Uchaguzi 2020 Kitanzi dhidi ya Wagombea wa Upinzani kimefichwa ndani ya Kanuni za Uchaguzi 2020

Uchaguzi 2020 Kitanzi dhidi ya Wagombea wa Upinzani kimefichwa ndani ya Kanuni za Uchaguzi 2020

safari hii wahuni wanaruka na wakurugenzi na network zao wajichanganye tu.
 
Mkuu hapo kwenye maandishi yaliyokolezwa wino (bold fonts) umemaliza kila kitu. Hilo jambo la kupoteza muda kwenye masuala madogo madogo ambayo hayana muendelezo wa kudumu nimeliongelea sana.

Watu wanataka jambo la kujipatia umaarufu wa haraka ambayo mengi ni mambo madogo ya jawaida sana siyo ya kukusaidia kushinda vita ya kumng'oa mpinzani wako kwenye madaraka.

Hiyo approach wanatumia wapinzani ndiyo sahihi mtu akiondolewa ndo vurugu litanzia hapo hapo na kuenea kama mgombea hafai aachwe akataliwe na wananchi kwenye sanduku la kura. Vinginevyo kutakuwa na vurugu kubwa sana na ndipo kila mtu atakumbuka umuhimu wa kuwa na tume huru.
 
Yaani ni mambo ya hovyo kabisa. Mkurugenzi wa NEC anaweka pingamizi dhidi ya mgombea halafu anakuwa ndiye mamlaka ya mwisho ya kusikiliza rufaa ya mgombea dhidi ya pingamizi (sick) aliloliweka yeye mwenyewe.

Mwezi mei vyama vya siasa vilipelekewa rasmu ya kanuni hizi ila inasikitisha kuona vyama havikujali wala kuona hatari ya njama zilizofichika ndani ya kanuni hizo.

Ninadhani, hata kama havisemi, vyama vya siasa viko under capacitated au pengine wanaona aibu kutafuta misaada ya policy experts kuwasaidia kuchambua kisha wao watumie refined expert output ku-engage NEC/ZEC.

We ulikuwa wapi mbona walisema ulitaka wafanyeje kama wao siyo wenye uamuzi wa mwisho. Kuna kanuni zimetolewa kuhusu online contents mdau gani alizijadili na mbona zimekuwa gazetted zinatumika hapo unamlaumu nani. Hii awamu kila hila imeonekana waziwazi hakuna namna ni kwenda nayo sambamba.
 
Na hawajipangi si kwa sababu hawajui vipengele hivyo bali inaonesha ni kwa aidha makusudi au wana ushirikiano wa siri na watawala.
Ikiwa si hivyo KWANINI HAWAKUPIGIA "KELELE" VIPENGELE OVU HIVYO? KUDAI TUME HURU INGALI KUNA VIPENGELE KAMA HIVYO NI "KIPENGELE!!"
UKWELI USEMWE

Wapige kele vipi mbona tume huru na katiba mpya wanapiga kelele haipatikani sasa wapige kelele kanuni zilizotokana na sheria mbovu ya tume isiyokuwa huru hayo si ndiyo matokeo ya tume isiyokuwa huru. Kelele zinatosha labda machafuko ndiyo bado.
 
Mkuu, huwezi kuanza kuomba kitu kikubwa ilhali vidogo hujapewa!! Hebu tazama hizo kanuni hata kama tutakuwa na tume huru itatusaidiaje? Kanuni zingekuwa rafiki hata tume ingekuwa mbaya na mbovu bado wangebanwa ana "wangeliona haya!" Twapaswa kwenda na yote vinginevyo kilio kikuu chaja
 
Wapige kele vipi mbona tume huru na katiba mpya wanapiga kelele haipatikani sasa wapige kelele kanuni zilizotokana na sheria mbovu ya tume isiyokuwa huru hayo si ndiyo matokeo ya tume isiyokuwa huru. Kelele zinatosha labda machafuko ndiyo bado.
Mkuu, huwezi kuanza kuomba kitu kikubwa ilhali vidogo hujapewa!! Hebu tazama hizo kanuni hata kama tutakuwa na tume huru itatusaidiaje? Kanuni zingekuwa rafiki hata tume ingekuwa mbaya na mbovu bado wangebanwa ana "wangeliona haya!" Twapaswa kwenda na yote vinginevyo kilio kikuu chaja
 
We ulikuwa wapi mbona walisema ulitaka wafanyeje kama wao siyo wenye uamuzi wa mwisho. Kuna kanuni zimetolewa kuhusu online contents mdau gani alizijadili na mbona zimekuwa gazetted zinatumika hapo unamlaumu nani. Hii awamu kila hila imeonekana waziwazi hakuna namna ni kwenda nayo sambamba.
=Siasa ni kupaza sauti. Sauti za vyama vya siasa (primary stakeholders' voice matters) ina nguvu kwenye maamuzi yahusuya uchaguzi. Their voice matters.
 
Ccm wanataka nchi iingie kwenye machafuko cha kushangaza wenyewe wanasema wamefanya mabadiliko makubwa lakini ukifka uchaguzi hawajiamini .
 
Wafanye tu wananchi wakichoka watajuta ujanjaujanja usio na kichwa wala miguu una mwisho wao sio kwamba wana akili sana ,sio kwamba watu hawajui wanachofanya na hao mashushushu uchwara wanaowabeba kijani kibichi ,Yuko wapi Omar Al Bashir.
 
