KISWAHILI: Naomba maana ya maneno haya...

KISWAHILI: Naomba maana ya maneno haya...

Nadhani hilo neno kwa kiingereza ni provided that-ilhali kwamba.Hata hivyo nitafanya utafiti kwenye vyanzo vyangu na kujua linatunikeje katika muktadha mbalimbali
 
Samahani, lakini nadhani kwamba "provided that" ni "ilimradi" (au 'alimradi'), "mradi", "isipokuwa kama". Maana ya "ilhali" ni "whereas".
 
Samahani, lakini nadhani kwamba "provided that" ni "ilimradi" (au 'alimradi'), "mradi", "isipokuwa kama". Maana ya "ilhali" ni "whereas".
wee umetuibia turudishie chenji whereas maana yake Kwa kuwa na sio ilhali.
 
wee umetuibia
!!!!!!!!!!
Nimekuibia nini?
Kwa nini unatumia lugha hii?

turudishie chenji whereas maana yake Kwa kuwa na sio ilhali.

ilhali* ku whereas. (Kar)[Kamusi ya Kiswahili-Kiingereza, TUKI]

ilhali kiunganishi neno la kuonyesha kinyume cha mambo; na hali; ingawa: Umeacha mpunga nje peke yake ilhali unajua kuwa kuna kuku watakakula [Kamusi ya shule za Msingi, Oxford University Press]

ilhali ku neno lionyeshalo hali ya kinyume cha mambo k.v. katika kulalamika; wakati: Umemwacha mtoto afanye atakavyo ilhali unajua anachezea moto, hali [Kamusi ya ya Kiswahili Sanifu, Oxford University Press]

ilihali: wakati; kumbe.
Mimi nilikuwa nikidhani hupo nyumbani, ilihali ulikuwa umelala [Kamusi ya maana na matumizi, Salim K. Bakhressa, OUP]

whereas conj 1 (fml) in contrast or comparison with the fact that; while: <He earns &#163;10 000 a year whereas she gets at least &#163;30 000. We thought she was rather arrogant, whereas in fact she was just very shy 2 (esp law) (at the beginning of sentences in official documents) taking into consideration the fact that [Advanced Learner's Dictionary, OUP]

Tafadhali tusitumie matusi.
 
Nino,punguza munkali jf ni sehemu ya vimbwanga pia ukiachilia majibu tunayopeana.Niliposema umetuibia sikumaanisha mwizi,ni moja ya lugha ya vijana ya kudadisi jibu au hali fulani ili kupata maelezo(chenji) zaidi toka kwa muhusika.au tukisema hapa turudishie kiingilio chetu tuna maana hatujakubaliana na wewe tushawishi zaidi.Huko ni kukua kwa lugha na tamathali za semi.Labda basi tufanye neno ilhali nalo ni kwakuwa manaake katika tafisiri nyingi zilifofanyika ikiwamo tafsiri ya katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania na mikataba mingi neno whereas linatafsiriwa kama KWAKUWA.Na ndio maana katiba kwenye utangulizi imeanza na neno KWAKUWA SISI yuaani WHEREAS WE, the people of ....Ok, hivyo ndivyo navyoelewa japo bado utafiti haujafungwa.
 
Nimewahi kusikia na kutumia lugha ya vijana, lakini ninazoea kujali muktadha, mazingira na uhusiano baina ya watu.

Tena, kwa bahati mbaya, ninazoea kutumia na kusikia maneno kama "tafadhali [Tafadhali punguza, kwa mfano], samahani, nk"...

Kuhusu maneno "ilhali" na "whereas" sina zaidi la kusema nilitoa mifano (hata visawe) ya kutosha: "ilhali" si "kwa kuwa", na anayetazama kamusi za Kiingereza (ingetosha kusoma dondoo yangu!) atagundua kwamba kwenye Katiba ya Tanzania "Whereas=Kwa kuwa" ni sahihi kabisa, ila kwenye lugha A=B si sawa na B=A.
 
Nino,punguza munkali jf ni sehemu ya vimbwanga pia ukiachilia majibu tunayopeana.Niliposema umetuibia sikumaanisha mwizi,ni moja ya lugha ya vijana ya kudadisi jibu au hali fulani ili kupata maelezo(chenji) zaidi toka kwa muhusika.au tukisema hapa turudishie kiingilio chetu tuna maana hatujakubaliana na wewe tushawishi zaidi.Huko ni kukua kwa lugha na tamathali za semi.Labda basi tufanye neno ilhali nalo ni kwakuwa manaake katika tafisiri nyingi zilifofanyika ikiwamo tafsiri ya katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania na mikataba mingi neno whereas linatafsiriwa kama KWAKUWA.Na ndio maana katiba kwenye utangulizi imeanza na neno KWAKUWA SISI yuaani WHEREAS WE, the people of ....Ok, hivyo ndivyo navyoelewa japo bado utafiti haujafungwa.
Tafadhali chunga unapobadili neno linavyoandikwa, kwa mfano umeandika "munkali", hilo si neno sahihi au umelikosea spelling kwa hiyo halileti maana yoyote. Nadhani ulitaka kutumia neno munkar.

siku hizi, watu wengi wamekuwa wakiki-haribu kiswahili chetu kwa kubadili penye neno la kutumia "r" huweka "l" na hiyo inachafuwa kiswahili kiongewapo au kiandikwapo.
 
