Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

Kisa cha pili .....

Nikiwa nimemaliza form six , basi ikabidi nitoke dar niende kagera kumsabai bibi yangu , Bibi yangu alikuwa akiishi bukoba mjini mitaa ya town kabisa.

Sasa pale kwake alikuwa na vyumba kama kumi na nne, amevipangisha , hivyo ni kawaida mimi kuonana na wapangaji pindi nitokapo ndani .

Sasa katika wale wapangaji kuna mdada alikuwa amepanga na pia anaishi mwenyew tu , ila story za watu eti ni malaya na pia ameathirika na gonjwa la taifa .

Hata bibi aliniambia hivyo pia , ila siku zilivyozidi pale nyumbani Mazoea na wale wapangaji yalizidi , sasa yakawa yamezidi kwa huyu dada, anayeishi pekee yake , Bibi akaendelea kunikanya kuwa niwe mbali na huyo binti , kwanza kanizidi umri pia ana tabia za umalaya .

Dah shetani , msikie tu , si nikajikuta nishaingia kwenye mazoea na yule dada , mwisho nikawa usiku nafungua geti taratibu naenda nalala kwake, asubuhi na mapema narudi, maisha yakawa safi , ila moyoni nikawa sina amani tena maana nilikuwa napiga kavu , hivyo nikawa najua nishaathirika .

Penzi likanoga kwa siri , Bibi hajui kitu kuwa mjukuu nishaingia kwenye penzi la mpangaji japo baadhi ya wapangaji walijua.

Sasa usiku mmoja kulikuwepo na mechi ya Arsenal na man u , nikamueleza bibi naenda mpirani akasema hapana, si uangalizie hapa , nikagoma akakubali niende atanifungulia mageti.

Sasa kumbe mwenzake sina mpango wa kurudi nyumba kubwa nataka nilale na mchuchu wangu , dah kweli baada ya mechi nilikuwa very frustrated sababu chama langu , man u tulikula nyingi .

Nikasema Ngoja nikamalizie hasira kwa mpangaji wetu bila kuwaza kuwa tayari nina ngoma toka kwake , lahaura , kumbe masikini mbibi wa watu hajalala anawaza mjukuu wake mbona harudi ?

Mida ya saa saba nikasikia mlango wa nyumba kubwa umefunguliwa mda huo nipo juu ya kifua cha dada mpangaji , sasa nikawaza mda huu bibi anatafuta nini ?kumbe mbibi hajalala anamuwaza mjukuu wake , saa ngapi asimgongee mpangaji mmoja hivi amuulize wapi tunaangaliziaga mpira , mda huo nawasikia.

Mara ghafla nikawa siwasikii tena , kumbe yule mpangaji kauza ramani ya vita , kamchana bibi kuwa mpira ulishaisha ila anadhani nitakuwa chumba cha dada mpangaji maana uwa ananiona naingia usiku .

Bibi wa watu , upendo kwa mjukuu ukamzidi uwezo akagonga hodi kwenye chumba chetu, mdada akaanza kutetemeka ni nini afanye, mimi nimeinama nawaza aibu , naiweka wapi?

Mara mdada kafungua mlango , Bibi kaingia anafoka kwanini unataka kumuua mwanangu , mara akague huku mara kule, muda huo nimejificha kwenye vyombo , Bibi aliponiona akaanza kumpiga mdada na ndala kwanini unataka kumuua mwanangu, akitamka hivyo , mdada alivaa kanga tu , mara akakimbia nje

Mda huo nimevaa boksa na shati tu , Bibi alivomfuata nikavaa suruali Chapu, nikavaa sendo nikatoka nakimbia huku aibu , maana watu wameamka ili kuona ni nini kimetokea.

Nikawaza sana njiani sijui wapi naelekea mwisho nikasema siwezi kufa kizembe, nikaenda moja kwa moja mpaka sitende ya mabasi ya mkoani , pale nikakuta kama mchana hivi , fasta nikauliza kama naweza mpata wakala wa mpesa , nikampata.

Nilitoa elfu themanini, maana ilikuwa kwenye simu , nikakata tiketi kwa elfu hamsini na tano , bukoba kwenda dar , baada ya kupewa hela na nikaoneshwa basi, nilienda mle nikakaa nawaza mengi mpaka najionea aibu mwenyewe mda huo , Bibi anapiga simu sipokei mara nikazima.

