Kisutu: Erick Kabendera ashtakiwa kwa Kujihusisha na mtandao wa uhalifu, ukwepaji kodi na kutakatisha fedha haramu

Kisutu: Erick Kabendera ashtakiwa kwa Kujihusisha na mtandao wa uhalifu, ukwepaji kodi na kutakatisha fedha haramu

Wanachofanya ni.kutumia mamlaka vibaya kwa kumkomoa kabendera baada ya kukosa ushahidi kwenye ile kesi ya Uraia.

Mahakama sasa ioneshe ukuu wake kwa kuendesha kesi ya kabendera mfululizo ili apate haki yake bila kuteswa gerezani bila hatia.

Mahakama iamke na kila mwenye kesi isiyo na dhamana,kesi isikilizwe mfululizo ili kuepusha dhulma na uonevu kwa watu wasio na hatia.

Kwa ushahidi wa mazingira Kabendera na wengine wasiopendwa wanapewa kesi ngumu ili kuwakomoa,na kuwaweka rumande muda mrefu kwa lengo la kuwakomoa ili hata wakishinda wawe wameshasota gerezani vyakutosha.

Ardhi yenye dhulma ni laana kwa vizazi
Tusishangilie haya.

MKuu umesahau ya Kitlya? imeisha kwani?
vipi ya IPTL ? Imeisha?
 
Dola ili isimame lazima iwe na uwezo wa kuchukua hatua kali dhidi ya wahalifu.

Hata hivyo dola lazima iwe na huruma,kwa sababu kuna baadhi ya wale walio ndani ya dola (baadhi ya wananchi) ,hukosea kwa bahati mbaya ,hivyo huitaitaji uangalizi ili wajifunze.

Kabendera kahurumiwa na serikali kwa kiwango kikubwa sana ,ashukuru kwa mikono miwili.
Kosa alilolifanya alistahili kupigwa risasi hadharani tukishuhudia .

Japo mahakama haijathibitisha hatia yake ,tukubali tukatae serikali imejiridhisha ni muhalifu ,ila imeachia mkondo wa sheria ufuatwe.
Ingekua china pumzi yake ingekua imekata kwa sasa .
Kwasasa kabendera yuko mikono salama ni jukumu lake kutafakari matendo yake kwa taifa.

Tanzania yenye watu millioni sitini ni muhimu sana kuliko kabendera na wanaomtumia kipumbavu.

Mwisho , serikali iache huruma ,kuna wengine hawastahili kuhurumiwa kwa matendo yao.
 
Victoire hebu basi tumia just your common sense kutafsiri trend of events ndugu yangu.

Nikweli kama mwanadamu mwingine yoyote huyu Erick aweza kuwa na makando kando yake. Lakini katika haya yanayoendelea juu ya huyu Erick haihitaji uwe na Kipaji Cha Shekhe Yahaya ili uelewe huku kukomolewa kwakwe kwenye malengo Maalum.

Rejea Matamko ya Mambo Baadae, Kisha Yule wa Uhamiaji alafu akamalizia Mwakyembe kwamba Huyu Sio Raia Kisha Uchochezi lakini leo wameona wampe hayo wakijua kuwa hayo Mengine Ni Mashtaka yenye dhamana.


Anyway tuendelee kuandika tuwezavyo kwa kutumia MB zetu lakini iko siku Mambo ya namna hii yakimgusa anayekuhusu naamini utaelewa na ku sympathize na wahusika.
Ni kweli kaka hata kesi yake hii ni kwa sababu tu na maandishi yake kwenye gazeti la The Economist.Nadhani aliona kama risk alokuwa anachukua.Unakumbuka yule mwandishi wa Saudi Arabia alivyokatwa katwa vipande vipande kule Uturuki?Basi mimi naona ukiwa kwenye serikali kama hizi zilizo tayari kufanya lolote kwa kulinda maslahi yao lazima uwe care sana unless upo tayari kwa lolote.Cha kusikitisha familia yake ndiyo itakayohangaika.
 
Pascall Mayalla Mungu anakuona ujue, wakati haka kajamaa kamekazana na viarticle vile wewe ulikuwa umekazana kuvipandisha humu Jamvini kwa mbwembwe.
Ona sasa kametiwa nyavuni. Mungu anakuona Pascall Mayalla.
 
