Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi

Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
Watoto kutoka Mtwara, Singida, Nairobi n.k wakutwa katika mazingira yasiyo rafiki ya malazi huku wakikosa elimu dunia msikitini Kiluvya wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani nchini Tanzania wakipatiwa mafunzo ya kidini.

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Petro Magoti akiwa na Kamati ya Ulinzi wamefanya ziara kwenye Msikiti huo ili kujionea mazingira ambayo watoto hao wanaishi. DC Magoti amesikitishwa na mazingira aliyoyakuta na kusema siyo salama kwa watoto hao ambao wengine walipaswa kuwa shule.

DC amemtaka Sheikh wa Msikiti huo kusitisha huduma hiyo mara moja na kuamuru watoto hao kurudishwa kwa wazazi wao mara moja kufikia Jumamosi.

Sheikh wa Msikiti huo akijitetea amesema kuwa wanawalea watoto hao kwakuwa Msikiti huo pia unafundisha Kuhifadhi Quran hivyo wamekuwa wakiendesha programu hiyo. Akijibu kuhusu wanakopata watoto hao amesema kuwa wanatoka mikoa mbalimbali nchini na wamekuwa wakiletwa na wazazi kwa mapenzi yao.

Kuhusu huduma ya chakula, sheikh huyo amesema kuwa wamekuwa wakipata ufadhili wa wazazi wa watoto hao ambao huchanga kwa ajili ya chakula.

Watoto wakihojiwa na DC Magoti wameonesha kuwa na baraka za wazazi wao, wengine wamedai wanasoma huko lakini wengi wao wakionesha kuishia darasa la saba na kujiunga na mafunzo hayo

DC Magoti amemtaka Sheikh huyo kufika kituo cha Polisi Kisarawe ili kuandikisha maelezo ya kina kuhusu kilichotokea na kujifunga kuwa anaondoa huduma hiyo.

Pia soma;

DC wa Kisarawe, Petro Magoti achangia Mifuko 300 ya Saruji Ujenzi wa bweli la Msikiti, ahimiza na wengine wachangie ili Watoto Warudi mapema kusoma

 
Kiongozi jenga utamaduni wa kushughulikia chanzo cha tatizo au chanzo cha uvunjifu wa sheria/utaratibu nk nani aliwaleta hapo hao watoto, kwa vibali gani..lengo ni nini? nk ili isije rudiwa tena na wale walioanzisha hili jambo wachukuliwe hatua wao binafsi. Sasa fungeni kituo, halafu baada ya muda wanakwenda kuanzisha jambo hilo hilo sehemu nyingine!
 
NI KAWAIDA KABISA HIZO NI BOARDING ZA ELIMU YA DINI YA KIISILAMU.

tatizo ni kwamba ikionekana watu wanalala katika misikiti watu hudhani wanafundishana ugaidi.

lakini kimsingi boarding kama hizo za masomo ya kiisilamu zipo nyingi sana Nchi hii katika mikoa mingi.

na boarding hizo hufundisha masmo ya kawaida kabisa katika uisilamu.

Kama vile kuhifadhi Qurani,kusoma hadithi,fiqhi,lugha ya kiarabu n.k

Japokuwa wstu wabaya hupitisha ajenda yao popote pale na hivyo hatà huko wapo wachache wanaweza kutumia huo upenyo.

Ila kimsingi Hapo hakuna viashiria vyovyote vya ugaidi.
 
10 July 2024

DC MAGOTI ASHTUKIZA MSIKITI UNAOLAZA WATOTO 90+ “NAWAPA SAA 24 FUNGENI KITUO, WATOTO WARUDI KWAO”



View: https://m.youtube.com/watch?v=eYUPhm8guek

Watoto kutoka Mtwara, Singida, Nairobi n.k wakutwa katika mazingira yasiyo rafiki ya malazi huku wakikosa elimu duniya msikitini Kiluvya wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani nchini Tanzania ... wakipatiwa mafunzo ya kidini ...

Inasikitisha sana kwa uongozi wa Msikiti na Bakwata kiujumla.
 
10 July 2024

DC MAGOTI ASHTUKIZA MSIKITI UNAOLAZA WATOTO 90+ “NAWAPA SAA 24 FUNGENI KITUO, WATOTO WARUDI KWAO”



View: https://m.youtube.com/watch?v=eYUPhm8guek

Watoto kutoka Mtwara, Singida, Nairobi n.k wakutwa katika mazingira yasiyo rafiki ya malazi huku wakikosa elimu duniya msikitini Kiluvya wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani nchini Tanzania ... wakipatiwa mafunzo ya kidini ...

Mohamed Said & Faiza Foxy njooni mlisemee hili.

Toeni matusi yote, lakn kuna agenda ya siri ndani ya hii miskitini kwa kivuli cha imani ya dini.

Muda utaongea. Pwani, Tanga, DSm ipo siku itafahamika.
 
10 July 2024

DC MAGOTI ASHTUKIZA MSIKITI UNAOLAZA WATOTO 90+ “NAWAPA SAA 24 FUNGENI KITUO, WATOTO WARUDI KWAO”



View: https://m.youtube.com/watch?v=eYUPhm8guek

Watoto kutoka Mtwara, Singida, Nairobi n.k wakutwa katika mazingira yasiyo rafiki ya malazi huku wakikosa elimu duniya msikitini Kiluvya wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani nchini Tanzania ... wakipatiwa mafunzo ya kidini ...

Bagamoyo,
Rejea kwenye hiyo video uitazame na usikilize ukiwa makini.
Hakuna mwanafunzi yeyote kutoka nje ya Tanzania.

Rejea usikilize tena hao wanafunzi wengi wameishia darasa la saba na wameletwa hapo na wazee wao waje wasome dini.

Tatizo labda liko hapa.
Nimetumia neno ''labda'' kwa makusudi ili ikiwa lipo tatizo lingine lisemwe.

Ikiwa wewe ni Muislam hutopata tabu unapambiwa watoto wengi wa Kiislam huishia darasa la saba.

Kitwana Kondo alipata kulizungumza hili Bungeni.
Nakuwekea hotuba yake uisome.

(Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma, 1999)

Waislam waliofanyiwa mtihani wa kuingia kidato cha kwanza majority yaani wengi walikuwa Waislam na Wengine walikuwa ndiyo wachache.

Waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza wengi walitoka katika wale Wengine na Waislam wakawa wachache.

Waislam kwa kuthamini elimu ndiyo wanawapeleka watoto wao katika shule hizi za ''kimasikini,'' kusoma.

Hatuna ubavu wa kushindana na shule za Wengine ambazo zinapewa ruzuku mabilioni ya kutoka serikalini kupitia Memorandum of Understanding (MUM) katika ya Serikali na Makanisa.

Yapo mengi katika matatizo yanayowakabili Waislam moja wapo ilikuwa NECTA kuhujumu shule za Waislam.

Naamini unayajua maandamano ya Waislam mwaka wa 2012.
Tutoke hapo.

Kama tatizo la kuvamia msikiti usiku wa manane DC na Kamati ya Amani mbona kuna shule za mbovu kupita kiasi hazijavamiwa na wanafunzi kurudishwa makwao?

Angalia ushahidi huo hapo chini:

1720694270799.png


Upo ushahidi mwingi lakini tuanze na huu.

Nipe jibu kwa nini shule hii haijavamiwa usiku wa manane na DC na Kamati ya Usalama?
 
Back
Top Bottom