Pre GE2025 Kitendo cha Mahakama kwenda kutoa hukumu ya TAMISEMI kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni kuzidi kubariki uovu wa CCM

Pre GE2025 Kitendo cha Mahakama kwenda kutoa hukumu ya TAMISEMI kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni kuzidi kubariki uovu wa CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Butiama, Mara
Tanzania

Butiama wajitokeza wengi kujiandikisha


View: https://m.youtube.com/watch?v=PegHAOJ9yE4

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya ajitokeza ktk zoezi la kuhuisha kitambulisho chake cha mpiga kura na awaomba wakaazi wengine wa mkoa wa Mara wajitokeze kwa wingi... Bw. Gerald Musabila Kusaya, amewahi pia kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, kabla ya uteuzi huu uliofanywa na Rais Samia Hassan, mbali ya vyeo hivyo Bw. Kusaya aliwahi kuwa Kamishna wa Mamlaka DCEA, Katibu mkuu wizara ya kilimo ....

Naye Gozebert Bernard afisa muandikishaji wapiga kura asema ..... huku wananchi nao wawahimiza wenzao kujitokeza ili waweze kushiriki baadaye kupiga kura na pia kuomba nafasi za uongozi ....
 
Ogopa serikali inayoongozwa kwa wasomi njaa.
Unakuta msomi hajielewi,na haelewi ni anatakiwa afanye kwa Taiga.
Ila kuajiriwa kwake,imekuwa kama zawadi au tunu na sio Hali yake.
Njaa mbaya,kujumlisha siasa chafu.
Std7,ndo anamkagua na kimpangia kazi PhD holders🤣🤣🤣
 

"Uboreshaji wa Daftari Ia Kudumu Ia Wapiga Kura hauhusiani na maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2024" asema Mkurugenzi wa Uchaguzi​


Imewekwa: 15 Jun, 2024
Uboreshaji wa Daftari Ia Kudumu Ia Wapiga Kura hauhusiani na maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2024  asema Mkurugenzi wa Uchaguzi

Uboreshaji wa Daftari Ia Kudumu Ia Wapiga Kura hauhusiani na maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu wa 2024.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima, R. K wakati akifungua mkutano wa Tume na Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri tarehe 15 Juni, 2024 jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo unahitimisha mfululizo wa mikutano ambayo Tume imefanya na wadau wake kauanzia tarehe 07 Juni, 2024.

Baadae Tume itafanya mikutano na wadau kwenye mikoa yote kwa kuzingatia ratiba ya uboreshaji wa Daftari.

Mikutano hiyo ina lengo Ia kuwapa wadau taarifa za uwepo wa zoezi la uboreshaji wa Daftari Ia Kudumu la Wapiga Kura na kuwapitisha katika vifaa (Biometric) na mifumo ya uandikishaji pamoja na kuona namna zoezi litakavyofanyika vituoni.

"Maafisa habari wa mikoa na halmashauri mnalo jukumu la kuelimisha wananchi na kuzuia kusambaa kwa taarifa za upotoshaji kama ile inayodai kwamba uboreshaji wa Daftari la Kudumu Ia Wapiga Kura unahusika na maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa," amesema Bw. Kailima.

Mkurugenzi huyo wa uchaguzi amenukuu kifungu cha 10(1) (c) cha Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Na. 2 ya Mwaka 2024 ambacho kinaelekeza kwamba Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi itasimamia uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kutumia sheria itaka yotungwa (Na Bunge).

"Kifungu cha 10(1)(c) cha Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Na. 2 ya Mwaka 2024 kinaweka sharti kwa Tume kusimamia na kuratibu uendeshaji wa uchaguzi wa serikali za mitaa na vitongoji Tanzania Bara kwa kuzingatia utaratibu utakaoainishwa katika Sheria itakayotungwa na Bunge. Sheria hiyo bado haijatungwa," amesema Bw. Kailima.

Mkrugenzi wa Uchaguzi amewaasa watu wanofanya upotoshaji huo waache kwa kuwa matokeo yake ni mabaya na yanaweza kuathiri mwenendo wa kupiga kura kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.

Amesisitiza kuwa sheria mbili zilizofutwa ambazo ni Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura ya 343 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa Sura ya 292 hazihusiani na uchaguzi wa serikali za mitaa, hivyo wananchi wawe makini na wapotoshaji

Source : www. inec.go.tz
 
ANGALIZO:
Wapiga kura na wagombea wanaweza kukosa fursa ya kuwa wapiga kura kwa kuwa hawajaandikIshwa katika daftari la mpiga kura maalum kwa uchaguzi wa serikali za mitaa.
 