Nilifika dar baada ya safari , nikakuta bibi alipiga simu anasema hajui alimuudhi nini mjukuu wake maana amekimbia nyumbani hayupo na hajaaga , dah bibi bwana ila hakusema nimefanya nini ?

Dah nilivoambiwa hivyo , nilijikuta nalia tu , nikaishia kusema nilimiss kurudi dar tu , ila moyoni najua bibi aliamua kuvunga ila baada ya siku kadhaa bibi , alinitafuta akanisihi nisirudie hiyo tabia na pia akaomba niende nikapime UKIMWI , alafu nimpe majibu , kweli nilipima nikajikuta negative .

Dah nilipomwambia bibi alifurahi sana , mpaka nikamsikia analia kwenye simu Ila yule Demu sikumtafutaga tena .

Dah bibi yangu mpaka leo ananipenda sana na hajawahi kunitobolea siri hii

Dah wewe mdada kama uko humu nisamehe bure ulikuwa ujana ndiyo maana sijawah kukutafta
 
Kitu pekee najuta ni kupenda kula mishangazi, hii hali ilianza wakati na balehe yaani nikiwa na umri wa miaka 17 tu nishamla mmama mwenye miaka 45+.

Kama ambavyo mnajua mazoea ni tabia, niliendelea kutoka na mishangazi kiasi kwamba ikaniharibu kisaikolojia nikawa sipendi tena mabinti wenye umri kama wangu.

Ingawa sijaacha bado lakini namshukuru Mungu kwasasa ninapita na mbususu ya umri wowote. Huo uraibu ni mbaya nyie kuliko hata madawa ya kulevya.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mimi at the age of 17 nilikuwa na aibu mno nisingeweza kumvulia mwanamke nguo. Nilichelewa kubalehe kimwili na kiakili
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mimi at the age of 17 nilikuwa na aibu mno nisingeweza kumvulia mwanamke nguo. Nilichelewa kubalehe kimwili na kiakili
Hahah mkuu mimi nimekulia mitaa ya wahuni sana, Nilianza kuwazoea wanawake nikiwa na miaka kumi ya mwanzo maana mabroo wa kitaa ndio walikuwa wanatutuma kuwaitia mademu zao 😂

Hiyo miaka 17 tayari ni kama nilishakuwa mtu mzima.
 
Majuto kwa Familia Nzima:Miaka ya Nyuma Tulikaa na ndugu yetu mmoja,Kukatokea Ugomvi kwa Jirani huyo ndugu yetu Akainuka kwenda kugombelezea(Tungejua Tungemzuia).
Alipofika Akapigwa yeye Ngumi ya Shingo Akafariki Hapohapo mpaka leo tumajutia hili Kwa nn tusingemzuiaa..Mpaka leo nikiona Ugomvi Nakimbiaa.
 
VISA NI VINGI,ILA ACHA NIANZE NA HIKI...

Ni 2010's niko form 4 shule ya kata hiyo mkoani Iringa huko. Nilikua mtoro sana,yani nikisema mtoro ni mtoro kweli. Kwa week naweza kuhudhulia shule mara mbili tu,siku nyingine zote nashinda Samora pale katika maroli ya mchanga,mawe fofali,n.k tunasubiri kazi za upakiaji. Au nakua Isakalilo nachimba zangu mchanga au mawe.

Licha ya mahudhulio yangu kuwa mabaya,ila walimu wengi wa ile shule walikua wananijua,haswa Headmaster. Huyu alinijua kwasababu alinisaidia sana kipindi naingia pale form 1.(Hili nilieleza katika ule uzi wa "Msoto")

Tatizo lilianzia hapa.Siku moja bila hata kutarajia alikuja ndugu yangu mmoja wa karibu kabisa akanichafua sana pale shule,wakati huo nimewekwa mtu kati ofisi za Walimu. Yani aliongea mambo mengi sana,kutokana nae ni mtu mzima na ana mwonekano wa busara busara! Basi walimuamini 100%.

