KISUTU: Mahakama upande wa Watoto yatupilia mbali shtaka la Hamisa Mobetto dhidi ya Diamond kuhusu malezi ya mtoto wao

KISUTU: Mahakama upande wa Watoto yatupilia mbali shtaka la Hamisa Mobetto dhidi ya Diamond kuhusu malezi ya mtoto wao

ukinipeleka mahakamani ukashindwa kesi jiandae kulipa huo usumbufu hata kama sio kwa njia ya pesa. Hamisa Right now atakua anajutia.
 
Naona mshauri wake wa mtandaoni kaangusha post ya kutuliza presha za team wema na hamisa. Huyu binti maisha ya mtandaoni anaonekana shujaa kwa baadhi ya watu ila halisi mateso tupu.
Cc mange
 
Mwanamitindo Hamisa Mobeto amekwaa kisiki mbele ya Diamond Platnumz baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu upande wa Watoto kutupilia mbali kesi aliyofunguliwa mwanamuziki huyo juu ya matunzo ya mtoto Prince Abdul.


Uamuzi huo umetolewa leo Ijumaa Novemba 10 ,2017 na Hakimu Devotha Kisoka wa Mahakama hiyo baada ya kusikiliza hoja za pande hizo mbili husika.
Diamond aliwasilisha pingamizi dhidi ya kesi hiyo iliyofunguliwa na Mobeto akidai kuwa kesi hiyo imefunguliwa kwa kutumia kifungu ambacho si sahihi. Hoja ambayo ilipingwa na Mobeto.


Mobeto alifungua kesi hiyo mahakamani hapo, pamoja na mambo mengine anaiomba matunzo ya mtoto waliozaa na msanii Diamond.
Mobeto anaiomba mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto ya kila mwezi na alifungua kesi hiyo kupitia mawakili wake Abdullah Lyana na Walter Godluck kutoka kampuni ya uwakili ya Century Attorneys.


Kupitia hati hiyo ya madai, Mobeto anaomba Diamond amuombe msamaha kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake.


Diamond aliwasilisha hati ya majibu hayo kinzani akipinga maombi hayo ya Mobeto akidai gharama anazodai kulipwa kwa mwezi ya Sh 5 milioni kwa ajili ya matunzo ya mtoto ni kubwa hawezi kuzimudu.

mobetto%2Bpic.jpg
 
Kwahiyo mkuu mahakama imesemaje sasa kwamba alipe kidogo au asilipe kabisa hata mia
 
Hivi huyu Dada kweli alishindwa kufikiri kama atulie aendelee kula hizo pesa za diamond?
Ujauzito tu Jamaa akamvutia gari!

Aulize wenzie huwa inakuwaje??

Hivi si angeendelea kujificha kwenye kivuli cha mtoto kumchuna Jamaa?

Wadada bwana akili zenu mnazijuaga wenyewe!!
 
Afadhali.. daah! huo ungekuwa unyonyaji wa karne..
 
Nakumbuka siku moja Babu aliniambia "Mjukuu wangu unatakiwa uwe na Masikio makubwa kama Ungo ila Mdomo uwe Mdogoo kama tundu ya Sindano" Siku zinavyozidi kwenda na ninayoyaona nazidi kuthibitisha kauli yake!!!
 
Hivi kwa nn familia haimpost huyu mtoto? Kwa nn mtoto akulie kwny chuki... Kati ya upande wa diamond na hamisa? Mi naona wangekaa chin wajadl kifamilia... Na diamond anashindwa kusolve tatzo dogo kama hili mmmmh
Kwani lazima impost?

Mama mtoto ndio kaanzisha chuki ili aifurahishe insta

Ulitaka dai asolve kwa kutoa hizo milion tano au
 
Sitaki kusoma JF, nataka kuwepo ktk vizimba vya mahakamani, nikirudi huku kijijini niwasimulie!
[emoji3] [emoji3] [emoji3] sasa c uwe unaandaa mashamba saiv
 
Naona mshauri wake wa mtandaoni kaangusha post ya kutuliza presha za team wema na hamisa. Huyu binti maisha ya mtandaoni anaonekana shujaa kwa baadhi ya watu ila halisi mateso tupu.
Mi nakwambia kipindi Wema karudiana na Domo nilikuwa naishi Sinza mori pale karibu na Meeda, Domo alikuwa anapanga mitaa hiyo..

Sasa mama ubaya akilewa anasimulia jinsi Domo bahili a.k.a mchumi [emoji23] hatoi hata mia labda kugegedwa tu, akanyoa hadi kipara, kuvaa madera nahisi unakumbuka?!

Huyo Hamisa namuonea huruma kushindana na Zari, kuna mtu wasafi hapa kitaa karopoka kuwa zari huwa anajihudumia kwa asilimia kubwa, na hata hii safari ya UK kajilipia nauli[emoji144] [emoji144]

Sasa bibie Hamisa kwenda court kutaka ulipwe 5m na Domo...akili itakukaa sawa mwaka huu
 
Back
Top Bottom