Mkuu mbona unataka kudanganya watu??

Wapi Sheria uliyoitaja imemtaja ofisa wa tume kuwa na uwezo wa kumwekea mgombea pingamizi.

Mbona hutaji kuwa mgombea mwingine anaweza mwekea mwenzake pingamizi??

Kwanini kutaka kuzua taharuki tu alimradi Sheria ionekane Mbaya??
 
Ni bahati mbaya sana kuona wapinzani hawajipangi wala kujishughulisha na masuala ya hatari kama haya isipokuwa muda wao mwingi wako 'busy' na trivial issues wakati vichwa vyao vinaelekezwa kibra!
Nahisi uelewa wako wa hiyo lugha upo chini ya wastani au umetumia kamusi ya english--swahili ambayo imekupeperushia
mbali
Kisome vizuri kufungu Cha nne,ukikielewa kitaondoa kabisa mchecheto wako
Si kila pingamizi lazima likubaliwe,pia mgombea anaruhusiwa kisheria kukata rufaa tume ya taifa ya uchaguzi,hili pia lilifanyika 2015,wakati ulikua shule
 
Nahisi uelewa wako wa hiyo lugha upo chini ya wastani au umetumia kamusi ya english--swahili ambayo imekupeperushia
mbali
Kisome vizuri kufungu Cha nne,ukikielewa kitaondoa kabisa mchecheto wako
Si kila pingamizi lazima likubaliwe,pia mgombea anaruhusiwa kisheria kukata rufaa tume ya taifa ya uchaguzi,hili pia lilifanyika 2015,wakati ulikua shule
Wewe uko kwenye ushabiki tu au kuendesha distortions za kulinda status quo; wala hujui hata kuwepo kwa conventional principle of impartiality of EMB. Maofisa wa serikali wala Tume hawapaswi kumuwekea pingamizi mgombea isipokuwa mgombea mwenzake. Kanuni hiyo imekuwa ikifuatwa miaka yote isipokuwa uchaguzi wa 2019 na sasa kwenye uchaguzi huu.

Hebu soma uchambuzi hapa chini:

Kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi Mkuu 2020, pamoja na kanuni nyinginezo kwenye kanuni hizo, Kanuni ya 30(1) inatamka kwamba watu wanaoweza kuruhusiwa kuweka pingamizi dhidi ya Mgombea Urais au Ubunge watakuwa:-
1. Mkurugenzi wa Uchaguzi;
2. Msajili wa Vyama vya Siasa ;
3. Msimamizi wa Uchaguzi;
4. Mwanasheria Mkuu wa Serikali; au
5. Wagombea/mgombea (m)wenzake

Aidha, Kanuni 30(5) inamtaka Msimamizi wa Uchaguzi [
pengine ndiye aliyeweka pingamizi - Mungu apishe mbali!] kutoa uamuzi wa pingamizi hilo na kisha kumfahamisha mgombea ubunge.

Lakini pia, Kanuni 31(3) inaelekeza mgombea ubunge aliyewekewa pingamizi asiporidhika na maamuzi ya Msimamizi wa Uchaguzi akate rufaa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (
hebu fikiria iwapo pingamizi hilo limewekwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi!) kupitia Msimamizi wa Uchaguzi (pengine ndiye huyo huyo aliyeweka pingamizi na kisha akasikiliza pingamizi lake mwenyewe)!

Kisha, [Kanuni 31(4)] inaelekeza kuwa Msimamizi wa Uchaguzi husika (
huyo huyo aliyeweka pingamizi na kisha kulitolea maamuzi) aandae nyaraka zote na ushahidi (wa mgombea ubunge aliyekata rufaa Tume dhidi ya maamuzi ya Msimamizi wa Uchaguzi (pengine aliyesilikiza pingamizi aliloliweka mwenyewe dhidi ya mgombea) kisha kuziwasilisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (fikiria hali itakuwaje iwapo pingamizi dhidi ya mgombea liliwekwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi, halafu apelekewe rufaa dhidi ya pingamizi lake iliyoamuliwa na mwajiriwa wake akimpendelea bosi wake!).

Hii model regulations (kanuni za mfano wa kuigwa) imechukuliwa kwenye kanuni na uzoefu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (vitongoji, vijiji na mitaa) wa mwaka jana (2019) 'uliofanikiwa' sana! Ni brand new electoral democracy ya Tanzania.

Kwenye uchaguzi huo (2019) kiasi cha wapiga kura 95% hawakuweza kupiga kura kwa kuwa wagombea wa upinzani katika vitongoji, vijiji na mtaa hiyo waliwekewa mapingamizi na wasimamizi wa uchaguzi kisha wagombea wa CCM wakapitishwa na kupewa ushindi a kupita bila kupingwa.

Asilimia 95 ya Wapiga kura wa Tanzania walizuiwa/walinyang'nywa haki yao ya kupiga kura (disenfranchised).

Tunaweza kuanza kujadili uhalali (legitimacy) wa viongozi wa kisiasa wanaochaguliwa kwa mtindo huo.

NEC/RPP kuwekea m(wa)gombea pingamizi inamaanisha partiality of the NEC or the Government vis-a-vis the
2020 elections!

kabombe be the first to know
 
Back
Top Bottom