Kitendo cha viongozi wengi kuendelea kuugulia kisiri na kufia India kinaashiria huduma za afya Tanzania bado ni duni na haziaminiki!

Kitendo cha viongozi wengi kuendelea kuugulia kisiri na kufia India kinaashiria huduma za afya Tanzania bado ni duni na haziaminiki!

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Ndani ya kipindi cha wiki tatu tu Tanzania tumeshuhudia vifo vya viongozi wawili wa kitaifa wakifariki wakati wakitibiwa kisiri huko India kinaashiria bado huduma zetu za kiafya hapa Tanzania ni duni, mbovu au haziaminiki na watanzania walio wengi wakiwemo viongozi wakubwa wa kitaifa.
Taifa lilipokea kwa mshtuko taarifa za kifo cha Laurence Mafuru na leo hii limepokea kwa mshtuko mkubwa kifo cha Ndugulile ambaye alikuwa mbunge wa Kigamboni, na mkuu mteule wa shirika la afya duniani (WHO) ukanda wa Afrika.

Katika hali ya kawaida, kwa nafasi walizokuwa nazo wahusika maana yake serikali ilikuwa ikigharamia matibabu yao kwa kipindi chote cha ugonjwa, kifo na kurejeshwa nchini miili yao kwa taratibu za maziko. Na kwa misingi hiyo, serikali ilitoa kibali cha wao kwenda India kutibiwa kwa kuwa huduma za kiafya hapa nchini hazikuwa zinakidhi viwango vya wahusika kupona au kupata nafuu.

Ikiwa, mbunge mwandamizi wa CCM, naibu waziri wa afya mstaafu, mkuu mteule wa kitengo cha afya cha umoja wa mataifa (WHO) ukanda wa Afrika, anaweza kuugua na kukimbilia India kutibiwa huku akikacha kutibiwa kwenye hospitali ya Muhimbili, Bugando, KCMC, Benjamin Mkapa, Aga Khan nk, hiyo inatoa taswira kamili kuwa kwenye ubora wa utoaji wa huduma za Afya Tanzania bado sana.

Siku ukiona viongozi wetu hawaendi tena India kutibiwa, na wanaugua mpaka kupona au kufariki hapa hapa Tanzania hapo ndipo tutatambua ubora wa huduma za afya zitolewazo hapa nchini.
 
Ndani ya kipindi cha wiki tatu tu Tanzania tumeshuhudia vifo vya viongozi wawili wa kitaifa wakifariki wakati wakitibiwa kisiri huko India kinaashiria bado huduma zetu za kiafya hapa Tanzania ni duni, mbovu au haziaminiki na watanzania walio wengi wakiwemo viongozi wakubwa wa kitaifa.
Taifa lilipokea kwa mshtuko taarifa za kifo cha Laurence Mafuru na leo hii limepokea kwa mshtuko mkubwa kifo cha Ndugulile ambaye alikuwa mbunge wa Kigamboni, na mkuu mteule wa shirika la afya duniani (WHO) ukanda wa Afrika.

Katika hali ya kawaida, kwa nafasi walizokuwa nazo wahusika maana yake serikali ilikuwa ikigharamia matibabu yao kwa kipindi chote cha ugonjwa, kifo na kurejeshwa nchini miili yao kwa taratibu za maziko. Na kwa misingi hiyo, serikali ilitoa kibali cha wao kwenda India kutibiwa kwa kuwa huduma za kiafya hapa nchini hazikuwa zinakidhi viwango vya wahusika kupona au kupata nafuu.

Ikiwa, mbunge mwandamizi wa CCM, naibu waziri wa afya mstaafu, mkuu mteule wa kitengo cha afya cha umoja wa mataifa (WHO) ukanda wa Afrika, anaweza kuugua na kukimbilia India kutibiwa huku akikacha kutibiwa kwenye hospitali ya Muhimbili, Bugando, KCMC, Benjamin Mkapa, Aga Khan nk, hiyo inatoa taswira kamili kuwa kwenye ubora wa utoaji wa huduma za Afya Tanzania bado sana.

Siku ukiona viongozi wetu hawaendi tena India kutibiwa, na wanaugua mpaka kupona au kufariki hapa hapa Tanzania hapo ndipo tutatambua ubora wa huduma za afya zitolewazo hapa nchini.
Tusionazo sasa tufanyeje? Inauma sana kwa kweli!
 
