Kisa cha rafiki yangu wa Mafia

Kisa cha rafiki yangu wa Mafia

Kiukweli Mafia mnayoisema mie siielewi ni ya wapi? Mie ni mkristo na nilipoenda mafia sikutegemea hata kitimoto ningeikuta Ila wazee Kuna pub na jamaa anatengeneza mbuzi katoliki safi sana na Kuna mangi mmoja anachoma mbuzi safi kabisa pale Mafia.

Haya mengine ni maneno ya kipuuzi ubaguzi huwa unakuwepo tu sababu ya kutozoea aina fulani ya maisha hata jamii ya kikristu huwabagua wengine sababu wanakuwa na Ile cultural shock ni Jambo la kawaida ambapo baada ya muda unakuja kuzoea tu.

Huu mchanganyiko wa jamii ndio husababisha watu kuzoeana na kuchukuliana na kuheshimiana Kama jamii iliyostaarabika ndio maana mzungu alipokuja alipewa maeneo na akakaribishwa akae wakajiweka kwenye maeneo yao kwa kuwa wenyeji wakiona Kama life ya wazungu ni tofauti.

Hata wahindi walipokuja nao walijitenga maeneo yao ya uhindini na wao kwa wao walijitenga unakuta wabohora Wana mtaa wao, jamatii Wana mtaa wao, waishamilia Wana mtaa wao, wasunni hivyohivyo basi ni ilikuwa wanaishi sababu ya kutozoea imani na maisha ya kila mwenzie.

Ila Mafia nguruwe nyama ipo Safi anayebisha aseme so huo ubaguzi wa kidini sijui na kama upo basi wa kawaida kwa familia na familia usigeneralize sheikh.
Sema wewe... ndo maana mwanzoni kabisa nami nikasema huo ni UONGO kwa sababu naifahamu Mafia vizuri sana! Home kwetu ukikaa dirishani unaona uwanja ambao Wahubiri wa Kikristo kibao walikuwa wanaenda pale wanatoa mahuburi ya Yesu ni Mungu lakini hawakuwahi kubughudhiwa hata siku moja!!

Na ule uwanja unapakana na Madrasa, kwahiyo wakati Wakristo wakiendelea na mahubiri yao, madogo upande wa pili wanasoma Quran lakini hakuna anayesumbuliwa!!

Pembeni tu mwa huo uwanja kuna Kanisa la KKKT, na limezungukwa na makazi ya Waislamu, lakini sijawahi kusikia wakibughudhiwa hata siku moja! Ukitoka hapo, ukashika barabara ya kwenda kwa akina Mzee Mwishehe, njia unakutana na baada, na inamilikiwa na Mkristo na ipo hatua chache tu kutoka ilipo Madrasa!

Ukifika pale kwa akina Mwishehe kwenyewe, kulia mzee Mwishehe, kushoto shemeji yake Idarous, kaskazini Mzee Idarous mwenyewe, na jirani yake wakati ule alikuwa Mama Mcaddam... wote hawa ni Waislamu lakini pembeni yao tu kulikuwa na baa!!!

Kwahiyo ni kiroja hasa kusikia mtu akisema eti Mafia kuna ubaguzi mkubwa wa kidini! Kwanza kama unataka kutaja maeneo yenye uvumilivu wa kidini Tanzania hii, Mafia inaweza kuwa among the top!!
 
Haya mambo yapo sana kuna Mwalimu wangu mmoja kwenye miaka ya mwanzoni mwa 2000 alipangiwa kazi huko Mbozi ndani ndani. Anafika kwenye huo mji yeye pekee ndio alikua Muislamu, kutokana na maelezo yake watu walikua wanamshangaa.

Kuna siku jioni yupo kwake akaja mzee mmoja na kumuuliza "Kijana nasikia wewe ni Muislamu". Jamaa akajibu "Ndio mzee mimi ni Muislamu". Mzee akauliza tena "Mbona upo kama sisi tu, hauna tofauti yoyote kabisa? Kwa maana tumekua tukiambiwa waislam sio watu kama sisi, wana manyoya mwili mzima na ni watu hatari sana". Ticha alibaki kushangaa tu.


