Kisa cha Kweli: Sitasahau nilivyopendwa na mchawi nikaishia kurogwa

Kisa cha Kweli: Sitasahau nilivyopendwa na mchawi nikaishia kurogwa

Inaendelea sehemu ya tisa.

Nilikuwa nimelala usiku, nikiwa na amani kidogo kwa kufahamu angalau waliokuwa wananitafuta wamekwama. Kichwani mwangu nilikuwa na mambo matatu yaliyokuwa yananiumiza kichwa na kunifikirisha.

Jambo la kwanza nilijiuliza kuhusu kurudi shule kuendelea na masomo, hili lilikuwa la kawaida halikuniumiza kichwa sana.

Jambo la pili nilijiuliza kama na mimi ningehusika tena kwenye mkakati wa kwenda kuwamaliza hao wabaya wangu. Nisiwe mnafiki tokea nilivyofahamu waliyonifanyia niliwachukia sana, hivyo nilifurahi niliposikia wanaenda kuuawa na sikuwa na shaka nilikuwa nishajua mizizi ya mzee Masele ni mirefu. Hili liliniumiza akili kwa sababu sikupenda kuhusika kwenye hayo mambo tena nilikuwa nimeshayachoka...

Jambo la tatu ambalo ndio liliniumiza kichwa kuliko yote, ilikuwa ni ukweli kwamba sikuwa na uwezo wa kumkatalia Vumilia kuhusu jambo la kuwa kwenye mahusiano na yeye. Nisingeweza kwa sababu kuu mbili, kwanza yeye ndiye aliyenisanua mimi boya mmoja kwamba kuna wajanja wananitafuta kwenye kumi na nane hivyo niliona napaswa kulipa fadhila. Mbili nimeshuhudia mwenyewe kwa macho yangu Vumilia ni mchawi, hivyo kumkataa na kama kweli ananipenda ingekuwa hatari kwangu. Ilikuwa ni lazima niwe naye, niliona hakukuwa na uamuzi mwingine wa kuamua tofauti.

Asubuhi kulikucha na makucha yake, tukaamka tukawa tunaendelea na ratiba za kawaida. Nakumbuka nilifagia asubuhi uwanja baada ya kumaliza nikawa nimekaa pale, Baadaye mzee Masele aliniambia kwamba mchana saa nane jua kali tutaongozana kwenda kumalizia ile kazi. Sikupenda lakini nisingeweza kusema hapana ilikuwa ni mwendo wa ndio mzee.

Mchana muda wa saa sita aliniita ndani ya kijumba chake cha nyasi, nikaingia nikakaa. Alikuwa amewasha moto na kuna mizizi na magome ya miti akawa anayachoma, pembeni ya ule moto mkono wa kulia kulikuwa na mkuki na mkono wa kushoto kulikuwa na chungu kilichokuwa na maji. Akawa anaongea ongea mara azungushie lile eneo na dawa mara aongee kwenye chungu, mara atoke nje azungukie eneo lote la pale kwake, hakuwa na utulivu kabisa. Akamaliza alinivalisha shingoni kidude ambacho ni kipande cha mti kidogo kilichochongwa kwa ustadi mkubwa na kimefungwa kamba nzuri ambayo ndio niliitumia kuvaa kile ki mti. Ni miaka ya mbele sana ndio nilikuja kujua ile inaitwa hirizi, sikuwahi kukiona kitu kinachoitwa hirizi kabla japo ni kitu nilichokuwa nakisikia mara kwa mara watu wakikizungumzia.

Baadaye mida ya saa saba aliniambia twende tukamalizie kazi yetu. Tulianza kutembea kwa miguu kuelekea kijiji chetu tena. Njiani watu tulikuwa tunakutana nao lakini huwezi amini hakuna aliyekuwa anatuona. Sikuamini

This is a daylight witchcraft!

Ndio nilichowaza kichwani. Wakati wote mimi nilikuwa naamini uchawi hufanyikaga usiku tu , kumbe hadi mchana. Maajabu haya!

