Kitabu kipya: Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania

Kitabu kipya: Dola, Kanisa na Tatizo la Udini Tanzania

''Ukimuuliza huyu mchochezi kwamba kati ya wazee wake hapo mtaa wa Gerezani amtaje shehe hata moja aliyetiwa kash kash au kuswekwa korokoroni na Wakoloni kwa uanaharakati wa kudai/kupigania uhuru wa Tanganyika ama na Wajerumani au Waingereza atabaki tu mdomo wazi!''
(Mag3)

Ndugu zangu,
Tuko 7K and counting...

Maswali hata kama yataambatana na lugha zisizopendeza huwa na faida yake.
Faida inakuja pale swali au maswali yanapokufanya ugeuze shingo kuangalia nyuma.

Babu yangu Salum Abdallah aliwahangaisha sana Waingereza wakati wa ukoloni lakini hawakumkamata na kumfunga.

Salum Abdallah alionja adha za jela mwaka wa 1964 katika Tanganyika huru.

Alifungwa Uyui Prison, Tabora pamoja na baadhi ya masheikh maarufu kati ya hao masheikh alikuwa Sheikh Jumanne Biasi.

Kama nilivyokwishaeleza Salum Abdallah aliongoza migomo mitatu ya wafanyakazi wa reli ambayo ilienea nchi nzima na kuwa ''general strike,'' mwaka wa 1947, 1949 na 1960 na huu mgomo wa 1960 ndiyo uliokuwa mkubwa kupita yote kwani ulidumu siku 82.

Miezi mitatu treni, meli na mabasi ya Tanganyika Railways vyote vilisimama.

Salum Abdallah alikuwa Rais na Christopher Kassanga Tumbo Katibu wa Tanganyika Railways African Union (TRAU).

Vipi waliweza kufanikisha mgomo huu?

Waliweza kufanikisha kwanza kwa kuwa na nidhamu ya hali ya juu ndani ya TRAU na pili kutokana na misaada ya fedha waliyopata kutoka Ujerumani ya Mashariki na kutoka kwa chama cha wafanyakazi wa reli Uingereza.

Fedha hizi ziliwawezesha kununua chakula na mahitaji muhimu kwa wafanyakazi ambao waligawiwa kwa kutumia kadi - chakula, mafuta ya kupikia, mafuta ya taa, viberiti nk.

Ilikuwa imebaki miezi michache Tanganyika ipate serikali ya madaraka ya ndani.

Ingawa TANU ilikuwa inaunga mkono harakati hizi lakini inaelekea Mwalimu Nyerere aliingiwa na hofu.

1578459701756.png

Kulia Christopher Kassanga Tumbo, Salum Abdallah na viongozi wengine wa TRAU
Nyerere alijua kuwa uhuru utakapopatikana mwaka wa 1961 ni lazima serikali yake itabidi ikabiliane na viongozi wa mfano wa Salum Abdallah na Kassanga Tumbo, viongozi ambao walikuwa wanapendwa na kusikilizwa na wananchi wafanyakazi.

Alipata hofu viongozi hawa watampa shida kama hii waliyokuwa wanaipa serikali ya Malkia.

Kukifanya kisa kirefu kuwa kifupi ni kuwa Salum Abdallah na viongozi wengine wa wafanyakazi walikamatwa na kuwekwa kizuizini mwaka wa 1964 mara baada maasi ya wanajeshi ili serikali ipate nafasi ya kuvunja vyama huru cha wafanyakazi na kuunda chama kipya kimoja NUTA kitakachokuwa chini ya TANU na serikali.

Harakati hizi hazijahifadhiwa katika historia ya uhuru wa Tanganyika wala katika historia ya vyama vya wafanyakazi wa Tanganyika.

Alfred Tandau ameandika kitabu, ''Historia ya Kuundwa Kwa TFL (1955-1962) na kuanzishwa kwa NUTA,'' (Dar es Salaam,1964) si babu yangu wala Kassanga Tumbo viongozi waliounda chama kilichokuja kuwa na nguvu na kikapigana bega kwa bega na TANU kudai uhuru wa Tanganyika wametajwa katika kitabu kile.

Nilikuwa nawashangaza sana walimu wangu Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam nilipokuwa nawaambia kuwa Tandau hajui historia ya vyama vya wafanyakazi aliyoandika katika kitabu chake na walipokuwa wananiomba ushahidi jibu langu lilikuwa rahisi na jepesi.

Nilikuwa nikisema babu yangu Salum Abdallah ni sehemu ya historia hiyo na historia ya TANU na juhudi za kudai uhuru wa Tanganyika.

Salum Abdallah alikuwa Mmanyema baba yake aliingia Tanganyika kama askari katika jeshi la Wajerumani.

Naomba ushauri wenu wasomaji wangu.

Nimfute Salum Abdallah katika historia ya uhuru wa Tanganyika kwa kuwa asili ya baba yake ni Belgian Congo?