06 September 2024

KATIBU MKUU CHADEMA AELEZEA SIRI NZITO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA " KADI PEKEE HAIKUFANYI UPIGE KURA "


View: https://m.youtube.com/watch?v=ZqdtW1I92bU

Uchaguzi wa serikali za mitaa ratiba na maandalizi mbaya, waangalizi wa uchaguzi yaani (elections observer and monitors ) wawe makini kufuatilia tarehe za uandikishaji, maeneo yao ya mitaa vijiji vitongoji vyenye migogoro wahakikishe imepatiwa ufumbuzi

Sababu wananchi wamepewa taarifa potofu kuwa kuwa na kadi ya mpiga kura kuna kupa uhalali kuwa eti unaweza kushiriki kupiga kura kwenye uchaguzi wa serikali za mtaa

Katibu mkuu wa CHADEMA anasisitiza kuwa wananchi wahakikishe wamejiandikisha katika daftari la mtaani, kitongoji na vijiji ili waweze kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa ...
 
ELIMU YA URAIA KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024

:FIRE: LIVE : WANAOPINGA TAMISEMI KUSIMAMIA UCHAGUZI WAIBUA MAPYA / WAHOJI UKIMYA WA WANANCHI 'KESI YAO'



View: https://m.youtube.com/watch?v=3SokBJXm6W8
  • Kinachoendelea mahakama kuu ya Tanzania ni Ombi la Kufungua Kesi kwa niaba ya waTanzania wote
  • Shauri lililofunguliwa mahakamani na raia watatu wa Tanzania ambao ni Nkya, Kaiza na Wangwe kwa niaba ya watanzania
  • Umuhimu wa ombi hili kwa watanzania wote
  • Wizara ya TAMISEMI ni batili kusimamia uchaguzi wa viongozi wa vijiji, mitaa na vitongoji
  • Ombi kama raia hao watatu wanaruhusiwa kufungua kesi
  • Yaliyojitokeza
  • Uongozi ni rasilimali namba moja ya kutuletea maendeleo
  • Media House / Waandishi wa Habari ni kama wamesusa kufuatilia Ombi hili la raia 3, pengine ni kwa kutofahamu uzito na umuhimu wa ombi hili
  • Unyoofu uadilifu integrity
 
24 September 2024
Mahakama Kuu ya Tanzania
Kivukoni Front
Dar es Salaam

MAWAKILI WAVUTANA MAHAKAMANI KESI YA TAMISEMI KUSIMAMIA UCHAGUZI/ SERIKALI YAPEWA SIKU 14 KUJIBU HOJA ZA WANANCHI


View: https://m.youtube.com/watch?v=IzuZftVKoTY

Hoja za wananchi Kaiza Buberwa, A. Nkya na Bob Wangwe wanaowakilishwa na jopo la mawakili
 
Tunategemea muda na saa yoyote Mahakama Kuu, kutoa hukumu ya kesi iliyofunguliwa na mawakili wasomi wakiongozwa na Bob Chacha Wangwe juu ya kupinga TAMISEMI kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Maono yangu kwakua nimeoteshwa ni kwamba Mahakama na Jaji atakayetoa hukumu atatoa maamuzi ya kubariki TAMISEM kuendelea kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Pia maono yangu uchaguzi wa 2025 nao utasimamiwa na tume ile ile, watu wale wale kwa kigezo au vigezo vitakavyotolewa katika hukumu hii.

Kipi cha kujifunza Tanzania tusitegemee kuja kuwa na uchaguzi wa huru na haki, tusitegemee kuitoa CCM kwa kupeleka kesi mahakamani kwakua mahakama zina maelekezo teyari.

Pia tujifunze kuwa Mahakama, na vyombo vya dola ndivyo vinatuumiza, pia mawakili wa kujitegemea msipende peleka kesi zenu kwenye mahakama za Tanzania hasa zinazo igusa CCM kwa lengo la kuiondoa madarakani bali unganisheni nguvu kwenye vyama vya upinzani na kutoa elimu ya uraia kwa watanzania hasa wa vijijini juu ya uzarimu wa Serikali na CCM hapo mtapata uungwaji mkono lakini mahakama siyo sehemu za kukimbilia.

