Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

Ni kweli kaka ila sometimes ugomvi wao hata kama bimkubwa alikuwa ana makosa mpk wakashindwa kuishi pamoja ila mie mtoto hayo hayanihusu mie nimeshuhudia bimkubwa anahangaika kunitafuta ada toka primary School ( miaka hiyo kulikuwa na ada) mpaka nafika chuo sijawahi kumuona mshua akijihusisha na mie automatically nitakuwa upande wa bimkubwa
We need to smart...Bi Mkubwa mara nyingi atapambana hadi akikishe kuna kula kusoma na maisha mengine mema yaje.Alafu hana kinyongo mdingi akirudi choka mbaya atampokea na kumshukuru Mungu...
Muendelezo ndio ule ule ususani sisi vijana tuache kujisahau na kuwatupa watoto wetu..Somo kubwa sana...
 
VISA NI VINGI,ILA ACHA NIANZE NA HIKI...

Ni 2010's niko form 4 shule ya kata hiyo mkoani Iringa huko. Nilikua mtoro sana,yani nikisema mtoro ni mtoro kweli. Kwa week naweza kuhudhulia shule mara mbili tu,siku nyingine zote nashinda Samora pale katika maroli ya mchanga,mawe fofali,n.k tunasubiri kazi za upakiaji. Au nakua Isakalilo nachimba zangu mchanga au mawe.

Licha ya mahudhulio yangu kuwa mabaya,ila walimu wengi wa ile shule walikua wananijua,haswa Headmaster. Huyu alinijua kwasababu alinisaidia sana kipindi naingia pale form 1.(Hili nilieleza katika ule uzi wa "Msoto")

Tatizo lilianzia hapa.Siku moja bila hata kutarajia alikuja ndugu yangu mmoja wa karibu kabisa akanichafua sana pale shule,wakati huo nimewekwa mtu kati ofisi za Walimu. Yani aliongea mambo mengi sana,kutokana nae ni mtu mzima na ana mwonekano wa busara busara! Basi walimuamini 100%.

Alisema mimi mhuni(Kibaka),MLEVI sana na nakunywa Ulanzi sanaaa! Nashinda na wahuni, sina nidhamu hata kidogo,n.k,n.k. Wakati huo kumbuka sijawahi kuishi nae tangu namaliza standard 7 huko,nikitelekezwa nikawa naishi tu kama mtoto wa mtaani. Nilikua Chokoraa ambae shule niliipenda ila nilikua nashindwa nijigawe vipi,huku nihudhurie shule au nitafute hela ya kula.

Basi ndugu zangu tuendelee, Headmaster na wale maticha hawakutaka hata kunipa nafasi nijitetee, na hata wangenipa nafasi ya kujitetea sidhani kama ningeweza,nilikua nacheka cheka tu kwa hasira. (Mimi nikikasirika sana huwa natabasamu sana na kakicheko kwa mbaliii).

Kama unavyojua shule zetu za kata,mimi nikadhani yanaishia pale,ajabu yule ndugu yangu akaamuru nichapwe viboko hadharani. Ikagongwa kengere pale,wanafunzi wakakusanyika pale,nikachafuliwa sana pale assemble,daah yani chafuliwa sanaaaa! Muda huo mimi hasira zimejaa level yake ila tabasamu limejaa usoni halikauki,ndio nilivyo.

Kama unavyojua wanafunzi, mashtaka yalikua kibao,ila points za msingi walizochukua ni "Mimi Kibaka" na "Mlevi,nakunywa sana Ulanzi".

Daah wakawa wananitania sana kila nikienda shule katika zile siku mbili zangu za week, nikawa nahisi karaha,basi nikapunguza mahudhulio kutoka siku mbili mpaka siku moja kwa week au siendi kabisa.

Basi kuna siku nikaenda shule ni kipindi tunakaribia kufanya mtihani wa Mock, Headmaster akaniita Ofisini. To be honest sijawahi kwenda shule nikiwa na "Majagi" kichwani,ila siku hiyo nilikua Majagi haswaa,ila nimekula majani ya mti wa limao ili kuzuia harufu. Daah kufika ofisi ya Headmaster si akaanza kunikumbushia yale ya siku zile,akawa kama ananisimanga na ule msaada ambao alinipa kipindi naanza form 1.

Siwafichi uvumilivu ulinishinda,nikawa natetemeka kwa hasira yule mzee yuko mbele yangu kakaa anaendelea kutema shombo zake. Nikagonga meza kwa hasira "Kaa kimya wewe mzee",...aah mzee akajaa upepo baada ya kuona kama namchimba mkwara,si akasimama tukawa tunatazamana ila yeye yuko upande wa pili wa meza.

