Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi

Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi

Aliyekwambia kuna usiri ni nani? Nani alienda kuuliza kinachoendelea hakujibiwa? Wazazi hawana uwezo wa kupeleka watoto shule binafsi za sekondari mlitaka wafanye nini? Mtoto asijue dini yake kisa mzazi hana uwezo? Acheni chuki za kipumbavu nyie
Mnavyojishtukia sasa itakuwa kuna jambo lisilo la kawaida mnafundishana huko
 
Mheshimiwa DC yupo sahihi wenye kituo wafuate taratibu Ili kutoa elimu hiyo bila changamoto zilizoainishwa. Watanzania wenye agenda zao za uchonganishi wanashadadia mambo ambayo hayajasemwa hasa kuhusu elimu itolewayo.Vyuo vya dini vipo vingi sana nchini vingine vikongwe hata kabla ya uhuru.Wapo wanafunzi Wa kutwa na wabweni kwa wanaotoka mbali.Hoja hapa ni mazingira ya bweni siyo elimu inayotolewa maana siyo Siri.
 
Wanafundisha kuvaa Suruwali fupi na kufuga Mzuzu na kuchukia Makafiri yaani Unbelievers.
Soma kwanza makubaliano ya sheikh wahab na ufalme wa saudia yalikuaje,Nina Imani itajifunza bwana wahab ni nani na alikuwepo lini,maana wafuga ndevu na suruali fupi jina jingine ni wahab,maarufu kwa tz answar Sunnah,yaani wanaonusuru Sunna za mtume
 
M
Kuanzia 2021-2024 nimebahatika kuishi mikoa 3-4 tofauti, 1 ukanda wa pwani ambapo nipo kwa sasa na hapo mtaani ipo na kote zilikuwepo madrasa zenye hao watoto wanaishi na kutunzwa humo kutoka ni kwa nadra sana, ni km wanajificha hivi, kinachofanyika humo hakijulikani hata kwa majirani kati ya hizo sehemu ni madrasa 2 nilikuwa jirani wa karibu,

ukichimba sana hizi ishu huwa zinaibuka pindi tu rais akiwa muislam,, kuna nini?
Maeneo gani mkuu?
 
kila nikiangalia hali za ndugu zetu katika imani napata maswali mengi ila unaweza uliza moja wakakutishia kukusomea alibadiru hapo ndio nachoka kabisaaaa
 
walio waletea dini wanakaa sehemu nzuri ni nchi baadhi tu zenye vita ndio wanapata taabu ila huku taabu inaanzia kwenye elimu na uelewa wa hao mashehe na maustazi na ukiona hali ni mbaya hivyo hata majumbani mwao malazi ni duni.... wanasitiriwa sana na marashi ya buku na kanzu nyeupe ukimuona unasema huyu mtu kumbe anaishi kama mnyama tu
 
DC yupo sahihi kabisa. Hakuna mahala DC ameponda dini Bali amezungumzia miundombinu mibovu na lishe duni ya watoto..pia ni kweli tangu kabla ya uhuru kulikuwapo madrasa kwa waislam na Sunday school kwa wakristu lakini hapakuwa na boarding (yani watoto walale huko huko) .Sasa kukusanya watoto mahali wanalala humohumo bila kibali sio sawa na ni kinyume na SHERIA za nchi hii. Mlitaka DC anyamazie mambo magumu hivyo. Acheni uchonganishi
 
Bagamoyo,
Rejea kwenye hiyo video uitazame na usikilize ukiwa makini.
Hakuna mwanafunzi yeyote kutoka nje ya Tanzania.

Rejea usikilize tena hao wanafunzi wengi wameishia darasa la saba na wameletwa hapo na wazee wao waje wasome dini.

Tatizo labda liko hapa.
Nimetumia neno ''labda'' kwa makusudi ili ikiwa lipo tatizo lingine lisemwe.

Ikiwa wewe ni Muislam hutopata tabu unapambiwa watoto wengi wa Kiislam huishia darasa la saba.

Kitwana Kondo alipata kulizungumza hili Bungeni.
Nakuwekea hotuba yake uisome.

(Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma, 1999)

Waislam waliofanyiwa mtihani wa kuingia kidato cha kwanza majority yaani wengi walikuwa Waislam na Wengine walikuwa ndiyo wachache.

Waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza wengi walitoka katika wale Wengine na Waislam wakawa wachache.

Waislam kwa kuthamini elimu ndiyo wanawapeleka watoto wao katika shule hizi za ''kimasikini,'' kusoma.

Hatuna ubavu wa kushindana na shule za Wengine ambazo zinapewa ruzuku mabilioni ya kutoka serikalini kupitia Memorandum of Understanding (MUM) katika ya Serikali na Makanisa.

Yapo mengi katika matatizo yanayowakabili Waislam moja wapo ilikuwa NECTA kuhujumu shule za Waislam.

Naamini unayajua maandamano ya Waislam mwaka wa 2012.
Tutoke hapo.

