Uchaguzi 2020 Kitendo cha Tundu Lissu kukubalika Kanda ya Ziwa kwa kiwango hiki inaashiria nini?

Uchaguzi 2020 Kitendo cha Tundu Lissu kukubalika Kanda ya Ziwa kwa kiwango hiki inaashiria nini?

Dah sema kanda ya ziwa ndo waliko mdekia lami mgombea wa chadema 2015 ila wakampigia kura kwa wingi mgombea wa ccm. Kanda ya ziwa iacheni tu ilivo
 
Nimetafakari na kujiuliza sana jambo hili , huyu mtu tuliyeaminishwa kwamba ni msaliti wa Taifa , akashambuliwa kinyama na kutelekezwa ili akafie mbali , kama haitoshi akavuliwa ubunge bila huruma na akatishwa asirudi nchini , bali pamoja na lundo la vitisho Lissu amerudi nyumbani kishujaa.

Cha ajabu ni kwamba kila anapopita kwenye kampeni zake za kuomba Urais watu wanajaa kupita kiasi , na cha kushangaza zaidi ni huko kanda ya ziwa ambako tuliaminishwa kwamba ni ngome ya watu wengine ndiko ilikovunjiwa rekodi ya umati kwenye mikutano yake , Katoro , Sengerema na Geita ni mifano hai ya hoja yangu

Swali langu ni hili , kwa umati huu unaojitokeza kwenye mikutano ya Lissu huko kanda ya ziwa ni kiashiria cha jambo gani ?

Hizi hapa ni picha za Geita , Mkoa unaosemekana alizaliwa Mgombea Urais wa CCM , jioneeni wenyewe .

Hivi hizi picha unazokesha unazitengeneza,kuna mtanzania wa wa kijijini anazaziona ili umdanganye?,kama Dar es salaam nasikia ni mabango ya Ccm tu,je huko Geita?
 
Huwezi shindana na mpango wa Mungu tofauti na yule aliyejikweza kwamba he has done wonders kiasi kwamba Sir God anatakiwa amtunuku cheo Cha kiongozi wa malaika huko mbinguni,hii ni kufuru kwa Muumba,muulizeni shetani alipatwa na nini alipodai ukuu.
 
Ni
Nimetafakari na kujiuliza sana jambo hili , huyu mtu tuliyeaminishwa kwamba ni msaliti wa Taifa , akashambuliwa kinyama na kutelekezwa ili akafie mbali , kama haitoshi akavuliwa ubunge bila huruma na akatishwa asirudi nchini , bali pamoja na lundo la vitisho Lissu amerudi nyumbani kishujaa.

Cha ajabu ni kwamba kila anapopita kwenye kampeni zake za kuomba Urais watu wanajaa kupita kiasi , na cha kushangaza zaidi ni huko kanda ya ziwa ambako tuliaminishwa kwamba ni ngome ya watu wengine ndiko ilikovunjiwa rekodi ya umati kwenye mikutano yake , Katoro , Sengerema na Geita ni mifano hai ya hoja yangu

Swali langu ni hili , kwa umati huu unaojitokeza kwenye mikutano ya Lissu huko kanda ya ziwa ni kiashiria cha jambo gani ?

Hizi hapa ni picha za Geita , Mkoa unaosemekana alizaliwa Mgombea Urais wa CCM , jioneeni wenyewe .

Ni kwa vile hujui historia ya mikoa hiyo, kama unayo kumbukumbu basi nitajie mwaka ambao upinzani ulikosa watu kanda ya ziwa?
Miaka yote mnajaza sana lakini siku ya mwisho huwa ni kilio kwa upinzani.
 
mwaka huu si lazima kichwa cha mbuzi kielekee kiblah, mbuzi atachinjwa hivyo hivyo alikojielekeza.
Mnatia hurumaa kumbe hampigi kampeni tena, balimnatafuta vichwa vya mbuziii?? Yaaniii wapinzani wa mwakaa huu mumevurugwa na nini??
 
Unachoka mwenyewe acha kulazimisha wengine wachoke kitu ambacho hakipo, wee lazimisha ni za zamani lakini wenye Akili wanakuwepo kwenye mikutano wanajua CCM mnatengeneza propaganda za kijinga kulazimisha kuwa ni picha za zamani na ndipo CCM inazidi kudharaulika zaidi
kama walivokuwa wanalazimisha eti chadema imekufa, upinzani umekufa, yan waNanunua viongozi njaa, wanawaacha wapiga kura then wanajidanganya upinzani umekufa...jamaa wanapenda kuishi kwenye illusions
 
Mimi naomba tarehe 29 na 30 mwezi ujao muwepo humu! Nina kuhakikishia hapa hakuna mkoa wowote wala jimbo lolote ambalo Lissu atashinda kwa ujumla wa Kura dhidi ya Magufuli tena uko kanda ya Ziwa ndio usiseme kabisa!

Mimi naomba usije ukalimbia jukwaa!
Kamwe Lissu awezi mshinda Magufuli kwenye jimbo lolote wala mkoa wowote hapa Tanzania!