Kutokana na mahali ulipozaliwa na kukulia unaweza kujikuta na mtazamo wa ajabu sana kuhusu watu wa jamii nyingine.
Huko mbozi ukiingia ndani ndani ata ukristo ujafika vizuri wengi wapagani.
 
Tatizo lako Chige uko hapa kutetea imani ya uislam na waislam,
Bila kujali niliyoandika au waliyochangia wengine kama yana ukweli au la.
Wewe unatetea tu uislam wako.
Bila shaka unafikiri mimi ni mkristo, mimi siyo mtu wa dini mkuu.
Mimi siamini katika Mungu wa wakristo, waislamu au yoyote yule.
Nimeshangaa umeandika kuwa eti nimefuta post yangu inayowazungumzia wakristo kufundisha kuwa kukaa karibu na mtoto muislam unapata majini, hizo ni stori za kipindi cha ukuaji mkuu, nimeiandika ili kujaribu kuweka usawa wa kuwa watu wa ukristo na usilamu wote wanawafundisha watoto wao chuki dhidi ya imani nyingi.
sasa unaposema nimeifuta nakushangaa.
 
Na.2 na 3 umetengeneza ya kwako, huenda unauelewa juu ya hayo.
Na 1 ndicho alichosema: harafu unajua na unajifanya hujui, poor you.

Kweli kabisa mkuu, huyu Chige yeye yuko hapa kutetea tu uislamu wake, hata kama waislamu wanafanya mabaya yeye hataki kukubali hilo, yeye amekazana kuwasafisha watu wa imani yake.
 
baada ya kumchunguza mtoa maada nimeona kuwa

YEYE SIO MUISLAM NA HAKUWAHI KUWA MUISLAM HATA SEKUNDE MOJA,
WALA SIO MKRISTO.
NI KAFIRI LILILOAMUA KUCHAFUA MAZINGIRA YA WATU, ILI WATU WAPIGISHANE MAKELELE.
VIZURI KULIPUUZA KAFIRI HILI LISILOKUWA NA NINI YOYOTE.
JAAHILI

Hawa ndiyo wapumbavu tunaowazungumzia hapa
 
Imani za ukristo na uislamu wote wanafundisha chuki dhidi ya wenzao, ni vile tu kila dini inafundisha chuki kwa aina yake.

Tatizo lako Chige una mahaba na uislamu, mimi sina dini mkuu, maana tayari inaonekana unadhani mimi ni mkristo nimekuja kuzungumzia uislamu vibaya.
Post unayokazania kuwa eti nimeifuta ni post namba 23, hiyo hapo juu nimeiquote.
Sasa sijui unakuja na hoja gani tena.
 
Kweli kabisa mkuu, huyu Chige yeye yuko hapa kutetea tu uislamu wake, hata kama waislamu wanafanya mabaya yeye hataki kukubali hilo, yeye amekazana kuwasafisha watu wa imani yake.
Tatizo lako Chige una mahaba na uislamu, mimi sina dini mkuu, maana tayari inaonekana unadhani mimi ni mkristo nimekuja kuzungumzia uislamu vibaya.
Post unayokazania kuwa eti nimeifuta ni post namba 23, hiyo hapo juu nimeiquote.
Sasa sijui unakuja na hoja gani tena.
Seeems like hujawahi kunisoma, no wonder unaleta mambo ya mahaba ya dini...

Keep reading me, na utaona misimamo yangu kuhusu dini! Humu jukwaani, si mara moja wala mara mbili nishawahi kusema "Christians and Muslims are the most insane community in the world" Sina muda ningekutafutia hadi posts zangu na threads!

Tatizo langu na wewe ni jinsi post yaKO ilivyo na viashiria vya chuki!

Look at michango ya watu... wanapita mule mule! Mafia hivi, Mafia vile wakati hata Mafia kwenyewe hawakujui! BUT why? Kwa sababu tu umesema Uislamu unafundisha Mkristo ni sawa au hata zaidi ya nguruwe au mbwa!