Hizo hela za kuboreshea hospitali si bora tuwape taifa stars tu. Kamilioni 700 kadogo mno hakatoshi kuboresha hizo hospitali mkuu.
 
Mara nyingi hufunga safari ikiwa wamechelewa sanaaa....huyu wa karibuni hakujua kuwa ana kansa damu hadi ilipomlipukia kuanguka job.......too late
 
Maelezo kuhusu kutibiwa bongo. Yako hapo
 
Ukifika Muhimbili ukauona msongamano uliopo pale ndio utajua bado tuna safari ndefu sana kama nchi.
Hii nchi iltakiwa iwe na Hospitali aina ya Muhimbili kama tano hivi, kila kanda iwe na Muhimbili yake.
 
Tanzania hatuna utamaduni wa kuweka afya zetu hadharani hasa kwa viongozi wetu wa umma sijui kwa nini tunafanya magonjwa siri.
Mtu kama unaumwa maradhi si unasema tu ili tukuweke kwa maombi - maombi ya wengi yanaweza kukuokoa.
 
Chawa watakwambia wapinzani wametuchelewesha sana
Hawana akili hao!

Na ukweli serikali haina nia ya dhati kabisa kuboresha sekta ya afya nchini,hizo ni fimbo wanapigwa kwa kudhani kwao kutibiwa nje ya nchi ni salama zaidi na kwamba wananchi wengine watategemea kudra kupona.
 
Wakiugua hatuambiwi halafu maombolezo tunashirikishwa

Hata India wawe wanakuja na miili na washiriki mazishi
 
Afadhali magufuri alikaaa hapahapa na akafia hapa
 
Ila Vigo vya Lawrence na huyu Ndugulile na mkuu wa TANROad eng Mfugale watakuwa waliwekewa sumu zinazosabbausha kucreate cancer ya damu inayoua haraka
 
Ndani ya kipindi cha wiki tatu tu Tanzania tumeshuhudia vifo vya viongozi wawili wa kitaifa wakifariki wakati wakitibiwa kisiri huko India kinaashiria bado huduma zetu za kiafya hapa Tanzania ni duni, mbovu au haziaminiki na watanzania walio wengi wakiwemo viongozi wakubwa wa kitaifa.
Taifa lilipokea kwa mshtuko taarifa za kifo cha Laurence Mafuru na leo hii limepokea kwa mshtuko mkubwa kifo cha Ndugulile ambaye alikuwa mbunge wa Kigamboni, na mkuu mteule wa shirika la afya duniani (WHO) ukanda wa Afrika.

Katika hali ya kawaida, kwa nafasi walizokuwa nazo wahusika maana yake serikali ilikuwa ikigharamia matibabu yao kwa kipindi chote cha ugonjwa, kifo na kurejeshwa nchini miili yao kwa taratibu za maziko. Na kwa misingi hiyo, serikali ilitoa kibali cha wao kwenda India kutibiwa kwa kuwa huduma za kiafya hapa nchini hazikuwa zinakidhi viwango vya wahusika kupona au kupata nafuu.

Ikiwa, mbunge mwandamizi wa CCM, naibu waziri wa afya mstaafu, mkuu mteule wa kitengo cha afya cha umoja wa mataifa (WHO) ukanda wa Afrika, anaweza kuugua na kukimbilia India kutibiwa huku akikacha kutibiwa kwenye hospitali ya Muhimbili, Bugando, KCMC, Benjamin Mkapa, Aga Khan nk, hiyo inatoa taswira kamili kuwa kwenye ubora wa utoaji wa huduma za Afya Tanzania bado sana.

Siku ukiona viongozi wetu hawaendi tena India kutibiwa, na wanaugua mpaka kupona au kufariki hapa hapa Tanzania hapo ndipo tutatambua ubora wa huduma za afya zitolewazo hapa nchini.
Pesa ipo ya kutosha lipeni kodi
Toto afya kadi imefutwa
 
Swali ni akinanani wanaendesha Kampeni ya kupoisoni baadhi ya viongozi,,ukichunuguza zaidi utamuona team Mwezi February marope wakiobgoza kuo doa watu wenye misimamo na walio msaada Kwa mama Samia
 
Back
Top Bottom