 
''Ukimuuliza huyu mchochezi kwamba kati ya wazee wake hapo mtaa wa Gerezani amtaje shehe hata moja aliyetiwa kash kash au kuswekwa korokoroni na Wakoloni kwa uanaharakati wa kudai/kupigania uhuru wa Tanganyika ama na Wajerumani au Waingereza atabaki tu mdomo wazi!''
(Mag3)

Ndugu zangu,
Tuko 7K and counting...

Maswali hata kama yataambatana na lugha zisizopendeza huwa na faida yake.
Faida inakuja pale swali au maswali yanapokufanya ugeuze shingo kuangalia nyuma.

Babu yangu Salum Abdallah aliwahangaisha sana Waingereza wakati wa ukoloni lakini hawakumkamata na kumfunga.

Salum Abdallah alionja adha za jela mwaka wa 1964 katika Tanganyika huru.

Alifungwa Uyui Prison, Tabora pamoja na baadhi ya masheikh maarufu kati ya hao masheikh alikuwa Sheikh Jumanne Biasi.

Kama nilivyokwishaeleza Salum Abdallah aliongoza migomo mitatu ya wafanyakazi wa reli ambayo ilienea nchi nzima na kuwa ''general strike,'' mwaka wa 1947, 1949 na 1960 na huu mgomo wa 1960 ndiyo uliokuwa mkubwa kupita yote kwani ulidumu siku 82.

Miezi mitatu treni, meli na mabasi ya Tanganyika Railways vyote vilisimama.

Salum Abdallah alikuwa Rais na Christopher Kassanga Tumbo Katibu wa Tanganyika Railways African Union (TRAU).

Vipi waliweza kufanikisha mgomo huu?

Waliweza kufanikisha kwanza kwa kuwa na nidhamu ya hali ya juu ndani ya TRAU na pili kutokana na misaada ya fedha waliyopata kutoka Ujerumani ya Mashariki na kutoka kwa chama cha wafanyakazi wa reli Uingereza.

Fedha hizi ziliwawezesha kununua chakula na mahitaji muhimu kwa wafanyakazi ambao waligawiwa kwa kutumia kadi - chakula, mafuta ya kupikia, mafuta ya taa, viberiti nk.

Ilikuwa imebaki miezi michache Tanganyika ipate serikali ya madaraka ya ndani.

Ingawa TANU ilikuwa inaunga mkono harakati hizi lakini inaelekea Mwalimu Nyerere aliingiwa na hofu.

View attachment 1315543
Kulia Christopher Kassanga Tumbo, Salum Abdallah na viongozi wengine wa TRAU
Nyerere alijua kuwa uhuru utakapopatikana mwaka wa 1961 ni lazima serikali yake itabidi ikabiliane na viongozi wa mfano wa Salum Abdallah na Kassanga Tumbo, viongozi ambao walikuwa wanapendwa na kusikilizwa na wananchi wafanyakazi.

Alipata hofu viongozi hawa watampa shida kama hii waliyokuwa wanaipa serikali ya Malkia.

Kukifanya kisa kirefu kuwa kifupi ni kuwa Salum Abdallah na viongozi wengine wa wafanyakazi walikamatwa na kuwekwa kizuizini mwaka wa 1964 mara baada maasi ya wanajeshi ili serikali ipate nafasi ya kuvunja vyama huru cha wafanyakazi na kuunda chama kipya kimoja NUTA kitakachokuwa chini ya TANU na serikali.

Harakati hizi hazijahifadhiwa katika historia ya uhuru wa Tanganyika wala katika historia ya vyama vya wafanyakazi wa Tanganyika.

Alfred Tandau ameandika kitabu, ''Historia ya Kuundwa Kwa TFL (1955-1962) na kuanzishwa kwa NUTA,'' (Dar es Salaam,1964) si babu yangu wala Kassanga Tumbo viongozi waliounda chama kilichokuja kuwa na nguvu na kikapigana bega kwa bega na TANU kudai uhuru wa Tanganyika wametajwa katika kitabu kile.

Nilikuwa nawashangaza sana walimu wangu Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam nilipokuwa nawaambia kuwa Tandau hajui historia ya vyama vya wafanyakazi aliyoandika katika kitabu chake na walipokuwa wananiomba ushahidi jibu langu lilikuwa rahisi na jepesi.

Nilikuwa nikisema babu yangu Salum Abdallah ni sehemu ya historia hiyo na historia ya TANU na juhudi za kudai uhuru wa Tanganyika.

Salum Abdallah alikuwa Mmanyema baba yake aliingia Tanganyika kama askari katika jeshi la Wajerumani.

Naomba ushauri wenu wasomaji wangu.

Nimfute Salum Abdallah katika historia ya uhuru wa Tanganyika kwa kuwa asili ya baba yake ni Belgian Congo?



Ndugu zanguni mbona barza imekuwa kimya?

Au mmechoshwa na historia ya Wazulu na Wamanyema?

Huenda hiyo hapo chini mmeshaisoma lakini hii barza kila siku inapokea wanachama wapya kwa hiyo so vibaya kujirudia:

ABDUL SYKES NA KAPENGURIA SIX 1950 TAA/TANU NA MAU MAU 1950s

Hawa Kapenguria Six ni akina nani na kwa nini walipewa jina hilo?