Aisee! Nilimpa ndonga (Kichwa) moja matata sana mpaka akajikuta kakaa chini bila kutarajia,alafu kimyaa!. Nikajua nimeua wakuu,ila nikavaa roho ngumu nikatoka mle ndani kama hakuna kitu kimetokea,nikatimkia mtaani.

KITU NAJUTIA
Ni kumpiga kichwa mtu ambae anakaribiana na babu yangu. Yani najuta sana.
Ulitakiwa kutiwa risasi ya kichwa.
 
No.1
Way back 2000 nikiwa bado barobaro
Kipindi cha ubabe wa madenti na makonda bado upo sana kuna mwamba mmoja alikuwa konda wa panya temeke-mikoroshini huyu anaitwa (faki)
Nami nilikuwa mkazi wa huko mikoroshini miaka hiyo
Kutokana na ubabe wa madenti na makonda one day hapo mwenge tukaingiana maungoni vibaya mno mida ya wanafunzi saa 12 ikatokea baada ya hapo tukawa washikaji kivile
Baadae maisha yakasonga tukahama huko mikoroshini to mbezi ya kimara
15/12/2000 jamaa yangu akanialika kwenye kipaimara ya mdogo wake mitaa ya ova huyu mshikaji tulikuwa nae secondary miaka hiyoo soo tukafanya yetu kwenye sherehe mixer safari lager zile fupi wakati huo
Kwakuwa mwana kwao njema midaa ya saa 7 usiku akaniaogeza na mkoko wa mzee wake mpaka mitaa ya home
Kumbuka miaka hiyo kipande cha mlandzi- ubungo ndio kinajengwa na mtaliano kampuni ya skamphil collars
Baada ya foleni kidogo tukakaribia home jamaa akaniacha nia home
Nikaanza kuswampa kwa miguu kama dk 5 nikafika home
Sasa nakawa namwaga kojo ili nilale bahati mbaya home hakukuwa na umeme wakati huo ila kwa jirani alishaweka
Huyu jirani (rip) brother Andrew sasa na like wenge la safari mbili nilizo piga kwenye kipaimara sijui hili wala lile lahaula
Kumbe wezi wamemvamia jiran brother Andrew wamepuliza dawa wapo hoi bi taabani na usingizi
Shughuli ipo hapo mie ndio naona kwa jirani kuna movement za watu mixer wengineo kujificha ili nimalizie kukojoa
Na mie nikavunga kama sijaona kitu
Mida hiyo ni very late middle of the night
Nikazunguka mlango wambele wa nyumba
Nimshitua mama kwamba kwa brother kumekucha huko wamama zetu Hawa sasa sikutetemeka mixer pressure kupanda
Bimkubwa akaanza kupagawa nini kifanyike
Akili ya kazi ikanijia nichukue panga na jiwe dada wa kazi na bimkubwa wao wapige nduru mimi nirushe jiwe kwenye paa la brother likifika nami niwe nimefka ilikuwa changanya
Plan ikafanikiwa jiwe linafika nduru juu mie nafika majizi yakachachawa yakapotezana mie nikakomaa na mmoja na panga langu kwenye machaka mixer gizan haoo sasa yule ninae mkimbiza kumbe ananondo si akajeuka kuniatack daa hapa namshuru Polomo huyu ni mwalimu wangu wa self defense walio insi mikoroshini na vertinary miaka hiyo wanajua watoto wa huko
Nika apply za Polomo nika jibu mashambulizi kwa mwizi panga ya kichwa nikashusha shingoni jamaa over bleeding ikamondo wananzengo wanafika kumulika mwizi hamadi ni yule Faki konda wa panya mwenge-mikoroshini nikakausha
Brother kule kaamka na mixer wameiba stabilizer tuu dundo Sony lipo
Kumbe brother ana mkuu huko police force
Simu moja londo likaja chukua mzoga
Baadae Jiji letu saa 12 afande tibaigana anarindima
Kwa taarifa ya jeshi ra porisi
Majambazi yamevamia nyumba ya brother ..... ila wananchi walifanikiwa kuwadhibit
Aisee umemkill Faki
 
At my early 20's, siku moja nilikuwa na ugwadu sana so nikaenda pale Manzese kwa malaya.

Kwa mbali nikamuona mmoja amenona sanaaa, kutokana na zile taa zao sikuweza muona vizuri.