Unavyoongea hivyo, una taarifa kamili kuhusu kesi hii??
Wakikuonesha ma transaction kwenye account yake jinsi yalivyo, utabishaa???
Tukae kimya, huku vyombo vya nchi vikiendelea kutenda haki.

Kama lini Mkuu ,la Mh Lissu ni mfano tosha kuwa Haki hamma na inavunjwa kwa Makusudi na waliopewa Dhamana.
 
duh! aisee
mleta uzi bando haitoshi kuelezea mkasa huo maana kama umebanwa vile way to maliwato
 
Mhakama kuu ina uwezo wa kufuta sheria kama haipo practical lakini hii sheria ipo dunia nzima ispokuwa inatumiwa vibaya. Lakini ikiwa kuna mtu ameshtakiwa kihalali mahakama haina ujanja wala sababu ya kutaka sheria ifutwe. Swala ni kujiridhisha kwamba hapa imetumika sawa hapa sivyo ndo ngoma ipo hapo
Nina shida na misingi ya utungaji wa sheria zetu. Jambo linalofanyika sehemu nyingine duniani sio lazima tulibebe kama lilivyo maana mazingira ya dunia yanatofautiana kutoka sehemu moja hadi nyingine

South Africa kosa la mauwaji (murder) linadhaminika. Sasa hapa kwetu mazingira ni tofauti kwasababu kwanza usalama wa mtuhumiwa umezingatiwa katika suala zima la kumnyima dhamana

Sasa sioni ugumu uko wapi wa shitaka hili la utakatishaji lisiwe na dhamana maana mazingira ya huko "duniani" tulipoikopi sheria hii ni tofauti na yakwetu na maranyingi fursa hii hapa kwetu hutumiwa na waendesha mashtaka kuwaadhibu watu kabda hawajkutwa na hatia

Nahoji misingi ya utungaji wetu wa sheria kwa sababu wakati mwingine utaona haziko reasonable

Leo hii mtu akikamatwa anasafirisha kilo hamsini za miraa/mirungi na akipatikana na hatia adhabu yake ni KIFUNGO CHA MAISHA!!!

Mirungi ambayo hapo nchi jirani ni biashara halali lakini sisi tumeweka capital purnishment huku jambazi wa kutumia silaha anaadhibiwa miaka 30 tu!!!
 
Halafu kinachoniboa kwa hizi kesi zao uchwara utakuta wanamsumbuaa mara ushahidi haujakamilika sijui upelelezi. Halafu mara afutiwe mashitaka kisha akamatwe tena! Yani ni full vurugu mechi. Ila naye Kabendera aliona jinsi huu utawala ulivyo then anaandika vile na kusalia Tanzania! Ashukuru Mungu hakuuawa ingawa mida ya usiku safari za STAKI SHARI zitamuhusu na kule ni kilio na kusaga meno. Wapo waliopelekwa kule na bahati mbaya sana au bila mpigaji kujua (Maana kuna giza sana) anashusha rungu sehemu mbaya na wengine wanapigwa vibaya wanaondoka jumla baadaye tunakutana ufukweni mwa bahari! Sitosahau kile kipindi aisee eti tunaambiwa ni raia haramu!
Mkuu embu nitag makala zake mbili tatu
 
Dola ili isimame lazima iwe na uwezo wa kuchukua hatua kali dhidi ya wahalifu.

Hata hivyo dola lazima iwe na huruma,kwa sababu kuna baadhi ya wale walio ndani ya dola (baadhi ya wananchi) ,hukosea kwa bahati mbaya ,hivyo huitaitaji uangalizi ili wajifunze.

Kabendera kahurumiwa na serikali kwa kiwango kikubwa sana ,ashukuru kwa mikono miwili.
Kosa alilolifanya alistahili kupigwa risasi hadharani tukishuhudia .

Japo mahakama haijathibitisha hatia yake ,tukubali tukatae serikali imejiridhisha ni muhalifu ,ila imeachia mkondo wa sheria ufuatwe.
Ingekua china pumzi yake ingekua imekata kwa sasa .
Kwasasa kabendera yuko mikono salama ni jukumu lake kutafakari matendo yake kwa taifa.

Tanzania yenye watu millioni sitini ni muhimu sana kuliko kabendera na wanaomtumia kipumbavu.

