Uchaguzi 2020 Kitendo cha Tundu Lissu kukubalika Kanda ya Ziwa kwa kiwango hiki inaashiria nini?

Uchaguzi 2020 Kitendo cha Tundu Lissu kukubalika Kanda ya Ziwa kwa kiwango hiki inaashiria nini?

Uzuri ni kuwa waathirika wakubwa na huu utawala wa Magufuli ni wasukuma! Mifugo yao imetaifishwa, wavuvi wengi wameuawa na mali zao kuchomwa moto! Waamue kusuka au kunyoa!
Acha uongo kama mnategemea kupata kura za wasukuma mmeula wa chuya! Tarehe 28/10/2020 tunafanya vitu vyetu!!
 
Anakubalika kwa percentage ngap?
Fuatilia statistics zilizotolewa na IPSOS juu ya wingi wa watu waliohudhuria kwenye vikao vya Kampeni vya CDM na CCM kanda ya ziwa hasa Mwanza.

Ni asilimia 90% kwa CCM na 10% kwa CDM. Ww huko kukubalika kwako umepima kwa metric gani?
Kama hauna data hauna haki ya kuzungumza.!
Nini maana ya data?
 
Tumeshawaambia hadi tumechoka picha zenu za kuchakachua za kitengo chenu cha uchakahuaji CHADEMA tumezichoka.Mwacheni Lowasa apumzike picha zake za mikutano yake mlizochakachua inatosha.
Kitendo cha wanaGeita kumpuuza Magufuli aliyewaambia Lissu akija wasiende ni ishara mbaya kwa Magufuli!
 
Mimi naomba tarehe 29 na 30 mwezi ujao muwepo humu! Nina kuhakikishia hapa hakuna mkoa wowote wala jimbo lolote ambalo Lissu atashinda kwa ujumla wa Kura dhidi ya Magufuli tena uko kanda ya Ziwa ndio usiseme kabisa!

Mimi naomba usije ukalimbia jukwaa!
Kamwe Lissu awezi mshinda Magufuli kwenye jimbo lolote wala mkoa wowote hapa Tanzania!

Najua sasa hivi utonielewa lakini tarehe 30 utanielewa! Kamwe Kamwe tena uko kanda ya Ziwa Lissu hatoweza kupanda ushindi hata ule unao mkaribia Magufuli hata chembe!

Naomba tuombe Mungu atuweke hai hadi tarehe 28 hakika tutaona na tutarudi hapa kusimuliana!
Kitendo cha wananchi kujitokeza wakati Magufuli aliwaambia akija Lissu wasiende kwenye mkutano wake ni ishara kwamba wamempuuza Magufuli!

Lissu huyu ni mpango wa Mungu!
 
Ugali mezani lazima.
Haaa haaaa vichekesho hivi viko Tanzania tu. Sishangai hitimisho hili, maana najua jinsi wajinga wanavyolishwa taarifa za kubumba, ndio maana ikitokea waelewa wa mambo kadhaa huwa mnapotea.

Mkuu inawezekana sikukuelewa vizuri hapa fafanua ?

Maana yangu mimi maoni yeyote yale ya mambo ya kiuchumi/Fedha ambayo ndio ajira yangu itabidi nitofautishe , ama maoni binafsi na hayana uhusiano na institution ninayo ifanyia kazi,
 
Nimetafakari na kujiuliza sana jambo hili , huyu mtu tuliyeaminishwa kwamba ni msaliti wa Taifa , akashambuliwa kinyama na kutelekezwa ili akafie mbali , kama haitoshi akavuliwa ubunge bila huruma na akatishwa asirudi nchini , bali pamoja na lundo la vitisho Lissu amerudi nyumbani kishujaa.

Cha ajabu ni kwamba kila anapopita kwenye kampeni zake za kuomba Urais watu wanajaa kupita kiasi , na cha kushangaza zaidi ni huko kanda ya ziwa ambako tuliaminishwa kwamba ni ngome ya watu wengine ndiko ilikovunjiwa rekodi ya umati kwenye mikutano yake , Katoro , Sengerema na Geita ni mifano hai ya hoja yangu

Swali langu ni hili , kwa umati huu unaojitokeza kwenye mikutano ya Lissu huko kanda ya ziwa ni kiashiria cha jambo gani ?