So nikaingia moja kwa moja ndani, hapo ndipo nilipoduwaa.


Aisee ni mama mtu mzima sana rika hata la mama yangu mzazi. Kwa kweli nilifanya ile sex hata utamu sikuusikia, mawazo yalikuwa mbali sana.


Nikajua njaa mbaya sana. Niliumia mno kwa bibi yule kufanya biashara ya namna ile.

Huwa naumia sana mpaka leo hii nikikumbuka ga hili suala.
 
Kisa cha pili .....

Nikiwa nimemaliza form six , basi ikabidi nitoke dar niende kagera kumsabai bibi yangu , Bibi yangu alikuwa akiishi bukoba mjini mitaa ya town kabisa.

Sasa pale kwake alikuwa na vyumba kama kumi na nne, amevipangisha , hivyo ni kawaida mimi kuonana na wapangaji pindi nitokapo ndani .

Sasa katika wale wapangaji kuna mdada alikuwa amepanga na pia anaishi mwenyew tu , ila story za watu eti ni malaya na pia ameathirika na gonjwa la taifa .

Hata bibi aliniambia hivyo pia , ila siku zilivyozidi pale nyumbani Mazoea na wale wapangaji yalizidi , sasa yakawa yamezidi kwa huyu dada, anayeishi pekee yake , Bibi akaendelea kunikanya kuwa niwe mbali na huyo binti , kwanza kanizidi umri pia ana tabia za umalaya .

Dah shetani , msikie tu , si nikajikuta nishaingia kwenye mazoea na yule dada , mwisho nikawa usiku nafungua geti taratibu naenda nalala kwake, asubuhi na mapema narudi, maisha yakawa safi , ila moyoni nikawa sina amani tena maana nilikuwa napiga kavu , hivyo nikawa najua nishaathirika .

Penzi likanoga kwa siri , Bibi hajui kitu kuwa mjukuu nishaingia kwenye penzi la mpangaji japo baadhi ya wapangaji walijua.

Sasa usiku mmoja kulikuwepo na mechi ya Arsenal na man u , nikamueleza bibi naenda mpirani akasema hapana, si uangalizie hapa , nikagoma akakubali niende atanifungulia mageti.

Sasa kumbe mwenzake sina mpango wa kurudi nyumba kubwa nataka nilale na mchuchu wangu , dah kweli baada ya mechi nilikuwa very frustrated sababu chama langu , man u tulikula nyingi .

Nikasema Ngoja nikamalizie hasira kwa mpangaji wetu bila kuwaza kuwa tayari nina ngoma toka kwake , lahaura , kumbe masikini mbibi wa watu hajalala anawaza mjukuu wake mbona harudi ?

Mida ya saa saba nikasikia mlango wa nyumba kubwa umefunguliwa mda huo nipo juu ya kifua cha dada mpangaji , sasa nikawaza mda huu bibi anatafuta nini ?kumbe mbibi hajalala anamuwaza mjukuu wake , saa ngapi asimgongee mpangaji mmoja hivi amuulize wapi tunaangaliziaga mpira , mda huo nawasikia.

Mara ghafla nikawa siwasikii tena , kumbe yule mpangaji kauza ramani ya vita , kamchana bibi kuwa mpira ulishaisha ila anadhani nitakuwa chumba cha dada mpangaji maana uwa ananiona naingia usiku .

Bibi wa watu , upendo kwa mjukuu ukamzidi uwezo akagonga hodi kwenye chumba chetu, mdada akaanza kutetemeka ni nini afanye, mimi nimeinama nawaza aibu , naiweka wapi?

Mara mdada kafungua mlango , Bibi kaingia anafoka kwanini unataka kumuua mwanangu , mara akague huku mara kule, muda huo nimejificha kwenye vyombo , Bibi aliponiona akaanza kumpiga mdada na ndala kwanini unataka kumuua mwanangu, akitamka hivyo , mdada alivaa kanga tu , mara akakimbia nje

Mda huo nimevaa boksa na shati tu , Bibi alivomfuata nikavaa suruali Chapu, nikavaa sendo nikatoka nakimbia huku aibu , maana watu wameamka ili kuona ni nini kimetokea.

Nikawaza sana njiani sijui wapi naelekea mwisho nikasema siwezi kufa kizembe, nikaenda moja kwa moja mpaka sitende ya mabasi ya mkoani , pale nikakuta kama mchana hivi , fasta nikauliza kama naweza mpata wakala wa mpesa , nikampata.

