Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

INAUMA niliua pasipo kujua kama ninaua hii kitu inaniuma sana maana hakuna aliejua zaidi yangu na hadi sasa sijui nitakuja kuitubia wapi hii dhambi maana hata Mimi mwenyewe sikujua kama ninaua, ila baada ya kifo kutokea ndio nikaunganisha dot nikagundua iam murder pasipokujua, Binadam ni watu wabaya sana na wanaweza kukutumia kuuwa then wakakudamp.

sio kila kitu cha kusimulia Mkuu, kuna siri nenda nazo kaburini.

Natumai hautoelezea ilikuwaje
 
Tulichapwa bakora siku ya kumaliza necta form six


Siku hiyo sitosahau nilikula mijeledi kama yesu msalabani bila kosa ndo nikaamini sio kila anayeenda jela ana makosa


Ilikua hivi Nakumbuka ilikua Alhamisi ile tunamalizia mtihani wa mwisho msimamizi akatuambia mkimaliza mtihani muende uwanjani msiondoke kwanza tukasema poa tulikua tunahisi sijui walimu wanakuja kutupongeza basi tukapiga pepa pale mpaka muda tunaambiwa pens down watu wakaanza kuvunja ruler wanatupa peni wengine wanachana mashati wanachana suruali kwa furaha ya kumaliza Mimi sikupanga kuchana ila kuna jamaa tulikua tunamuita Mjita(mtu wa ukerewe)alikua amekaa nyuma yangu akachukua kiwembe akaanza kuchana shati langu mgongoni
Nilimuacha achane tu kwani halina kazi tena (Najuta kumuacha achane lile shati)



Basi msimamizi akakusanya mitihani na kuondoka zake lile darasa nililokuwepo watu hawakuchana sana uniform nilishangaa nilichokiona baada ya kutoka nje kuna darasa lingine hao walichana nguo sio poa unaweza sema ni machizi wameachiliwa kifungoni kila mtu kachana anavyojua basi(kumbuka mjita alichana shati langu mgongoni)
Basi tukakusanyika uwanjani kama tulivyoambiwa tunashangaa tunaambiwa tukae chini na wale mapolisi waliokuwa wanasimamia mitihani tukawa tunajiuliza nini kina endelea


Kumbe Jana yake kuna baadhi yaform six walichana magodoro na mashuka ya form five na hiyo taarifa ikamfikia mkuu wa shule ndo akawaambia wale form five waandike majina ya watu wanaowahisi kufanya hicho kitendo na majina yalipelekwa kwa mwalimu mkuu ndo akawaambia polisi hawa vijana wakimaliza mtihani kuna haya majina shughulika nayo hiyo ndo ilikua sababu ya kuitwa pale uwanjani



Basi Yale majina yakaitwa wakasimamishwa pembeni alafu yule afande akasema mbona naona watu wamechana uniform..dah akasema wote waliochana uniform na nyie simameni jiungeni na hawa waliochana mashuka maskinii mjita aliniponza na Mimi nikajumuishwa Kwenye msala.tulikua kama 25 hivi tukaambiwa pangeni mstari mmoja kuelekea ofisini.wale ambao hawakuchana uniform zao waliruhusiwa waondoke sisi tukabaki
Polisi akaanza kusema nyie ndo wahuni eeh basi tutaonyeshana uhuni niliogopa sana



Tukapelekwa mpaka assembly ground tukaanza kupigishwa kwata na wale mapolisi dah Mara headmaster akaja akasema Leo nawachapa nawaaga kwa kuwachapa dah niliona kama ndoto hivi nachapwa siku ya kumaliza Necta Moyoni mwangu naendelea kumlaumu mjita kwa kuniponza,tulijitetea kwamba sisi hatuhusiki na kuchana mashuka sisi tumechana nguo zetu tu majina yao si yapo hapo sisi hatuhusiki ila wale polisi hawakutaka kuelewa wakaona ni wale wale tu wachanaji magodoro na wachanaji uniform