Samahani, Zomba, ninavyojua mimi "munkari" ni kisawe cha "kitu kibaya, kitendo haramu, jambo ovu". Lakini watu kadhaa hutumia "munkali" kama kisawe cha "hasira", tazama hapa: Mzee Cheche alisema kwa ghadhabu,kitendo kile kilimpandisha hasira Mode na kujikuta akimvaa Jose,ambaye hakukubali wakaanza kupigana. Ilibidi mzee Cheche awe mpole ili kupunguza munkali wa Mode
"Mode ninyi wote ni wapenzi wangu usiwe na hofu utapata kile ulichokikosa"
http://maisha.co.tz/kurasa.php?soma=sukari&habariNamba=641

Unaonaje?

Mwishowe, uliandika "... hiyo inachafuwa...". Je, ulitaka kuandika "inachafua"?

Asante sana.
 
Samahani, Zomba, ninavyojua mimi "munkari" ni kisawe cha "kitu kibaya, kitendo haramu, jambo ovu". Lakini watu kadhaa hutumia "munkali" kama kisawe cha "hasira", tazama hapa: Mzee Cheche alisema kwa ghadhabu,kitendo kile kilimpandisha hasira Mode na kujikuta akimvaa Jose,ambaye hakukubali wakaanza kupigana. Ilibidi mzee Cheche awe mpole ili kupunguza munkali wa Mode
"Mode ninyi wote ni wapenzi wangu usiwe na hofu utapata kile ulichokikosa"
http://maisha.co.tz/kurasa.php?soma=sukari&habariNamba=641

Unaonaje?

Mwishowe, uliandika "... hiyo inachafuwa...". Je, ulitaka kuandika "inachafua"?

Asante sana.
Bila samahani, kwani kiswahili ni lugha inayokuwa kwa haraka sana kwa uchanga wake na kusambaa kwake, inawezekana neno "munkali" lipo nami silijuwi. Nilijuwalo mimi ni munkar(i).

Lakini bado hoja ya kuwa wengi hubadili "r" ikawa "l" ipo pale pale, inawezekana pia hiyo "munkali" ni katika huko kubadili hizo "r" lakini hapo likawa ni neno linaloleta maana nyingine kama ulivyofafanuwa (wala sikusudii fafanua).

kuhusu "inachafuwa" au "inachafua", ni makusudio yangu kutumia "inachafuwa" na wala sikuwa na kusudio la kutumia "inachafua"
 
Hm.
Ninavyojua mimi "-juwa", "-fafanuwa", "-chafuwa" si Kiswahili sanifu. Wataalamu [k.m. TUKI, BAKITA] hutumia "-jua", "-fafanua", "-chafua".

Nakushukuru.
 
Bwana mmoja hapa kasema eti thread ni utepe lakini la thread ni Uzi na utepe ni 'Tape', n kwa issue ya thread kama hizi za JF naonelea ziitwe 'nyuzi' kama ingewezekana. na mimi naulizaje Matongo kwa Kiingereza yaitwaje.....wanugu ebu niambieni....KTY (kwa taarifa yenu) nchi jirani kenya Nugu ni aina ya sokwe....lol
 
Bwana mmoja hapa kasema eti thread ni utepe lakini la thread ni Uzi na utepe ni 'Tape', n kwa issue ya thread kama hizi za JF naonelea ziitwe 'nyuzi' kama ingewezekana. na mimi naulizaje Matongo kwa Kiingereza yaitwaje.....wanugu ebu niambieni....KTY (kwa taarifa yenu) nchi jirani kenya Nugu ni aina ya sokwe....lol

Wakuu naomba kuwasilisha.Kutegema na kama uko Uropa ama Marekani neno matongo huitwa Goop,Crud au Rheum (medical terminology). Wengine huita matongo Crystals...wamarekani hawa!
 
Millipede nadhani huitwa jongoo naye centipede huitwa ninii?
 
tandu Ndo Yule Mwenye Miguu Mingi Na Ku-sting Kama Nge?
 
Back
Top Bottom