Uislamu wa wapi unaofundisha hivyo? Yaani hata aibu huoni kuongea uongo kiasi hicho? Unaweza kusema hapa LIKE A MAN, kwamba hivyo ndivyo ulivyofundishwa kwenye dini?

Hata huyo Gama uliyem-quote ku-defend hivi mara vile, yeye nae ana tabia kama za kwako... CHUKI!

Tatizo lako Chige uko hapa kutetea imani ya uislam na waislam,
Bila kujali niliyoandika au waliyochangia wengine kama yana ukweli au la.

Wewe unatetea tu uislam wako.
Bila shaka unafikiri mimi ni mkristo, mimi siyo mtu wa dini mkuu.
Kwanini nidhani wewe ni Mkristo?!
Mimi siamini katika Mungu wa wakristo, waislamu au yoyote yule.
And I saw this... umeandika! Sasa kwanini nidhani wewe ni Mkristo wakati huko nyuma ulishaandika?
Nimeshangaa umeandika kuwa eti nimefuta post yangu inayowazungumzia wakristo kufundisha kuwa kukaa karibu na mtoto muislam unapata majini, hizo ni stori za kipindi cha ukuaji mkuu,
ULIANDIKA, HUKUANDIKA?
nimeiandika ili kujaribu kuweka usawa wa kuwa watu wa ukristo na usilamu wote wanawafundisha watoto wao chuki dhidi ya imani nyingi.
Ala! Kumbe uliandika!!
sasa unaposema nimeifuta nakushangaa.
Hapo juu umeshakiri kwamba uliandika halafu hapa tena unanishangaa kuhoji mbona umefuta? Ipo hiyo post?


Acha kuruka ruka! Man up! KWANINI UMEFUTA POST AMBAYO ULIANDIKA WAKRISTO WANAKATAZA WATOTO WAO WASIKUTANE NA WAISLAMU KWA SABABU WATAPATA MAJINI Kwa sababu hata huyo Gama uliyem-quote alidhani nimekusingizia kuhusu wewe kuandika Wakristo wanawaambia watoto wao wasiwe karibu na waislamu kwa sababu watapata majini hapa!

Again, MAN UP... KWANINI UMEFUTA?!

Habari kwamba hizo zilikuwa s
 
Chige wewe ni mtu wa ajabu!
Post unayosema nimeifuta ni post namba 23, si mpaka nimeiquote hapo juu huioni?
Gama amesema mwanzoni pale wewe hutaki kuelewa bali unarukaruka.
Ndiyo maana nimekwambia wewe una mahaba na uislamu.
Unang"ang'ania tu eti nimefuta post, wakati post iko namba 23, mbona hutaki kuelewa?
Jambo dogo kama hilo unashindwa kulielewa, unadhani nilichokiwasilisha kwenye uzi wangu utakielewa?

Unakazana kusema nimefuta post, wakati post iko namba 23.
Wewe una mahaba na uislamu tu mkuu kubali.
 
Habari zenu wakuu, rafiki yangu wa mafia ananiambia hivi.

Mimi nimezaliwa na kukulia kisiwani mafia, shuleni kwetu tangia naanza darasa la awali mpaka namaliza darasa la saba, hapakuwahi kuwa na mwanafunzi mkristo, sote tuliwa wa imani ya uislamu. Aliwahi kuja mwalimu mmoja wa imani ya ukristo lakini hakukaa sana akaondoka.

Kwa ufupi sisi tangu utotoni katika ukuaji wetu tulifundishwa kwa msisitizo sana kuwa mtu ambaye si wa imani yetu, huyo mtu haifai hata kumsogelea kwa namna yoyote ile, mtu ambaye si muislamu ni sawa au ni zaidi ya nguruwe au mbwa. Mara kadhaa walipokuja watalii wa kizungu, hao ndiyo tuliaminishwa kabisa ni watu wanaopigana na Mungu anayetupatia uwezo wa kuishi. Alipopita mzungu tulikuwa tukitema mate kwa nyuma kuashiria ni kitu ambacho hata kukiona ni dhambi.

