Kiswahili fasaha kinatoweka

Kiswahili fasaha kinatoweka

Kwenye salamu ndio nachoka kabisa.
Vijana anamwambia mwenzake oi na yeye anajibu oi.Eti ndio wamesalimiana hapo.
Kuna hii nyingine ya wozaa anayesalimiwa anajibu woza woza
Ni Gani ? Ni Og
Mjomba=Jombaa
Mama =mazaa
Haina shida=Haina kwele
Umeenda nae? =Umetimba nae?

Yapo mengi sana
 
IMG_20240418_162022.JPG
 
Kwaiyo -ko
Mdogowangu Huwa anatumia Yani niliona smszake kaandika hivo nachefukwa 🥲
Siku Imani ikanishinda nikamwambia km hutak kuandika neno vizuri usinitumie sms
 
Kwaiyo -ko
Mdogowangu Huwa anatumia Yani niliona smszake kaandika hivo nachefukwa 🥲
Siku Imani ikanishinda nikamwambia km hutak kuandika neno vizuri usinitumie sms
‘Kwaiyo-ko’ maana yake nini?
 
mm naww xax bac uminiuz sn = hapo anakwambia mimi nawewe sasa basi (mmeachana) umeniudhi sana

kazi kweli[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Kwa utafiti wangu mdogo hakujawahi kutokea matumizi mabovu ya lugha ya kiswahili kama muda huu tulionao.

Kibaya zaidi hata baadhi ya vyombo vya habari vikubwa vinashiriki dhambi hii.

Maneno mazuri ya kiswahili yamepindishwa kiasi inaleta kichefuchefu hata kusikiliza. Hapa nitaweka baadhi ya maneno.

Alikuwa = alikua
Kwa hiyo = ko
Baadhi = baazi
kufanikiwa = kujipata
sasa = saivi
Ndio hivyo = ndoivo
Ndio nini = ndonini
serikali = serekali/selekale
yaani = yani
mtaa = kitaa/kitaani
kwa sababu = co

Pasipo kuchukuliwa hatua za makusudi lugha hii inaelekea kupotea.

Chanzo kikuu cha haya ni uholela wa vyombo vya habari hasa habari za mtandaoni.

Nashauri mambo makubwa mawili yafanyike kwa haraka.

Kuwe na takwa la lazima kwa waleta habari kwa jamii wote kuwa na ufaulu mzuri wa lugha hii

vyombo vya habari vyote yaani vya kawaida na mitandaoni lazima visajiliwe kwanza na mamlaka za kiserikali kabla ya kuanza kupeleka habari yoyote kwa jamii.

Tuungane pamoja kuinusuru tunu yetu kuu ya lugha ya kiswahili
Let me see - lemme see.
 
Lakini kamusi si huandikwa na wataalamu wa lugha?

Ina maana wataalamu hao walikosea?

Na siyo kamusi moja tu. Za TUKI zinalo hilo neno ‘onyesha’.

Za Oxford zinalo hilo neno’onyesha’.

Wote hawa wamekosea?
Kama tunavyosema hapa, unaweza kushangazwa sana unapokutana na taasisi kubwa kama TUKI nayo inaboronga Kiswahili.

Wamekosea, hilo si neno sahihi.
 
Wengi wanafupisha neno KWAHIYO kwa kusema KO.

Ko vipi sasa?

Ko unakuja au?

Hivi ni viswahili vya watu wasio na upeo wa kitaaluma au kielimu A.K.A MANGUMBARU / MABICHWA KOMWE.
mkuu ndio najua leo kumbe

bichwa komwe = ngumbaru
 
Shida ilianza pale ambapo VILAZA waliajiriwa kuwa WALIMU.
Walimu wangu shule ya msingi,95% walikua walimu wa upe,yaani hawakufija sekondari,lakini walinifunza kiswahili fasaha na nilielewa,mi nadhani walimu hawana wito tu,wanawaza kuuza bagia kwa watoto na kuwafundisha twisheni mapema asubuhi kabla ya vipindi,tunatoka la pili kuingia la tatu hapakuwa na mtu aliyeshindwa kusoma na kuandik
 
Walimu wangu shule ya msingi,95% walikua walimu wa upe,yaani hawakufija sekondari,lakini walinifunza kiswahili fasaha na nilielewa,mi nadhani walimu hawana wito tu,wanawaza kuuza bagia kwa watoto na kuwafundisha twisheni mapema asubuhi kabla ya vipindi,tunatoka la pili kuingia la tatu hapakuwa na mtu aliyeshindwa kusoma na kuandik
Siku hizi walimu wenyewe ni mabishoo halafu ni VILAZA hatari
 
Back
Top Bottom