Uchaguzi 2020 Kitanzi cha CCM Kawe: Watia nia 176 wa ubunge dhidi ya Halima Mdee CHADEMA

Uchaguzi 2020 Kitanzi cha CCM Kawe: Watia nia 176 wa ubunge dhidi ya Halima Mdee CHADEMA

Wewe unajua uchawi tuu hesabu wala huzijui... tufanye tuu kwa mfano hapo kawe Halima mdee amepigiwa na wajumbe 71 halafu papo hapo watia nia tuu wa CCM hapo kawe wameshafika 120 yani zaidi ya wajumbe walio mpigia kura Mdee! Kwa kifupi tuu....Kawe kuna wana chama wa CCM wengi kuliko chadema ba uwezekano wa CCM kulipata jimbo hilo ni mkubwa sana kuliko chadema......


Halafu wana CCM kujitokeza wengio sio kawe tuu ni majimbo mengi ya Dares-salaam na ni demokrasia...
 
Hili linaweza kuwa ajabu lingine la dunia ama linaweza kuingia kwenye kitabu cha rekodi za dunia World Guinness Book of Records, ama linaweza kuvunja rekodi ya nchi na dunia kwa jimbo moja la ubunge kuwa na watia nia wengi kuwahi kutokea na karibia asilimia mia moja wa chama kimoja.

Pamoja na kwamba kibubu cha tume ya uchaguzi ya CCM kitatuna kwa mapato na pengine kuwa jimbo lililoingiza mapato mengi zaidi kwa kuuza form nyingi zaidi lakini madhara yake ni makubwa kuliko hayo mapato.

1. Katika watia nia wote hao 80 nina hakika hawapungui walau 20 wenye nguvu ya pesa, ushawishi ndani ya chama na wale wa mbeleko na vimemo. Kwa kuzingatia hili pekee tayari yatatokea makundi yasiyopungua 10 hivi. Makundi yenye nguvu na misuli ya kila aina. Hapa badala ya kupambana na adui yataanza kupambana yenyewe kwa yenyewe.

Jimbo la Kawe lililomegwa kutoka Kinondoni limekuwa na umaarufu mkubwa kuliko hata Kinondoni yenyewe na hii pengine ni kutokana na jiografia yake na aina ya mtu anayelishikilia.

3. CCM wanalitaka hilo Jimbo kwa hali na mali. Na wamewekeza muda mrefu sana tena kwa gharama kubwa mno. Hivyo kitendo cha kulikosa kitakuwa aibu kubwa, fedheha na hasara kubwa kisiasa.

4. Kitendo cha wanaume na uwekezaji wao wote kuja kushindwa na mwanamke mmoja ni ndoto ya kutisha sana na jinamizi wasilolipenda CCM

5. Kuonesha umwamba na ubabe kuwa wakitaka kitu hawashindwi kwakuwa wana kila kitu kila nyenzo ya kupata ushindi

Ni kwa muktadha huo wa kukamia kulikopitiliza hilo jimbo.. Wamejikuta wanatoa boko. Kwakuwa watatumia muda mwingi sana kwenye:
Mchujo
Kupata tano bora
Kwenye kupata mgombea mmoja
Kwenye kuunganisha makundi
Kwenye kuponya majeraha kabla ya uchaguzi

Kumbuka kila hatua kati ya hizo zote itaacha maumivu kwa kundi fulani
Ni wakati wakihangaika na yote haya Halima Mdee atakuwa busy kuimarisha himaya yake.

Matokeo yake ni nini? Muda utasema




Napata tabu kuelewa kuhusu maana halisi ya neno Demokrasia, neno uhuru wa mtu binafsi, neno uwazi, neno maamuzi nk

Napata tabu sana Leo mwezi wa saba, mwanachama wa CHadema badala ya kunadi sera na matarajio ya wagombea wa chama chake, yeye anajadili kuhusu watia nia tu. Deductively Hapo Ni wanachama 80 wa hiyo CCM and so hiyo CCM Ina idadi kubwa ya wanachama.

Napata Shida mpinzani anashindwa kuonyesha kwa data Mafanikio ya mbunge Wake aliyekuwa Hapo ili watu waelewe why wamchague,!wewe sio tu kwamba unaandika yasiyokuhusu Lakini pia unaweka na mipasho. Then unaitaka Tz iendelee.

Watanzania Ni Nini Priorities zenu. Mipasho au maendeleo. Huwezi kuwa na yote hasa kwa watz wavivu na wapiga majungu as if uchaguzi unafanyika kila mwaka. Ukiingiia Insta ndo utajua mind za watz na Sasa JF. Kila mtu anajua kuongea Tz. It’s time kuongelea mikakati zaidi kuliko watu. Mdee amefanya Nini? Hao watu wa Kawa wamchague MDEEE kwa nini nk. Emperical evidence.

Mwisho wa siku utaskia Kura zimeibiwa Lakini hamsemi kwa sifa gani za mgombea. Sasa mmeanza kuhusu Mdee. Kafanya Nini.
 
Wewe unajua uchawi tuu hesabu wala huzijui... tufanye tuu kwa mfano hapo kawe Halima mdee amepigiwa na wajumbe 71 halafu papo hapo watia nia tuu wa CCM hapo kawe wameshafika 120 yani zaidi ya wajumbe walio mpigia kura Mdee! Kwa kifupi tuu....Kawe kuna wana chama wa CCM wengi kuliko chadema ba uwezekano wa CCM kulipata jimbo hilo ni mkubwa sana kuliko chadema......


Halafu wana CCM kujitokeza wengio sio kawe tuu ni majimbo mengi ya Dares-salaam na ni demokrasia...
Karibu upate tiba
 
Mdee amegombea nafasi ya jimbo na nafasi ya vitu maalum; ni kweli kwamba CHADEMA wanajua kitakachotokea na wamejiandaa tayari. Ni hakika kwamba Mdee atapoteza jimbo mbele ya mzee wa Amfifiro na yeye anatinga bungeni kwa tiketi ya viti maalum.
 
Mdee angefanya kama Mnyika na Kubenea tu. Kawe na majimbo mengine ya Dar yapo kimkakati, hata kwa faulu tatanishi lazima mengi yaende kwa mataga.
 
Unaweza kusema kwamba wamechukua fomu ili kujenga majina kwa awamu ijayo lakini utajengaje jina kati ya watu 80
 
Mimi mtazamo wangu ni tofauti,nadhani wingi wa watia nia ni advantage kwa CCM,maana watia nia 80 mpaka hapo kila mtia nia kisaikolojia ameshakata tamaa! Hata watakaoshindwa wataona ni kawaida tu,labda kama kutakuwa na mizengwe ya waziwazi.Hatari ingekuwa kama wagombea wangekuwa wachache,labda 4 hivi hapo kila mmoja angekuwa anaona chance ya kupata uteuzi ni kubwa kuliko hali ilivyo sasa.Kisaikolojia wote wameshakata tamaa,hata wasipoteuliwa "reaction" yao sio kubwa kihivyo.
Watia nia wengi wenye njaa wengi. katika kugombea basi lazima kusumana kuumia si ajabu!
 
Tunaomba Karatasi Majina ya Wagombea wote isije ikawa ni Propaganda!
 
Back
Top Bottom