Kisutu: Ajali ya Mwendokasi makutano ya Jamhuri na Morogoro Road

Kisutu: Ajali ya Mwendokasi makutano ya Jamhuri na Morogoro Road

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Basi la Mwendokasi likiwa linatoka Kivukoni limeacha njia na kuparamia maduka na miundombinu mingine pembezoni mwa barabara ya Morogoro kwenye makutano ya Jamhuri St.

Eneo hilo ni viambaza vya maduka, njia ya waenda kwa miguu na limekuwa linatumika na watu wasio na makazi kulala

Ukiangalia picha kwa umakini utaona baadhi ya virago vya kulalia ombaomba. Tuombe Mungu pasiwepo na madhara ya uhai.

====
Basi la Mwendokasi leo February 22, 2023 limepata ajali eneo la makutano ya Jamhuri na Morogoro baada ya kugongana na gari ndogo kisha kuparamia ukuta wa duka likijaribu kulikwepa. Imeripotiwa kutokea majeruhi kadhaa.



20230222_110718.jpg


img-20230222-wa0009-jpg.2526142

------
Baada ya kuibuka sintofahamu ya mwanaume aliyeonekana akijaribu kulikwepa gari la mwendokasi wakati wa ajali (tazama video au picha hapo juu) kuwa amepona au amefariki dunia, Hospitali ya Taifa Muhimbili kupitia kitengo cha mifupa MOI walitoa taarifa kuwa mwanaume huyo hakufariki ila alipata majereha makubwa na kulazwa chumba cha wagonjwa mahututi.

Zaidi soma:
MOI: Mwanaume aliyegongwa na Basi la Mwendokasi yuko ICU
 
Again nchi hii bado tumepotea, kelele za mashabiki wa mpira tungekuwa tunawapigia wanasiasa ingekuwa vema sana, why traffic officer's hawakuenda na breatherlizers ili kumpima dereva ulevi on the spot?

Au why hawakumpeleka hospital ili apimwe kiwango cha alcohol kwenye blood yake? Maana hii sitofahamu isingekuwepo
 
Hii mitaa huwa ni Mungu tu anaepusha ajali ni hatari sana, nyumba ziko karibu sana na barabara, jioni hasa kuanzia saa moja kuna ombaomba wegi sana, tena vingine ni vitoto vidogo vinazurura ovyo, sasa kibaya mabasi ya mwendo kasi kwakuwa ni barabara yao mwendo wanaotembea kwakweli si rafiki kabisa, yaani kama una ma stress yako ya familia usipende sana kukatiza hayo maeneo.
 
Again nchi hii bado tumepotea, kelele za mashabiki wa mpira tungekua tunawapigia wanasiasa ingekuwa vema sana,why traffic officer's hawakuenda na breatherlizers ili kumpima dereva ulevi on the spot?,au why hawakumpeleka hospital ili apimwe kiwango cha alcohol kwenye blood yake?maana hii sitofahamu isingekuwepo

Hata wa STK, STL na ya namna hiyo ingekuwa hivi hivi.

Bila katiba mpya yenye kuhakikisha maslahi yetu sote yanazingatiwa, tutayaona mengi na bado.
 
Hii njia mi naona dereva labda alikua anajaribu kukwepa kitu Kama sio mtu basi Gari, haiwezekani uniambie dereva asubuh yote hii kalewa mleta habari hapa umebuni tu.

Ungesema uenda labda bado anawenge la usingizi wa asubuhi hapo sawa atleast kidogo ungeeleweka... alafu we mwenyw ulikua unapita na mwendokasi ukapiga picha ulijuaje kama dereva kalewa!!?
 
Back
Top Bottom