Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi

Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi

Waislam badilikeni vinginevyo kila wakati mtasema mnaonewa.

Mtoto akifeli darasa la saba siyo mwisho wa dunia au kumpeleka kwenye mafunzo ya dini , anapaswa kuendelezwa kwa mfumo mwingine wa elimu, kwa mfano kupitia mafunzo ya VETA au shughuli zozote zitakazoweza kumpatia Ujuzi ambao utamsaidia kujitegemea na kuendesha maisha yake, sasa hao watoto mnaowaficha huko misikitini na mabwenini mwisho wa siku mnataka wafanye shughuli gani za kuendesha maisha yao ikiwa hawana ujuzi wowote.?
 
Vyuo vya dini vipo muda mrefu tu .Mfano Chuo Cha TAMTA,Zaharau na Maawal vya Tanga vimefundisha masheikh wengi wakubwa kutoka pande mbalimbali za nchi na hata nje ya nchi.Hapajakuwepo shida yoyote katika vyuo hivyo pamoja na wanafunzi wengine kukaa bweni.Kulaza wanafunzi kwa kufuata Sheria hakuna shida.Waacheni watu wasome dini zao mradi wafuate Sheria.Wanaopinga watu kusoma dini ndiyo siwaelewi.
Hao hapo hawajafuata sheria. Iko wazi kabisa, na MAZINGIRA ni hatarishi
 
From...
Unawafananisha Waislam masikini ya Mungu na Wakatoliki wanaopewa ruzuku ya mabilioni na serikali?

Unaijua Memorandum of Understanding (MUM)?
Si umeona hapo Kuna neno foundation unakuta inapokea mabillioni ya pesa mipesa kutoka kwa wafadhili zinaingia mifukoni mwenu huku mkiwatumia watoto kama chambo na kuhusu wakatokiliki kupewa fedha za uendeshaji wa taasisi zake ni zile taasisi zinazahudimia jamii kwa ujumla Sasa jiulize kama hospital kama bugando waislam hawatibiwi?
 
MUM au MoU ?
N
Boarding mnaKwenda kufunzwa dini badala ya masomo ambayo yanatakiwa kufunzwa? Huu upuuzi wa dini yenu ndio unaoharibu jamii, serikali ikicheka na hawa vilaza, tutakuja kulia, muda wa watoto kuwa shule ninyi mnawapeleka misikitini kuwajaza upuuzi ambao hauna msaada kwa maisha yao wala kwa Taifa,
Na peponi hawaendi kwa sababu ya mtihani mkubwa wa umaskini walionao Waafrika.


Mpaka karne hii watu wanafungiwa kufundishwa dini tena kwa kukaririshwa sio kupanua maarifa ya kuhoji na kubaini ukweli na uhalisia wa hizi dini ambazo wale waliozipokea mwanzo hawana habari nazo zaidi ya kuhangaika na mali ili waondoe umaskini kwenye jamii zao
 
Kiongozi jenga utamaduni wa kushughulikia chanzo cha tatizo au chanzo cha uvunjifu wa sheria/utaratibu nk nani aliwaleta hapo hao watoto, kwa vibali gani..lengo ni nini? nk ili isije rudiwa tena na wale walioanzisha hili jambo wachukuliwe hatua wao binafsi. Sasa fungeni kituo, halafu baada ya muda wanakwenda kuanzisha jambo hilo hilo sehemu nyingine!
Pia ni vyema kuwasikiliza lengo na nia ya hao kuanzisha hicho kituo kama haitishii usalama sioni shida kwa maana tunatafutiana mitazamo na matarajio ya mbeleni, wengine hawana mpango na hii elimu ya darasani tayari wana mifumo yao ya jinsi ya kupata maisha uona kama inawapotezea mda tu.
 
Bagamoyo,
Rejea kwenye hiyo video uitazame na usikilize ukiwa makini.
Hakuna mwanafunzi yeyote kutoka nje ya Tanzania.

Rejea usikilize tena hao wanafunzi wengi wameishia darasa la saba na wameletwa hapo na wazee wao waje wasome dini.

Tatizo labda liko hapa.
Nimetumia neno ''labda'' kwa makusudi ili ikiwa lipo tatizo lingine lisemwe.

Ikiwa wewe ni Muislam hutopata tabu unapambiwa watoto wengi wa Kiislam huishia darasa la saba.

Kitwana Kondo alipata kulizungumza hili Bungeni.
Nakuwekea hotuba yake uisome.

(Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma, 1999)

Waislam waliofanyiwa mtihani wa kuingia kidato cha kwanza majority yaani wengi walikuwa Waislam na Wengine walikuwa ndiyo wachache.

Waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza wengi walitoka katika wale Wengine na Waislam wakawa wachache.

Waislam kwa kuthamini elimu ndiyo wanawapeleka watoto wao katika shule hizi za ''kimasikini,'' kusoma.

Hatuna ubavu wa kushindana na shule za Wengine ambazo zinapewa ruzuku mabilioni ya kutoka serikalini kupitia Memorandum of Understanding (MUM) katika ya Serikali na Makanisa.

Yapo mengi katika matatizo yanayowakabili Waislam moja wapo ilikuwa NECTA kuhujumu shule za Waislam.

Naamini unayajua maandamano ya Waislam mwaka wa 2012.
Tutoke hapo.

Kama tatizo la kuvamia msikiti usiku wa manane DC na Kamati ya Amani mbona kuna shule za mbovu kupita kiasi hazijavamiwa na wanafunzi kurudishwa makwao?

Angalia ushahidi huo hapo chini

Upo ushahidi mwingi lakini tuanze na huu.

Nipe jibu kwa nini shule hii haijavamiwa usiku wa manane na DC na Kamati ya Usalama?
Shekhe wangu Mzee Mohamed Said, kwa hili la Bagamoyo,ungeliacha tu lipite. Si jema kwa afya za watoto.
Kosa la mmoja halimhalalishi muovu
 
NI KAWAIDA KABISA HIZO NI BOARDING ZA ELIMU YA DINI YA KIISILAMU.

tatizo ni kwamba ikionekana watu wanalala katika misikiti watu hudhani wanafundishana ugaidi.

lakini kimsingi boarding kama hizo za masomo ya kiisilamu zipo nyingi sana Nchi hii katika mikoa mingi.

na boarding hizo hufundisha masmo ya kawaida kabisa katika uisilamu.

Kama vile kuhifadhi Qurani,kusoma hadithi,fiqhi,lugha ya kiarabu n.k

Japokuwa wstu wabaya hupitisha ajenda yao popote pale na hivyo hatà huko wapo wachache wanaweza kutumia huo upenyo.

Ila kimsingi Hapo hakuna viashiria vyovyote vya ugaidi.
Ni kweli......lakini hapa mazingira ya kuishi vijana sio rafiki kabisa.......bila shaka umeona video fupi juu ya hayo mazingira. Ni bora kufunga na kufanya marekebisho ila vijana waishi maisha rafiki kwa elimu yao.
 
Huyo DC toka apelekwe huko ameonesha chuki za waziwazi kwa wenyeji wa huko na ni kama anajiona yeye ndiye anawaweza na atawakomesha,wacha tuone mwisho wake utakuwaje.
 
Back
Top Bottom