Kisutu: Kesi ya Erick Kabendera yaendelea. Jamhuri yaweka kisiki Erick kushiriki msiba wa mama yake mzazi

Kisutu: Kesi ya Erick Kabendera yaendelea. Jamhuri yaweka kisiki Erick kushiriki msiba wa mama yake mzazi

Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.
Suala la huruma ni upande mmoja lakini ni vizuri kujua utaratibu uliopo kwenye mazingira kama haya; huwa hatua gani zinachukuliwa?
 
Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.

Sheria inasemaje juu ya haki ya kuhudhuria msiba kama uko mahabusu?? Leta substance!
 
Hakuna cha kazi yeyote hapa, ziko wapi trilion 2.5 Mkuu? Hata Nduli Idd Amin Dadaa alijitambulisha kama mchapa kazi kweli kweli, katika utawala wake uliogubikwa mauaji ya kikatili, uvunjifu wa haki za binadamu na mazongwe mengine mengi tu.
Ulidanganywa sana,Idd Amin hajauwa watu,walikupa taarifa za uongo ukaziamini
 
Kumbe kabendera na yeye huwa analia!
Wako wapi akina Zitto waliokua hawakosi kwenye kesi zake hapo mwanzo mwanzo
Mahabusu wote nchi wakiomba ruhusa ya kuzika wapendwa wao itakuaje
Kabendera sasa ni wakati wake wa kulipa ujahili na usaliti,atamkumbuka sana mama yake kwan alishamuasa aachane na kutukana viongozi na serikali
 
Sisi siku hizi haturopoki sana...Matokeo yatatoka wala usiwe na wasiwasi! Kuna siku utakuwa unalia sana humu Jf kwa ajili ya fulani! Short time ahead my friend! Hatunaga maneno maneno sana baada ya kugundua tunapokwama ni wapi! Discipline itatembea tu mkuu mark me!
Mkwara mbuzi huu😂😂😂😂
 
Usiandike kutoka kwenye hisia tu. Hivi, mnajua kuna Watanzania wangapi wako rumande au jela na wamepoteza wapendwa wao? Suala hapa lilitakiwa kuulizwa (badala ya kuomba) ni utaratibu gani uliopo kisheria wa mfungwa au mshtakiwa aliye rumande anapopata msiba? Na je utaratibu huo kwanini usitumike (kama upo) kwa Eric Kabendera? Hili ndilo swali langu badala ya kutoa lawama tu. Maana binadamu wote ni sawa. Ila kama huwa hawaruhusiwi kwenda kwenye misiba hata kama ni wa baba au mama, au mtoto, kwanini iwe tofauti kwa Kabendera? Tuwe na ubinadamu, mwenzetu kafiwa na Mungu ampe faraja sana lakini tusije tukajiona miungu wa kudhania tunajua majibu ya maswali ya umilele.
Enzi hizo ungekuwa unalaani kweli kweli hapa! We jamaa ni mnafiki sana, na ndio maana FaizaFox aliwahi kukuambia wazi kwamba critics zako kwa JK zilikuwa zinasukumwa na udini wako!!!
 
Hizo kesi zingekuwa halali ushahid ungeshakamilika kitambo.Eti mwaka Wa tano sasa ushahidi haujakamilika utadhani umefatwa mwezini.Wao wameshawakamata kwa kesi walizowapa si wawahukumu basi.Maana hata kutowahukumu ni uvunjifu Wa haki za binadamu

Nakubali, na nimesema Kabendera kafanyiwa dhulma. Hawakupenda anachoandika wakambambika kesi. Serikali zetu dhalimu za dunia ya tatu ndivyo zinavyo operate.

Lakini napinga kusema apewe fursa kuzika kwa sababu tu wanahabari wenzie wamekuwa wakimpazia sauti.

Wangapi wamefungwa kwa dhulma hatuwasikii wakifiwa?

Ukitetea haki tetea ya kila mtu, sio ya mwenye sauti tu.
 
Kwani alizaliwa peke yake? Lini mshitakiwa aliwahi ruhusiwa kwenda kwenye mazishi? Au hii iwe special kwa huyu, mwandishi habari? Wakulima je? Wafugaji je?
Tusiishie kusikitika, tuepuke kujiingiza kwenye mambo ya kujitakia. Kulikuwa na kila njia ya kuachana na hayo lakini naona alijivunia ushujaa.

Tofautisha kati mshitakiwa na mahabusu unaposeama mshitakiwa unamaanisha kashahukumiwa


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Katika utawala huu wa Magufuli, Tanzania imekuwa ni Taifa la kidikteta lisilojali Utu,Haki,Usawa na Sheria kwa raia wake.
Anayotendewa Erick ni zaidi ya Unyama na Ukaburu ulokuwa unafanywa na Makaburu wa enzi za Utawala wa weupe wachache nchini Afrika Kusini.

Mtu kafiwa na mamake mzazi tena kuna uwezekano mkubwa kifo cha mama huyu kitakuwa kimechangiwa na Utawala huuhuu! Huu ni ukatili wa hali ya juu sana.

RIP Mama Mujahwuzi na pole sana Erick! Mungu ndiye atakayekulipia kwa watesi wako.
Imagine, kama mahabusu wote wangeruhusiwa kuhudhuria mazishi, kipa imara, arobaini, kubatizwa, kuchezwa, harusi, n. k. Za wapendwa na jamaa zao, bila kukataliwa!
 
Shetani mkubwa wewe! Yaani unaongea ushenzi kwa sababu tu ya kutetea mabwana zako waliopo kwenye mamlaka?! Kima wewe.
Suppose mimi ni kima, does it make any difference in the fate of the accused? Au unaamini nchi inaendeshwa kupitia JF? Tunao ndugu wengi waliofia Mahabusu na jela na haijawahi kuwa taabu kwa serikali. Hiyo ni kote duniani. kasirika, cheka, galagala, do whatever stupid you cana manage, it is irreversible!
 
Suala la huruma ni upande mmoja lakini ni vizuri kujua utaratibu uliopo kwenye mazingira kama haya; huwa hatua gani zinachukuliwa?
Watu wako heated kwa kuamini wakipiga kelele sana, Serikali itampa wanachokitaka. NIliuliza ni sheria au utaratibu gani hutumika. Kama huwa hakuna uataratibu kama huo, hakuna sababu ya kutaka huyu ndo apewe nafasi hiyo. Iko siku mtu ataomba amtembelee mke au mumewe aliyemumiss. NAkumbuka Sigh aliwahi kuomba nafasi ya kutibiwa kwa sababu eti alikuwa na 'puto' tumboni. Alinyimwa nafasi hiyo hadi leo!
 
Mjibu vizuri alichosema, je kuna utaratibu wa kisheria kwa mfungwa au mahabusu wa kutolewa gerezani na kwenda kushiriki msiba au tukio lolote?

Sent using Jamii Forums mobile app
Tumia akili. Huyu siyo mfungwa. Ni mtuhumiwa tu. Na mwisho wa siku anaweza asipatikane na hatia. Mbaya zaidi sote tunajua mashtaka yenyewe ni ya kumbambikia.
 
Back
Top Bottom