Kapenguria Six ni wazalendo sita wa KAU waliofungwa na Waingereza kwa shutuma za kunyanyua silaha dhidi ya ukoloni.

Wazalendo hawa ni Jomo Kenyatta, Bildad Kaggia, Kung'u Karumba, Fred Kubai, Paul Ngei, na Achieng' Oneko.

Kapenguria ni jina la mji ambamo wazalendo hawa walihukumiwa kifungo cha miaka saba.

Hapo chini naweka historia ya nyakati hizi za Mau Mau Kenya na uhusiano uliokuwapo kati viongozi wa TAA na KAU.

Mkutano wa Abdul Sykes 1950 na ile timu nzima ya Kapenguria Six yaani Jomo Kenyatta, Bildad Kaggia, Kung'u Karumba, Fred Kubai, Paul Ngei, na Achieng' Oneko alinihadithia Ahmed Rashad Ali ingawa kwenye taarifa hii limeongezeka jina la Peter Mbiu Koinange.

Laiti habari hii angelinieleza mtu mwingine yeyote mimi nisingeitia katika kitabu cha Abdul Sykes kwani kwangu lilikuwa jambo kubwa sana kwani wakati ule Abdul alikuwa kijana mdogo wa miaka 26 na Jomo Kenyatta sifa zake na Mau Mau zilikuwa kubwa sana.

Hili lingenitia wasiwasi wa ukweli wa historia ile.

Nilimuamini Ahmed Rashad Ali kwani alinihadithia mengi katika maisha ya Abdul Sykes ambae walijuana mwaka wa 1939 hapo Arab Association Ring Street (sasa Jamhuri Street) walipokutana wakati wa Bank Holiday wote wawili wakiwa watoto wadogo wameongozana na wajomba zao.

Jim Brennan mwanahistoria bingwa kutoka University of Illinois, Champaign aliponirushia taarifa hiyohapo juu ya Special Branch ya 1953 kutoka majalada ya Waingereza inayothibitisha mkutano wa Abdul Sykes na Kenyatta Nairobi 1950 nilinyanyua mikono juu nikamshukuru Allah kwa kusadikisha ukweli wa Ahmed Rashad na kunisadikisha mimi mbele ya wasomaji wangu kuwa Abdul Sykes alikuwa
mwanasiasa hodari aliyezitoa siasa za TAA nje ya mipaka ya Tanganyika.

Haya hapo chini ndiyo niliyoandika katika kitabu cha Abdul Sykes kuhusu mkutano wake na Kapenguria Six:

''Mwaka 1950, Abdulwahid alisafiri kwenda Nairobi kukutana na Jomo Kenyatta ili kuanzisha uhusiano na Kenya African Union (KAU).

Abdulwahid alifunga safari hii wakati wa mashindano ya kandanda ya Kombe la Gossage.
'
Haya yalikuwa mashindano ya kila mwaka ambayo nchi tatu za Afrika ya Mashariki pamoja na Zanzibar zilikuwa zikishiriki.

Huenda Abdulwahid alichagua wakati huu mahsusi ili kuficha dhamiri ya safari yake.

Kama mtu labda angetaka kujua sababu ya safari yake ingewezekana kwa urahisi kabisa kuelezwa kuwa alisafiri kwenda Nairobi kutazama mashindano ya Gossage.

Abdulwahid alifikia Railway Hotel na alikwenda kuonana na Kenyatta usiku akifuatana na rafiki yake mpenzi kutoka Zanzibar, mmoja wa wacheza mpira katika timu ya Zanzibar.

Abdulwahid na rafiki yake walikwenda nje kidogo ya Nairobi kwenye nyumba moja iliyokuwa imegubikwa na giza na kuzungukwa na walinzi wa Mau Mau.

Abdulwahid alikuwa anatarajiwa.

Kenyatta alipofahamishwa kuwa Abdulwahid amefika na yupo nje, alitoka kumlaki.

Kenyatta alikuwa akimfahamu Ally Sykes tangu mwaka 1946.

Inawezekana kuwa kazi ya Abdulwahid ilirahisishwa na uhusiano huu wa Kenyatta na mdogo wake.

Mzanzibari huyu aliyemsindikiza Abdulwahid alikutana na Kenyatta na wakapeana mikono.

Baada ya kutambulishwa Kenyatta, Abdulwahid, Fred Kubai, Bildad Kaggia na Kungu Karumba waliingia kwenye chumba kingine ambako mkutano ulifanyika. Mzanzibari, rafiki yake Abdulwahid alibakia nje na mlinzi.

Huyu Mzanzibari ni Ahmed Rashad Ali ambae alinomba nisitaje jina lake.

Ahmed Rashad sasa ni marehemu.

Minongíono ilikuwa ikisikika kutoka Kanda ya Ziwa kuwa kiongozi wa wapiganaji wa Mau Mau, Dedan Kimathi alikuwa anaonekana mjini Mwanza. Wakati ule pale Mwanza
kulikuwa na Wakikuyu wengi wakifanya biashara sokoni.