Tulitembea hadi tulipofika hapo alipokuwa anakaa bibi yangu, tukafika hadi kwenye njia ya kuelekea pale kwake. Yaani sehemu ambayo ndio kama geti la kuingilia. Tulivuka na tulitembea hadi katikati ya uwanja wa nyumba yake, alikuwepo lakini hakuweza kutuona kabisa. Mzee Masele aliniacha pale katikati ya uwanja halafu yeye akawa anazunguka maeneo yale. Nilimuona kama anaenda maeneo tofauti tofauti anachimbia dawa na kwenda eneo jingine. Alivyomaliza alikuja akachimba kishimo kidogo kwa kutumia kisu ambacho tulikuwa tumebeba akaweka dawa na kufukia. Alifanya mambo mengi sana ambayo mengine nayaacha kwa sababu ya muda..

Baada ya pale aliniambia "tuondoke sasa ili twende nikakufanyie dawa, Baadaye leo leo jioni utarudi hapa, utamkuta bibi yako pale amekaa peke yake" alisema huku akinionyesha kwenye mti wa size ya kati wa mhare akimaanisha ndiyo sehemu ambayo ningemkuta bibi yangu mchawi amekaa.

"ukifika msalimie kwa adabu, halafu muombe maji ya kunywa. Akikubali tu kufata maji jua kazi yetu imeisha"

"Hivyo akikuletea hayo maji wewe
, Yapokee halafu yamwage chini bila kusema lolote"

Tuliondoka tukarudi hadi nyumbani kwake. Kweli alinifanyia dawa. Siku hii mzee alitumia muda mwingi akifanya mambo yake ya ajabu ajabu ambayo sikuelewa yalikuwa na maana gani.

Mida ya jioni kweli tuliondoka maeneo yale, safari hii tuliondoka na baiskeli. Mimi ndiye niliyekuwa naendesha...

Tulienda hadi nyumbani kwetu tukaiacha ile baiskeli. Halafu tukatembea kwenda kwa huyo bibi. Tulipofika mganga aliniambia simama kidogo halafu utaenda baada ya dakika kama tano. Aliondoka hadi kwenye shamba lililokuwa pembeni na maeneo yale. Au niseme shamba ambalo lilikuwa la babu yangu ambalo mwanamke huyo alipewa kama mali yake baada ya kifo cha babu.

Nilikadiria muda baada ya kuona dakika tano zinaweza kuwa zimetimia niliondoka na kwenda pale nyumbani. Huwezi amini nilimkuta kweli yuko peke yake, nilienda moja kwa moja hadi alipokuwa amekaa pale kwenye mti.

Nilitamani nisimsalimie kwa hasira niliyokuwa nayo. Lakini nikakumbuka mzee Masele aliniambia nikifika nimsalimie kwanza tena kwa adabu.

"Bibi umeshindaje" kisukuma hakina shikamoo.

"Salama tu babu yangu" alijibu lakini alionekana dhahiri alishtuka ni kama hakutegemea kuniona pale kwa wakati ule.

Nilivyomaliza sikutaka kupoteza muda, nilimuomba maji ya kunywa.

"Nilimuona akisimama na kufata maji ndani"

Jambo hili lilinifanya niwaze na kuona kwamba kweli dawa zina nguvu zinaweza zikakufanya ukafanya maamuzi bila wewe kujua. Niliwaza hivyo kwa sababu kwanza mimi haikuwa mara ya kwanza kwenda pale, nilikuwa mwenyeji na niseme ni kama nimekulia pale. Kwa sababu toka enzi za marehemu babu yangu tulikuwa tunaenda pale kucheza nikiwa mtoto bado, hivyo nilijua vizuri sehemu ambayo maji yalikuwa yanatunzwa. Na siku zingine za nyuma kabla ya uhasama ulioletwa na kugombania ardhi nilikuwa naenda pale, nikisikia kiu naingia ndani nachota maji mwenyewe bila hata kuomba. Hivyo siku hiyo mimi kuomba pale maji yalikuwa ni maajabu! Bibi kunifatia maji yalikuwa ni maajabu zaidi, kwani kikawaida angeniambia niende tu nikachote maana sikuwa mgeni pale.

La pili nilikuwa ninaamini anajua nimeenda kwa mganga, kutokana na yeye mwenyewe kunifukuzia usiku nikiwa na Vumilia wakati tunaenda kwa mganga. Sasa kitendo cha kufika na kuomba maji moja kwa moja yeye kama mshirika wa haya mambo ya ushirikina nilidhani labda angeshtuka! Nilitegemea angegundua kuna mchezo mchafu anataka kufanyiwa.