Hizi hapa ni picha za Geita , Mkoa unasemekana alizaliwa Mgombea Urais wa CCM , jioneeni wenyewe .

Duh tujiandae tu kulinda ushindi wetu LISSU asibadilishiwe akapewa kura hafifu za mtu wa CCM.
 
Eti kwa umati huu ! Ina maana huo umati Jpm hakua nao nyie Nyumbu mbona mnadanganyana sana ! Hivi lissu amshinde Jpm Geita kweli kwa picha zenu za kuunga unga hizo!

Ahaaaa ahaaaa, kwanza ufahamu inasemekana ccm imekuwa imara sana chini ya Magufuli, huku ikisemekana kuwa cdm imekufa. Imefikia mahali inasemekana Magufuli ni mzalendo na kafanya makubwa sana, huku ikisemekana kuwa Lisu Lisu ni kibaraka. Sasa maajabu inakuwa mbona wananchi wanafurika kwa chama cha msaliti kilichokufa? Kumbuka kuwa hicho chama kilichokufa hakina pesa kama ccm, wala wasanii wa kuvuta watu. Subiri siku Lipumba, Mgombea wa NCCR nk wakifika huko kama watapata watu kama hicho chama kilichokufa.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Watanzania tumesema kama uchaguzi ni HURU na wa HAKI 👋🏽👋🏽👋🏽👋🏽 JIWE wasalimie UHUTU.

Nimetafakari na kujiuliza sana jambo hili , huyu mtu tuliyeaminishwa kwamba ni msaliti wa Taifa , akashambuliwa kinyama na kutelekezwa ili akafie mbali , kama haitoshi akavuliwa ubunge bila huruma na akatishwa asirudi nchini , bali pamoja na lundo la vitisho Lissu amerudi nyumbani kishujaa.

Cha ajabu ni kwamba kila anapopita kwenye kampeni zake za kuomba Urais watu wanajaa kupita kiasi , na cha kushangaza zaidi ni huko kanda ya ziwa ambako tuliaminishwa kwamba ni ngome ya watu wengine ndiko ilikovunjiwa rekodi ya umati kwenye mikutano yake , Katoro , Sengerema na Geita ni mifano hai ya hoja yangu

Swali langu ni hili , kwa umati huu unaojitokeza kwenye mikutano ya Lissu huko kanda ya ziwa ni kiashiria cha jambo gani ?

Hizi hapa ni picha za Geita , Mkoa unasemekana alizaliwa Mgombea Urais wa CCM , jioneeni wenyewe .

 
Ni kuweweseka. Unajua Magufuli alikuwa hajaingia kwenye siasa za hoja kulikuwa hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumkosoa. Akajidanganya na kujiona anapendeka sana. Sasa ajabu moja ni kuwa hata kwenye ''ngome'' yake ameona wanampuuza.

Je sehemu nyingine itakuwaje? Uchaguzi huu unaweza kumwangusha vibaya sana... labda afanye mkakati kabambe na wa siri wa kuiba. Hali ilivyo sasa akajifinya kuiba kinguvunguvu anaweza kuamsha hasira kali nchi nzima na yeye akaishia pabaya mno. Mbaya zaidi ndani ya CCM wengi wanachekea kwa pembeni.
Wewe ni mbumbumbu kabisa wa siasa za Kanda ya Ziwa tafuta video clips za 2015 za Lowassa then uje utuambie ilikuaje hakupata hata mbunge mmoja Mkoani Geita wakati kulikuwa na mafuliko?? Subiri tarehe 28/10/2020 ndiyo utajua!
 
Kitendo cha wananchi kujitokeza wakati Magufuli aliwaambia akija Lissu wasiende kwenye mkutano wake ni ishara kwamba wamempuuza Magufuli!
😁😁😁,Lissu huyu ni mpango wa Mungu!
Acha uongo sehemu gani alisema hivyo. Kwanza watu waliohudhuria mikutano ya Rais Magufuli ni wengi kuliko wa Lissu na Mwanza mlisema hivyo lakini Magufuli alifunika kabisa. Lakini msema kweli ni tarehe 28/10/2020.
 
Eti kwa umati huu ! Ina maana huo umati Jpm hakua nao nyie Nyumbu mbona mnadanganyana sana ! Hivi lissu amshinde Jpm Geita kweli kwa picha zenu za kuunga unga hizo!
Aisee!!! Hata Mimi nimesema hizo picha za Lisu Geita ni za kuunga unga na ni za miaka ya elfu mbili.Sio za mwaka huu, Ila ule umati wa Prezida Geita haikuwa mchezo! Mr Prezida Hoyee! Jpm hata bila kupiga kura anatangazwa asubuhi tu!
 
