Kiswahili fasaha kinatoweka

Kiswahili fasaha kinatoweka

Yaani wewe ndio umenikoroga kabisa 🤯 Nlikuwaga simpendi mwalimu wangu wa kiswahili alikua anaitwa Sekule kwasababu ya kufinya. Yule mwalimu hapana jamani 🙌🏾 Hadi nimesikia maumivu ya vifinyo vyake upya. Basi na somo nkalichukia completely hata sikumbuki tena kiambishi ndio ki nini 😏
du
kazi ipo
 
Yaani wewe ndio umenikoroga kabisa [emoji2962] Nlikuwaga simpendi mwalimu wangu wa kiswahili alikua anaitwa Sekule kwasababu ya kufinya. Yule mwalimu hapana jamani [emoji1487] Hadi nimesikia maumivu ya vifinyo vyake upya. Basi na somo nkalichukia completely hata sikumbuki tena kiambishi ndio ki nini [emoji57]
daah pole sana kiongozi.

tatizo kuna walimu hawajitambui namna wanavyoweza kuathiri maisha ya wanafunzi kwa matendo yao tu.
 
maneno kama vile mhanga ,mwathirika ,rindima na zizima huwa mara nyingi yanatumika ndivyo sivyo.
 
Sipo nyumbani sasa hivi. Nikirudi nitakuwekea picha ya ukurasa yenye neno ‘onyesha’ na fasıli yake toka kamusi tatu tofauti zilizochapiswa na taasisi tofauti.

Ni vigumu sana mimi kukubali kwamba, wataalamu tofauti wa lugha ya Kiswahili, kutoka taasisi tofauti tofauti, wote wakosee katika kuliweka hilo neno kwenye kamusi walizozichapisha na kuzihariri.

Uzuri wa hizi kamusi, huwa zinachapisha majina ya wataalamu waliohusika katika kuzitengeneza.

Nitakuwekea picha ya kurasa zenye majina yao.

Ni watu wenye shahada za juu za lugha ya Kiswahili. Ni watu waliofanya tafiti na kuandika juu ya lugha ya Kiswahili.

Kwa ufupi, ni wataalamu wa lugha ya Kiswahili. Hivyo, ni watu ambao wanatambulika kama mamlaka katika fani zao.

Wataalamu wa Kiswahili kutoka chuo kikuu cha Oxford, kutoka chuo kikuu cha Nairobi, kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam, wote hawa wakosee katika kuliweka kwenye kamusi hilo neno?

Au siku hizi kamusi siyo kitabu cha mamlaka na marejeo katika kutafuta fasili na maana za maneno?

Anyway, nitarudi na screenshots. Ngoja nimalizie kubeba boksi kwanza.
Shukran Wakili Msomi Ngabu, hebu tunaomba utuwekee hapa hizo picha tujifunze zaidi.

Lakini pia nikutonye sikio kwamba, hata watu wenye elimu za juu sana wanaweza kufanya makosa ya kijinga sana mpaka ukashangaa.

Ninaheshimu elimu zao na kwa kweli ninakiri ni watu manguli mno wa Lugha, lakini makosa ya kimaskhara kwenye kazi zao ni jambo la kutarajia kwa wakati mwingi.

Hao oxford nadhani wananakili taarifa kutoka TUKI na taasisi zingine za elimu ya Kiswahili na kuzifanyia uhariri kidogo, kwahiyo kuna uwezekano mkubwa wa kubeba na makosa yaliyomo.
 
Naomba niwe tofauti kidogo nanyi.
Lugha yoyote huwa inabadilika over time. Old English haifanani na kiingereza tunachoongea leo. Sawa na Kiswahili cha zamani. Ukimfufua mtu aliyekufa mwaka 1970 leo mzungumze Kiswahili hamtaelewana.

Kufanikiwa.....kujipata, yote ni maneno ya Kiswahili, na lugha ni sauti za nasibu, kama tunaelewana na ikakubalika ndio basi unakuwa msamiati mpya. Shida iko wapi? Ndio maana kuna maneno mapya yanazuka kama vile UNYAMA SANA, MUKIDE........

Unataka tuongee lugha za uandishi? Kama vile mzungu akiongea Kiswahili, yeye anaongea cha kujifunza kwenye vitabu.
 
Kwa utafiti wangu mdogo hakujawahi kutokea matumizi mabovu ya lugha ya kiswahili kama muda huu tulionao.

Kibaya zaidi hata baadhi ya vyombo vya habari vikubwa vinashiriki dhambi hii.

Maneno mazuri ya kiswahili yamepindishwa kiasi inaleta kichefuchefu hata kusikiliza. Hapa nitaweka baadhi ya maneno.

