Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 3,585
- 8,106
Wadau hamjamboni nyote?
Naambiwa kuwa Kisa hiki Al-BaKisa cha Al-Baqarah (Ng’ombe)i kimetokea miongoni mwa Wana Israel enzi za Nabii Mussa nduguye Haruni
Kwamba yupo Muisrael mmoja tajiri aliuawa na watu walianza kuwatuhumu baadhi kuhusika na mauaji yao na waliwaaminisha jamii nzima kuwa huo ndiyo ukweli.
Kwamba wenye hekima hilo hawakulikubali hivyo walimfuata Nabii Mussa awaamulie na yeye
aliwaambia amjuaye muuaji ni Mungu
Kwamba Nabii aliagiza wamletee ng'ombe dume wa njano na akachinjwa na kisha nyama yake akaigawa kwa watu wote kama sadaka
Kwamba sehemu ndogo ya nyama Nabii Mussa akaichukua na kuiweka kifuani mwa yule maiti ambaye alifufuka na alipoulizwa nani aliyemuua alimtaja KAKA/ Binamu yake
Kisa hili kimenifundisha mambo mengi sana kubwa ni kuwa Mwenyezi Mungu ndiye anayejua
Niwatakie mchana mwema ndugu
NB: kama Kuna sehemu nimekosea kuhadithia kisa hili naomba radhi na mnisahihishe
KISA KWA UREFU
Aya 67 – 73: Mwenyezi Mungu Anawaamrisha Mchinje Ng’ombe
Muhtasari Wa Kisa
#Al-Islam.org
Mzee mmoja tajiri katika Waisrail aliuliwa na binamu/ kaka yake kwa tamaa ya kurithi mali yake; kisha akadai kuwa ameuliwa na watu wengine, na wakatakiwa walipe fidia. Ukazuka ubishi mkubwa na wakamwendea Musa (a.s.).
Kwa vile hakukuwa na ushahidi wowote wa kugundua mambo walimtaka Musa-kama kawaida yao- kumwomba Mwenyezi Mungu awabainishie muuaji.
Ndipo Mwenyezi Mungu akampa wahyi kuwa wachinje ng’ombe na sehemu ya huyo ng’ombe wampige yule aliyeuliwa atafufuka na ataeleza yule aliyemuua.
Baada ya udadisi mwingi walifanya vile walivyotakiwa kufanya na Yule aliyeuliwa akafufuka na akamtaja aliyemuua.
Maana:
Wakasema: Je unatufanyia mzaha?
Yaani tunakuuliza kuhusu kuuliwa mtu nawe unatuamrisha kuchinja ng’ombe hakika huu ni mzaha.
Akasema: Najikinga kwa Mwenyezi Mungu kuwa miongoni mwa wajinga.
Yaani mimi sifanyi mzaha,hata katika mambo yasiyokuwa ya kufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu, sembuse hayo ya kufikisha neno la Mungu ambaye umetukuka msemo Wake?
Ilikuwa inatosha tu wamchinje ng’ombe yoyote, kwa sababu waliamrishwa wachinje ng’ombe tu; lakini kwa udadisi wao.
Wakasema: Tuombee Mola wako atupambanulie ni ng’ombe gani?
Wakajibiwa kuwa ni ambaye yuko katikati si mkubwa wala si mdogo, basi fuateni amri wala msingoje, lakini wakarudia tena kuuliza
Wakasema: Tuombee Mola wako atupambanulie rangi yake ni ipi?
Akasema ni wa manjano, lakini tena wakazidi kudadisi na kuuliza swali mara ya tatu, kwa sababu ng’ombe walio katika rangi hii na umri huu ni wengi. Akawaambia kuwa ni yule asiyefanyishwa kazi na asiyekuwa na kasoro yoyote.
Wakamtafuta mpaka wakampata, wakamchinja; kisha wakampiga maiti kwa kipande cha nyama akafufuka na siri ikafichuka baada ya kumtaja aliyemuua.
Ndivyo hivi Mwenyezi Mungu huwahuyisha wafu na anawaonyesha ishara zake ili mpate kufahamu..