Nilitoa elfu themanini, maana ilikuwa kwenye simu , nikakata tiketi kwa elfu hamsini na tano , bukoba kwenda dar , baada ya kupewa hela na nikaoneshwa basi, nilienda mle nikakaa nawaza mengi mpaka najionea aibu mwenyewe mda huo , Bibi anapiga simu sipokei mara nikazima.

Nilifika dar baada ya safari , nikakuta bibi alipiga simu anasema hajui alimuudhi nini mjukuu wake maana amekimbia nyumbani hayupo na hajaaga , dah bibi bwana ila hakusema nimefanya nini ?

Dah nilivoambiwa hivyo , nilijikuta nalia tu , nikaishia kusema nilimiss kurudi dar tu , ila moyoni najua bibi aliamua kuvunga ila baada ya siku kadhaa bibi , alinitafuta akanisihi nisirudie hiyo tabia na pia akaomba niende nikapime UKIMWI , alafu nimpe majibu , kweli nilipima nikajikuta negative .

Dah nilipomwambia bibi alifurahi sana , mpaka nikamsikia analia kwenye simu Ila yule Demu sikumtafutaga tena .

Dah bibi yangu mpaka leo ananipenda sana na hajawahi kunitobolea siri hii

Dah wewe mdada kama uko humu nisamehe bure ulikuwa ujana ndiyo maana sijawah kukutafta
[emoji23][emoji23][emoji23]
Mkuu we noma sana

Endelea kushusha kama bado zipo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tulichapwa bakora siku ya kumaliza necta form six

Siku hiyo sitosahau nilikula mijeledi kama yesu msalabani bila kosa ndo nikaamini sio kila anayeenda jela ana makosa

Ilikua hivi Nakumbuka ilikua Alhamisi ile tunamalizia mtihani wa mwisho msimamizi akatuambia mkimaliza mtihani muende uwanjani msiondoke kwanza tukasema poa, tulikua tunahisi sijui walimu wanakuja kutupongeza basi tukapiga pepa pale mpaka muda tunaambiwa pens down watu wakaanza kuvunja ruler wanatupa peni wengine wanachana mashati wanachana suruali kwa furaha ya kumaliza

Mimi sikupanga kuchana ila kuna jamaa tulikua tunamuita Mjita(mtu wa ukerewe)alikua amekaa nyuma yangu akachukua kiwembe akaanza kuchana shati langu mgongoni
Nilimuacha achane tu kwani halina kazi tena (Najuta kumuacha achane lile shati)

Basi msimamizi akakusanya mitihani na kuondoka zake lile darasa nililokuwepo watu hawakuchana sana uniform nilishangaa nilichokiona baada ya kutoka nje kuna darasa lingine hao walichana nguo sio poa unaweza sema ni machizi wameachiliwa kifungoni kila mtu kachana anavyojua basi(kumbuka mjita alichana shati langu mgongoni)

Basi tukakusanyika uwanjani kama tulivyoambiwa tunashangaa tunaambiwa tukae chini na wale mapolisi waliokuwa wanasimamia mitihani tukawa tunajiuliza nini kina endelea

Kumbe Jana yake kuna baadhi yaform six walichana magodoro na mashuka ya form five na hiyo taarifa ikamfikia mkuu wa shule ndo akawaambia wale form five waandike majina ya watu wanaowahisi kufanya hicho kitendo na majina yalipelekwa kwa mwalimu mkuu ndo akawaambia polisi hawa vijana wakimaliza mtihani kuna haya majina shughulika nayo hiyo ndo ilikua sababu ya kuitwa pale uwanjani

Basi Yale majina yakaitwa wakasimamishwa pembeni alafu yule afande akasema mbona naona watu wamechana uniform..dah akasema wote waliochana uniform na nyie simameni jiungeni na hawa waliochana mashuka maskinii mjita aliniponza na Mimi nikajumuishwa Kwenye msala.tulikua kama 25 hivi tukaambiwa pangeni mstari mmoja kuelekea ofisini.wale ambao hawakuchana uniform zao waliruhusiwa waondoke sisi tukabaki
Polisi akaanza kusema nyie ndo wahuni eeh basi tutaonyeshana uhuni niliogopa sana

