Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi

Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi

Bantu...
Kwa nini watotowatoroshwe?

Wangekuwa wametoroshwa kungekuwa na ulinzi hapo msikitini kuwalinda wasikimbie.

Volo...
Tujadiliane kwa heshima.
Hapana haja ya kutukana.

Kwani hauruhusiwi kulala msikitini?

Waislam kulala msikitini ni jambo la kawaida sana na limekuwa likifanyika karne kwa karne.
Kupumzika baada ya swala sawa, ila si kufanya Msikiti kuwa bweni la kulala wanafunzi.
 
Sitafuti kuaminiwa nimechangia mada kuwa hizo madrasa zinazolea watoto zipo sio hiyo ya kisarawe tu huenda hiyo ikawa na idadi kubwa ya watoto tu, lakini hizo madrasa zipo sehemu nyingi tu tatizo ni usiri unaoendelea ndani ya hizo madrasa!

Habari za ugaidi umezileta wewe kumbe ndo kinachofundishwa?Ka
Kapeace,
Mahakama zipo endapo kuna kosa wapelekwe mahakamani.
 
Joseph,
Ikiwa kuna ushahidi kuwa watoto hawa wanafunzwa ugaidi hili ni kosa la jinai.
Walimu wakamatwe wafikishwe mahakamani.

Haipendezi kuwa unatoa shutuma zisizo na ushahidi.

Hawa watoto wangekuwa hawali waingekuwa kama wanavyoonekana kwenye video.

Una la kusema kuhusu shule hii hapo chini?:
View attachment 3039358
Si mshutumu mtu ina naongea kwa kutumia experience ya Boko Haram,ukitizama Documentary walianza hivi hivi, leo Nigeria kuna maeneo haya tawaliki.

Halafu hilo darasa ni la serikali, hata content ya kinacho fundishwa serikali ndio wanakiandaa na kukimonitor,wana mifumo inayo tambulika ya kuandaa walimu.Halafu hapo wakimaliza kila mtoto anarudi kwa wazazi wake,still bado wazazi wanammonitor na kumlisha vizuri na hata akiumwa wanajua wamtibie vipi. Hivi kwa kuwaona tu inamaana ndio wanakula vizuri au wanatibiwa vizuri? Huwezi fananisha treatment ya mtu baki na ya mzazi kwa mtoto.

Leo nikikuambia silabasi wanayo tumia kufundisha watoto unayo/unaijua. Haya kama yasipo angaliwa yakitokea hayajali,ww ni dini gani,Boko Haram wanateka na kuwaangamiza mpaka wale wenye imani sawa na wao.
 
Kupumzika baada ya swala sawa, ila si kufanya Msikiti kuwa bweni la kulala wanafunzi.
Babuu.

Waislam hawana mabilioni wanayopokea Makanisa kutoka serikalini kupitia Memorandum of Understanding (MUM).

Waislam tunatumia kile kilicho chetu kujisaidia wenyewe na ndiyo hii misikiti ambayo tunayo mingi.

Tungekuwa na fedha kama hizo wanazopewa Wengine tungejenga mabweni mazuri kama wenzetu.
 
Si mshutumu mtu ina naongea kwa kutumia experience ya Boko Haram,ukitizama Documentary walianza hivi hivi, leo Nigeria kuna maeneo haya tawaliki.

Halafu hilo darasa ni la serikali, hata content ya kinacho fundishwa serikali ndio wanakiandaa na kukimonitor,wana mifumo inayo tambulika ya kuandaa walimu.Halafu hapo wakimaliza kila mtoto anarudi kwa wazazi wake,still bado wazazi wanammonitor na kumlisha vizuri na hata akiumwa wanajua wamtibie vipi. Hivi kwa kuwaona tu inamaana ndio wanakula vizuri au wanatibiwa vizuri? Huwezi fananish treatment ya mtu baki na ya mzazi kwa mtoto.