Kama tatizo la kuvamia msikiti usiku wa manane DC na Kamati ya Amani mbona kuna shule za mbovu kupita kiasi hazijavamiwa na wanafunzi kurudishwa makwao?

Angalia ushahidi huo hapo chini:

View attachment 3039350

Upo ushahidi mwingi lakini tuanze na huu.

Nipe jibu kwa nini shule hii haijavamiwa usiku wa manane na DC na Kamati ya Usalama?
Sheikh wangu katika paragraph ya pili wasema watoto walipelekwa na wazee wao wakasome dini..jua tu watoto ni Mali ya serikali.

Nimeusoma waraka wako mrefu, kwa kiasi kikubwa unalalamika kwamba wanafunzi waislam WANAONEWA na hawapati nafasi ya kupata elimu (hawachaguliwi kuendelea na masomo).. Jua nyakati hizi zimebadilika tunae Rais mwislamu na sio mara moja tumepata Rais mwislamu, tuna mawaziri waislam, wakuu wa mikoa, wakurugenzi, DC, na wengineo, hii inadhihirisha waislam wanasoma na wanafaulu na ndo mana tunawachagua wanakuwa viongozi wetu.

Kuna matajiri wakubwa sana waislam washaurini wafanye harambee wajenge maskuli na vyuo vingi na vituo vya afya . Kuna wafadhili wenye fedha nyingi huko arabuni pia ambao nanyi mnaweza kuingia nao hizo MOU.
 
Vyuo vya dini vipo muda mrefu tu .Mfano Chuo Cha TAMTA,Zaharau na Maawal vya Tanga vimefundisha masheikh wengi wakubwa kutoka pande mbalimbali za nchi na hata nje ya nchi.Hapajakuwepo shida yoyote katika vyuo hivyo pamoja na wanafunzi wengine kukaa bweni.Kulaza wanafunzi kwa kufuata Sheria hakuna shida.Waacheni watu wasome dini zao mradi wafuate Sheria.Wanaopinga watu kusoma dini ndiyo siwaelewi.
 
Vyuo vya dini vipo muda mrefu tu .Mfano Chuo Cha TAMTA,Zaharau na Maawal vya Tanga vimefundisha masheikh wengi wakubwa kutoka pande mbalimbali za nchi na hata nje ya nchi.Hapajakuwepo shida yoyote katika vyuo hivyo pamoja na wanafunzi wengine kukaa bweni.Kulaza wanafunzi kwa kufuata Sheria hakuna shida.Waacheni watu wasome dini zao mradi wafuate Sheria.Wanaopinga watu kusoma dini ndiyo siwaelewi.
HIzi ni madrasa za boarding ni za kawaida sana.

Ila kwa kuwa uisilamu unaangaliwa kwa jicho la tofauti inakuwa ni tabu watu kuelewa.
 
Vyuo vya dini vipo muda mrefu tu .Mfano Chuo Cha TAMTA,Zaharau na Maawal vya Tanga vimefundisha masheikh wengi wakubwa kutoka pande mbalimbali za nchi na hata nje ya nchi.Hapajakuwepo shida yoyote katika vyuo hivyo pamoja na wanafunzi wengine kukaa bweni.Kulaza wanafunzi kwa kufuata Sheria hakuna shida.Waacheni watu wasome dini zao mradi wafuate Sheria.Wanaopinga watu kusoma dini ndiyo siwaelewi.
Haki za mtoto ziheshimiwe
 
Shule nyingi nchi hii zinachangamoto za miundombinu kwenye utoaji wa elimu sio za serikali ama binafsi , Magoti aseme anataarifa gani ambazo hajazisema wazi, mana hakuna UKAGUZI wa miundombinu unaofanywa USIKU.
 
vishawishi vya kuwaingiza njia mbaya ni vingi
Hapo walipo hawawezi kupata vishawishi?
Tunaongelea watoto wale wanafugwa km mifugo pale kwa nia gani bila taarifa.
Hata sheikh wenu mkuu hajui,ustaadh anaulizwa anajichanganya tu.
Kakiri kosa,kaachiwa na DC ila sidhani km limeisha hilo.
Kwa hali hiyo huyo ustaadh anaweza kuwa anabeba na kuwaingilia vilevile usiku maana ni kawaida kusikia hilo.
 
Hapo walipo hawawezi kupata vishawishi?
Tunaongelea watoto wale wanafugwa km mifugo pale kwa nia gani bila taarifa.
Hata sheikh wenu mkuu hajui,ustaadh anaulizwa anajichanganya tu.
Kakiri kosa,kaachiwa na DC ila sidhani km limeisha hilo.
Kwa hali hiyo huyo ustaadh anaweza kuwa anabeba na kuwaingilia vilevile usiku maana ni kawaida kusikia hilo.
Hapo walipo kinachotakiwa hao wasimamizi wafate sheria za nchi.

Vishawishi havikosi popote lakini mafunzo ya Qur'an na Salat tano kwa wakati ni kinga kubwa sana.
 
Back
Top Bottom