Basi headmaster akaagiza mzigo wa fimbo ukaletwa akaanza kutupelekea moto afu anachapa fimbo za mgongoni na kiunoni lazima akuachie alama kama sio Kukutoa damu.dah tulipelekewa moto sana kwa bahati nzuri na mjita nae alichana nguo Kwahyo tulikua wote tunasulubiwa (ningeumia sana kama mjita asingekuwepo) basi nikiona mjita anakula mijeledi na Mimi nafarijika
Kumbuka hapo tushamaliza mtihani wa necta wale wasimamizi ndo wa nasubiri lile gari linalozunguka kusambaza na kufuata mitihani mashuleni lije kuwafuata kwahyo hapo pona yetu ni mpaka lile gari lifike dah basi headmaster akaendelea kutupiga mijeledi na walimu wengine wakaunga tela tulichakazwa haswaa alama kibao mgongoni na kiunoni mpaka lile gari linafika tulikua tupo juu ya Mawe(lawama zote ziende kwa mjita)



Tulikubali kusulubiwa japokua tulikua tumemaliza necta tungeweza kugoma kuchwapwa lakini hatukuwa na jeuri hiyo kwa sababu polisi walikuwepo dah Kwahyo ukigoma tu polisi wanakuchezeshea mikwaju na unaenda kulala kituoni dah ikabidi tuache tu headmaster atupelekee moto chini ya uangalizi wa polisi,baada ya kipindi cha muda mrefu hatimae gari la kukusanya mitihani likafika ndo wale polisi wakaondoka na headmaster akatuacha ila hakutucha hivi hivi aliandika majina yetu ili siku ya kuja kuchukua result slip tulipe magodoro dah ilikua siku ya kihistoria Magodoro sikuchana,nguo sikuchana kwa mikono yangu,na mijeledi nimesulubiwa

Mjita popote ulipo mataccor yakooo!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
[emoji2]
Ulitokea mgomo shuleni na umeme ulikuwa umekata wana wameenda kumtia adabu headmaster mimi nikaamua kujificha bwenini nkalala deka la juu, maana mshua aliniasa mambo ya migomo nisishiriki sisi ni masikini.

Ebwana eeh majamaa wameenda wakakuta headmaster kakimbia wakaona waje kuzimalizia hasira kwa waliolala bwemi waliokataa kugoma aisee

Bwemi la mbele kuna wanawakadakwa wakaanza kushambuliwa kwa bakora huku wengine wakivunja vioo,

Nilijikuta tuu nipo sakafuni natimua mbio kuelekea kwenye shamba la mahindi, kumbe kuna mmasai na wenzake walikuwa mle ndani nao nilishangaa wameibuka kama mizimu tunaongozana kwenye mahindi
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaaaah
 
Ninachojutiaa ni 2016 dem mmoja hv sister aliniombaa niendee kwakee nikamsaidiee kufungaa kitandaa chake alinunuaa ,nikaendaa bhanaa kilichonikutaaa baada ya kufungaa kitandaa nikaanza kupigishwa story za hapa napale wkt nataka kusepaa akaniambia unaondokaje ujanywa hata soda c ndio akaletaa coca na wine bhanaaa tukaanza kunywa hapo ilikuwaa mida ya saa nne asubuh cku ya jpili huku tunapiga story ,maraa akasemaa ngojaa aandaee breakfast bhanaa bhanaa breakfast ikajaa tukaendeleaa na winee nikamtaniaa ,wine aipandi bhanaa nifanyie mpng wa safari mbili kubwaa nikampaa ten afate dukani akakataa akasemaa nisijali ataninuliaaa bhanaa akafata safar akaja nazo ,yy nikamwachia wine [emoji485] mm nikaanza kunywa safari mdg mdg tu ,baada safari zikakoleaa na dem wine ishamlegeza macho full kujichekeshaa tu mwishowee nikatakaa kusepaa ndipo dem akaniambia JIONGEZE nikamwambia hapanaaa ww n km sister tu bhanaa ,weeee akakimbilia mlango akafungaa na funguo akachomoaaa bhanaa bhanaa akawaa sasaa ananitaka tuduuu wt uku akiongeaaa mambo mengi na jinc anavyonizimiaaa tokaa cku aliponionaaa mtaani kwangu tokaa ameamia akaona mm ndio mwanaume namfaaaa bhanaa ajaongeaa mengi mwishowee ALINIBAKAAA ,,,baada yakubakwaa na yulee dem ckutegemeaa kbs kilichokujaa tokeaa maishan maana nawaambiaaga watu nilibakwa na mwanamkeee hawaamini kbs
Ok
20220327_152844.jpg
 