Alisema mimi mhuni(Kibaka),MLEVI sana na nakunywa Ulanzi sanaaa! Nashinda na wahuni, sina nidhamu hata kidogo,n.k,n.k. Wakati huo kumbuka sijawahi kuishi nae tangu namaliza standard 7 huko,nikitelekezwa nikawa naishi tu kama mtoto wa mtaani. Nilikua Chokoraa ambae shule niliipenda ila nilikua nashindwa nijigawe vipi,huku nihudhurie shule au nitafute hela ya kula.

Basi ndugu zangu tuendelee, Headmaster na wale maticha hawakutaka hata kunipa nafasi nijitetee, na hata wangenipa nafasi ya kujitetea sidhani kama ningeweza,nilikua nacheka cheka tu kwa hasira. (Mimi nikikasirika sana huwa natabasamu sana na kakicheko kwa mbaliii).

Kama unavyojua shule zetu za kata,mimi nikadhani yanaishia pale,ajabu yule ndugu yangu akaamuru nichapwe viboko hadharani. Ikagongwa kengere pale,wanafunzi wakakusanyika pale,nikachafuliwa sana pale assemble,daah yani chafuliwa sanaaaa! Muda huo mimi hasira zimejaa level yake ila tabasamu limejaa usoni halikauki,ndio nilivyo.

Kama unavyojua wanafunzi, mashtaka yalikua kibao,ila points za msingi walizochukua ni "Mimi Kibaka" na "Mlevi,nakunywa sana Ulanzi".

Daah wakawa wananitania sana kila nikienda shule katika zile siku mbili zangu za week, nikawa nahisi karaha,basi nikapunguza mahudhulio kutoka siku mbili mpaka siku moja kwa week au siendi kabisa.

Basi kuna siku nikaenda shule ni kipindi tunakaribia kufanya mtihani wa Mock, Headmaster akaniita Ofisini. To be honest sijawahi kwenda shule nikiwa na "Majagi" kichwani,ila siku hiyo nilikua Majagi haswaa,ila nimekula majani ya mti wa limao ili kuzuia harufu. Daah kufika ofisi ya Headmaster si akaanza kunikumbushia yale ya siku zile,akawa kama ananisimanga na ule msaada ambao alinipa kipindi naanza form 1.

Siwafichi uvumilivu ulinishinda,nikawa natetemeka kwa hasira yule mzee yuko mbele yangu kakaa anaendelea kutema shombo zake. Nikagonga meza kwa hasira "Kaa kimya wewe mzee",...aah mzee akajaa upepo baada ya kuona kama namchimba mkwara,si akasimama tukawa tunatazamana ila yeye yuko upande wa pili wa meza.

Aisee! Nilimpa ndonga (Kichwa) moja matata sana mpaka akajikuta kakaa chini bila kutarajia,alafu kimyaa!. Nikajua nimeua wakuu,ila nikavaa roho ngumu nikatoka mle ndani kama hakuna kitu kimetokea,nikatimkia mtaani.

KITU NAJUTIA
Ni kumpiga kichwa mtu ambae anakaribiana na babu yangu. Yani najuta sana.
 
Tobaaa kumbe we ni mhenga eeeh? Nimeghairi kukutongoza. Ni bibi kabisa
KWani hujui kuwa hata nyie mnatongozwa km sisi??? au umesahau?? usijitetee?? unatongozwa!! unabisha?? kwa kuwa naniliu haina cha uzeee!! ukiona vepi njoo nikuunganishe utongozwe make huwezi nitongoza mie!!!...... umekiri kushindwa hadharani !
 