Ilivumishwa kuwa Dedan Kimathi alikuwa akiwasiliana na Wakikuyu wenzake waliokuwa Tanganyika na wao walikuwa wakimkusanyia fremu za baiskeli za zamani ili zitumike
kutengenezea magobole ili zitumiwe misituni dhidi ya majeshi ya Waingereza.

Mapigano yalipoonza kati ya Mau Mau na Waingereza na Wakikuyu kama 16, 000 wakiishi na kufanya kazi kaskazini ya Tanganyika. Kama tahadhari, Wakikuyu wachache walioonekana kuunga mkono Mau Mau, walikamatwa na kupelekwa Kenya ambako waliwekwa kizuizini katika kambi mbali mbali.

Uongozi wa TAA baada ya uchaguzi wa April, 1953 ulikuwa kama hivi ifuatavyo:

J. K. Nyerere, Rais, Abdulwahid Sykes, Makamu wa Rais; J. P. Kasella Bantu, Katibu Mkuu; Alexander M. Tobias na Waziri Dossa Aziz, Katibu wa pamoja wa muhtasari; Wajumbe wa Kamati: Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said
Tewa, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.

Muundo wa uongozi katika TAA unaonyesha ule mshikamano wa Afrika ya Mashariki uliokuweko wakati wa harakati za uhuru.

Wazalendo wa Kenya walichaguliwa kama viongozi wa TAA bega kwa bega na ndugu zao Watanganyika.

Dome Okochi Budohi na Patrick Aoko hawakuweza kuliepuka jicho la Special Branch.

Mara tu baada ya kuundwa kwa TANU mwaka wa 1954 wazalendo hawa wa Kenya wakakamatwa.

Kwa miezi sita walihojiwa na kuwekwa rumande Central Police Station huku wamefungwa minyororo.

Budohi na Aoko walikuwa wakifuatwa na makachero (Special Branch) toka mwaka wa 1952 baada ya hali ya hatari kutangazwa Kenya.

Dome Budohi aliponzwa na barua iliyotoka Kenya ambayo ilikamatwa na makachero.

Barua hii ilikuwa inamuhusisha Budohi na Mau Mau.
Inasemekana Budohi alisalitiwa na Mkenya mwenzake aliyeitwa Martin.

Askari waliokuwa wakiwalinda kule rumande walitoa habari kwa TANU kuwa kulikuwa na mpango wa kuwapa sumu Budohi na Aoko.

Baadaye wafungwa hawa walihamishiwa Handeni ambako kulikuwa na kambi ya kuwafunga watuhumiwa wa Mau Mau.

Baada ya TANU kuundwa ili kupunguza nguvu ya uongozi New Street Ally Sykes alipewa uhamisho kwenda Mtwara kisha ukabalishwa na kupelekwa Korogwe.

Kawawa akahamishiwa kwenda Handeni kwenye Kambi ya Mau Mau.

Kawawa alikuwa akifahamiana na wengi kati ya wafungwa wale.

Kawawa aliwaangalia wafungwa hawa kwa moyo wa huruma akijaribu kupunguza shida zao pale kambini kila alipopata mwanya wa kufanya hivyo.

Wakati Budohi na Wakenya wengine walipopita Korogwe wakati wakirudishwa Kenya kupitia Taveta, Ally Sykes, ambaye alikuwa amehamishiwa Korogwe, alikwenda hadi stesheni ya reli kuwaaga.

Watuhumiwa hawa wa Mau Mau walikuwa wametiwa katika mabehewa ya kubebea ng'ombe huku wamefungwa minyororo.

Dome Budohi na wazalendo wengine waliwekwa kizuizini kwa miaka saba."

Sent using Jamii Forums mobile app
 
''...
Nyerere alijua kuwa uhuru utakapopatikana mwaka wa 1961 ni lazima serikali yake itabidi ikabiliane na viongozi wa mfano wa Salum Abdallah na Kassanga Tumbo, viongozi ambao walikuwa wanapendwa na kusikilizwa na wananchi wafanyakazi.

Alipata hofu viongozi hawa watampa shida kama hii waliyokuwa wanaipa serikali ya Malkia.

These are your own imaginations (histohisia) which are the basis of your flawed and misleading narrations.
 
These are your own imaginations (histohisia) which are the basis of your flawed and misleading narrations.
Nanren,
Hapana tatizo ikiwa wewe unadhani kitabu nilichoandika ni hadithi za kutunga.

Wala mimi sikulaumu ila nitakueleza jambo.

Kitabu kilishtua wasomi wengi wa African History kiasi nikatiwa kwenye miradi miwili mikubwa ya Oxford University Press Nairobi na New York mmoja ukihusisha Havard.

Kitabu changu kimesababisha pia kuanzishwa mradi chini ya Prof. Issa Shivji wa kutafiti na kuandika upya historia ya TANU na historia ya Mwalimu Nyerere.

Kitabu kimependwa sana na kimechapwa mara tatu toka 1998 na mimi nimeandika vitabu saba tokea hapo.
 