Lakini haikuwa hivyo aliniletea maji, nikayamwaga chini. Nilipomaliza tu lile zoezi la kumwaga maji chini,nilisikia anatoa sauti ya maumivu kama amejiumiza sana sehemu fulani au amechomwa na kitu fulani kinachomletea maumivu.

"Ishiiiiiii! Nakufa" alijisemea mwenyewe

Palepale nikajua kazi imeanza!

Itaendelea

NB: huu uzi nimeuandika nikiwa na usingizi sana ila naamini unaeleweka! Usipoeleweka mnisamehe nitaelezea vizuri zaidi kwenye miendelezo inayofata.

Itaendelea. Usiku mwema.
 
Inaendelea sehemu ya tisa.

Nilikuwa nimelala usiku, nikiwa na amani kidogo kwa kufahamu angalau waliokuwa wananitafuta wamekwama. Kichwani mwangu nilikuwa na mambo matatu yaliyokuwa yananiumiza kichwa na kunifikirisha.

Jambo la kwanza nilijiuliza kuhusu kurudi shule kuendelea na masomo, hili lilikuwa la kawaida halikuniumiza kichwa sana.

Jambo la pili nilijiuliza kama na mimi ningehusika tena kwenye mkakati wa kwenda kuwamaliza hao wabaya wangu. Nisiwe mnafiki tokea nilivyofahamu waliyonifanyia niliwachukia sana, hivyo nilifurahi niliposikia wanaenda kuuawa na sikuwa na shaka nilikuwa nishajua mizizi ya mzee Masele ni mirefu. Hili liliniumiza akili kwa sababu sikupenda kuhusika kwenye hayo mambo tena nilikuwa nimeshayachoka...

Jambo la tatu ambalo ndio liliniumiza kichwa kuliko yote, ilikuwa ni ukweli kwamba sikuwa na uwezo wa kumkatalia Vumilia kuhusu jambo la kuwa kwenye mahusiano na yeye. Nisingeweza kwa sababu kuu mbili, kwanza yeye ndiye aliyenisanua mimi boya mmoja kwamba kuna wajanja wananitafuta kwenye kumi na nane hivyo niliona napaswa kulipa fadhila. Mbili nimeshuhudia mwenyewe kwa macho yangu Vumilia ni mchawi, hivyo kumkataa na kama kweli ananipenda ingekuwa hatari kwangu. Ilikuwa ni lazima niwe naye, niliona hakukuwa na uamuzi mwingine wa kuamua tofauti.

Asubuhi kulikucha na makucha yake, tukaamka tukawa tunaendelea na ratiba za kawaida. Nakumbuka nilifagia asubuhi uwanja baada ya kumaliza nikawa nimekaa pale, Baadaye mzee Masele aliniambia kwamba mchana saa nane jua kali tutaongozana kwenda kumalizia ile kazi. Sikupenda lakini nisingeweza kusema hapana ilikuwa ni mwendo wa ndio mzee.

Mchana muda wa saa sita aliniita ndani ya kijumba chake cha nyasi, nikaingia nikakaa. Alikuwa amewasha moto na kuna mizizi na magome ya miti akawa anayachoma, pembeni ya ule moto mkono wa kulia kulikuwa na mkuki na mkono wa kushoto kulikuwa na chungu kilichokuwa na maji. Akawa anaongea ongea mara azungushie lile eneo na dawa mara aongee kwenye chungu, mara atoke nje azungukie eneo lote la pale kwake, hakuwa na utulivu kabisa. Akamaliza alinivalisha shingoni kidude ambacho ni kipande cha mti kidogo kilichochongwa kwa ustadi mkubwa na kimefungwa kamba nzuri ambayo ndio niliitumia kuvaa kile ki mti. Ni miaka ya mbele sana ndio nilikuja kujua ile inaitwa hirizi, sikuwahi kukiona kitu kinachoitwa hirizi kabla japo ni kitu nilichokuwa nakisikia mara kwa mara watu wakikizungumzia.

Baadaye mida ya saa saba aliniambia twende tukamalizie kazi yetu. Tulianza kutembea kwa miguu kuelekea kijiji chetu tena. Njiani watu tulikuwa tunakutana nao lakini huwezi amini hakuna aliyekuwa anatuona. Sikuamini

This is a daylight witchcraft!

Ndio nilichowaza kichwani. Wakati wote mimi nilikuwa naamini uchawi hufanyikaga usiku tu , kumbe hadi mchana. Maajabu haya!