Najua sasa hivi utonielewa lakini tarehe 30 utanielewa! Kamwe Kamwe tena uko kanda ya Ziwa Lissu hatoweza kupanda ushindi hata ule unao mkaribia Magufuli hata chembe!

Naomba tuombe Mungu atuweke hai hadi tarehe 28 hakika tutaona na tutarudi hapa kusimuliana!
ukiona panya anamringishia paka tako ujue kuna shimo karibu. jifarijini na tume
 
Amini usiamini watarudi na kauli ya "TUMEIBIWA KURA" wako kama wajinga tu

Siasa ni hesabu na hakuna chama hapa Afrika kinacho shinda mbinu za CCM ikifuatiwa na ZANU PF, ANC.

Zaidi ya yote wananchi hawa wameshajua wazi Magufuli ni jembe,macho na masikio vinaona na kusikia kile Rais anachofanya, leo hii aje mtu na kuanza kumponda nani atamuelewa?ni vile tu wanachi hawawezi kusimama jukwaani na wao wanadhani watu wakifika kwenye mikutano yao ni kama wameshinda na kumbe hakuna kitu

Mikoa mitano ya Mwanza,Tabora, Geita, Simiyu na Shinyanga JPM atashinda kwa 90% na ndiyo mikoa yenye watu wengi kuliko yote hapa Tanzania hasa huko vijijini ambako hawawaoni Chadema wala act

Vyama pinzani viko Twitter, Jamii foruma na youtube

Nani anakwenda twitter kujua Tundu Lisu kaongea nini

Tulioko mijini 85% tunajua Tundu Lisu ni mhaini wa nchi na tunamsikiliza,mwisho wa siku tunaenda kumpiga chini kwenye sanduku la kura

Mtu asiye tueleza atatufanyia nini,kazi yake ni wivu tu dhidi ya Magufuli na kutueleza kua alipigwa risasi, tunajua alipigwa risasi na hawezi kutulazimisha kua Serikali au Magufuli ndo alisababisha hayo

Kweni tutamuaminije kua hana maadui? Yeye ni MALAIKA?

Apite hivi[emoji117] atupishe tafadhari tuchague mpambanaji
Takataka, kumuamuru mkurugenzi amtangaze mtu kuwa kashinda wakati hakushinda hizo ndizo mbinu.

Ccm hawana mbinu yoyote tofauti na hiyo, hawawezi kushinda uchaguzi wowote ule ulio huru na haki, labda ukawadanganye walevi wa viroba huko baa.
 
Mkuu hiyo rahisi sana.. ni kuwa Tundu Lissu ndio Rais wetu mtarajiwa. Tunajipanga tu kujumuika kwenye kuapishwa kwake.
 
Mimi naomba tarehe 29 na 30 mwezi ujao muwepo humu! Nina kuhakikishia hapa hakuna mkoa wowote wala jimbo lolote ambalo Lissu atashinda kwa ujumla wa Kura dhidi ya Magufuli tena uko kanda ya Ziwa ndio usiseme kabisa!

Mimi naomba usije ukalimbia jukwaa!
Kamwe Lissu awezi mshinda Magufuli kwenye jimbo lolote wala mkoa wowote hapa Tanzania!

Najua sasa hivi utonielewa lakini tarehe 30 utanielewa! Kamwe Kamwe tena uko kanda ya Ziwa Lissu hatoweza kupanda ushindi hata ule unao mkaribia Magufuli hata chembe!

Naomba tuombe Mungu atuweke hai hadi tarehe 28 hakika tutaona na tutarudi hapa kusimuliana!
Labda Kama ataiba kura

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna kila ukweli kwa baadhi ya unayo sema, lakini nyinyi sio wafatiliaji wa data wazuri.

Kuna ongezeko la wanaoenda shule za msingi na sekondari za kata kwa kanda nzima watoto 750,000 kwa ngazi ya shule za msingi na sekondari, jee mnajua ni Maendeleo gani yatatokea baada ya miaka kumi ?

Jee Mabadiliko gani tuyategemee, hasa maendeleo na vurugu itakayo kuja kielimu baada ya miaka ishirini ?.
sababu hii na ukweli kwamba misingi na taswira ya CHADEMA ina mvuto mkubwa sana kwa vijana na lwa kizazi kipya kiujumla ndivyo hunifanya niamini katu gurudumu la mabadiliko Tanzania halitokaa lirudi nyuma tena. ni ngumu sana labda yatokee mabadiliko ya kidunia yatakayobadilisha uwepo wa vyama vingi. CCM Hakitokaa kirudie kilivyokuwa enzi za Mwalumu Nyerere na siku kikishindwa tu uchaguzi yan kinajizika chenyewe siku hiyo hiyo sababu kimsingi tunachokiona sasa ni matawi tu ya ccmlakini mizizi hakina, kinatumia mizizitumeccm, mizizi policcm; Na tatizo kubwa zaidi ni kuwa hawa polisi na tume nao wameshashtuka, wanajua wanatumika ila siku likimbuluka tu kila mtu ataachiwa jumba lake bovu limwangukie mwenyewe huko ze hegi
 
Back
Top Bottom