Tukapelekwa mpaka assembly ground tukaanza kupigishwa kwata na wale mapolisi dah Mara headmaster akaja akasema Leo nawachapa nawaaga kwa kuwachapa dah niliona kama ndoto hivi nachapwa siku ya kumaliza Necta Moyoni mwangu naendelea kumlaumu mjita kwa kuniponza,tulijitetea kwamba sisi hatuhusiki na kuchana mashuka sisi tumechana nguo zetu tu majina yao si yapo hapo sisi hatuhusiki ila wale polisi hawakutaka kuelewa wakaona ni wale wale tu wachanaji magodoro na wachanaji uniform

Basi headmaster akaagiza mzigo wa fimbo ukaletwa akaanza kutupelekea moto afu anachapa fimbo za mgongoni na kiunoni lazima akuachie alama kama sio Kukutoa damu.dah tulipelekewa moto sana kwa bahati nzuri na mjita nae alichana nguo Kwahyo tulikua wote tunasulubiwa (ningeumia sana kama mjita asingekuwepo) basi nikiona mjita anakula mijeledi na Mimi nafarijika

Kumbuka hapo tushamaliza mtihani wa necta wale wasimamizi ndo wa nasubiri lile gari linalozunguka kusambaza na kufuata mitihani mashuleni lije kuwafuata kwahyo hapo pona yetu ni mpaka lile gari lifike dah basi headmaster akaendelea kutupiga mijeledi na walimu wengine wakaunga tela tulichakazwa haswaa alama kibao mgongoni na kiunoni mpaka lile gari linafika tulikua tupo juu ya Mawe(lawama zote ziende kwa mjita)

Tulikubali kusulubiwa japokua tulikua tumemaliza necta tungeweza kugoma kuchwapwa lakini hatukuwa na jeuri hiyo kwa sababu polisi walikuwepo dah Kwahyo ukigoma tu polisi wanakuchezeshea mikwaju na unaenda kulala kituoni dah ikabidi tuache tu headmaster atupelekee moto chini ya uangalizi wa polisi,baada ya kipindi cha muda mrefu hatimae gari la kukusanya mitihani likafika ndo wale polisi wakaondoka na headmaster akatuacha ila hakutucha hivi hivi aliandika majina yetu ili siku ya kuja kuchukua result slip tulipe magodoro dah ilikua siku ya kihistoria Magodoro sikuchana,nguo sikuchana kwa mikono yangu,na mijeledi nimesulubiwa

Mjita popote ulipo mataccor yakooo!
Oya sasa kwanini hukutimua mlivyoitwa na maafande?

Ulihofia nini tena kama mitihani ulishamaliza?

Sisi tulikuwa tunaogopa kufukuzwa shule tu lakini baada ya mitihani walimu ndio walikuwa wanatembea watatu watatu kuepuka kichapo cha revenge katika miaka minne yote waliyotutesa
 
At my early 20's, siku moja nilikuwa na ugwadu sana so nikaenda pale Manzese kwa malaya.

Kwa mbali nikamuona mmoja amenona sanaaa, kutokana na zile taa zao sikuweza muona vizuri.

So nikaingia moja kwa moja ndani, hapo ndipo nilipoduwaa.


Aisee ni mama mtu mzima sana rika hata la mama yangu mzazi. Kwa kweli nilifanya ile sex hata utamu sikuusikia, mawazo yalikuwa mbali sana.


Nikajua njaa mbaya sana. Niliumia mno kwa bibi yule kufanya biashara ya namna ile.

Huwa naumia sana mpaka leo hii nikikumbuka ga hili suala.
Shukuru hukumkuta na upele
 
Kwenye Maisha tunajifunza kutokana na makosa na makosa yanaleta majuto kabla ya funzo.

Aidha ufanye kosa kwa siri au hadharani, ni lazima likugharimu kwa namna moja au nyingine na hivyo kupelekea majuto.

Kuna vitu huwezi kuzungumza na watu wanaokufahamu vizuri, kuna vitu vinabaki mioyoni mwetu kwa muda mrefu sana.

Lakini sehemu kama JamiiForums ambapo kila mtu ni kama mgeni tusiyemfahamu panafaa kabisa kutoa yale ambayo tunayabeba mioyoni mwetu kama majuto labda huenda yakamsaidia mtu mwingine kwa namna yake.

Unajutia vitu gani kwenye maisha yako?

Binafsi nina vitu fulani ambavyo niliwahi kujutia sana. Nitakuwa nashare kimoja kimoja kadiri navyopata muda.

Kipindi fulani miaka kadhaa nyuma, wakati nasoma Chuo niliwahi kuingia katika harakati haramu za kuforge receipt za Malipo ya Ada. Ilinigharimu Sana!