Naambiwa kuwa Kisa hiki Al-BaKisa cha Al-Baqarah (Ng’ombe)i kimetokea miongoni mwa Wana Israel enzi za Nabii Mussa nduguye Haruni
Kwamba yupo Muisrael mmoja tajiri aliuawa na watu walianza kuwatuhumu baadhi kuhusika na mauaji yao na waliwaaminisha jamii nzima kuwa huo ndiyo ukweli.
Kwamba wenye hekima hilo hawakulikubali hivyo walimfuata Nabii Mussa awaamulie na yeye
aliwaambia amjuaye muuaji ni Mungu
Kwamba Nabii aliagiza wamletee ng'ombe dume wa njano na akachinjwa na kisha nyama yake akaigawa kwa watu wote kama sadaka
Kwamba sehemu ndogo ya nyama Nabii Mussa akaichukua na kuiweka kifuani mwa yule maiti ambaye alifufuka na alipoulizwa nani aliyemuua alimtaja KAKA/ Binamu yake
Kisa hili kimenifundisha mambo mengi sana kubwa ni kuwa Mwenyezi Mungu ndiye anayejua
Niwatakie mchana mwema ndugu
NB: kama Kuna sehemu nimekosea kuhadithia kisa hili naomba radhi na mnisahihishe
KISA KWA UREFU
Aya 67 – 73: Mwenyezi Mungu Anawaamrisha Mchinje Ng’ombe
Muhtasari Wa Kisa
#Al-Islam.org
Mzee mmoja tajiri katika Waisrail aliuliwa na binamu/ kaka yake kwa tamaa ya kurithi mali yake; kisha akadai kuwa ameuliwa na watu wengine, na wakatakiwa walipe fidia. Ukazuka ubishi mkubwa na wakamwendea Musa (a.s.).
Kwa vile hakukuwa na ushahidi wowote wa kugundua mambo walimtaka Musa-kama kawaida yao- kumwomba Mwenyezi Mungu awabainishie muuaji.
Ndipo Mwenyezi Mungu akampa wahyi kuwa wachinje ng’ombe na sehemu ya huyo ng’ombe wampige yule aliyeuliwa atafufuka na ataeleza yule aliyemuua.
Baada ya udadisi mwingi walifanya vile walivyotakiwa kufanya na Yule aliyeuliwa akafufuka na akamtaja aliyemuua.
Maana:
Wakasema: Je unatufanyia mzaha?
Yaani tunakuuliza kuhusu kuuliwa mtu nawe unatuamrisha kuchinja ng’ombe hakika huu ni mzaha.
Akasema: Najikinga kwa Mwenyezi Mungu kuwa miongoni mwa wajinga.
Yaani mimi sifanyi mzaha,hata katika mambo yasiyokuwa ya kufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu, sembuse hayo ya kufikisha neno la Mungu ambaye umetukuka msemo Wake?
Ilikuwa inatosha tu wamchinje ng’ombe yoyote, kwa sababu waliamrishwa wachinje ng’ombe tu; lakini kwa udadisi wao.
Wakasema: Tuombee Mola wako atupambanulie ni ng’ombe gani?
Wakajibiwa kuwa ni ambaye yuko katikati si mkubwa wala si mdogo, basi fuateni amri wala msingoje, lakini wakarudia tena kuuliza
Wakasema: Tuombee Mola wako atupambanulie rangi yake ni ipi?
Akasema ni wa manjano, lakini tena wakazidi kudadisi na kuuliza swali mara ya tatu, kwa sababu ng’ombe walio katika rangi hii na umri huu ni wengi. Akawaambia kuwa ni yule asiyefanyishwa kazi na asiyekuwa na kasoro yoyote.
Wakamtafuta mpaka wakampata, wakamchinja; kisha wakampiga maiti kwa kipande cha nyama akafufuka na siri ikafichuka baada ya kumtaja aliyemuua.
Ndivyo hivi Mwenyezi Mungu huwahuyisha wafu na anawaonyesha ishara zake ili mpate kufahamu..