Kitambulisho cha Mjasiriamali kilivyoleta mateso katika jamii

Kitambulisho cha Mjasiriamali kilivyoleta mateso katika jamii

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Ndugu yangu ni mkulima wa jembe la mkono. Analima shamba lake na analimia watu ili kupata pesa ya sukari na sabuni. Kuna siku kazi za kulimia watu zinakosekana. Ikifika hali hii mke wake anadamka alfajiri kuwahi soko la matunda. Ananunua ndizi na machungwa anatembeza kwenye beseni lake kichwani

Mtaji wake ni sh 10,000 na ikifika jioni anakuwa amepata sh 15,000. Hii ni pesa ya kununua unga na mboga akapikie familia. Fikiria huyu mama ili atembeze beseni lake la ndizi na machungwa inabidi anunue kitambulisho cha mjasiliamalu 20,000.

Mama huyu siku za mvua hawezi kufanya biashara. Katika faida anayopata inabidi aweke kidogo senti zitakazosaidia siku akikosa biashara pia watoto wakiugua.
 
Ndugu yangu ni mkuluma wa jembe la mkono. Analima shamba lake na analimia watu ili kupata pesa ya sukari na sabuni. Kuna siku kazi za kulimia watu zinakosekana. Ikifika hali hii mke wake anataka alfajiri kuwahi soko la matunda. Ananunua ndizi na machungwa anatembeza kwenye beseni lake kichwani...
Wewe mama huna point hapa. Kama kwa siku anaingiza 5000, kwa mwaka anaingiza 1,590,000/=. Kuna ubaya gani akichangia 20,000 kwa mwaka kwa ajili ya ulinzi wa nchi, huduma za jamii na miundombinu kwa manufaa yetu wenyewe?

Wenzetu huko mbele huona fahari kulipa kodi, sisi tunaona ni adhabu.
Chadema mtajenga nchi kwa fedha kutoka wapi? Kodi mmsema mnafuta, madini mnaweka rehani. Au misaada ya kuhimiza ushoga?
 
Wewe mama huna point hapa. Kama kwa siku anaingiza 5000, kwa mwaka anaingiza 1,590,000/=. Kuna ubaya gani akichangia 20,000 kwa mwaka kwa ajili ya ulinzi wa nchi, huduma za jamii na miundombinu kwa manufaa yetu wenyewe?
Si kila siku anauza biashara hii, Kuna siku za mvua na katika 5,000 inabidi aweke akiba kidogo. Huyu alitakiwa kusaidiwa si kukamuliwa 20,000 kwa mwaka.
 
Wewe mama huna point hapa. Kama kwa siku anaingiza 5000, kwa mwaka anaingiza 1,590,000/=. Kuna ubaya gani akichangia 20,000 kwa mwaka kwa ajili ya ulinzi wa nchi, huduma za jamii na miundombinu kwa manufaa yetu wenyewe?
You must be crazy na mtu hopeless! Out of 5,000 anakula ngapi na familia for a day?
 
Sky Eclat hao wachuuzi wadogo hapo kabla walikuwa wakilipa ushuru wa shilingi 100/= hadi 500/= kwa siku kutegemea na halmashauri. Hapo bado 100/= nyingine kwa siku kama ushuru wa usafi. Piga hesabu kwa mwezi tu alikuwa analipa shilingi ngapi?

Baada ya kuingia Rais Magufuli akaagiza walipe 20,000/= tu kwa mwaka kupitia vitambulisho vya mjasiriamali.

Kwa muktadha huo juu, nani anawatetea wajasiriamali; Lissu au Magufuli? Wajasiriamali, za kuambiwa changanya na zako!!!
 
Kuchangia chochote kwenye nchi yako ni fahari kubwa. 20K kwa mwaka ni Sawa na 1800 approx kwa mwezi, na 56Tsh kwa siku. Ni program inayofaa na nyepesi zaidi kwa mjasiriamali kuliko ile inayotozwa holela masokoni. Ila hapa uliandika, ili ionekane Serikali ya JPM inawanyanyasa wajasiriamali, sio Sawa hata kidogo.
 
Si kila siku anauza biashara hii, Kuna siku za mvua na katika 5,000 inabidi aweke akiba kidogo. Huyu alitakiwa kusaidiwa si kukamuliwa 20,000 kwa mwaka.
Tatizo chadema mnategemea fedha kutoka kwa wahisani ili kutuharibia nchi yetu.
 
Kuna ubaya gani akichangia 20,000 kwa mwaka kwa ajili ya ulinzi wa nchi, huduma za jamii na miundombinu kwa manufaa yetu wenyewe?

Wenzetu huko mbele huona fahari kulipa kodi, sisi tunaona ni adhabu.
Hizi 20K zimeingia kwenye mfuko gani manake inasemekana Kwenye fuko kuu "Hazina "Hazipo. Halafu Magufuli alishasema ni hiyari, Ingawa si Kweli. Inakuwaje wewe unatokwa povu hapa?
 