Leo nikikuambia silabasi wanayo tumia kufundisha watoto unayo/unaijua. Haya kama yasipo angaliwa yakitokea hayajali,ww ni dini gani,Boko Haram wanateka na kuwaangamiza mpaka wale wenye imani sawa na wao.
Joseph,
Soma historia ya Waislam wa Tanganyika achana na historia ya Nigeria.
Historia ya Nigeria ni tofauti sana na historia ya Tanzania.

Unaujua mchango wa Waislam wa Tanganyika katika kupigania uhuru wa Tanganyika?

Soma historia hii utaongeza maarifa yako.
 
Bagamoyo,
Rejea kwenye hiyo video uitazame na usikilize ukiwa makini.
Hakuna mwanafunzi yeyote kutoka nje ya Tanzania.

Rejea usikilize tena hao wanafunzi wengi wameishia darasa la saba na wameletwa hapo na wazee wao waje wasome dini.

Tatizo labda liko hapa.
Nimetumia neno ''labda'' kwa makusudi ili ikiwa lipo tatizo lingine lisemwe.

Ikiwa wewe ni Muislam hutopata tabu unapambiwa watoto wengi wa Kiislam huishia darasa la saba.

Kitwana Kondo alipata kulizungumza hili Bungeni.
Nakuwekea hotuba yake uisome.

(Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma, 1999)

Waislam waliofanyiwa mtihani wa kuingia kidato cha kwanza majority yaani wengi walikuwa Waislam na Wengine walikuwa ndiyo wachache.

Waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza wengi walitoka katika wale Wengine na Waislam wakawa wachache.

Waislam kwa kuthamini elimu ndiyo wanawapeleka watoto wao katika shule hizi za ''kimasikini,'' kusoma.

Hatuna ubavu wa kushindana na shule za Wengine ambazo zinapewa ruzuku mabilioni ya kutoka serikalini kupitia Memorandum of Understanding (MUM) katika ya Serikali na Makanisa.

Yapo mengi katika matatizo yanayowakabili Waislam moja wapo ilikuwa NECTA kuhujumu shule za Waislam.

Naamini unayajua maandamano ya Waislam mwaka wa 2012.
Tutoke hapo.

Kama tatizo la kuvamia msikiti usiku wa manane DC na Kamati ya Amani mbona kuna shule za mbovu kupita kiasi hazijavamiwa na wanafunzi kurudishwa makwao?

Angalia ushahidi huo hapo chini:

View attachment 3039350

Upo ushahidi mwingi lakini tuanze na huu.

Nipe jibu kwa nini shule hii haijavamiwa usiku wa manane na DC na Kamati ya Usalama?
Mkuu MS
Hehima yako mkuu

Hoja na picha uliyo ambatanisha kwangu mimi naona Haina mashiko Kwa sababu

1. Hii shule( s/m mlevo) sio ya bweni kwahiyo hata ikivamiwa usiku wa manane na kamati ya ulinzi na usalama hakuna kitu/watu watakuta hapo shule ni uchakavu tu wa jengo Lakini shughuli za ufundishaji na utekelezaji wa mtaala zinafuatwa

2. Hoja ni kitu gani kinafundishwa hapo ambacho kimewafanya wachukue watoto 90+kutoka kwa familia zao?je ni elimu ya Dini au kuna ajenda za Siri (chuki) zinapenyezwa apo?

3. Je mazingira yanaruhusu kuwaudumia hao watoto 90+ malazi mavazi na chakula ukizingatia hapo sio shule na Wala hakuna mabweni ya kuwalaza hao watoto?
 
Mohamed Said unajitahidi sana kuutetea Uislamu lakini ni dhahiri shahiri hoja nyingine hazina utetezi.
Babuu,
Unajitia hofu isiyokuwa na sababu.
Waislam wamefanya makubwa katika nchi hii.

Soma historia yao.

Soma historia ya Mtwa Abdallah Mkwawa, Abushiri bin Salim, Hassan Omari Makunganya, Khadija Mkomanile, Abdulrauf Songea Mbano, Kleist Abdallah Sykes na mwanae Abdulwahid Abdallah Kleist, Hamza Mwapachu, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Sheikh Haidar Mwinyimvua kwa kuwataja wachache.

