Kitu ambacho Membe hatokaa amsamehe Rais Magufuli maishani!

Kitu ambacho Membe hatokaa amsamehe Rais Magufuli maishani!

Huyo Membe akubali tu sasa akalime korosho na kuendesha hotel yake. Mambo ya siasa yamekwisha mpita mkono wa kushoto hivyo akubali tu yaishe kwani hakuna jinsi Jiwe atakuja kumfikiria kwa nafasi yeyote!!
Huo upuuzi wao hauna faida kwa watanzania
 
Uliwahi kujiuliza waliompa Sumu JPM mwaka 2012 akiwa Waziri kwa bahati akapona haikumdhuru walitumwa na nani na walikuwa na lengo gani!?.. unadhani JPM kaingia kwenye kinyang'anyiro cha uraisi kwa bahati mbaya!?.. Umewahi kujiuliza kwanini tangu 2012 JPM analindwa na mabodyguard tofauti na mawaziri wengine au huna taarifa!?.. Kuna mengi usiyoyajua kuhusu Siasa za nchi hii.
 
Membe analia njaa mpaka leo A/C zako zote zilifumgwa hana pesa anaishi kwa kudundukiza tu amejaa mawazo balaa
 
Membe ni muhuni kama wahuni wengine.
Sidhani kama ni muhuni lakini kwa kweli ni unprincipled man! Hana tofauti kabisa na Lowassa na Sumaye! Hana uhuni wala ujanja wowote. Wote wabebanwa na the so called system. Hamna jipya, tuishi tu tungalipo hai, tusitegemee chochote labda kifo na umaskini.
 
Stories za vijiweni nazo unazileta tuzijadili hapa?

Sidhani kama wakuu wa EAC wanaweza kupendekeza mtu atoke nchi fulani halafu wakaipangia hiyo nchi kwamba lazima awe fulani. Membe wasn’t and still isn’t the best of any diplomat in the country to deserve to be handpicked by the EAC heads in that manner, even if any appointee would ultimately have to be approved by them!
 
Uchaguzi uliopita ndo nilimwona membe master of failure ,nilikuwa namwonaga smart ila hata vijana kama Zitto wamemzidi sana akili,alikuwa anaonekana comedian tu.

From hero to zero heri hata angestaafu siasa
 
Kazi kweli kweli, Umeandika lugha gani mkuu usiofuata kanuni za uandishi

English ina miundo na mifumo

"Rubbish content ever posted" unaelewa ulichoandika

"Content" means you have understood concept and details of the writer

"Rubbish" means negation of what you have understood

"Rubbish Content" Hakuna kiingereza kama hicho cha kukubali na kuikataa sentensi labda kama unatafsiri kichaga kwenda kiswahili halafu kwenda kiingereza

Haya ndio madhara ya kutafsiri kiswahili na kuandika kwa kiingereza

Hakika wapumbavu hawataisha nchi hii

Madhara ya shule za kata na vyuo vya kata haya ndio mavuno yake

Utaweza wewe kuongea kiingereza kwa dakika tano kwa uandishi wa hovyo namna hiyo

English ni somo pana sana ukitaka ujifunze nenda kwa watu wanaoongea lugha hiyo tu mwezi mzima bila kuchanganya utajifunza kitu

Achana na walimu wako wa kata hao nao ni vilaza kama wewe
Lol! This is totally an embecile comment..you know nothing when it comes to english words and their uses bro..you better stop comment if you are politically motivated..we should be pro-Tanzania and not Pro-maembe.
 
Uliwahi kujiuliza waliompa Sumu JPM mwaka 2012 akiwa Waziri kwa bahati akapona haikumdhuru walitumwa na nani na walikuwa na lengo gani!?.. unadhani JPM kaingia kwenye kinyang'anyiro cha uraisi kwa bahati mbaya!?.. Umewahi kujiuliza kwanini tangu 2012 JPM analindwa na mabodyguard tofauti na mawaziri wengine au huna taarifa!?.. Kuna mengi usiyoyajua kuhusu Siasa za nchi hii.
duuuuuuh
Hapa mjinga mimi nimeunganisha dots
 
Uchaguzi uliopita ndo nilimwona membe master of failure ,nilikuwa namwonaga smart ila hata vijana kama Zitto wamemzidi sana akili,alikuwa anaonekana comedian tu.

From hero to zero heri hata angestaafu siasa

Bure kabisa; sijui ni kachero mbobezi gani huyo asiyekuwa na mbinu zozote za maana! Siwezi hata kumpigia kura kuwa mwenyekiti wa kitongoji changu.
 
Hayo yote ni maccm na roho mbaya ndio sifa yao kuu jiwe kayaharibu maisha ya watanzania wengi sana zaidi ya huyo membe wako
Mbona mbowe hataki covid 19 wawe bungeni
 
Nawasalimu wanabodi.