Tulitembea hadi tulipofika hapo alipokuwa anakaa bibi yangu, tukafika hadi kwenye njia ya kuelekea pale kwake. Yaani sehemu ambayo ndio kama geti la kuingilia. Tulivuka na tulitembea hadi katikati ya uwanja wa nyumba yake, alikuwepo lakini hakuweza kutuona kabisa. Mzee Masele aliniacha pale katikati ya uwanja halafu yeye akawa anazunguka maeneo yale. Nilimuona kama anaenda maeneo tofauti tofauti anachimbia dawa na kwenda eneo jingine. Alivyomaliza alikuja akachimba kishimo kidogo kwa kutumia kisu ambacho tulikuwa tumebeba akaweka dawa na kufukia. Alifanya mambo mengi sana ambayo mengine nayaacha kwa sababu ya muda..

Baada ya pale aliniambia "tuondoke sasa ili twende nikakufanyie dawa, Baadaye leo leo jioni utarudi hapa, utamkuta bibi yako pale amekaa peke yake" alisema huku akinionyesha kwenye mti wa size ya kati wa mhare akimaanisha ndiyo sehemu ambayo ningemkuta bibi yangu mchawi amekaa.

"ukifika msalimie kwa adabu, halafu muombe maji ya kunywa. Akikubali tu kufata maji jua kazi yetu imeisha"

"Hivyo akikuletea hayo maji wewe
, Yapokee halafu yamwage chini bila kusema lolote"

Tuliondoka tukarudi hadi nyumbani kwake. Kweli alinifanyia dawa. Siku hii mzee alitumia muda mwingi akifanya mambo yake ya ajabu ajabu ambayo sikuelewa yalikuwa na maana gani.

Mida ya jioni kweli tuliondoka maeneo yale, safari hii tuliondoka na baiskeli. Mimi ndiye niliyekuwa naendesha...

Tulienda hadi nyumbani kwetu tukaiacha ile baiskeli. Halafu tukatembea kwenda kwa huyo bibi. Tulipofika mganga aliniambia simama kidogo halafu utaenda baada ya dakika kama tano. Aliondoka hadi kwenye shamba lililokuwa pembeni na maeneo yale. Au niseme shamba ambalo lilikuwa la babu yangu ambalo mwanamke huyo alipewa kama mali yake baada ya kifo cha babu.

Nilikadiria muda baada ya kuona dakika tano zinaweza kuwa zimetimia niliondoka na kwenda pale nyumbani. Huwezi amini nilimkuta kweli yuko peke yake, nilienda moja kwa moja hadi alipokuwa amekaa pale kwenye mti.

Nilitamani nisimsalimie kwa hasira niliyokuwa nayo. Lakini nikakumbuka mzee Masele aliniambia nikifika nimsalimie kwanza tena kwa adabu.

"Bibi umeshindaje" kisukuma hakina shikamoo.

"Salama tu babu yangu" alijibu lakini alionekana dhahiri alishtuka ni kama hakutegemea kuniona pale kwa wakati ule.

Nilivyomaliza sikutaka kupoteza muda, nilimuomba maji ya kunywa.

"Nilimuona akisimama na kufata maji ndani"

Jambo hili lilinifanya niwaze na kuona kwamba kweli dawa zina nguvu zinaweza zikakufanya ukafanya maamuzi bila wewe kujua. Niliwaza hivyo kwa sababu kwanza mimi haikuwa mara ya kwanza kwenda pale, nilikuwa mwenyeji na niseme ni kama nimekulia pale. Kwa sababu toka enzi za marehemu babu yangu tulikuwa tunaenda pale kucheza nikiwa mtoto bado, hivyo nilijua vizuri sehemu ambayo maji yalikuwa yanatunzwa. Na siku zingine za nyuma kabla ya uhasama ulioletwa na kugombania ardhi nilikuwa naenda pale, nikisikia kiu naingia ndani nachota maji mwenyewe bila hata kuomba. Hivyo siku hiyo mimi kuomba pale maji yalikuwa ni maajabu! Bibi kunifatia maji yalikuwa ni maajabu zaidi, kwani kikawaida angeniambia niende tu nikachote maana sikuwa mgeni pale.