Mkuu inawezekana sikukuelewa vizuri hapa fafanua ?

Maana yangu mimi maoni yeyote yale ya mambo ya kiuchumi/Fedha ambayo ndio ajira yangu itabidi nitofautishe , ama maoni binasi na hayana uhusiano na institution ninayo ifanyia kazi,

Nimecheka kidogo. Hebu tuachane na haya maana sio mjadala husika. Ulipaswa kunijibu kulekule maana uliniamhia utatolea ufafanuzi. Sitaki tuhamishe mjadala ule kwenye mjadala mwingine.
 
Eti kwa umati huu ! Ina maana huo umati Jpm hakua nao nyie Nyumbu mbona mnadanganyana sana ! Hivi lissu amshinde Jpm Geita kweli kwa picha zenu za kuunga unga hizo!
Waache wajidanganye ila tarehe 28/10/20 ndiyo watajua kuwa Geita ina wenyewe!
 
Acha uongo kama mnategemea kupata kura za wasukuma mmeula wa chuya! Tarehe 28/10/2020 tunafanya vitu vyetu!!
Sasa chagueni huyo msukuma wenu aendelee kuwanyoa, sisi hatuna cha kupoteza. Maendeleo tutayapata miaka ijayo kwani sasa siyo mwisho wa dunia!
 
Acha uongo sehemu gani alisema hivyo. Kwanza watu waliohudhuria mikutano ya Rais Magufuli ni wengi kuliko wa Lissu na Mwanza mlisema hivyo lakini Magufuli alifunika kabisa. Lakini msema kweli ni tarehe 28/10/2020.

Hiyo tarehe 28 tume itakuwa huru? Maana hata matokeo ya 2015 bado tume ilikuwa hiihii. Kwa tume hii na msajili wa vyama vya siasa waliyokuwa kimya Mrema na Cheyo wakimuunga mkono Magufuli, lakini kitendo cha ACT kusema tu watamuunga mkono Lisu wametoa povu la hatari, hapo unaweza kutamba mbele ya wanaume kuwa wangoje tarehe 28 October?
 

Hizo ndizo picha halisi zinazoonesha joto analolipata kanda hii. Hizo zingine za kwao ni za kubumba. Leo alikuwa afanye mkutano katika viwanja vya shule ya msingi Mabatini, wilaya ya Ilemela mkoa Mwanza. Hakuna hata mtu mmoja aliyehudhuria na ikabidi mkutano uahirishwe. Lakini kesho nina uhakika tutaoneshwa mafuriko aliyoyapata kwenye mkutano huo wa Ilemela jijini Mwanza. Figisu tupu.
 
Hakuna mtu mshenzi Kama Peter Zakaria. Enzi za Kikwete Peter Zakaria alikuwa anaweza kuamrisha abiria wote kwenye basi lake wachapwe viboko na wakachapwa na mtu asiseme kitu.

Humjui Peter Zakaria wewe, hivyo kaa utulie
Halafu nasika huyu mwamba enzi za JK akiitwa Polisi, huyo Polisi atakayefika home kwake anamlamba vibao. Amri nyingi za Serikali alizipinga huyo mwamba, ndio maana Mheshimiwa Magufuli alimwonesha jeuri ya Serikali.
 
Tumeshawaambia hadi tumechoka picha zenu za za kitengo chenu cha uchakahuaji CHADEMA tumezichoka.Mwacheni Lowasa apumzike picha zake za mikutano yake mlizochakachua inatosha.
Acha uongo !!! Mapokezi hayo ni uhalisia . Mimi ni mwanachama wa Chama cha Mapinduzi .
 
Sasa chagueni huyo msukuma wenu aendelee kuwanyoa, sisi hatuna cha kupoteza. Maendeleo tutayapata miaka ijayo kwani sasa siyo mwisho wa dunia!
Kwanza nataka nikuambie hizo picha zinazotembea mitandaoni siyo hali halisi ilivyokuwa pale Geita leo naona wameziedit ndiyo maana nasema tusubiri October 2020 tutaona nani ni kidume!
 
Back
Top Bottom