Hiyo 5000 ni makadirio ya chini, kitambulosho kinamsaidia hata yeye kufanya biashara yake kwa amani.

Kama kwa mwaka 20000 means kwa mwezi analipia 1666 na nikiwango kidogo sana ukulinganisha na zile hela za ushuru walizokuwa wanatozwa kila siku.

Kuliko kubeza ni bora tuangalie swala hili kwa upande wa manufaaa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla mana vimesaidia hata serikali kupata mapato yake na kuendeleza miindombinu na utolewaji wa huduma za kijamii ambazo hata huyo Mjasiriamali zitamnufaisha.
 
Kumbukeni mjasiriamali naye anafamilia, inayosomeshwa bure na kujifungua bure kwenye hospitali na shule za serlikali, hivyo na yeye kwa sehemu yake ndogo ya kipato anawajibu wa kuchangia maendeleo ya taifa. Kwani mjasilia mali huyohuyo, anahitaji barabara ya lami, umeme wa uhakika, maji, ulinzi wa vyombo vya dola, matibabu hospitalini, n.k, n.k.

Hivyo anawajibu wa kuchangia sehemu ndogo ya pato lake kama mtanzania. Kwahiyo kuja kubwabwaja hapa eti kitambulisho cha mjasiliamali ni mateso, huu ni uelewa wako mdogoo saanaa. Na kwa hali hiiii husitahili hata kuwa kiongozi wa familia. Maendeleo ya taifa lolote, yanajengwa na wanataifa lile kwa kuzingatia uwezo wao wa kipato chao.
 
Wanaokujibu wengi wapo karibu na ujasiriamali kwahio wanajua faida zake, hili suala msiliguse mtapoteza kura za hata wabunge wenu. Mtu akipata kitambulisho na wigo wa kufanya biashara unaongezeka, anaweza kuingia hadi Halmashauri kwenda kuuza bidhaa zake bila bugdha yoyote.
 
Wenye kipato kidogo hupewa msaada na serikali ili waweze kuboredha maisha yao. Kosa la huyu mama ni kuwatafutia wanawake rizik kidogo lakini akiamua kukaa nyumbani hatadaiwa 20,000.
 
Kwanza matumizi ya vitambulisho hivi yalikuja tu kwa ghafla kupitia tamko la Mheshimiwa. Kama yeye mwenyewe asemavyo, ilitegeme na jinsi alivyoamka siku hiyo. Hakukuwa na utaratibu ulioeleweka juu ya kuanza kwa matumizi yake wala hata haikutungwa sheria ndogo ili kuhalalisha matumizi yake.

Sisi tuliona tu maRAC na maDC wakipewa maagizo, na kisha wakaanza kugawana vitambulisho hivyo, na kisha kuanza kuja na vitisho kama kawaida yao dhidi ya wanyonge wanaowanyonga kwa kisingizio cha kuwatetea. Hatimaye wakazidi kuwajenga hofu ili kuwalazimisha wavinunue pasipo kukosa.

Napata hisia ktk utekelezaji wa zoezi hili, wapo waliotumbuliwa baada ya zoezi kuthibitika kudorora ktk mikoa ama wilaya zao.
 
Wewe mama huna point hapa. Kama kwa siku anaingiza 5000, kwa mwaka anaingiza 1,590,000/=. Kuna ubaya gani akichangia 20,000 kwa mwaka kwa ajili ya ulinzi wa nchi, huduma za jamii na miundombinu kwa manufaa yetu wenyewe?

Wenzetu huko mbele huona fahari kulipa kodi, sisi tunaona ni adhabu.
Chadema mtajenga nchi kwa fedha kutoka wapi? Kodi mmsema mnafuta, madini mnaweka rehani. Au misaada ya kuhimiza ushoga?
Unamlaumu sky ushawahi fanya biashara wewe,unajua mama anaepika maandazi anapata faida isiyozidi 1000tu kwa siku,Tena hapo maandazi yaishe,huyu atapata lini 20000 ya kulipia kitambulisho? Elfu moja inatosha kwa mahitaji ya siku ya mtanzania? Au unadhani wanapata hela nyingi Sana?
 
Wenye kipato kidogo hupewa msaada na serikali ili waweze kuboredha maisha yao. Kosa la huyu mama ni kuwatafutia wanawake rizik kidogo lakini akiamua kukaa nyumbani hatadaiwa 20,000.
Taifa lolote linahamasisha uwajibikajii, wa kila raia ili lisonge mbele, zaidi. Kwahiyo kila mtanzania kwa kiwango cha pato lake, achangie maendeleo. Hawa wajasiliamali kuchangia elfu 20000 kwa mwaka mzima ni serikali kuwabeba pakubwa saana. Hivyo tunaomba zilaaniwe sera za mwanasiasa yoyote anayepinga ulipaji wa kodi kwa wajasiriamali wadodo wadogo
 
Back
Top Bottom