La pili nilikuwa ninaamini anajua nimeenda kwa mganga, kutokana na yeye mwenyewe kunifukuzia usiku nikiwa na Vumilia wakati tunaenda kwa mganga. Sasa kitendo cha kufika na kuomba maji moja kwa moja yeye kama mshirika wa haya mambo ya ushirikina nilidhani labda angeshtuka! Nilitegemea angegundua kuna mchezo mchafu anataka kufanyiwa.

Lakini haikuwa hivyo aliniletea maji, nikayamwaga chini. Nilipomaliza tu lile zoezi la kumwaga maji chini,nilisikia anatoa sauti ya maumivu kama amejiumiza sana sehemu fulani au amechomwa na kitu fulani kinachomletea maumivu.

"Ishiiiiiii! Nakufa" alijisemea mwenyewe

Palepale nikajua kazi imeanza!

Itaendelea

NB: huu uzi nimeuandika nikiwa na usingizi sana ila naamini unaeleweka! Usipoeleweka mnisamehe nitaelezea vizuri zaidi kwenye miendelezo inayofata.

Itaendelea. Usiku mwema.
Dah
Shukrani sana kwa kutukumbuka leo

Naona mambo yanazidi kuwa moto
Tuko pamoja
 
Ahsante mkuu,
Tunasubiri kwa hamu episode zinazofuata,

Mm siamin uchawi, but I am here to enjoy the story 😊🙏
 
Inaendelea sehemu ya sita.

Tulikuwa tumeshafika kwenye mlango wa kuingia kwa mganga. Unajua familia nyingi za usukumani zinakuwa na wigo au tuseme uzio ambao mara nyingi unakuwa wa miti fulani inaitwa minyaa au "manara" kwa kisukuma, lakini pia wigo mwingine ulikuwa wa mkonge "katani" kwa kisukuma. Na kwenye wigo huu huwa kuna sehemu ya kutokea ambao ndio kama geti la kuingilia. Sasa tulikuwa tumesimama kwenye hiyo sehemu ya kuingilia, lakini tulivyopita tu kuingia Sasa kwa mganga tukawa hatuoni chochote. Nyumba tulizokuwa tunaziona za mganga pindi tukiwa nje ya ule wigo tukawa hatuzioni, ni miti na vichaka tu ndio tukawa tunaona.

"Oooh! nini hiki" alisema Vumilia kwa sauti iliyoashiria kufadhaika na hali ile.

Nilimuangalia kwa sababu nilikosa sababu hata nimjibu nini, kwangu kila kitu kilionekana kama mazingaombwe. Baadaye aliniambia unajua mganga huyu ameweka madawa ya kuzindika eneo lake kwa hiyo sitaweza kupita, hadi nivue nguvu za kichawi nije kawaida ndio nitapita.

"Utavuaje?" Nilimuuliza

"Inabidi tuende kwa bibi"

Tulianza kutembea kwenda kwa bibi yake ambapo ilikuwa ni palepale kijijini kwetu. Sio muda mrefu tulikuwa tumeshafika. Aliingia ndani kwenye moja ya nyumba za pale kwao, akakaa kidogo halafu akarejea.

Safari hii alikuwa amevaa nguo za kawaida . Alikuwa amejifunga kitenge kiunoni na kitenge kingine amekizungusha kwa juu kifuani. Alinyoosha mkono na kunionyesha kopo, akaniambia nichote na kujipaka usoni. Nilichota kitu ambacho ni kama yalikuwa mafuta yakiwa yamechanganywa dawa, ambayo yalifanya kuwa kama mchanganyiko wa mafuta na unga unga. Yalikuwa ni mafuta yenye harufu kali ya kama kitu kilichooza lakini sikujali nilijipaka bila kujiuliza mara mbili. Aliniambia yalikuwa ni mafuta ya aina fulani ya mjusi ambaye kwa kiswahili sijui jina lake yamechanganywa na unga wa mizizi ya miti minne ambayo hakunitajia wala hakunambia matumizi yake.

"Inabidi tutembee haraka, nahisi tuko hatarini" aliongea huku uoga ukiwa dhahiri machoni mwake.

"kwa nini"

" Nahisi wanakutafuta kukuchukua na sasa wako njiani wanakuja, inabidi tufanye haraka tufike kwa mganga. Wakitukuta njiani kabla hatujafika utakuwa hatarini"

"Wamejuaje tumekuja huku" niliuliza nikionyesha mshangao kidogo.