Alikuwa = alikua
Kwa hiyo = ko
Baadhi = baazi
kufanikiwa = kujipata
sasa = saivi
Ndio hivyo = ndoivo
Ndio nini = ndonini
serikali = serekali/selekale
yaani = yani
mtaa = kitaa/kitaani
kwa sababu = co

Pasipo kuchukuliwa hatua za makusudi lugha hii inaelekea kupotea.

Chanzo kikuu cha haya ni uholela wa vyombo vya habari hasa habari za mtandaoni.

Nashauri mambo makubwa mawili yafanyike kwa haraka.

Kuwe na takwa la lazima kwa waleta habari kwa jamii wote kuwa na ufaulu mzuri wa lugha hii

vyombo vya habari vyote yaani vya kawaida na mitandaoni lazima visajiliwe kwanza na mamlaka za kiserikali kabla ya kuanza kupeleka habari yoyote kwa jamii.

Tuungane pamoja kuinusuru tunu yetu kuu ya lugha ya kiswahili
Bongo fleva pia inachangia sana kuua lugha ya taifa
 
Kwakweri habali hii inakela sana sipendi kiswahiri kikichezewa hivyo ndo mahana najitorea kufundisha kiswahiri
 
Shukran Wakili Msomi Ngabu, hebu tunaomba utuwekee hapa hizo picha tujifunze zaidi.

Lakini pia nikutonye sikio kwamba, hata watu wenye elimu za juu sana wanaweza kufanya makosa ya kijinga sana mpaka ukashangaa.

Ninaheshimu elimu zao na kwa kweli ninakiri ni watu manguli mno wa Lugha, lakini makosa ya kimaskhara kwenye kazi zao ni jambo la kutarajia kwa wakati mwingi.

Hao oxford nadhani wananakili taarifa kutoka TUKI na taasisi zingine za elimu ya Kiswahili na kuzifanyia uhariri kidogo, kwahiyo kuna uwezekano mkubwa wa kubeba na makosa yaliyomo.
Dah! Kutoka mbeba maboksi mpaka wakili msomi! Umenipendelea sana. Usomi huo mi mbeba maboksi niutoe wapi? 😀

Hata hivyo, ahadi ni deni. Nimechoka kama mbwa, lakini naamini katika kutimiza ahadi.

Haya, twende kazi;

Kama nilivyosema hapo awali, maneno yote mawili, ‘onesha’ na ‘onyesha’, ni sahihi.

Neno sahihi katika kuelezea utumikaji wa hayo maneno ni ‘kibadala’ au ‘vibadala’. Kwa kimombo nadhani ni ‘alternate’.

Kama picha ya sehemu ya ukurasa inavyoonyesha hapo chini, kibadala ni moja kati ya maneno mawili au zaidi yanayotofautiana kidogo kwenye maandishi au matamashi, lakini yanakuwa na maana sawa; onyesha/ onesha. Na unakumbuka niliongelea mambo ya lahaja? Hata wao watu wa TATAKI wamelizungumzia hilo [2009 walibadili jina kutoka TUKI]. TATAKI ni Taasisi ya Taaluma za Kiswahili.

IMG_6309.jpeg


Uzuri wa hizi kamusi za siku hizi, huwa zina maelezo mazuri sana kuhusu masuala ya lugha.

Kwa mfano, moja ya hizi kamusi nilizonazo ina orodha kabisa ya vibadala vya maneno na mojawapo ya hayo maneno ni ‘onyesha’ na ‘onesha’.

IMG_6312.jpeg


Huu hapa ukurasa yaliyopo hayo maneno.

IMG_6313.jpeg


Hapa chini ni kipande cha ukurasa wa kamusi ya Kiswahili sanifu tu. Yaani Kiswahili peke yake.

Angalia hayo maneno ‘onesho’ na ‘onesha’ utaona yakifuatiwa na neno ‘pia’ “onyesho “ na “onyesha”.

IMG_6311.jpeg


Hiyo’pia’ maana yake ni kwamba hicho kibadala cha hilo neno, nacho ni sahihi pia!

Tukienda kwenye kamusi ya Kiingereza.- Kiswahili, neno ‘show’ wao wamelitafsiri kama ‘onyesho’.

IMG_6305.jpeg


Hii hapa orodha ya watu waliohusika kuzitengeneza hizi kamusi. Wachache kati yao nafahamiana nao. Ni watu wanaoaminika kwa uwezo wao kwenye fani yao.

IMG_6307.jpeg


Haya bana, baadaye. Nimechoka kama mbwa koko leo.

