Usiku mmoja nikiwa katika harakati za kutafuta elimu nipo mikoa ya watu shuleni kwetu dinning Hall ilikua pia inakodishwa kwa ajili ya shughuli nyingine za kijamii kama harusi na send off.
Hio siku prepo haikuepo kwa kua kulkua na shereh dinning mimi na wanangu wachache wahuni tukapanga tuvamie sherehe Ile ilosifika kua ya watoto wa matajiri wa mji ule.
Nikatoka general wa vita kwenda kutazama ulinzi na usalama na kuandaa plan ya kuzamia..kufika eneo la tukio nkascan haraka nkaona dress code suti nyeus na tai kwa wanaume uzur na shuleni ni maeneo ya baridi tulkua tunavaa suti pia.
Wanaume tukabadilika tukafika eneo la tukio mimi nkatokea kwenye parking kulkua na discovery imepaki nafika getini mlinzi wa getini ni jamaa wa mtaani ambae ananijuaga mm ni dent miyeyusho spend shule (huyu jamaa alkua anauza viatu raba nlkua naenda kuchukua za kwendea club usiku) wenzngu walifanikiwa kupenya mm ikashindikana
Kufika mishale ya saa 4 kwendea 5 akatoka dada mmoja mrembo tu akawa anaongea na simu (nafikiri alipigiwa na mmewe akitakiwa nyumban) nkamfata akanpa kadi akawasha gari yake akaondoka
Nkarudi getini tena yule jamaa anataka kunsukumizia mabaunsa nkatoa kadi akawa ananiangalia kwa kuntaman. Mwanaume nikazama ndani na kukuta wenzngu washapata na wachumba nkachagua angle moja nzuri ya nkatulia muda ukakatika mziki tukacheza na misosi tukala sana
Sasa kuna ule utaratb wa watu kukusanya vinywaji na makulaji na kufunga ili kwenda navyo majumban basi mwshon kabisa mwa shughul nikaona package kubwa ipo inazagaa zagaaa (sjui roho gan ikaniingia inanambia unaacha vinono ivo kesho utakinga ugal maharage nikajikuta nasogelea ule mzgo) katika malez yangu mm kitu sijawezaga ni kuchukua cha mtu basi nikachukua kile kifurushi aisee Ile nageuka nilipigwa mibanzi (yule mzee hatar anapiga mibanz kama sokwe) nkabak nimekua mdgo kusema nmuanzshie vagi yule mzee ningeweza ila ningezua soo kubwa ukizingatia nlizamia so yule mzee alinzaba mikofi kama 6 ivi na wala hakuongea na mm wala sikusema nikageuka kutazama wenzngu naona wanaparty na kina mama nkatoka nje nkaenda kulala uku nikiomba Ile mibanzi kusiwe na mtu ameiona na ndo ikawa ivo
Sent from my SM-G960U1 using
JamiiForums mobile app