Mwaka 2015 Mwanadiplomasia mahiri na kachero mbobezi Bernard Membe alijaribu kuusaka Urais kupitia CCM lakini akakatwa jina lake hatua za mwisho.

Macho na masikio ya wengi yalikuwa ni kwa Edward Lowassa na Membe lakini ngekewa ikamdondokea John Magufuli ambaye sasa ni Rais.

Mwaka 2016 mwezi Machi Jumuiya ya Madola (CommonWealth) ilitoa nafasi ya Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo ambapo ilikuwa ni zamu ya Afrika Mashariki kumtoa mtu. Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki ilipendekeza mtu huyo atoke Tanzania huku wakipendekeza awe ni Membe. Utarayibu wa Jumuiya hiyo ni kwamba anayependekezwa lazima apate kibali na ruhusa ya mkuu wa nchi yake.

Kinachosikitisha, Rais Magufuli akamwekea "bambi" Membe na nafasi hiyo ikaenda nchi nyingine. Membe akakosa nafasi hiyo.

Kama angefanikiwa kwanza angeenda kuishi jijini London. Angelipwa mshahara wa $50,000 kwa mwezi. Marupurupu $23,000, angesafiri na ujumbe wa watu 25 kila safari ya kikazi. Hizo ni faida binafsi.

Faida za kinchi ni pamoja na kupaa kidiplomasia duniani tofauti na sasa ambapo diplomasia yetu inaishia Buguruni. Tanzania ingezidi kusifika kwa kutoa viongozi hodari katika ngazi ya kidunia baada ya kina Dk. Salim Ahmed Salim, Dk. Asha-Rose Migiro, Balozi Mahiga (marehemu) nakadhalika. Unajiuliza ni kwa nini Magufuli alimkatili Bernard Membe?

Namshauri Magufuli, vichwa vya watu kama Membe si wa kuacha kuzurura nje ya utawala. Ni watu wa kuwa nao karibu. Mchukue Membe awe mshauri wako wa masuala ya diplomasia na usalama.

Nawasilisha!
Wewe utakuwa
1. Membe mwenyewe
2. Mke/ndugu ya Membe
3. Mpambe

Membe hajawahi kuwa smart kiasi hata robo ya unavyomfikiria. Alivyo sasa ndiyo nafasi pekee inayomfaa.
 
Nawasalimu wanabodi.

Mwaka 2015 Mwanadiplomasia mahiri na kachero mbobezi Bernard Membe alijaribu kuusaka Urais kupitia CCM lakini akakatwa jina lake hatua za mwisho.

Macho na masikio ya wengi yalikuwa ni kwa Edward Lowassa na Membe lakini ngekewa ikamdondokea John Magufuli ambaye sasa ni Rais.

Mwaka 2016 mwezi Machi Jumuiya ya Madola (CommonWealth) ilitoa nafasi ya Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo ambapo ilikuwa ni zamu ya Afrika Mashariki kumtoa mtu. Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki ilipendekeza mtu huyo atoke Tanzania huku wakipendekeza awe ni Membe. Utarayibu wa Jumuiya hiyo ni kwamba anayependekezwa lazima apate kibali na ruhusa ya mkuu wa nchi yake.

Kinachosikitisha, Rais Magufuli akamwekea "bambi" Membe na nafasi hiyo ikaenda nchi nyingine. Membe akakosa nafasi hiyo.

Kama angefanikiwa kwanza angeenda kuishi jijini London. Angelipwa mshahara wa $50,000 kwa mwezi. Marupurupu $23,000, angesafiri na ujumbe wa watu 25 kila safari ya kikazi. Hizo ni faida binafsi.

Faida za kinchi ni pamoja na kupaa kidiplomasia duniani tofauti na sasa ambapo diplomasia yetu inaishia Buguruni. Tanzania ingezidi kusifika kwa kutoa viongozi hodari katika ngazi ya kidunia baada ya kina Dk. Salim Ahmed Salim, Dk. Asha-Rose Migiro, Balozi Mahiga (marehemu) nakadhalika. Unajiuliza ni kwa nini Magufuli alimkatili Bernard Membe?

SNamshauri Magufuli, vichwa vya watu kama Membe si wa kuacha kuzurura nje ya utawala. Ni watu wa kuwa nao karibu. Mchukue Membe awe mshauri wako wa masuala ya diplomasia na usalama.

Nawasilisha!
Jiwe ana roho ya kichawi sababu amelelewa katika mazingira ya uchawi
 
Bure kabisa; sijui ni kachero mbobezi gani huyo asiyekuwa na mbinu zozote za maana! Siwezi hata kumpigia kura kuwa mwenyekiti wa kitongoji changu.

..akisalimu amri mbele ya Jpm mtaanza kumpamba na kumsifia.

..sasa hivi Membe ni mbaya kwasababu ametofautiana na mwenyekiti.
 
Back
Top Bottom