No.1
Way back 2000 nikiwa bado barobaro
Kipindi cha ubabe wa madenti na makonda bado upo sana kuna mwamba mmoja alikuwa konda wa panya temeke-mikoroshini huyu anaitwa (faki)
Nami nilikuwa mkazi wa huko mikoroshini miaka hiyo
Kutokana na ubabe wa madenti na makonda one day hapo mwenge tukaingiana maungoni vibaya mno mida ya wanafunzi saa 12 ikatokea baada ya hapo tukawa washikaji kivile
Baadae maisha yakasonga tukahama huko mikoroshini to mbezi ya kimara
15/12/2000 jamaa yangu akanialika kwenye kipaimara ya mdogo wake mitaa ya ova huyu mshikaji tulikuwa nae secondary miaka hiyoo soo tukafanya yetu kwenye sherehe mixer safari lager zile fupi wakati huo
Kwakuwa mwana kwao njema midaa ya saa 7 usiku akaniaogeza na mkoko wa mzee wake mpaka mitaa ya home
Kumbuka miaka hiyo kipande cha mlandzi- ubungo ndio kinajengwa na mtaliano kampuni ya skamphil collars
Baada ya foleni kidogo tukakaribia home jamaa akaniacha nia home
Nikaanza kuswampa kwa miguu kama dk 5 nikafika home
Sasa nakawa namwaga kojo ili nilale bahati mbaya home hakukuwa na umeme wakati huo ila kwa jirani alishaweka
Huyu jirani (rip) brother Andrew sasa na like wenge la safari mbili nilizo piga kwenye kipaimara sijui hili wala lile lahaula
Kumbe wezi wamemvamia jiran brother Andrew wamepuliza dawa wapo hoi bi taabani na usingizi
Shughuli ipo hapo mie ndio naona kwa jirani kuna movement za watu mixer wengineo kujificha ili nimalizie kukojoa
Na mie nikavunga kama sijaona kitu
Mida hiyo ni very late middle of the night
Nikazunguka mlango wambele wa nyumba
Nimshitua mama kwamba kwa brother kumekucha huko wamama zetu Hawa sasa sikutetemeka mixer pressure kupanda
Bimkubwa akaanza kupagawa nini kifanyike
Akili ya kazi ikanijia nichukue panga na jiwe dada wa kazi na bimkubwa wao wapige nduru mimi nirushe jiwe kwenye paa la brother likifika nami niwe nimefka ilikuwa changanya
Plan ikafanikiwa jiwe linafika nduru juu mie nafika majizi yakachachawa yakapotezana mie nikakomaa na mmoja na panga langu kwenye machaka mixer gizan haoo sasa yule ninae mkimbiza kumbe ananondo si akajeuka kuniatack daa hapa namshuru Polomo huyu ni mwalimu wangu wa self defense walio insi mikoroshini na vertinary miaka hiyo wanajua watoto wa huko
Nika apply za Polomo nika jibu mashambulizi kwa mwizi panga ya kichwa nikashusha shingoni jamaa over bleeding ikamondo wananzengo wanafika kumulika mwizi hamadi ni yule Faki konda wa panya mwenge-mikoroshini nikakausha
Brother kule kaamka na mixer wameiba stabilizer tuu dundo Sony lipo
Kumbe brother ana mkuu huko police force
Simu moja londo likaja chukua mzoga
Baadae Jiji letu saa 12 afande tibaigana anarindima
Kwa taarifa ya jeshi ra porisi
Majambazi yamevamia nyumba ya brother ..... ila wananchi walifanikiwa kuwadhibit
 
Angevuta ingekuwa bonge la msala...Mungu ni mwema...
Mkuu nilicho gundua maugomvi ya wazazi jua kuna upande una makosa na sisi kama watt wao wana tusisha sana,Na wazazi nao wanatupotezea kitu si sahihi.
Baadae huko wanajirudi na kuona hatuwajali...
Ni kweli kaka ila sometimes ugomvi wao hata kama bimkubwa alikuwa ana makosa mpk wakashindwa kuishi pamoja ila mie mtoto hayo hayanihusu mie nimeshuhudia bimkubwa anahangaika kunitafuta ada toka primary School ( miaka hiyo kulikuwa na ada) mpaka nafika chuo sijawahi kumuona mshua akijihusisha na mie automatically nitakuwa upande wa bimkubwa
 
we acha tu sikuwa na furaha kabisa kuanzia hapo najuta kabisa kusoma chuo
Inauma asikuambie mtu. Hakuna kitu kibaya kama njaa, na ukiwa. Itafute movie ya paid in full utaelewa.

Huoni umuhimu wa kuishi tena, hasa machizi uliyoshibana nao wakiondoka. Inauma sana hasa giza likianza kuingia.

Unasikia kwa mbali sauti za ndege
 
Back
Top Bottom