Nikiwa sekondari nilikuwa na masela wangu tunatoroka daily. Yaani tukiona shuleni tuu haukueleweki tunasepa. Mtoto wa headmaster ndiyo alikuwa kiongozi alikuw na mkasi wa kukatia fensi, anakata raia tunayeya. Basi bana siku moja tuko njemba kama sita. Wa kwanza akapita kweny tundu la fens akaruka, kulikuwa na kimtaro halaf ndiyo unaingia main road. Watano Tukapita wote frexh tukaanza kuicha main road tunazitafuta CHOCHO, sasa yule wa Sita anaingia tuu main road mara gari ya headmaster hii hapa ikasimama mbele yake. Headmaster akamuita jamaa anatukimbilia sisi, headmaster akatucheki na sisi pia japo kwa mbali tukawa hatuna namna ikabidi tuongeze spidi. Kufika chocho zaidi Tukamlaum sana jamaa katupa msala bora asingemkimbia headmaster angeend wamalizane. [emoji16] kesho yake school ikapigwa ambush ya maana jamaa akataja alikuw na sisi tulichezea haswa na tukanunua fensi ya shule nzima
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaah
 
sio kila kitu cha kusimulia Mkuu, kuna siri nenda nazo kaburini.

Natumai hautoelezea ilikuwaje
siwez kuielezea lakin hata nikiamua kuielezea haina madhara kabisa maana nilifanya bila kujua kama ninafanya uovu na matokeo yake hayakuonekana mda huo huo,

Ilichukua mda sana hadi baadae ambapo matokeo yalionekana kwa hiyo nilijua ukweli kwa kuunganisha matukio ila ndi ikawa tayari yalishamwagika hayawezi kuzoleka na hata kama ningejua sikuwa na namna ya kumnasua maana tayar alikuwa anakufa ndani kwa ndani hapa kinachoniuma ni kujua kuwa nimetumiwa kuuwa pasipokujua
 
Mim mpaka leo najuta kuwahadithia washkaj zangu namna nilivyomla jimama la miaka 45+.

Yaan mpaka leo wakimuona lazima wanizingue halaf jimama lenyewe halivungi likiniona na washkaj lazima lije[emoji51][emoji51]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaah.
 
siwez kuielezea lakin hata nikiamua kuielezea haina madhara kabisa maana nilifanya bila kujua kama ninafanya uovu na matokeo yake hayakuonekana mda huo huo, ilichukua mda sana hadi baadae ambapo matokeo yalionekana kwa hiyo nilijua ukweli kwa kuunganisha matukio ila ndi ikawa tayari yalishamwagika hayawezi kuzoleka na hata kama ningejua sikuwa na namna ya kumnasua maana tayar alikuwa anakufa ndani kwa ndani hapa kinachoniuma ni kujua kuwa nimetumiwa kuuwa pasipokujua
Vipi aliyekutumia alijua kuwa umegundua mchezo wake?
 
Kuna utumwa FULANI umeasisiwa na Dini hasa kikristo ambao ni KUFUNGA ndoa tena ndoa ya mke MMOJA tu!!!kwamba bila jicho ndoa unakua mdhambi na mnateseka kweli!!!KWA Kuwa una kipato Chako Kuwa HURU Angalia mtu ambaye unajivunia hata ukiwa nae Karibu mtu ambae anatosha nafsini mwako na usiwe na wazo la kuvaa shela utumwa bali ukaribu ule wa KILA siku wa kushea changamoto zote hata kama ameoa wewe kama una mfeel Kuwa nae!!wala Dini sijui moto sijui ujinga GANI na presha za Maisha zisikuchanganye!!mradi awe anazingua kwako na kutoka na WATU wanaona kwamba mwamba anamiliki!!ukipigiwa kelele coz ameoa we sema mi mke wa pili na fresh tu SIJALI!!!usifinyangwe moyo I na wazo la ndoa na shela wakati ubikira ulishaupoteza!!wanaofunga ndoa na sio bikra wanajidanganya kwani ndoa yao ya kweli ni ile siku wamepoteza bikra hizo nyingine ni tafrija za kula wali na picha za kwenye fremu!!!!Achana na matazamio makubwa ya uongo AMBAYO yatakuumiza usifurahie Maisha!!!!IMANI ZA KIDINI ZINATESA WATU SANA COZ ZIMAZUIA ASILI HALISI ZA BINADAMU NA UUMBAJI!!!!CHANGAMKA WEWE MBONA MSOMI!HALAFU UNATUANGUSHA !!!
Nipe tano mkuu
 
And Another!

