Uchaguzi 2020 Kitendo cha Tundu Lissu kukubalika Kanda ya Ziwa kwa kiwango hiki inaashiria nini?

Uzuri ni kuwa waathirika wakubwa na huu utawala wa Magufuli ni wasukuma! Mifugo yao imetaifishwa, wavuvi wengi wameuawa na mali zao kuchomwa moto! Waamue kusuka au kunyoa!
Acha uongo kama mnategemea kupata kura za wasukuma mmeula wa chuya! Tarehe 28/10/2020 tunafanya vitu vyetu!!
 
Nini maana ya data?
 
Tumeshawaambia hadi tumechoka picha zenu za kuchakachua za kitengo chenu cha uchakahuaji CHADEMA tumezichoka.Mwacheni Lowasa apumzike picha zake za mikutano yake mlizochakachua inatosha.
Kitendo cha wanaGeita kumpuuza Magufuli aliyewaambia Lissu akija wasiende ni ishara mbaya kwa Magufuli!
 
Kitendo cha wananchi kujitokeza wakati Magufuli aliwaambia akija Lissu wasiende kwenye mkutano wake ni ishara kwamba wamempuuza Magufuli!

Lissu huyu ni mpango wa Mungu!
 
Ugali mezani lazima.
Haaa haaaa vichekesho hivi viko Tanzania tu. Sishangai hitimisho hili, maana najua jinsi wajinga wanavyolishwa taarifa za kubumba, ndio maana ikitokea waelewa wa mambo kadhaa huwa mnapotea.

Mkuu inawezekana sikukuelewa vizuri hapa fafanua ?

Maana yangu mimi maoni yeyote yale ya mambo ya kiuchumi/Fedha ambayo ndio ajira yangu itabidi nitofautishe , ama maoni binafsi na hayana uhusiano na institution ninayo ifanyia kazi,
 
Duh tujiandae tu kulinda ushindi wetu LISSU asibadilishiwe akapewa kura hafifu za mtu wa CCM.
 
Eti kwa umati huu ! Ina maana huo umati Jpm hakua nao nyie Nyumbu mbona mnadanganyana sana ! Hivi lissu amshinde Jpm Geita kweli kwa picha zenu za kuunga unga hizo!

Ahaaaa ahaaaa, kwanza ufahamu inasemekana ccm imekuwa imara sana chini ya Magufuli, huku ikisemekana kuwa cdm imekufa. Imefikia mahali inasemekana Magufuli ni mzalendo na kafanya makubwa sana, huku ikisemekana kuwa Lisu Lisu ni kibaraka. Sasa maajabu inakuwa mbona wananchi wanafurika kwa chama cha msaliti kilichokufa? Kumbuka kuwa hicho chama kilichokufa hakina pesa kama ccm, wala wasanii wa kuvuta watu. Subiri siku Lipumba, Mgombea wa NCCR nk wakifika huko kama watapata watu kama hicho chama kilichokufa.
 
Reactions: BAK
Watanzania tumesema kama uchaguzi ni HURU na wa HAKI 👋🏽👋🏽👋🏽👋🏽 JIWE wasalimie UHUTU.

 
Wewe ni mbumbumbu kabisa wa siasa za Kanda ya Ziwa tafuta video clips za 2015 za Lowassa then uje utuambie ilikuaje hakupata hata mbunge mmoja Mkoani Geita wakati kulikuwa na mafuliko?? Subiri tarehe 28/10/2020 ndiyo utajua!
 
Kitendo cha wananchi kujitokeza wakati Magufuli aliwaambia akija Lissu wasiende kwenye mkutano wake ni ishara kwamba wamempuuza Magufuli!
😁😁😁,Lissu huyu ni mpango wa Mungu!
Acha uongo sehemu gani alisema hivyo. Kwanza watu waliohudhuria mikutano ya Rais Magufuli ni wengi kuliko wa Lissu na Mwanza mlisema hivyo lakini Magufuli alifunika kabisa. Lakini msema kweli ni tarehe 28/10/2020.
 
Eti kwa umati huu ! Ina maana huo umati Jpm hakua nao nyie Nyumbu mbona mnadanganyana sana ! Hivi lissu amshinde Jpm Geita kweli kwa picha zenu za kuunga unga hizo!
Aisee!!! Hata Mimi nimesema hizo picha za Lisu Geita ni za kuunga unga na ni za miaka ya elfu mbili.Sio za mwaka huu, Ila ule umati wa Prezida Geita haikuwa mchezo! Mr Prezida Hoyee! Jpm hata bila kupiga kura anatangazwa asubuhi tu!
 