Nanren,
Hapana tatizo ikiwa wewe unadhani kitabu nilichoandika ni hadithi za kutunga.

Wala mimi sikulaumu ila nitakueleza jambo.

Kitabu kilishtua wasomi wengi wa African History kiasi nikatiwa kwenye miradi miwili mikubwa ya Oxford University Press Nairobi na New York mmoja ukihusisha Havard.

Kitabu changu kimesababisha pia kuanzishwa mradi chini ya Prof. Issa Shivji wa kutafiti na kuandika upya historia ya TANU na historia ya Mwalimu Nyerere.

Kitabu kimependwa sana na kimechapwa mara tatu toka 1998 na mimi nimeandika vitabu saba tokea hapo.

Congrats.
Achievements zako kwenye uandishi haziondoi ukweli kuwa, msingi wa simulizi zako ni hisia zako binafsi.
Mfano ni hapo ulipoandika "...Nyerere alipata hofu..."
Hizo ni hisia zako tu
 
Hiki ndicho ulicho kiandika mzee M.S


1. Unasahau uislamu unawataka mpambane na imani zingine kivita (jihad) tena ni lazima.
2. Unasahau uislamu unatamka waziwazi aliye amini katika imani hiyo akitoka auwawe.
3. Unasahau uislamu una lengo la kuitawala dunia kwa namna yeyote.
4. Unasahau mimi nikitaka kumuoa binti wa kiislamu itanibidi nisilimu na ikitokea nimemvuta huyo binti kuja kwenye Ukristo basi ni mwendo wa laana na midua mibaya juu yake.
.
Mfano mzuri ni mwanamuziki Kadjanito aliyeolewa na kijana wa Kikristo na kuamua kuokoka. familia yake imemtenga hadi waleo na imemtamkia laana na kumnenea mabaya mno kisa midini ya kuletewa😢
.
Mzee M.S kwa makusudi kabisa unaamua kulipotosha hili eti uislamu haulazimishi kitu katika mambo ya imani kisa tu ni kitu unachokiamini pole sana
Mimi nimezaliwa na kukulia kwenye Uislamu hadi nilipofikisha umri wa miaka 24 ndio nikabadiri dini na kua Mkristo; ukweli ju ya dini hi, huwezi kuineza bila kufitinisha watu, huwezi pia kuineza bila kuwanenea watu uongo na hata kuwasingizia. Ukisikia mara nyingi kule kwenye nchi za Kiarabu hasa Iran, Pakistan nk eti kijana anauawa kwasababu sijui ya kubaka nk, wengi wao hua sio kweli, ujue kijana huyo huenda kabadiri dini na kua Mkristo then lazima auawe so anatafutiwa KOSA ambalo hata hakulifanya; mifano ipo mingi hata hapa kwetu, binafsi pia niliwahi hadi kusomewa Albadiri, kulaaniwa na ndugu zangu hasa baba na baadhi ya kaka zangu, nawapongeza sana dada zangu, moja kati ya dada yangu ni mke wa sheikh kabisa but alinitetea sana, wanawake kwa asili wana HURUMA sana; sasa hvi mimi na wao ni ndugu kabisa, sijui kama ni hasira zao kwisha au kwasababu nina KIPATO kidogo, that much sina HAKIKA. Huyu Mohamedi Said hanaga kitu kingine anachoweza kukifundisha kuhusu dini yake bila kupandikiza CHUKI kwa watu na ndio maana kitabu chake kinauzwa msikitini/misikitini na sio kwenye bookshops, malengo yake kwa haraka haraka ni wateja wake ni well defined, WAISLAM. Binafsi, kama dini yako haihubiri UPENDO then hiyo ni dini ya shetani sio ya Mungu, dini inayohubiri visasi na chuki, hiyo ni dini ya shetani, hahihitajiki elimu ya mbinguni kulijua hilo
 
Congrats.
Achievements zako kwenye uandishi haziondoi ukweli kuwa, msingi wa simulizi zako ni hisia zako binafsi.
Mfano ni hapo ulipoandika "...Nyerere alipata hofu..."
Hizo ni hisia zako tu
Nanren,
Hapana shida binadamu lazima tughitilafiane.

Mimi nimeona kukamatwa kwa viongozi wa vyama vya wafanyakazi na kuvifuta ili pawepo chama kimoja chini yake ni hofu lakini wewe unaona hapakuwa na hofu.

Mambo ndiyo yalivyo.

Mimi niko tofauti sana na wengi hapa barzani kwani nimeishi ndani ya historia hii ndiyo maana nimeweza kuandika histotia ya TANU na ya Mwalimu Nyerere mwenyewe na kueleza mengi ambayo yamewashangaza wengi.

Wanajiuliza huyu kayajuaje haya?
Mnapenda majibu mepesi.

Mnajiambia kuwa ni hisia.
Labda mnafarajika.

Mfano propaganda iliyokuwa imeenezwa ni kuwa hawa viongozi wa hizi ''trade unions,'' walikuwa wamekula njama na askari walioasi kupindua serikali.

