Hakukuwa sababu yoyote ile ya Maana au ya Kijinga ya kufanya hivyo .
Hii ni kwa vile huko Korea hakuna anayemjua Samia, Wala hakuna Jimbo lolote la Uchaguzi wa Tanzania huko, kiasi cha hao wanaoitwa Wasanii ambao pia ni Chawa kulazimika kufanya Kampeni na kuvaa mafulana ya kiwango cha chini yenye picha ya Mtanzania mwenzao.
Ni kweli kwamba Tajiri hanuniwi, maana ndio kawapa hiyo Koneksheni, lakini tulidhani badala ya kuweka mapicha ya watu wangeweza kuweka picha za Vivutio vya Nchi yao ambavyo ni vingi mno, ambapo tunaamini utalii ungeongezeka Nchini, Ni laana kwa nchi kutukuza watu binafsi kwa kiwango hicho hata kama watu hao wanatupa hela, Watu huisha na Nchi hubaki, ndio maana Nyerere alikwenda lakini Tanzania ikabaki, Maandiko matakatifu yameandika hivi, nanukuu, "
AMELAANIWA MTU YULE AMTEGEMEAYE MWANADAMU" mwisho wa kunukuu
Kuna haja sasa ya Nchi hii kuruhusu Uraia pacha ili sisi wengine tujivunie nchi nyingine badala ya kuwa Watanzania tu huku tukidhalilishwa mara kwa mara
View attachment 3034819View attachment 3034820View attachment 3034821