"Wewe huyajui haya mambo, tafadhali tuwahi tuondoke"

Safari hii hatukutembea kama mwanzo isipokuwa tulikuwa tunakimbia ili tuwahi kufika. Na miongoni kati ya vitu vilivyonishangaza mwanzoni tulikuwa tunatumia muda kidogo sana kutembea umbali mrefu, lakini safari hii tulitumia muda mrefu. Haikuchukua muda mrefu toka tuanze ile safari, akaniambia wako nyuma yetu wanatufata. Wakitupata tu umekwisha. Niliogopa sana nikawa natamani hadi kupaa. Niliwaza pia vipi tukifika tena kwa mganga halafu tusipaone halafu huku nyuma tunafukuziwa.

It was probably the most terrifying moment in my life.

Muda sio mrefu nikaanza kusikia vishindo vya watu vinatufuata kwa nyuma. Wakati akili haijakaa sawa nikasikia kishindo kwa mbele yetu ni kama kitu fulani kilikuwa kimerushwa. Tokea pale tukawa tunapata ugumu sana wa kukimbia, miguu ilikuwa mizito sana au niseme ni kama kuna nguvu fulani unakuvuta kwa hiyo unapiga hatua kwa tabu sana. Tulijikongongoja hadi tulipovuka pale ambapo kile kitu kilikuwa kimedondokea. Tulipokivuka tu tukaanza kukimbia tena kwa kasi. Kufupisha story zoezi hili likawa endelevu ikawa kila tukivuka muda sio mrefu, kile kitu (ambacho kwa wakati huo bado sikukijua ni kitu gani) kinarushwa tena, tukivuka baada ya dakika chache kinarushwa tena. Lakini tukikivuka kasi yetu ya kukimbia inaongezeka, kikirushwa kasi inapungua inakuwa kama tunavutwa. Tulihangaika hivyo hadi tulipofika kwenye geti la kuingilia kwa mganga.

"rudini sasa watoto wangu mmewashindwa"

Ilikuwa ni sauti ya kiume ambaye nilikuja kumugundua ni mzee Nkelebe. Alikuwa akiwaamuru wale wachawi warudi walikotoka. Alitupokea na kutupeleka hadi kwenye mojawapo ya kijumba kilichopo pale kwake kilichojengwa kwa nyasi mwanzo mwisho.

Aliingia kwenye nyumba na kuja na viti vidogo aina ya vigoda viwili akatupatia na kutuamuru tukae.

"Unajua mwanzoni niliwaona mlivyokuja mkarudi. Wewe Vumilia ni mwenyeji hapa nilijua umekuja kwa nia njema Na lazima kuna shida hivyo nilijua lazima utarudi tu, hivyo nilikaa kukusubiri"

"Na huyu msabato umemtoa wapi, hadi akawa anakimbizana na wajanja usiku huu" aliendelea kusema huku akiniangalia Kwa unafiki fulani

Ni kama alikuwa ananikumbusha mwaka mmoja uliopita tu, nikiwa na brother mmoja mwinjilisti wa kanisani kwetu muuza vitabu vya dini ambapo nikiwa naye tuliwahi kumtembelea huyo mganga kumhubiri neno la Mungu. Nilikumbuka mwinjilisti yule aliyekuwa hamung'unyi maneno akimwambia mganga wewe unafanya kazi ya shetani utachomwa moto. Na sisi tunaofanya kazi ya Mungu tutaenda mbinguni. Sasa ilikuwaje mtoto wa Mungu anayesubiri mbingu, kwenda kutafuta msaada kwa wachomwa moto.

Ukistaajabu ya Musa, utayaona ya firauni.

"Tuachane na hayo baba huyu kijana anahitaji msaada" alisema Vumilia

"Sawa"

Mzee alisogeza maji kwenye karai dogo akaweka dawa fulani. Akamaliza akachukua kitu kama mkia wa mnyama wenye rangi nyeusi. Kama unaujua mkia wa ng'ombe kule chini huwa unakuwa kama una manyoya manyoya marefu, alichukua mkia wa hivyo sasa. Akamaliza akaanza kupiga manyanga huku akiimba nyimbo na kuongea ongea kama aliyepandwa na wazimu. Baada ya dakika kadhaa akanipa kakipande ka mti wa mnyaa na kuniambia nizungumze shida zangu bila kutoa sauti. Ni kama mtu anavyonuia kitu fulani.