Soma historia za watu hawa utawajua Waislam na mafunzo yao na alama walizoacha.

1720698465762.jpeg

 
Joseph,
Soma historia ya Waislam wa Tanganyika achana na historia ya Nigeria.
Historia ya Nigeria ni tofauti sana na historia ya Tanzania.

Unaujua mchango wa Waislam wa Tanganyika katika kupigania uhuru wa Tanganyika?

Soma historia hii utaongeza maarifa yako.
Ya Nigeria ni real example ya Boko Haram ilivyo anza ilianza hivi hivi,tatizo wao hawa kuyakemea na gundua mapema.

Kweli kiimani ni mkrisho,ila ukiniambia nichague amani ya nchi yangu na dini yangu,nitachagua amani ya nchi yangu,sababu kwenye amani hata ule utulivu wa kusali unaupata.

Sasa nikishaujua huo mchango wa dini yako,then .......... inahusiana nini na hiki kikicho tokea Kisarawe.
 
Mkuu MS
Hehima yako mkuu

Hoja na picha uliyo ambatanisha kwangu mimi naona Haina mashiko Kwa sababu

1. Hii shule( s/m mlevo) sio ya bweni kwahiyo hata ikivamiwa usiku wa manane na kamati ya ulinzi na usalama hakuna kitu/watu watakuta hapo shule ni uchakavu tu wa jengo Lakini shughuli za ufundishaji na utekelezaji wa mtaala zinafuatwa

2. Hoja ni kitu gani kinafundishwa hapo ambacho kimewafanya wachukue watoto 90+kutoka kwa familia zao?je ni elimu ya Dini au kuna ajenda za Siri (chuki) zinapenyezwa apo?

3. Je mazingira yanaruhusu kuwaudumia hao watoto 90+ malazi mavazi na chakula ukizingatia hapo sio shule na Wala hakuna mabweni ya kuwalaza hao watoto?
Hatari sana hii...
 
DC alifanya uchunguzi kutafuta content ya mafundisho yanayotolewa hapo?
DC alifanya uchunguzi kujua kwanini hao vijana wapo hapo?

Maeneo mengi ya Pwani huu ni utaratibu wa kawaida Kwa baadhi ya misikiti kuwa inatoa elimu ya kidini na uwepo wa wanafunzi kwenye shule hizo muda wote mpaka watakapohitimu.
 
Mkuu MS
Hehima yako mkuu

Hoja na picha uliyo ambatanisha kwangu mimi naona Haina mashiko Kwa sababu

1. Hii shule( s/m mlevo) sio ya bweni kwahiyo hata ikivamiwa usiku wa manane na kamati ya ulinzi na usalama hakuna kitu/watu watakuta hapo shule ni uchakavu tu wa jengo Lakini shughuli za ufundishaji na utekelezaji wa mtaala zinafuatwa

2. Hoja ni kitu gani kinafundishwa hapo ambacho kimewafanya wachukue watoto 90+kutoka kwa familia zao?je ni elimu ya Dini au kuna ajenda za Siri (chuki) zinapenyezwa apo?

3. Je mazingira yanaruhusu kuwaudumia hao watoto 90+ malazi mavazi na chakula ukizingatia hapo sio shule na Wala hakuna mabweni ya kuwalaza hao watoto?

Ya Nigeria ni real example ya Boko Haram ilivyo anza ilianza hivi hivi,tatizo wao hawa kuyakemea na gundua mapema.

Kweli kiimani ni mkrisho,ila ukiniambia nichague amani ya nchi yangu na dini yangu,nitachagua amani ya nchi yangu,sababu kwenye amani hata ule utulivu wa kusali unaupata.

Sasa nikishaujua huo mchango wa dini yako,then .......... then inahusiana nini na hiki nilicho kiona.
Joseph,
Katika uandishi unaweka dot 3 ... zinatosha.
 