Wakati huo maisha ya Chuo yamekuwa magumu sana, mambo ya ujana ni mengi halafu mpunga naotumiwa nyumbani hautoshi kabisa.

Basi bhana, ilivyotokea hiyo story ya kuwa kuna namna unaweza kutoa pesa kidogo kama robo tu ya Ada unayolipa kisha ukapokea receipt halali ya Bank yenye malipo ya Ada kamili nikajikuta nimeingia mkenge kirahisi.

Tafuta connection mpaka nikakutana na jamaa mmoja ambaye ndio anaratibu huo mchongo. Kazi ikaanza. Wakati huo nipo mwaka wa mwisho ila Sem ya kwanza.

Nikaona maisha si ndio haya. Nakumbuka nilikua nalipa kama Mil 2 kasoro hivi ya Ada ya mwaka mzima. Kwahiyo nikawa nikitumiwa pesa ya Ada natoa kama jiwe 5 tu, receipt ya ada kamili hii hapa. Nikienda kwa mhasibu ni mhuri Twacha! Nishaingia kwenye kundi la walipa Ada naanza kupambana na Modules.

Sem ya kwanza ikaisha, Sem ya II ikaanza kama kawaida nikamcheck mzee wa michongo akanifanyia utaratibu chap maisha yakasonga.

Kipindi hicho mpaka washkaji zangu wakawa kama hawanielewi elewi, si unajua tena zile umetoka na mwana kitaa kimoja anajua uchumi wenu vizuri halafu anashangaa mwana ghafla tu kila kitu huulizi bei na hukaukiwi Mchuzi! Duh, wangejua nilipojiingiza hata wasingekubali kupokea mia yangu.

Muda ukaenda, wiki zikakatika. UEs zikaanza. Kizaazaa kikaja!

Nakumbuka zilikua zimebaki kama paper 2 tu nimalize Chuo, katikati ya mtihani anaingia Dean of Student na maafande.

Heh! Moyo ukafanya Paah, Mkono ukaanza kutetemeka mpaka kalamu ikaanguka chini. Sijamalizia kuokota kalamu nasikia jina langu linaitwa, Mama yangu! Nimekwisha!

Nikasimama nikatoka nje wajomba wakaniambia kijana uko chini ya ulinzi. Kila mtu hapo ndani ya chumba cha mtihani wanashangaa. Laskaboza kafanya nini tena jamani? Mbona hanaga shida na mtu.

Unajua kuna kitu watu huwa hawajui kuhusu kukamatwa na mapolisi. Siku wanakuchukua huwa wanakuchukua kama utani vile, kama vile wanaenda kukuhoji tu kidogo kesho yake unatoka.

Aaah thubutu, nilikaa Central karibu wiki mbili, mpaka nikahamishiwa Magereza Bulalifuu. Naona kama ni Movie ya kihindi inanitokea lakini ni painful reality. Nimeshakuwa Mfungwa!

Wazee wakafunga safari kutoka mkoani wakaja Chuoni kujua kulikoni. Sitasahau aibu niliyoipata wakati namuona mzee wangu. Laskaboza? Imekuaje Mwanangu? Uliomba nini hukupewa? Pesa zote ulikuwa unapeleka wapi? Uchungu niliuokuwa nao jumlisha na uchungu wa mzee, hali ikazidi kuwa Mbaya.

Story zikasambaa Chuo kizima, Laskaboza ni tapeli, ametapeli Chuo. Ubaya wa haya mambo, akikamatwa mwingine anasema wewe ndio ulimwambia kwahiyo mimi ndio nabanwa niseme mashine za kufyatulia Receipt ziko wapi. Niliteseka sana.

Kwa sababu hata yule jamaa aliyeniingiza huko alishamaliza Chuo mwaka mmoja kabla yangu. Kwaiyo alikua mtaani tayari. Alivyosikia nimedakwa, akapotea. Akawa hapatikani tena.

Aisee, hakuna rangi niliacha kuona. Hii story ni ndefu sana, ila ki ufupi nilikuja kuachiwa baada ya miezi 4.. walikuja kugundua hata mimi sijui mahali hizo receipt zinafyatuliwa.

Waliofanya mpango uvuje ni Auditors. Maana Chuo kilikuja kugundua pesa hazionekani Bank lakini zipo kwenye makaratasi.

Kwaiyo wakaguzi wa mahesabu wakishirikiana na Bank ndio wakagundua huo mchongo. Ki ukweli ulinigharimu sana. Nilijuta sana. Watu wa nyumbani kwetu walihisi nimelogwa ili nisimalize Chuo, Duh

Nilikuja kumaliza masomo yangu miaka miwili mbele, maana hapa katikati habari zangu zilikua zimeshasambaa sana.