Babu yangu Salum Abdallah ni mmoja katika hao waliotuhumiwa kwa hilo.
Baba yangu alihangaika sana kutaka kujua kama kweli baba yake atashitakiwa kwa kosa hilo kwani ni uhaini.

Ulikuwa uongo mtu.
Hapakuwa na njama yoyote kati ya hawa viongozi na jeshi.

Wewe hujaguswa na lolote katika historia ya si ya TANU wala chochote katika harakati za kudai uhuru.
Bila shaka mtazamo wako utakuwa tofauti sana na wangu.

Unataabika kuambiwa kuwa Mwalimu alikuwa na watu akiwaogopa.

Unataabika nikikwambia kuwa TANU ni brainchild ya Abdul Sykes nk. nk.na hiyo African Association iliyokuja kuzaa TANU iliasisiwa na baba yake mwaka wa 1929.

Siku hizi wanasema AA iliasisiwa na Cecil Matola.

Wanataka kuleta tu ushidani usiokuwa na maana na sababu ni kuwa hawamjui Kleist alikuwa mtu wa aina gani katika mji wa Dar es Salaam ya 1930s.

Mimi hubakia kucheka.

Hii ndiyo sababu historia ya TANU ilipoandikwa ikawa si historia ya TANU.
Hofu iliwafanya waandishi wawakwepe baadhi ya wazalendo kama Salum Abdallah.
 
Mimi nimezaliwa na kukulia kwenye Uislamu hadi nilipofikisha umri wa miaka 24 ndio nikabadiri dini na kua Mkristo; ukweli ju ya dini hi, huwezi kuineza bila kufitinisha watu, huwezi pia kuineza bila kuwanenea watu uongo na hata kuwasingizia. Ukisikia mara nyingi kule kwenye nchi za Kiarabu hasa Iran, Pakistan nk eti kijana anauawa kwasababu sijui ya kubaka nk, wengi wao hua sio kweli, ujue kijana huyo huenda kabadiri dini na kua Mkristo then lazima auawe so anatafutiwa KOSA ambalo hata hakulifanya; mifano ipo mingi hata hapa kwetu, binafsi pia niliwahi hadi kusomewa Albadiri, kulaaniwa na ndugu zangu hasa baba na baadhi ya kaka zangu, nawapongeza sana dada zangu, moja kati ya dada yangu ni mke wa sheikh kabisa but alinitetea sana, wanawake kwa asili wana HURUMA sana; sasa hvi mimi na wao ni ndugu kabisa, sijui kama ni hasira zao kwisha au kwasababu nina KIPATO kidogo, that much sina HAKIKA. Huyu Mohamedi Said hanaga kitu kingine anachoweza kukifundisha kuhusu dini yake bila kupandikiza CHUKI kwa watu na ndio maana kitabu chake kinauzwa msikitini/misikitini na sio kwenye bookshops, malengo yake kwa haraka haraka ni wateja wake ni well defined, WAISLAM. Binafsi, kama dini yako haihubiri UPENDO then hiyo ni dini ya shetani sio ya Mungu, dini inayohubiri visasi na chuki, hiyo ni dini ya shetani, hahihitajiki elimu ya mbinguni kulijua hilo
Mzee Mohamed Said msome kijana wako.
Katika vyote alivyoviandika nimevutiwa zaidi na hiki
.
ukweli ju ya dini hi, huwezi kuineza bila kufitinisha watu, huwezi pia kuineza bila kuwanenea watu uongo

Kitolee ufafanuzi maana hii ndio kazi uliyobakisha duniani mengine yote umekwishafanya hakuna jipya tena kwako
 
These are your own imaginations (histohisia) which are the basis of your flawed and misleading narrations.
Yani huyu aliingia kwenye was nyerere nakujua kitakachofuata, hakika wazee wake walimpa sumu mbaya sana. Mungu awasamehe hao wazee na yeye mwenyewe.
 
Vyamavingi,
Vitabu haviuzwi msikitini.

Mfano wa maduka haya ni kama mafano wa Cathedral Bookshop ndani ya kanisa la St. Joseph's.

Ndani ya eneo la kanisa hili kuna bookshop ya miaka mingi sana na mimi nimenunua vitabu hapo toka nasoma shule hapo.

Ibn Hazm Media Centre maduka yake ya vitabu wala huwezi kufananisha na Cathedral Bookshop.

Haya maduka yako katika mitaa ambako iko misikiti hiyo na maduka haya ni vijumba vidogo tu vya kupangisha katika hali duni na mnunuzi haingii ndani ya duka kama lile la Cathedral ambako kuna viyoyozi nk.

Mnunuzi anasimama barabarani kama yuko katika duka lolote na pilipili bizari Manzese au Buguruni.

Duka la Msikiti wa Mtoro liko katika kichochoro kinachounganisha Mtaa wa Narung'ombe na Mahiwa ulipo msikiti duka ni nyumba ya kupanga jirani na msikiti.

