory Robinson Mtoto wa Mama Sabuni.
Kipindi cha michezo na kina steve Moyo mchonge na Baruani Muhuza.

Nadhani hii ndio redio bora ya miaka ya 2010 kurudi nyuma ilikuwa imesheheni vipaji vya waandishi na watangazaji hodari sana...
Sijui walifeli wapi?
Mungu akupe nini kwankunikumbusha majina kama Rahabu fredi, Muhuza na Zuberi msabaha(alipenda kujiita Zubegh).
 
Nadhani hii ndio redio bora ya miaka ya 2010 kurudi nyuma ilikuwa imesheheni vipaji vya waandishi na watangazaji hodari sana...
Sijui walifeli wapi?
Nafasi yake ikachukuliwa na mawingu FM, pamoja na EA Radio ambayo ilikuwa na watu wenye vipajo vya kufa na kuona kama George Bantu, Rwenyagira, George David AKA Kampista, Mkuwe Isale mwite mamy baby nk.
 
Back
Top Bottom