Mimi nilipomaliza darasa la saba nilitafutiwa uhamisho na nikahamia Vikindu, na hapo nilianza kidato cha kwanza. Kwakweli niliteseka sana siku za mwanzo pale shuleni, maana nyumbani Mafia nilifundishwa kuwa mtu asiye wa imani yangu ni haramu na haitakiwi hata nimsogelee.

Darasani nilipangwa dawati moja na mkristo, aliyeitwa Yohana Frank, kwakweli nilikaa naye kwa taabu sana nikiamini kukaa dawati moja na yeye natenda madhambi na nitaikosa pepo. Baada ya kuzoea mazingira ya shuleni nilipata rafiki wa imani yangu aliyeitwa Omari.

Cha kusikitisha huyo Omari alikuwa na marafiki wa imani ya kikristo, na walikuwa wakigawana vyakula pale shuleni. Mimi kwa mazingira niliyokulia na mafundisho niliyofundishwa tangu utotoni nilikuwa na wakati mgumu sana pale shuleni. Watu nilioaminishwa ni haramu na haitakiwi hata kuwasogelea, iweje leo nikae nao meza moja na kula pamoja nao?

Kwakweli nilikuwa nikijiuliza maswali mengi sana, na nikaanza kuyafikiria upya mafundisho yote niliyofundishwa tangu utotoni ikiwa yana mantiki au la! Nilianza kuifikiria imani yangu yote kwa ujumla. Mpaka leo nimeanza kufikiria kama kweli Mungu yupo? Huyu Mungu niliyefundishwa tangu utotoni yupo? na vipi kuhusu hawa miungu wa imani nyingine tofauti na imani yangu?
Wewe wale mabikra 70 mloahidiwa hutoipata hata mmoja nakwambia
 
Hata huyo @Gama uliyem-quote ku-defend hivi mara vile, yeye nae ana tabia kama za kwako... CHUKI
Mkoa wa PWANI Umetoa mawaziri watano


1. Ridhiwani Kikwete Mbunge wa Chalinze

2. Mchengelwa Mbunge wa Rufiji

3. Jafo Mbunge wa Kisarawe

4. Kipanga Mbunge wa Mafia

5. Abdalah Ulega Mbunge wa Mkuranga
 
nimekulia katika uislamu tangu mdogo mpaka namaliza form four sijawai kufundishwa kumchukia mkristo unaoandikaahapo ni uongo mtupu kuna haki za jirani ambay sio muislamu acha kupotosha uma sio uislamu huo

unaleta chuki na fitina

ajenda yako kutaka kueneza chuki kama huamini mungu ni wewe acha ushamba
 
Eti ndicho ulichosema...

Usichojua ni kwamba Post #2 kai-edit na akafuata aliposema Wakristo wanafundishwa wasikae na Waislamu kwa sababu watapata majini!

Na kama ndivyo alivyosema, ilikuaje anijibu:-

aise,

How come umefuta post yako ulipoandika habari za Wakristo kufundisha watoto wao kwamba wasikae na Waislamu kwa sababu watapata majini? Mbona umefuta simulizi za rafiki yako Swaumu na kwamba ukawa unahisi vyote vina majini?

NI kwamba ulidanganya sio?

Wewe unayejiita Gama siwezi kukushangaa kwa sababu nilishawahi kukutana na wewe kwenye mjadala mmoja uliokuwa unatetea mauaji ya Rohingya na bila aibu ukasema kwanza hao Waislamu wa Rohingya kule Myanmar sio kwao, wamefuata nini!!

Nilipokuambia wewe mwenyewe kwa hilo jina utakuwa Mngoni, na Wangoni Tanzania wamekuja tu kutoka SA, je itakuwa sahihi tukianza mauaji dhidi ya Wangoni... ukakimbia, na hukurudi tena!

Na kama wewe ni Mkristo kweli, utakubali angalau nafsini mwako kama utaona aibu kukiri hadharani kwamba nilichosema hapo juu ni KWELI KWA 100%!