Kwaiyo hata kurudi ikawa ngumu mnoo. Nilikuja kukubaliwa miaka miwili mbeleni baada ya mabadiliko katika uongozi wa Chuo kufanyika.

Hakika nilijutia sana

Kamwe usije ukaingia kwenye michongo meusi. Maana ina tabia ya kukolea kama sukari halafu ikishakolea unajisahau, na ndio hapo unapoingia mtegoni unadakwa na kila kitu kinakua kichungu.

Kisa kipi kilikufanya na wewe ujute sana?
Pole sana mwamba
 
FUJO ZA WANAFUNZI NA WANAKIJIJI


Dah miaka hiyooo. Nipo sekondari O-level mkoa fulani hiviii waliosoma hapo wataikumbuka hii story maana nilikua aina ya wale wanafunzi ambao anafahamika shule mzima na nilikua nataniwa na kila mtu.

Kulikua na shida kubwa sana ya maji katika mji huo hivyo kulazimika wanafunzi wa shule za boarding za hapo kuwa na kawaida ya kutoka nje ya shule kutafuta maji huko mitaani yaani ilikua ni ubabe na vurugu maana kilichokua kinahitajika ni maji yawe ya kisima salama, kisima cha wazi/shimo ama hata ya mfereji lakini maji yafike shule kwa matumizi binafsi na matumizi ya jikoni endapo darasa lako litakua na zamu na kipindi hiki hata ratiba za darasani hazikua sawa maana wenye zamu ya jikoni wakizingua basi uji mnakunywa saa sita mchana[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] au kula wali saa sita usiku kosa maji yamechelewa ilikua kawaida.

Kipindi hicho ilikua inafika hatua mtu ukimaliza kula inabidi uilambe sahani yako kwani hakukua na maji ya kuoshea, tulikunywa maji machafu yaani machafu unayoyajua wewe yaani ile ndoo mnayoingia nayo bafuni(nadhani mnajua hali ya maliwato za shule za bweni za serikali) ndio hiyo mnaitumbukiza kisimani mnachota maji kwa matumizi yooote kuanzia kunywa, kuoshea, kufulia, kupikia,nk hapo kutumia maji chooni ilikua anasa zaidi ya makaratasi na magodoro[emoji2955][emoji2955][emoji2955].

Basi nilikua na kakundi kangu tunajikuta manundaaa hatuogopi mbuzi yeyote baada ya chakula cha jioni tumeenda kunyanyua vyuma ikabidi tushuke kitaa kusaka maji na kuoga hukohuko ilikua mida ya saa mbili usiku no body caring about the so called night prepo.
Sasa kufika kwenye kisima cha wazi kikubwa zaidi hatukukuta foleni tukajichotea maji na kuoga. Wakati tunaoga kuna majamaa wawili ambao ofcourse tulikua tunafahamiana nao (kutokana na harakati zetu chafu na uhuni za mtaani) walikua wanaishi jirani kabisa na kisima na walikua wamelewa, sasa wakaanza kututolea maneno machafu sana na ninaamini hawakututambua kutokana na kulewa.

Kikatuuma sana wana tulikua 6 tukaamua tukiwashe, ukumbuke ni usiku sasa hiyo inaenda saa nne basi tukawachezeshea kichapo na walipiga kelele kinoma nadhani hadi wanakijiji wengine wakasikia. Ili kuonesha sisi ni wababe zaidi tukaanza kurusha mawe mazito kwenye paa la nyumba ya washkaji ASALALEEEEH kumbe wanakijiji wamejikusanya waje kutoa msaada.

Sasa kutokana na jeuri ya wanafunzi wanapokua wanafuata maji kijijini kulikua na chuki imejengeka kwa wanakijiji juu ya wanafunzi ni vile tu walikua wanakosa namna ya kulipiza sasa na sisi ndio tukawa tumeingia king wenyeweee. Ebwanaee, baada ya kumaliza hilo timbwili letu kuwapiga majamaa na kufanya vurugu tukaamua tusepe sasa njia ilikua ni ile ya imesongwa na nyasi so mnavyopita mnakaa kama msululu kama bata na wanae mimi nikiwa wa mwisho kabisa nikiwa nimebeba maji nusu ndoo na tochi mkononi.