Baada ya kumaliza zoezi lile alikichukua kile kipande akakiloweka kwenye yale maji. Akamaliza akakitoa kisha akaanza kukiangalia.

Akaanza kuniambia.

"Kijana una matatizo makubwa sana. Umefanya vizuri kuja hapa leo la sivyo leo ulikuwa mwisho wako. Kwanza ninaona watu wameandaa sherehe sehemu fulani kufurahia kukukaribisha huko kwenye makazi ya misukule"

"Na ninawaona hadi sasa wamekaa pale nje ya wigo wangu wanakusubiri utoke hapa"

Alisema na kuniangalia, nilikaa kimya sikuwa na la kuongea bado.

Alichukua kopo fulani akalisogeza kwenye mdomo wake, akaongea maneno fulani halafu akachukua dawa nyeusi na kunipaka usoni kisha akaniambia nitoke nje na kuangalia angani. Huku akinielekeza maneno fulani ya kutamka hadi mara tatu. Nilitoka nje huku nikiogopa nikafika nikatazama hewani na kutamka maneno aliyoniambia mara tatu. Yalikuwa maneno sio ya kiswahili wala kisukuma.

Ghafla kilijitokeza kitu cha ajabu angani, ambacho sikukitarajia. Ni kama ilitokea luninga iliyokuwa inaonyesha matukio mbali mbali. Kwa ufupi niliwaona wachawi kuanzia siku ile walivyonichukua wakanipeleka makaburini na kunichanja chale na kila kitu walichokifanya. Kilichonisikitisha zaidi niliwaona bibi yangu na mama yangu mdogo wakiwa na mwanamke mwingine ambaye naye alikuwa wa palepale kijijini. Bibi huyu alikuwa ni mmojawapo wa wake za babu yangu mzaa mama ambaye kwa wakati huo alikuwa marehemu na mama mdogo ni mtoto wa kuzaliwa na huyo bibi. Nilivyoona tu nilijua sababu ya yale yote ni nini.

Kulikuwa na mgogoro baina ya watoto wa mke wa kwanza wa babu yangu ambao ni mjomba wangu, mama mkubwa na mama yangu mzazi ambaye alikuwa ni kitinda mimba. Huyu bibi niliyemuona kwenye luninga ya mzee Nkelebe alikuwa ni mke wa pili kuolewa. Sababu ilikuwa ni mgogoro wa ardhi ambapo mke huyu alidai kuna sehemu ambayo mama yangu na mama mkubwa walichukua, ambayo ilinunuliwa yeye akiwa ndio ameolewa hivyo yeye ndiye haki nayo.

Kumbe nalogwa kisa mgogoro wa ardhi niliwaza!

Baada ya muda luninga ile ilikata matangazo nikarudi kwenye kijumba cha mganga. Kufika tu Vumilia alifungua mdomo wake na kuniambia.

"Nafikiri sasa umeanza kuniamini, mwanzoni nilipokuambia ndugu zako wanakutafuta labda hukunielewa"

Mzee Nkelebe alimtuliza Vumilia kisha akaanza kuniambia.

"Una matatizo mawili ambayo nimeyaona kwako yanayotakiwa kushughulikiwa. Tunaanza na tatizo la kwanza"

Mganga aliniangalia kisha akanambia nikunje suruali yangu. Aliliona kovu ambalo nililipata miaka mingi, siku ile nimeona wachawi nikiwa darasa la tatu. Aliniambia

"Kuna kitu uliwekewa kwenye mwili wako muda mrefu sana nimekiona unacho, tatizo lenu wafiadini hamtembeagi hadi mambo yawafike shingoni, ulitakiwa uwe umeshakiondoa muda mrefu sana" alisema mganga huku akiniangalia kwa umakini pale kwenye kovu.

"Labda nikuulize swali" alisema mganga akatulia kidogo kisha akaendelea

"hivi unadhani kwa nini siku ile unaona wachawi wakati ukiwa bado mdogo, kwa nini wewe peke yako ndio ulizisikia zile kelele za wachawi?. Na unadhani kwa nini ulipotoka nje ulifanikiwa kuwaona wachawi pasipo kutumia dawa yoyote, wakati kikawaida huwezi kuwaona wachawi bila Dawa?"

Aliniuliza lakini niliona dhahiri sikuwa na jibu kamili. Hivyo nikamwambia sijui chochote.