Mkuu inawezekana sikukuelewa vizuri hapa fafanua ?

Maana yangu mimi maoni yeyote yale ya mambo ya kiuchumi/Fedha ambayo ndio ajira yangu itabidi nitofautishe , ama maoni binasi na hayana uhusiano na institution ninayo ifanyia kazi,

Nimecheka kidogo. Hebu tuachane na haya maana sio mjadala husika. Ulipaswa kunijibu kulekule maana uliniamhia utatolea ufafanuzi. Sitaki tuhamishe mjadala ule kwenye mjadala mwingine.
 
Eti kwa umati huu ! Ina maana huo umati Jpm hakua nao nyie Nyumbu mbona mnadanganyana sana ! Hivi lissu amshinde Jpm Geita kweli kwa picha zenu za kuunga unga hizo!
Waache wajidanganye ila tarehe 28/10/20 ndiyo watajua kuwa Geita ina wenyewe!
 
Acha uongo kama mnategemea kupata kura za wasukuma mmeula wa chuya! Tarehe 28/10/2020 tunafanya vitu vyetu!!
Sasa chagueni huyo msukuma wenu aendelee kuwanyoa, sisi hatuna cha kupoteza. Maendeleo tutayapata miaka ijayo kwani sasa siyo mwisho wa dunia!
 
Acha uongo sehemu gani alisema hivyo. Kwanza watu waliohudhuria mikutano ya Rais Magufuli ni wengi kuliko wa Lissu na Mwanza mlisema hivyo lakini Magufuli alifunika kabisa. Lakini msema kweli ni tarehe 28/10/2020.

Hiyo tarehe 28 tume itakuwa huru? Maana hata matokeo ya 2015 bado tume ilikuwa hiihii. Kwa tume hii na msajili wa vyama vya siasa waliyokuwa kimya Mrema na Cheyo wakimuunga mkono Magufuli, lakini kitendo cha ACT kusema tu watamuunga mkono Lisu wametoa povu la hatari, hapo unaweza kutamba mbele ya wanaume kuwa wangoje tarehe 28 October?
 
Hizo ndizo picha halisi zinazoonesha joto analolipata kanda hii. Hizo zingine za kwao ni za kubumba. Leo alikuwa afanye mkutano katika viwanja vya shule ya msingi Mabatini, wilaya ya Ilemela mkoa Mwanza. Hakuna hata mtu mmoja aliyehudhuria na ikabidi mkutano uahirishwe. Lakini kesho nina uhakika tutaoneshwa mafuriko aliyoyapata kwenye mkutano huo wa Ilemela jijini Mwanza. Figisu tupu.
 
Hakuna mtu mshenzi Kama Peter Zakaria. Enzi za Kikwete Peter Zakaria alikuwa anaweza kuamrisha abiria wote kwenye basi lake wachapwe viboko na wakachapwa na mtu asiseme kitu.

Humjui Peter Zakaria wewe, hivyo kaa utulie
Halafu nasika huyu mwamba enzi za JK akiitwa Polisi, huyo Polisi atakayefika home kwake anamlamba vibao. Amri nyingi za Serikali alizipinga huyo mwamba, ndio maana Mheshimiwa Magufuli alimwonesha jeuri ya Serikali.
 
Tumeshawaambia hadi tumechoka picha zenu za za kitengo chenu cha uchakahuaji CHADEMA tumezichoka.Mwacheni Lowasa apumzike picha zake za mikutano yake mlizochakachua inatosha.
Acha uongo !!! Mapokezi hayo ni uhalisia . Mimi ni mwanachama wa Chama cha Mapinduzi .
 
Sasa chagueni huyo msukuma wenu aendelee kuwanyoa, sisi hatuna cha kupoteza. Maendeleo tutayapata miaka ijayo kwani sasa siyo mwisho wa dunia!
Kwanza nataka nikuambie hizo picha zinazotembea mitandaoni siyo hali halisi ilivyokuwa pale Geita leo naona wameziedit ndiyo maana nasema tusubiri October 2020 tutaona nani ni kidume!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…