Ghafla tunakutana na nyomi la wananzengo mzee mwenye jiwe, fimbo na silaha nyingine za jadi kumbe wanatulia timing basii nilichosikia ni WEZI WENYEWE HAWA HAPAAA KAMATAAA.

Ilikua ni nyuma geuka, mimi nikawa wa kwanza nilikimbia nikapaa kile kisima ambapo hadi leo sijui niliwezaje mbele kulikua na matuta yale ya majaruba nikajikwa nikaanguka, hapo ujue wanakijiji wametuungia na kelele za weziiii weziiiiii[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91].
Ile nataka kuinuka nikasukumwaa na mwenzangu nikarudi chiniiii wanakijiji hawa hapaaa, usiombe babaangu, ndani ya sekunde kadhaa nilikua nakiona kifo hiki hapa nilipiga kelele ambazo sijawahi kupiga maishani mwangu nikijitetea kuwa mimi sio mwizi bali ni mwanafunzi wa hiyo shule.

Nashkuru kuna mzee mmoja pale wenye hekima akaingilia kati nisiendelee kupigwa japo wanakijiji kila mmoja alikua na hasira na tabia chafu za wanafunzi mfano kuchota maji kibabe wakikuta foleni( yaani unaweza kuwa na kisima kwako ila tukifika tunakusubirisha kuchota hata ya kupikia), kuiba mazao ya bustani kama miwa na matunda, kuiba mademu zao, nk ambazo nyingine hata mimi nilikua nazo basi nikawa nimepelekwa sehemu kuna taa nahojiwa pale ratiba inayofuatia ni kupelekwa polisi kwa uharibifu tulioufanya na wakati huohuo kuna baadhi ya raia wenye hasira wananipa ngumi au makofi ya kuvizia, sisahau mshkaji mmoja yuliwahi kula demu wake namkumbuka vizuri kabisa alinipa kichwa cha pua aisee nikaishia kuona nyotanyota.

Lakini akatokea mwana ambaye alikua tunafanya nae michongo flani haramu akateteaa pale uwongo na ukweli nikaachiwa kwa mkwara mzito, hapo nahisi maumivu kila sehemu.
***********
Sasa wale wenzangu wengine walifanikiwa kufika shule na kugonga kengele ya dharula(ile shule ni moja ya shule inayoheshimu lengele za dharula yaani mtu anaweza asikimbilie kengela ya chakula ila ya dharula usiku ni dk chache tu wapo assembly. Basi jamaa mmoja fala sana akatangaza kuwa nimedakwa na wanakijiji huko wananibaka na tunavyozidi kuchelewa watakuta nimekufa hivyo washuke fasta kuniokoa.

Mwanaaa usiombeeee, ofisi ya vifaa ikavamiwa wa kutoka na fyekeo, jembe, fito za mafagio, mwenye jiwe, na silaha yoyote alibeba shule nzima yenye 800+ students ikashuka village na hasira maana ujue hapo wanafunzi na wanakijiji hawapatani.

Aisee mimi nimeachiwa pale hata wanakijiji hawajatawanyika, nakatisha kona ya kwanza kusepa nachechemea taratibu nipo na mwana aliyenitoa kwenye msala nakutana na wale vimbelembele wa skaut aisee wataka waanze na yule mshkaji nikawapooza nikamwambia mshkaji potea jeshi la kazi limefika hapo ukumbuke wanakijiji bado hawajatawanyika pale walipokua wakinihoji na wanafunzi wanazidi kuja wananiuliza hali yangu palee nikawaambia wabaya wote wapo hapo nyuma kama vipi tuwaibukie.

Kilichotokea huwa sipendi kukumbuka kilitembea kichapo hapo yaani palichafuka, yule mshkaji aliyenipiga kichwa cha pua aisee sikumuacha tulilipana palepaleee nadhani ndie aliyejeruhiwa zaidi maana wana walikua wananiuliza nioneshe aliyenipiga wote wamewekwa mtu kati alitia huruma sana maana alipasuliwa kweli kuna jamaa alimkata na jembe kichwani ameloa damu kichwa choteee. Basi mida ya saa saba operation ya kuniokoa ikaisha tukakusanyana wale wote tuliokua kwenye kisanga tukatunga story moja na kama tulijua, polisi hawa hapa shule tukabebwa hadi kituoni tukahujiwa kila mmoja peke yake na tukatoa story inayofanana.

Pamoja hayo yote ila ni shule ninayojivunia kwa shule zote na levels zote za kielimu nilizopitia ma huwa naimiss sana.

Hahahahaha nmecheka eti ana bakwa huko
 
Back
Top Bottom