Mwisho , serikali iache huruma ,kuna wengine hawastahili kuhurumiwa kwa matendo yao.
Limsiba hili
 
Mwandishi wa Habari za uchunguzi, Erick Kabendera amefikishwa Mahakama ya Kisutu leo

Anashtakiwa kwa makosa matatu chini ya sheria uhujumu Uchumi ambayo ni...

1. Kujihusisha na mtandao wa uharifu, 2015-2019 katika maeneo ya Dar Es Salaam aliongoza kundi la uhalifu kwa lengo la kupata faida au manufaa mengine

2. Kukwepa kulipa kodi. Katika tarehe tofauti kati ya 2015 hadi 2019 katika jiji la Dar es Salaam alikwepa kulipa kodi zaidi ya Tsh milioni 173

3. Kutakatisha fedha haramu.

View attachment 1172905
View attachment 1172906
View attachment 1172907
Halafu unaunga mkono huu utawala...My brother my University mate emb jitafakari. Ukiona utawala unaojisifia sana, kuminya uhuru wa kusema, kuwepo makesi ya ajabu kwa watu makini na watu kupotea hovyo jua kuwa huo ni UTAWALA WA KIDIKTETA kama zile za kina Idd Amin! Hazina tofauti yoyote ile!

"Udikteta ni utawala wa kikundi kidogo cha watu ambao neno la mkuu wao ndiyo sheria na halihojiwi popote pale"
huyu jamaa anaumiza watu wengi sana Erick siyo mharifu tusingepiga kelele angepotezwa wako wapi viongozi wa dini waliokuwa natoa waraka enzi za jk
 
alifanya nini kiasi kuwa tuone kuwa tuna haki na Damu yake iwe mikononi mwetu.
hebu tueleze tuelewe vizuri inaelekea kuna kitu unajua sisi wengine hatujui ili itusaidie katika kumuhukumu na kumuonea huruma kwa makosa aliyotenda kwa kuwa na yeye ni mwanadamu dhaifu tu kama wengine.
 
Wewe ni mpumbavu mwingine tu unayedhani uhai wa mtu ni kitu kidogo. Damu ya mtu iliyomwagwa bila hatia kamwe haitaenda bure. Kama mtu ni mhalifu ashitakiwe kwa kosa halisi alilofanya. Sio unamkamata kwa shida ya uraia unapokosa ushahidi unamshtaki kwa kosa la kutakatisha pesa. Wekeni wazi. Kama ni zile makala za kukosoa jiwe, semeni sio unasema kutakatisha pesa tu ili umkomoe mtu kwa kumnyima dhamana. Malipo yake yanakuja na wala hayatakawia.
 
Wewe Ndiyo mjinga aka stupid kwa kuandika mbupu! MTU shujaa huyu.
He was too stupid/naive kuandika makala kama zile halafu unaishi bongo na unaona kinachoendelea..He had it coming to him

Angeweza kuandika makala kama zile under a false ID, pia unaweza kufuatilia kila kitu bongo ukiwa nje, dunia ni kijiji hiki, zile makala zake zilikuwa zinachambua tu hotuba za magufuli, miradi anayoifanya na sera zake ambazo hata ukiwa Australia huko ukifuatilia utafahamu tu, au unaweza kuniambia ni vitu gani aliandika ambavyo mtu ukiwa nje huwezi kuvijua? vyote vipo wazi tu, sema yeye ameandika katika kuvikosoa

pia unaweza kuwa na watu wako bongo wanaokupa taarifa za ndani ambazo haziwekwi kwa waandishi, akina Mange kimambi, Ngurumo wanapata intel nzuri tu na wapo nje, hivyo ndivyo waandishi pragmatic, wanavyoishi kulingana na uhalisia wa hali, sio kujifanya unakufa kishujaa, kesho wanakusahau, unaacha familia inateseka na hakuna mabadiliko yoyote uliyofanikiwa kuyaleta sababu ulienda kiboya
 
Kumbe kuna watu ambao mnaijua kesi hii nje ndani. Maoni yangu yalikuwa, kama hatuna habari au taarifa kamili, hatuna haja ya kulaumu vyombo husika, kwa maaa wao wamejiridhisha mpaka wakampeleka mahakamani kwa mashtaka hayo.
Mashtaka yepi
Mara uraia mara uchochezi
Leo kesi ya kubambikizwa
Yana mwisho haya
 
Back
Top Bottom