Nimekukumbusha hayo ili kukuambia ACHA CHUKI!!!
Sijawahi kufundishwa kokote kwamba nikikaa na muislam nitapata majini. Sijaimaliza biblia ila naamini hata kwenye biblia hakuna hiyo sehemu.

Tupo kwenye huu uzi tunajadili maneno ambayo mtu amefundishwa katika familia yake na anaaminisha watu ni mafunzo ya Mafia nzima.

Kaka yangu alienda kufanya kazi Mafia aliondoka akiwa anaamini Mafia ni mwendo wa kupelekana kidini, alienda 2015 akawa anarudi likizo, 2020 ndiyo karudi Tanganyika mazima na anasema kuna vitu vingi siyo vya kweli haswa kupelekana kidini.
 
[emoji23][emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Jipange kisawasawa aisee..
Kuna wenzenu huku Unguja wao ndo mapadri lkn cha ajabu wao ndo walisilimu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Unakuta mtu hajausoma uislamu afu eti anaanza kuuchambua, unaishia kuwaangalia tu.
Mtume muhamad (s.a.w) alikuwa anaishi na asiye muislam ndani kwake hakumuua ndio iwe sisi? Jombaa kama vitu huelewi ni bora kuuliza na sio kukurupuka
 
Sijawahi kufundishwa kokote kwamba nikikaa na muislam nitapata majini. Sijaimaliza biblia ila naamini hata kwenye biblia hakuna hiyo sehemu.

Tupo kwenye huu uzi tunajadili maneno ambayo mtu amefundishwa katika familia yake na anaaminisha watu ni mafunzo ya Mafia nzima.

Kaka yangu alienda kufanya kazi Mafia aliondoka akiwa anaamini Mafia ni mwendo wa kupelekana kidini, alienda 2015 akawa anarudi likizo, 2020 ndiyo karudi Tanganyika mazima na anasema kuna vitu vingi siyo vya kweli haswa kupelekana kidini.
Na ndio nimemwambia mleta mada aseme wazazi wake na chuki zao ndo wamemfundisha hivyo lakini asiseme Watu wa Mafia wanafundisha hivyo! Na hata hilo la kwamba ukikaa na Waislamu utapata majini najua hakuna Ukristo unaosema hivyo bali aseme kuna watu wanawaambia hivyo watoto wao!

Kwanza pale Mafia mmoja wa washikaji zangu alikuwa Padri Likoko... the guy was very humble! Tulikuwa tunatimba na washikaji hadi home kwake!!

Binafsi, 99% of my friends ni Christians! Nakumbuka ni mshijaki mmoja tu wakati huo tukiwa vijana wadogo ndie alikuwa anapigwa beat na mama yake kuwa na sisi!

Hata hivyo, sio kwa sababu ya dini zetu, ni vile tu sie tulionekana watoto watukutuna tumepinda , na kweli tulikuwa tumepinda ingawaje baada ya kwenda chuo, nikaja kubaini kama mimi ni shetani basi mwana ambae alikuwa Seminary Boy alikuwa Shetani Pro manake vijiwe vyote vya malaya alikuwa anavijua lakini home alikuwa kama uncle ake na Jesus... full bible na kwenda church kila jioni 😂😂!!
 
Chige wewe ni mtu wa ajabu!
Post unayosema nimeifuta ni post namba 23, si mpaka nimeiquote hapo juu huioni?
Gama amesema mwanzoni pale wewe hutaki kuelewa bali unarukaruka.
Ndiyo maana nimekwambia wewe una mahaba na uislamu.
Unang"ang'ania tu eti nimefuta post, wakati post iko namba 23, mbona hutaki kuelewa?
Jambo dogo kama hilo unashindwa kulielewa, unadhani nilichokiwasilisha kwenye uzi wangu utakielewa?

Unakazana kusema nimefuta post, wakati post iko namba 23.
Wewe una mahaba na uislamu tu mkuu kubali.
Ilikuwa na Post #2!

Anyway, nimeshajua! You can't stand by yourself! HUJIAMINI na unachosema na ndo maana huwa unakimbiliaku-quote wengine ili wakusaidie kuku-defend!!