View attachment 1314346

View attachment 1314336
Ibn Hazm Media Centre Msikiti wa Mtoro
Unaweza kufananisha kiduka hiki na Cathedral Bookshop?
Suala kwanini vitabu vyako huuzi kwenye maeneo mengineyo tofauti na duka hilo lisambazalo vitabu vya kiislamu na kiirabu?

Au watu wengine sio walengwa!!!
 
Mzee Mohamed Said msome kijana wako.
Katika vyote alivyoviandika nimevutiwa zaidi na hiki
.


Kitolee ufafanuzi maana hii ndio kazi uliyobakisha duniani mengine yote umekwishafanya hakuna jipya tena kwako
Khali...
Hayo aliyosema mimi si mjuzi wa hayo huo ni uwanja wa masheikh wao wangeweza kuchangia.
Mimi nimeandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kwa zaidi kueleza historia za wazalendo ambao historia imewasahau.
 
Suala kwanini vitabu vyako huuzi kwenye maeneo mengineyo tofauti na duka hilo lisambazalo vitabu vya kiislamu na kiirabu?

Au watu wengine sio walengwa!!!
Torch,
Maduka ya Ibn Hazm wako tayari muda wowote kusambaza vitabu vyangu ndiyo maana vingi vinapatikana hapo.
Wauzaji vitabu wengine huwa wanakuwanavyo lakini vikisha huwa hawana haraka sana ya kuchukua vingine.

Vimekuwapo vitabu vyangu Tanzania Publishing House (Samora Avenue), Novel Idea (Slip Way Masaki), Tusome (Mikocheni), Elite Bookshop (Mbezi) na kwengine lakini hawa si wachukuajii wa nakala nyingi.

Elewa mimi sihusiki na uuzaji wa vitabu ninavyoandika hii ni kazi ya publisher na maduka ya vitabu.
Mimi nikashaandika kitabu kazi yangu inaishia hapo.

Sidhani kama kuwa na vitabu vya Kiislam na Kiarabu ni tatizo kwani Cathedral Bookshop (Katoliki) na Dar es Salaam Bookshop (Lutheran) wanauza vitabu vya Kikristo na Kiingereza.

Sijui kama umapata kutaabishwa na hili.
Je unazo taarifa kuwa hairuhusiwi kuuza vitabu vya Kiislam na Kiarabu?
 
Mimi nimezaliwa na kukulia kwenye Uislamu hadi nilipofikisha umri wa miaka 24 ndio nikabadiri dini na kua Mkristo; ukweli ju ya dini hi, huwezi kuineza bila kufitinisha watu, huwezi pia kuineza bila kuwanenea watu uongo na hata kuwasingizia. Ukisikia mara nyingi kule kwenye nchi za Kiarabu hasa Iran, Pakistan nk eti kijana anauawa kwasababu sijui ya kubaka nk, wengi wao hua sio kweli, ujue kijana huyo huenda kabadiri dini na kua Mkristo then lazima auawe so anatafutiwa KOSA ambalo hata hakulifanya; mifano ipo mingi hata hapa kwetu, binafsi pia niliwahi hadi kusomewa Albadiri, kulaaniwa na ndugu zangu hasa baba na baadhi ya kaka zangu, nawapongeza sana dada zangu, moja kati ya dada yangu ni mke wa sheikh kabisa but alinitetea sana, wanawake kwa asili wana HURUMA sana; sasa hvi mimi na wao ni ndugu kabisa, sijui kama ni hasira zao kwisha au kwasababu nina KIPATO kidogo, that much sina HAKIKA. Huyu Mohamedi Said hanaga kitu kingine anachoweza kukifundisha kuhusu dini yake bila kupandikiza CHUKI kwa watu na ndio maana kitabu chake kinauzwa msikitini/misikitini na sio kwenye bookshops, malengo yake kwa haraka haraka ni wateja wake ni well defined, WAISLAM. Binafsi, kama dini yako haihubiri UPENDO then hiyo ni dini ya shetani sio ya Mungu, dini inayohubiri visasi na chuki, hiyo ni dini ya shetani, hahihitajiki elimu ya mbinguni kulijua hilo
Kuhusu kuzaliwa katika uislamu hilo halina shaka kwani hata mapapa na viongozi wote wa kikristo na hata kibuda walizaliwa wakiwa waislamu.Ama kuhusu kubadili dini ukawa mkristo naona kama kwamba baada ya kuzaliwa hukulelewa na waislamu au hukuleleka kiislamu kwani hakuna yoyote anayelelewa kiislamu na akauelewa uislamu halafu akaamua kubadili dini na kuwa mkristo.Ikitokea hivyo basi huwa ni njaa na matamanio ya kishetani ndiyo yaliyomvuta huko..Wewe najuwa ni muathirika wa hayo ndipo ukabadili dini.Vinginevyo utakuwa ni muongo ili unogeshe kijeli na kuubeza ukweli kuwa ukristo Tanzania umejaribu sana kujikweza kwa kufuta ukweli wa kihistoria inayowahusisha waislamu.
Upendo na huruma ni moja ya mafunzo muhimu katika uislamu.Iwapo mpaka ulipofikia 24 hukuwahi kulijuwa hili basi shetani alikuzidi maarifa kwa sana na ndio maana mpaka leo unapendelea historia ya uongo iendelee kusomeshwa na kuwadhuru waislamu..Bahati nzuri kazi nzuri ya Mohamed Said na hii ni kwa uongozi wa Mwenyezi Mungu na huruma zake ili ukweli ujulikane na kwa hilo matakwa yako yatakuwa hayana nafasi tena kurudisha nyuma ufahamu wa ukweli uliokuwa umefichwa.
 
