Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
- Thread starter
- #221
22. Ibrahim alizaliwa Nuhu bado akiwa hai. Nuhu alikufa Ibrahim akiwa na Miaka 55
Hivyo hadithi zote za tangu Adamu Ibrahim alizipata Kwa Babu yake, Nuhu.
Robert Heriel Mtibeli ilikuwaje Baba yake Ibrahimu mzee Tera kuwa mwabudu miungu na wakati amekekuwa chini ya Nuhu na Mwanaye Ibrahimu kuwa mcha Mungu wa kweli?
Ukisoma kitabu cha Jasher kinaeleza kuwa Tera alikuwa moja ya watumishi wa Ikulu ya Nimrodi(mjukuu wa Hamu) ambaye alikuwa mfalme wakati huo.
Tera alikuwa mchonga vinyago vya miungu hapo Uru. Naye alikuwa anatumikia miungu aliyoichonga.
Ibrahim alienda kwa Nuhu Babu wa Babu zake sio kwa kupenda bali ni baada ya tukio la usiku wa kuzaliwa Ibrahim ambapo tukio la kuogofya lilitokea na wanajimu wakamshauri Nimrodi amuue mtoto wa Tera kwani mtoto huyo nyota yake ilionyesha kuwa atakuwa mwiba kwenye utawala wa Nimrodi hapo baadaye.
Tera akampeleka mtoto wa mwingine wa mfanyakazi wake badala ya Ibrahim na Ibrahim akaenda kumficha mapangoni kwa zaidi ya miaka 10.
Alipofikisha miaka hiyo 10 ndio wakampeleka kwa Nuhu kumficha.
Nuhu alikuwa akiishi na Shem mtoto wake na babu wa kina Ibrahim.