✌️
 
Dah! Kutoka mbeba maboksi mpaka wakili msomi! Umenipendelea sana. Usomi huo mi mbeba maboksi niutoe wapi? 😀

Hata hivyo, ahadi ni deni. Nimechoka kama mbwa, lakini naamini katika kutimiza ahadi.

Haya, twende kazi;

Kama nilivyosema hapo awali, maneno yote mawili, ‘onesha’ na ‘onyesha’, ni sahihi.

Neno sahihi katika kuelezea utumikaji wa hayo maneno ni ‘kibadala’ au ‘vibadala’. Kwa kimombo nadhani ni ‘alternate’.

Kama picha ya sehemu ya ukurasa inavyoonyesha hapo chini, kibadala ni moja kati ya maneno mawili au zaidi yanayotofautiana kidogo kwenye maandishi au matamashi, lakini yanakuwa na maana sawa; onyesha/ onesha. Na unakumbuka niliongelea mambo ya lahaja? Hata wao watu wa TATAKI wamelizungumzia hilo [2009 walibadili jina kutoka TUKI]. TATAKI ni Taasisi ya Taaluma za Kiswahili.

View attachment 2967852

Uzuri wa hizi kamusi za siku hizi, huwa zina maelezo mazuri sana kuhusu masuala ya lugha.

Kwa mfano, moja ya hizi kamusi nilizonazo ina orodha kabisa ya vibadala vya maneno na mojawapo ya hayo maneno ni ‘onyesha’ na ‘onesha’.

View attachment 2967856

Huu hapa ukurasa yaliyopo hayo maneno.

View attachment 2967857

Hapa chini ni kipande cha ukurasa wa kamusi ya Kiswahili sanifu tu. Yaani Kiswahili peke yake.

Angalia hayo maneno ‘onesho’ na ‘onesha’ utaona yakifuatiwa na neno ‘pia’ “onyesho “ na “onyesha”.

View attachment 2967860

Hiyo’pia’ maana yake ni kwamba hicho kibadala cha hilo neno, nacho ni sahihi pia!

Tukienda kwenye kamusi ya Kiingereza.- Kiswahili, neno ‘show’ wao wamelitafsiri kama ‘onyesho’.

View attachment 2967870

Hii hapa orodha ya watu waliohusika kuzitengeneza hizi kamusi. Wachache kati yao nafahamiana nao. Ni watu wanaoaminika kwa uwezo wao kwenye fani yao.

View attachment 2967871

Haya bana, baadaye. Nimechoka kama mbwa koko leo.

✌️
Wakili Msomi Ngabu umeupiga mwingi mno hapa, ndio maana nimekutunuku uwakili bila kupitia mafunzo ya Law School.

Unastahili tunu ya uwakili japokuwa hii si tiketi au garantii ya wewe kuacha kubeba maboksi. Endelea. Chakula ni muhimu zaidi kuliko uwakili.

Nikirejea kwenye ujumbe wako hapa, niseme tu kwamba, hichi kibadala cha ONESHA vis-a-vis ONYESHA ni kibadala TATANISHI mno kwenye akili yangu na kiukweli kinanitusi ujuzi wangu wa Lugha.

Hawa manguli wa lugha siwapingi kwenye hili na ninawaheshimu mno, lakini wameninyong'onyeza na kunisikitisha mpaka najiuliza inawezekanaje kosa la kimaskhara kama hili likachukuliwa na kudhaniwa ni Kiswahili sanifu ati kwa msingi kuwa ni KIBADALA!

Kwa kutumia msingi wa maelezo yao ya utangulizi wa maana ya KIBADALA, nimegundua kuwa wameridhia usanifu wa neno ONYESHA kwa sababu linatumika sana miongoni mwa watu kama LAHAJA MBADALA.

Hii ni hoja fikirishi na yenye utata, kwa sababu watu wengi wanaotumia Lugha hawana weledi au upeo, na wanaweza kutengeneza maneno yao mabovu yasiyo na usahihi wa kisarufi au usanifu.

Kuyachukua maneno ya hawa watu wasio na upeo wa Lugha na kuyaingiza rasmi katika Kiswahili sanifu ni kututusi sisi wenye ujuzi na umahiri wa Lugha.

Lakini nitasema nini? Manguli wameshaamua.

Nimeridhika kinyonge sana. Kama kungekuwa kuna Baraza la Kukata rufaa kwa mambo yanayohusu usanifu wa Lugha, ningekata rufaa na kuomba hili neno LITENGULIWE au lihakikiwe upya usahihi wake.
 
Back
Top Bottom