Kuhusu kuzaliwa katika uislamu hilo halina shaka kwani hata mapapa na viongozi wote wa kikristo na hata kibuda walizaliwa wakiwa waislamu.Ama kuhusu kubadili dini ukawa mkristo naona kama kwamba baada ya kuzaliwa hukulelewa na waislamu au hukuleleka kiislamu kwani hakuna yoyote anayelelewa kiislamu na akauelewa uislamu halafu akaamua kubadili dini na kuwa mkristo.Ikitokea hivyo basi huwa ni njaa na matamanio ya kishetani ndiyo yaliyomvuta huko..Wewe najuwa ni muathirika wa hayo ndipo ukabadili dini.Vinginevyo utakuwa ni muongo ili unogeshe kijeli na kuubeza ukweli kuwa ukristo Tanzania umejaribu sana kujikweza kwa kufuta ukweli wa kihistoria inayowahusisha waislamu.
Upendo na huruma ni moja ya mafunzo muhimu katika uislamu.Iwapo mpaka ulipofikia 24 hukuwahi kulijuwa hili basi shetani alikuzidi maarifa kwa sana na ndio maana mpaka leo unapendelea historia ya uongo iendelee kusomeshwa na kuwadhuru waislamu..Bahati nzuri kazi nzuri ya Mohamed Said na hii ni kwa uongozi wa Mwenyezi Mungu na huruma zake ili ukweli ujulikane na kwa hilo matakwa yako yatakuwa hayana nafasi tena kurudisha nyuma ufahamu wa ukweli uliokuwa umefichwa.
Duh! Wewe Hutumii kichwa chako vizuri. Yaani unamfananisha huyo jamaa aliye- ritadi na Papa!

Vv

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waelimishe waislamu wafanyeje ili kujikwamua hapa sasa hivi walipo, sio kuwajaza chuki kwa mambo yaliyopita ambayo hayarekebishiki, wewe ni mchochezi mkubwa wa chuki, kwa iyo unataka waislamu wabebe mapanga wawakate waliowadhulumu, kuwa na busara hata kidogo

Kuna njia mtu akipita, Dhahiri shari unajua hata fika. Hii njia, shekhe naona anaingia chakani. Nyerere amekufa long ago. Hatusogei mbele kama Taifa tunahangaika na marehemu?
 
Kuna njia mtu akipita, Dhahiri shari unajua hata fika. Hii njia, shekhe naona anaingia chakani. Nyerere amekufa long ago. Hatusogei mbele kama Taifa tunahangaika na marehemu?
Rogojin,
Kwanza napenda nikufahamishe mimi si sheikh na sijui imekuwaje hapa barazani wengi wanadhani mimi ni sheikh.

Elimu yangu yote mimi ni sekula.

Hakika Nyerere kafa kama alivyokuwa Abdul Sykes ambae nimeandika kitabu cha maisha yake na ndicho kilichofanya nijulikane JF na kwengine kwingi.

Kitabu kimechapwa miaka zaidi ya 20 iliyopita na kama ni safari basi nilishawasili niendako miaka mingi.

Unaona niko hapa majibu maswali sababu kubwa ni kuwa akili za wengi zinakataa kuwa yale niliyoeleza katika kitabu changu ndiyo historia ya kweli ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Kila uchao wanarudi kwangu kuniuliza maswali nami niko hapa kujibu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
iv chuki mnazopandikiza kwa waislam wenzenu mnamanisha nn

Baada ya kifo cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Rais wa Kwanza wa Tanganyika na pia Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) tarehe 14 Oktoba 1999 mengi yamesemwa na kuandikwa kuhusu msimamo wake na uadilifu kuhusu Uislam Tanzania.

Nia ya kitabu hiki ni kueleza jinsi Mwalimu Nyerere katika kipindi chake cha uongozi alivyoshughulikia suala la Uislam na Waislam wa Tanzania.

Hii ni historia ya uhusiano wa Mwalimu Nyerere na Waislam kwa kipindi cha takriban robo karne toka pale aliposhika madaraka ya nchi mwaka 1961 hadi alipoachia madaraka mwaka 1985.

Ni mategemeo ya mwandishi kuwa kitabu hiki kidogo kitaweka wazi yale ambayo hayafahamiki kwa wengi.

Kitabu kinapatikana Ibn Hazm Media Centre: Msikiti wa Manyema, Mtoro na Mtambani kwa bei ya Shs: Elfu Mbili.


 
Back
Top Bottom