TOKA MAKTABA:
USHINDI WA KIUFUNDI WA TAMISEMI MBELE YA MAHAKAMA KUU 28 OCTOBER 2024
Mambo mazito yaelezewa kwa kina :

MAZITO :
BUNGE KUTOTUNGA SHERIA INAIPA TAMISEMI KUSIMAMIA UCHAGUZI
View: https://m.youtube.com/watch?v=zsVIiXNjhlg
2024 Majukumu ya Tume INEC:
10.-(1) Kwa kuzingatia matakwa ya Ibara za 74(6), 75 na 78 za Katiba, Tume itakuwa na majukumu yafuatayo:
(a) kusimamia na kuratibu uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Rais na Wabunge katika Jamhuri ya Muungano na uchaguzi wa Madiwani kwa Tanzania Bara;
(b) kusimamia na kuratibu uendeshaji wa uchaguzi
wa Rais na Wabunge na uchaguzi wa Madiwani
kwa Tanzania Bara;
(c) kusimamia na kuratibu uendeshaji wa uchaguzi
wa serikali za vijiji, mitaa na vitongoji TanzaniaBara kwa kuzingatia utaratibu utakao ainishwa
katika Sheria itakayotungwa na Bunge;
(d) kuchunguza mipaka na kuigawa Jamhuri ya
Muungano katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya
uchaguzi wa Wabunge;
(e) kuteua na kuwatangaza Wabunge Wanawake wa
Viti Maalumu katika Jamhuri ya Muungano na Madiwani Wanawake wa Viti Maalumu kwa Tanzania Bara;
(f) kuandaa na kusimamia Kanuni za Maadili ya.....
Source :
SHERIA YA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YA MWAKA
2024 (22nd March, 2024
ACT SUPPLEMENT To The Gazette of the United Republic of Tanzania No. 12 Vol. 105 Dated 22
nd March, 2024Printed by The Government Printer, Dodoma by Order of Government)
Wakili msomi anafafanua mkanganyiko uliopo katika jamii, Tume Huru ya Uchaguzi pamoja ya kupewa mamlaka ya kusimamia chaguzi, tatizo bunge la chama kimoja haijapitisha sheria bungeni kuipa meno kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa November 2024 mawakili wasema.....
Zaidi ya hilo uchaguzi wa serikali ya mitaa ili uweze kupiga kura lazima uwe unaorodhoshwe ktk daftari ikiwemo .... bila kujiandikisha kwenye daftari hutaweza kupiga kura uchaguzi wa TAMISEMI November 2024...
Mpaka itapotungwa sheria bungeni waziri wa TAMISEMI ataendelea kusimamia uchaguzi wa November 2024 ....
Bandiko #63 hapo juu : Kama kule Butiama zoezi ni la uchaguzi mkuu wa 2025 , hivyo wananchi wasichanganye uandikishaji kule Butiama ni mahsusi kwa uchaguzi mkuu 2025
Ni lazima tena kujiandikisha ktk daftari la Serikali ya Mitaa ili uweze kupiga kura November 2024 .....