Huyo Gama alisema hivyo kwa sababu alisema hivyo kwa sababu alikuta UME-DELETE hiyo post!!

Kwako ni jambo dogo lakni kwangu ni kubwa kwa sababu, watu wanadhani ni mimi ndie nimesema habari za Wakristo na Majini kumbe ni wewe mtu usiye na ujasiri wa kusimamia ulichosema mwenyewe!!!

Narudia, ILIKUWA NI POST #2, ACHA UONGO WAKO!

Na tuseme nina mahaba na Uislamu... is there any problem with that! Sio bora kuwa na mahaba na unachokiamini kuliko kuwa MNAFIKI UNAYESHINDWA KUSIMAMIA UNACHOKIAMINI!!

Halafu acha kujifanya unanijua WAKATI HUNIJUI!!
 
Tatizo lako Chige una mahaba na uislamu, mimi sina dini mkuu, maana tayari inaonekana unadhani mimi ni mkristo nimekuja kuzungumzia uislamu vibaya.
Post unayokazania kuwa eti nimeifuta ni post namba 23, hiyo hapo juu nimeiquote.
Sasa sijui unakuja na hoja gani tena.
Umebaki kuji-quote! ACHA KUJIFANYA UNANJIJUA, WAKATI HUNIJUI!

Baada ya kukubana wakati unajaribu kukataa suala la ku-edit post, baada ukaja kuandika hii hapa chini:-
Nimeshangaa umeandika kuwa eti nimefuta post yangu inayowazungumzia wakristo kufundisha kuwa kukaa karibu na mtoto muislam unapata majini, hizo ni stori za kipindi cha ukuaji mkuu, nimeiandika ili kujaribu kuweka usawa wa kuwa watu wa ukristo na usilamu wote wanawafundisha watoto wao chuki dhidi ya imani nyingi.
sasa unaposema nimeifuta nakushangaa.
Kila mwenye akili timamu anaona hapo unakiri ni wakati wa utoto ndo mlikuwa mnafundishwa kukaa karibu na mtoto Muislamu unapata majini!!

Post unayodanganya eti ndiyo nakutuhumu ulifuta ambayo ni Post #23 ni hii hapa:-
Imani za ukristo na uislamu wote wanafundisha chuki dhidi ya wenzao, ni vile tu kila dini inafundisha chuki kwa aina yake.
Nioneshe ni wapi kwenye hiyo post umeandika habari za majini, au kuashiria kauli yako hii
post yangu inayowazungumzia wakristo kufundisha kuwa kukaa karibu na mtoto muislam unapata majini, hizo ni stori za kipindi cha ukuaji mkuu,
Onesha ni wapi uliandika hayo kama unakataa hujafuta?!

In short, wewe ni MUONGO!! Yaani wewe huyo huyo Wazazi Wako Waislamu walikundisha Wakristo ni wabaya sawa na hata kuzidi nguruwe au mbwa! Hapo hapo tena wakati wa utoto huo ukafundishwa ukikaa karibu na mtoto Muislam unapata majini!!

Sasa ni wazazi wako Waislamu ndio walikufundisha Wakristo ni zaidi ya mbwa au nguruwe! Sasa ni nani tena alikufundisha ukikaa karibu na mtoto muislamu unapata majini?! Ni hao hao hao wazazi wako Waislamu, au?

The problem unataka kujifanya Atheist!

Kwa bahati mbaya, Atheist ninaowafahamu karibu wote ni Big Brain! Wewe huna hiyo Big Brain ndo maana unaishia kujikanganya kanganya! Huwezi kuwa Atheist bila kuwa na intelligence ya ku-argue, na ndo maana ALL ATHEISTS argue about God's Existence na sio dini!

Si kwamba wanaamini katika dini bali wanafahamu Dini ni matokeo ya kuamini Existence of God!!

Kwa kupitia maandiko yako, mtu hana sababu ya kuwa na PhD ku-conclude HUNA intelligence ya kuweza ku-argue logically na ndo maana unaishia kuleta stori za uongo!
 
Back
Top Bottom