Baada ya kusema hayo ngoja nirudi ofisini kupitia mafaili yenu.

Pia soma
- Kuelekea 2025 - Bob Wangwe aiomba Mahakama Kuu iizuie TAMISEMI kusimamia shughuli za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
Hapa Tanzania hamna Mahakama!!

Mahakama Iko Kenya, hapa Pana makada wa CCM waliovalishwa majoho ya UJAJI.

Hakuna kuheshimiwa na Sheria!!! ni kama nchi Iko kwenye LAWS OF JUNGLE 😃😃🤣🤣🤣
 
Tunategemea muda na saa yoyote Mahakama Kuu, kutoa hukumu ya kesi iliyofunguliwa na mawakili wasomi wakiongozwa na Bob Chacha Wangwe juu ya kupinga TAMISEMI kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Maono yangu kwakua nimeoteshwa ni kwamba Mahakama na Jaji atakayetoa hukumu atatoa maamuzi ya kubariki TAMISEM kuendelea kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Pia maono yangu uchaguzi wa 2025 nao utasimamiwa na tume ile ile, watu wale wale kwa kigezo au vigezo vitakavyotolewa katika hukumu hii.

Kipi cha kujifunza Tanzania tusitegemee kuja kuwa na uchaguzi wa huru na haki, tusitegemee kuitoa CCM kwa kupeleka kesi mahakamani kwakua mahakama zina maelekezo teyari.

Pia tujifunze kuwa Mahakama, na vyombo vya dola ndivyo vinatuumiza, pia mawakili wa kujitegemea msipende peleka kesi zenu kwenye mahakama za Tanzania hasa zinazo igusa CCM kwa lengo la kuiondoa madarakani bali unganisheni nguvu kwenye vyama vya upinzani na kutoa elimu ya uraia kwa watanzania hasa wa vijijini juu ya uzarimu wa Serikali na CCM hapo mtapata uungwaji mkono lakini mahakama siyo sehemu za kukimbilia.

Baada ya kusema hayo ngoja nirudi ofisini kupitia mafaili yenu.

Pia soma
- Kuelekea 2025 - Bob Wangwe aiomba Mahakama Kuu iizuie TAMISEMI kusimamia shughuli za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Utawala na mihimili yake leo inapimwa ndani na nje ya nchi kuhusu uwepo wa haki (fairness) kwa wote, au taasisi ya urais na chama chake dola kongwe ndiyo pekee wenye haki katika suala la chaguzi za TAMISEMI

Kikao kile cha baraza la mawaziri kiluchokutana Tunguu Zanzibar je kilikuwa cha kuambizana ukweli kuwa jumuiya ya kimataifa na wadau wa maendeleo wamekosa imani na utawala wa awamu ya sita hivyo kila mtu kivyake hakuna kubebana au mbeleko. Au jeuri ya chama dola kongwe kuhodhi mchakato wa uchaguzi ili CCM kujitengenezea ushindi usio na ushindani huru wa haki katika uchaguzi wa TAMISEMI kazi iendelee.

1730111064379.jpeg

Picha maktaba : Oktoba 2024 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mama Samia Suluhu Hassan aongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika katika Ikulu ndogo ya Tunguu Zanzibar.
 
Tatizo mnaenda kufungua kesi huku tayari mkiwa mmeshafanya hukumu zenu kichwani. Mkipewa nchi muongoze mahakama zitapata tabu sana.
 
Mahakama za Tanzania ni sehemu ya uozo mkubwa kwenye nchi hii...Rostam alikua sahihi kabisa
 
TAMISEMI ipo chini ya mkwe

..Tamisemi iko chini ya Mwenyekiti mwenyewe.

..kwa mfano, ukisikia Wizara iko chini ya Ofisi ya Makamu wa Raisi, kisheria Waziri ni Makamu wa Raisi.

..kuna wakati Dr.Seng'ondo Mvungi alimshitaka Raisi Mkapa kwa nafasi yake kama Waziri wa Tamisemi.
 
Mahakimu na majaji wanateuliwa na Mwenyekiti wa CCM taifa, halafu unataka waende kinyume na mamlaka ya UTEUZI, hahaha.
"Nakuteua nakupa pesa na gari halafu ufanye tofauti na matakwa yangu" Hiii bhagosha.
 
Back
Top Bottom