Akaniambia ulipokuwa mtoto ulikuwa na nguvu za asili na ukoo wenu una mizimu mikali sana. Hizo nguvu ndio zilikusaidia kuwaona na kusikia zile kelele, japo sasa hivi zimepungua na ni kawaida kupungua kadri unavyozidi kukua.

"Sasa wachawi hawakufurahishwa na wewe kuwaona, ilibidi wakufate baadae ulipokuwa umelala wakuchane mguu na kukuwekea dawa fulani iliyo kwenye kakipande kadogo ka mti"

"Kazi ya dawa hizo ni kukuzuia wewe ushindwe kusema chochote kila unaposhuhudia tukio la kichawi. Hebu niambie tokea ulivyoona tukio lile ulishawahi kumsimulia mtu kama ulitokewa na jambo kama lile"

"hapana" nilijbu kwa mshangao huku nikikumbuka jinsi moyo ulivyokuwa unakuwa mzito na kuogopa sana kila nilipotaka kumwambia mtu yeyote kuhusu tukio lile.

"Kumbe dawa zile zilikuwa zinafanya kazi" niliwaza

"Amini hata hili tukio la kuchanjwa usingeweza kumwambia yeyote. Na hautaweza kuja kumwambia yeyote kuhusu tukio la kishirikina utakalolishuhudia hadi siku unaingia kaburini, kama tusipoitoa hiyo dawa mwilini mwako" alisema mganga

"Hata baba yako najua usingemwambia, najua ungepata nia ya kumwambia lakini usingethubutu, hivyo watu wasingejua shida yako na usingepata msaada"

Baada ya kumaliza alichukua wembe na kunichana kidogo kwenye kovu.Alipaka dawa kisha akachomoa kipande cha mti kidogo kama vimisumari vile vidogo.

" Sasa uko huru kuongea. Tunaenda kwenye tatizo la pili".alisema kisha akaendelea

"Hili nadhani umejionea mwenyewe, wachawi tayari wana mamlaka juu ya mwili wako maana wameshamaliza maagano na mizimu ya kwenu, kwa tambiko lililofanyika makaburini. Kazi iliyobaki ni kukuchukua. Sasa ili tukurudishe kuna damu yako waliichukua wakati wanafanya tambiko inabidi tuirudishe kwanza" alitulia kidogo kisha akaendelea

"damu hiyo mwanzoni ilikuwa imefichwa kwenye dari la nyumba ya kwa bibi yako. Ila baada ya kujua umeshaanza kutembea kwa waganga kuna sehemu imepelekwa kufichwa pa siri zaidi ambayo mimi kwa uwezo wangu siwezi kuichukua huko. Inabidi nikupeleke kwa mganga ambaye naamini yeye anaweza kukusaidia. Ila ni mpaka nimtaarifu kwanza baba yako kwanza ajue kila kitu. Maana kuna vitu vitahitajika"

Nilikubali kwa sababu sikuwa na ujanja. Hata hivyo nilijua kama mama yangu angejua ndio angeleta kipingamizi lakini baba yangu hakuwa na shida, hakuwa mtu wa dini sana. Nilimshauri wasimshirikishe mama kwenye hilo, kwa sababu nilijua kwanza ni lazima angepinga kwenda kwa mganga. Pili sikutaka kumuona akiyajua matatizo yangu yangemfanya asononeke sana.

Mganga aliniambia nisiondoke pale kwake maana ndio ilikuwa sehemu salama kwangu. Hadi ile damu yangu irudishwe, lakini akamwambia Vumilia aondoke kesho asubuhi ila asipite kwenye njia ya kutokea kwa mganga wakati anatoka. Yaani apite sehemu pasipo na njia rasmi, mganga alihofia kuna mitego imeachwa ni mpaka aitegue kwanza.

Itaendelea
Kuna picha imenijia nikakumbuka siku moja nikiwa zamu kazini alikuja binti akilalama kwamba anahisi kuna vitu kama vijiti mwilini mwake kama njiti za uzazi wa mpango mikononi na sehemu za mapajani nikamdadisi huenda alichomwa na vitu lakini alikataa kata kata baada ya kufanya examination nilivibaini lakini hakukuwa na port of entry nilistaajabu nilitoa sindano nyeusi 5 mapajani 3 na mikononi 2 nikiri haikuwa rahisi leo nimeanza kuelewa sasa nini kilifanyika
 
Back
Top Bottom