Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

Daah wazungu walikuheshim sana mkuu .hiyo mitaa ulikua ukiishi ni ushuani sana ,haipishani sana na spring valley ni uzunguni kama osterbay na masaki kwa bongo
 
Duuh how ? Ndiyo origin of this name Terminator?
 
JKT

Katika harakati za kutafuta Ugali nilijikuta nimeomba kujiunga na jeshi la JKT. Nikatupiwa Kigoma, kule Bulombora 821KJ.

Nikapigishwa jaramba na kulishwa vumbi huku nikitazama ziwa Tanganyika kwa ukaribu kabisa lililozungukwa na mawese ya kutosha. Ruka Juu, Kanyaga Chini kwa nguvu mpaka mguu utoke nje ya kiatu.


Mikesha ilivyozidi nikaona hapa nitakufa. Nikaanza harakati za kutafuta nafasi ya kulala vizuri maana zile Dakika 5 unazopewa za kulala hazitoshi kabisa. Nikaanza kutafuta machimbo. Wenzangu wakienda mkesha, mimi najipeleka porini. Siku nyingine nakutana na ma afande na wao wamedoji kwenda lindo wananitimua najikuta nimerudi kulala uvunguni.

Tabia yangu ya kujizoesha kulala ikaanza kunigharimu. Ikafika mahali nikawa siwezi kabisa kwenda kukesha hata siku moja. Nikaanza kuona hadi uvivu wa kwenda kulala mbali na anga letu. Nakumbuka nilikua Eagle Coy.

Siku hiyo nimelala uvunguni nakoroma kabisa, saa ngapi afande asiingie ndani kutafuta watoro. Si akaniskia navyokoroma kule chini ya kitanda. Dah sitasahau hiyo kipigo niliyopewa. Nakumbuka al manusura nipoteze jicho. Maana vile vitanda vimechomelewa kwaiyo kuna kama vichuma flani hivi kama nondo vimejitokeza kwa juu, alinibamiza kichwa kwenye kile kitanda ile nondo ikachubua kidogo pembeni ya jicho.

Sijui nilipata wapi ujasiri nikamsukuma pembeni nikasogeza kioo cha dirisha nikarukia nje nikaanza kukimbia huku nachechemea machozi yananitoka ya kutosha. Jamaa nadhani aliniangalia navyokimbia kwa tabu akanionea huruma akaamua kuachana na mimi huku akisema "Nitakuua Mbwa Wewe".

Nilivyofika walipo wenzangu kwenye mkesha nikapokelewa tena na adhabu za kubiringita na kukwepa ndege za kivita. Dah.. nilihisi mwisho wangu umefika, nikasema kwa sauti "Nakufa" huku machozi yanatoka ili hata jamaa anionee huruma lakini wapi. Yeye kakazana kunioshea na kunifanya mfano kwa wengine. Saiyo pumzi imekata, maumivu kila mahali, machozi yameshatoka mpaka yamekauka, siwezi kuongea tena. Ni kwa Neema za Allah pekee nilifanikiwa kuona tena Jua siku iliyofuata maana nilikua nahisi kabisa nakufa. Hali yangu ilikua mbaya sana!

Sikuwahi kujuta kwenye maisha yangu kama hiyo siku. Nililaani uamuzi wangu wa kwenda huko. Kile kitu kilinikaa sana moyoni kwa muda mrefu. Niliona kabisa huku sio kwangu. Course ilivyoisha, wakati wengine wanasikilizia kwenda JWTZ na Polisi, mimi nikaandaa nauli yangu, nikavizia ule muda tunaotumwa kwenda town...nikatorokea huko mazima na nikaapa sitarudi tena. Ikawa imeisha hiyo!

Kwa kweli mambo ya Jeshi yana watu wake. I was not one of them!
 
🤣🤣🤣 Daah! Nimecheka sana
 
😆😆😆 inafurahisha na kusikitisha at the same time. Vipi magodoro ulilipa?
 
Pambana baharia, ndo matokea ya nature yenu wanaume. Halafu mnajiuliza why wanaume hufa mapema...jibu ni kwasababu ya hizo stress zenu za kujitakia.
 
Njia pekee ya kuishi kwa amani kama wanao wanajitambua muombe mkeo mje muishi nao,wanawake somtym tuna mambomengi

Kwanza kufanya watoto wetu ndo sehemu ya kumaliza shida zetu la pili unaweza jikuta unawekwa mbali na mwanao siku ambayo utamjibu huna kitu so kuepusha hayo Lea wanao kma unaweza kuwahudumia wakiwa mbali sidhani km itashindikana.
 
Ukiua bila kukusudia siyo murder ni manslaughter kwakuwa hakukuwa na malice afforethought.Katubu moja kwa moja kwa Mungu wako unayemuamini na Toba yako itapokelewa.
 
Nikiwa sekondari nilikuwa na masela wangu tunatoroka daily. Yaani tukiona shuleni tuu haukueleweki tunasepa. Mtoto wa headmaster ndiyo alikuwa kiongozi alikuw na mkasi wa kukatia fensi, anakata raia tunayeya.

Basi bana siku moja tuko njemba kama sita. Wa kwanza akapita kweny tundu la fens akaruka, kulikuwa na kimtaro halaf ndiyo unaingia main road. Watano Tukapita wote frexh tukaanza kuicha main road tunazitafuta CHOCHO, sasa yule wa Sita anaingia tuu main road mara gari ya headmaster hii hapa ikasimama mbele yake.

Headmaster akamuita jamaa anatukimbilia sisi, headmaster akatucheki na sisi pia japo kwa mbali tukawa hatuna namna ikabidi tuongeze spidi. Kufika chocho zaidi Tukamlaum sana jamaa katupa msala bora asingemkimbia headmaster angeend wamalizane. [emoji16]

Kesho yake school ikapigwa ambush ya maana jamaa akataja alikuw na sisi tulichezea haswa na tukanunua fensi ya shule nzima
 
Hahahah- pole sana mkuu, kisa chako najiona kabisa ni mimi, japo tofauti ni ndgo, mimi nlifanya nikiwa sekondari shule ya private, nlifanya kuanzia form 3 na 4 then advance nkafanya mwaka mmoja nlipata msala tofaut na huo nkafukuzwa mazima, nlimfanyia pia mdgo angu form 3 na 4 akamaliza flesh na haikuwah kugundulika

nlikua nikipewa ada lets say laki tano mim natumia si zaid ya elfu 30 kukamilisha mchakato wote . Inayobk ni bata tu, nlienjoy sanaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…