Niliwahi kuandika kuwa hii ni mbinu ya awamu ya sita kuwapa ufadhili watoto wa deen ya haki. Itafanyika kama ilivyofanyika kwa wale waliokutwa wamerundikwa katika kituo kimoja kule Dodoma. DC alinyamazishwa, serikali ikawapeleka kwenye kituo cha malezi cha serikali pale Dodoma. Ni ufadhili wa bure kwa kodi za watu wa dini mbalimbali nchini. Hata hii utasikia wamelelekwa kwenye kituo cha serikali Dodoma
Lup...
Unajua kuwa Makanisa yanapokea ruzuku ya mabilioni kutoka serikalini na Waislam hawana firsa kama hiyo?
 
Bagamoyo,
Rejea kwenye hiyo video uitazame na usikilize ukiwa makini.
Hakuna mwanafunzi yeyote kutoka nje ya Tanzania.

Rejea usikilize tena hao wanafunzi wengi wameishia darasa la saba na wameletwa hapo na wazee wao waje wasome dini.

Tatizo labda liko hapa.
Nimetumia neno ''labda'' kwa makusudi ili ikiwa lipo tatizo lingine lisemwe.

Ikiwa wewe ni Muislam hutopata tabu unapambiwa watoto wengi wa Kiislam huishia darasa la saba.

Kitwana Kondo alipata kulizungumza hili Bungeni.
Nakuwekea hotuba yake uisome.

(Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma, 1999)

Waislam waliofanyiwa mtihani wa kuingia kidato cha kwanza majority yaani wengi walikuwa Waislam na Wengine walikuwa ndiyo wachache.

Waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza wengi walitoka katika wale Wengine na Waislam wakawa wachache.

Waislam kwa kuthamini elimu ndiyo wanawapeleka watoto wao katika shule hizi za ''kimasikini,'' kusoma.

Hatuna ubavu wa kushindana na shule za Wengine ambazo zinapewa ruzuku mabilioni ya kutoka serikalini kupitia Memorandum of Understanding (MUM) katika ya Serikali na Makanisa.

Yapo mengi katika matatizo yanayowakabili Waislam moja wapo ilikuwa NECTA kuhujumu shule za Waislam.

Naamini unayajua maandamano ya Waislam mwaka wa 2012.
Tutoke hapo.

Kama tatizo la kuvamia msikiti usiku wa manane DC na Kamati ya Amani mbona kuna shule za mbovu kupita kiasi hazijavamiwa na wanafunzi kurudishwa makwao?

Angalia ushahidi huo hapo chini:

View attachment 3039350

Upo ushahidi mwingi lakini tuanze na huu.

Nipe jibu kwa nini shule hii haijavamiwa usiku wa manane na DC na Kamati ya Usalama?
Hivi Mzee wangu unajua baadhi ya rejea hupoteza uhalisia wake baada ya muda mrefu kupita kutokana na mabadiliko kadhaa ambayo huwa yanatokea?
Kitendo cha kutumia rejea ya 1999 ambayo kiuhalisia kwasasa kuna mabadiliko makubwa kwenye baraza la Taifa la Mitihani na kuongezeka kwa ufaulu kutokana na ongezeko la shule nyingi za Sekondari kunapoteza credibility ya andiko lako.
Kinacholalamikiwa si uchakavu wa majengo wala vijana kukosa fursa ya kwenda Sekondari, bali Mkuu wa Wilaya ana detailed information kuwa kuna vijana wamefaulu na hawajaenda sekondari ila wamesafirishwa na wazazi wao kupelekwa hapo kupata hiyo elimu ya dini.
Huoni kuna kitu cha kufikirisha hapo juu ya kinachoendelea maana ukiachilia mbali shuleni kuwa na somo la dini na huko walipotoka kuna misikiti na madrasa, kwanini wakatishwe masomo walipotoka na kuletwa hapo ilihali hiyo elimu ya dini walikuwa wana uwezo wa kuipata hata huko walipotoka?
 
Back
Top Bottom