Katika harakati za kutafuta Ugali nilijikuta nimeomba kujiunga na jeshi la JKT. Nikatupiwa Kigoma, kule Bulombora 821KJ.

Nikapigishwa jaramba na kulishwa vumbi la kutosha huku nikitazama ziwa Tanganyika kwa ukaribu kabisa lililozungukwa na mawese ya kushato. Ruka Juu, Kanyaga Chini kwa nguvu mpaka mguu utoke nje ya kiatu.


Mikesha ilivyozidi nikaona hapa nitakufa. Nikaanza harakati za kutafuta nafasi ya kulala vizuri maana zile Dakika 5 unazopewa za kulala hazitoshi kabisa. Nikaanza kutafuta machimbo. Wenzangu wakienda mkesha, mimi najipeleka porini. Siku nyingine nakutana na ma afande na wao wamedoji kwenda lindo wananitimua najikuta nimerudi kulala uvunguni.

Tabia yangu ya kujizoesha kulala ikaanza kunigharimu. Ikafika mahali nikawa siwezi kabisa kwenda kukesha hata siku moja. Nikaanza kuona hadi uvivu wa kwenda kulala mbali na anga letu. Nakumbuka nilikua Eagle Coy.

Siku hiyo nimelala uvunguni nakoroma kabisa, saa ngapi afande asiingie ndani kutafuta watoro. Si akaniskia navyokoroma kule chini ya kitanda. Dah sitasahau hiyo kipigo niliyopewa. Nakumbuka al manusura nipoteze jicho. Maana vile vitanda vimechomelewa kwaiyo kuna kama vichuma flani hivi kama nondo vimejitokeza kwa juu, alinibamiza kichwa kwenye kile kitanda ile nondo ikachubua kidogo pembeni ya jicho.

Sijui nilipata wapi ujasiri nikamsukuma pembeni nikasogeza kioo cha dirisha nikarukia nje nikaanza kukimbia huku nachechemea machozi yananitoka ya kutosha. Jamaa nadhani aliniangalia navyokimbia kwa tabu akanionea huruma akaamua kuachana na mimi huku akisema "Nitakuua Mbwa Wewe".

Nilivyofika walipo wenzangu kwenye mkesha nikapokelewa tena na adhabu za kubiringita na kukwepa ndege za kivita. Dah.. nilihisi mwisho wangu umefika, nikasema kwa sauti "Nakufa" huku machozi yanatoka ili hata jamaa anionee huruma lakini wapi. Yeye kakazana kunioshea na kunifanya mfano kwa wengine. Saiyo pumzi imekata, maumivu kila mahali, machozi yameshatoka mpaka yamekauka, siwezi kuongea tena. Ni kwa Neema za Allah pekee nilifanikiwa kuona tena Jua siku iliyofuata maana nilikua nahisi kabisa nakufa. Hali yangu ilikua mbaya sana!

Sikuwahi kujuta kwenye maisha yangu kama hiyo siku. Nililaani uamuzi wangu wa kwenda huko. Kile kitu kilinikaa sana moyoni kwa muda mrefu. Niliona kabisa huku sio kwangu. Course ilivyoisha, wakati wengine wanasikilizia kwenda JWTZ na Polisi, mimi nikaandaa nauli yangu, nikavizia ule muda tunaotumwa kwenda town...nikatorokea huko mazima na nikaapa sitarudi tena. Ikawa imeisha hiyo!

Kwa kweli mambo ya Jeshi yana watu wake. I was not one of them!
Nimecheka kama mazuri ila jamaa yangu unaonekana ni mtundumtundu sana
 
Nitaleta yangu jinsi mbuzuza ilivyotaka kuniua sitasahau aisee duh nimeshikiwa bastola kiss mbuzuza
 
Kitu pekee najuta ni kupenda kula mishangazi, hii hali ilianza wakati na balehe yaani nikiwa na umri wa miaka 17 tu nishamla mmama mwenye miaka 45+.

Kama ambavyo mnajua mazoea ni tabia, niliendelea kutoka na mishangazi kiasi kwamba ikaniharibu kisaikolojia nikawa sipendi tena mabinti wenye umri kama wangu.

Ingawa sijaacha bado lakini namshukuru Mungu kwasasa ninapita na mbususu ya umri wowote. Huo uraibu ni mbaya nyie kuliko hata madawa ya kulevya.
 
Back
Top Bottom