Kituko cha utotoni ambacho sitakisahau

Mi nakumbuka kuna demu alimzingua jamaa mmoja kitaa..Basi yule jamaa kwa asira akamwambia "ujue ntakubikiri"..Basi mi nikalipenda hilo neno bila hata kujua maana yake..Nikihisi kuwa litakuwa linamaanisha ntakupiga....Siku tumekaa sitting room na wazee pamoja na wagen tunacheki Tv tukaanza kugombania rimoti na sista..yeye akiwa anataka kubadili chanel..Ndo kumwambia "ujue ntakubikiri,we endelea tu"...

Nilipelekwa chemba nikapewa stiki za kutoha..Zen baadae darsa ndo likafwata..Ndo ikawa chanzo cha kupunguza kuokotaokota maneno kitaa
 
Kijana kumbe we ni bro wangu kwenye hizo vitu..Nakumbuka mi first time kuangalia nilikuwa form one..Basi baada ya kutoka kuangalia kila msichana ninayekutana naye namuona kama yupo uchi vile
[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13]
 
Teh teh..Hii hujawahi kunisimulia
 
Hii ilikuwa miaka 1988 -89 nikiwa darasa 2 mkoani Kil.
Huwa tunatoka mapema(shuleni) kidogo siku hiyo nilitengewa ugali nyama paka akaniwahi akala nyama yote muda niliofika ndio anavutana na mfupa .Nilichofanya nilimfungia nikatafuta kisu nikakinoa vizuri kisha kazi ikanza mimi na paka hiyo vita yake usiombe .Nifanikiwa kumkata kichwa (kutenganisha kiwiliwili na kichwa) Mimi nililazwa kwani alifanikiwa kuniparua vibaya mno .Nakumbuka mama alilia hujui wapi na wapi nmeumia kwani mwili umetapakaa damu ya paka na yangu huku akisema wewe utakuwa mtu wa sambuli gani.
Nilipona nilikuwa mtemi wa rika langu kwani kila mmoja aliujua ukatili wangu. Kama unavyojua maisha ya watu wa Kil.na Arusha huwa wanakuwa na marika na mtemi wa rika fulani
 
Mimi nilikulia Ushuani geti kali kutoka na gari kurudi na gari na home after homework tunakaa na familia kwa utulivu hatukuwa kama nyie home kwenu nothing lazima muwe wajinga na vituko.mfano hapo juu kuna mchangiaji alikuwa haendi shule kazi kujificha.


swissme
 
Kwa kwa kwa kwa
 
Mmewasumbua sana wazazi wenu mkumbuke kuwapelekea chochote na watoto wakiwafanana msianze kulialia mjue maji hufuata mkondo
 
Mimi nakumbuka tulikuwa na mchezo wa kufunga Barabara kwa kamba wakati usiku baiskeli ikipita au wakipita watu tunanyanyua ile kamba juu ili wajikwae. Tulikuwa na tunajificha kwenye fensi za michongoma kila mtu na upande. Ilikuwa balaa sana.
 
ha hahahahahaha duh
 
Wewe ni wa kiswahili pretender tu.....
 
ha hah ahaha haha uwiiii... yani umeniacha hoi
 

Umenikumbusha neno la kichaga mjomba wetu alikuwa anapenda kulitumia, "tulu" (sina uhakika na spelling) kumbe ilimaanisha matako bana. Sasa sisi tukameza tulivyorudi mjini tukaanza kuitana hivyo, "Iyo nyi itulu!" ah! zamani tulichapwa kwa mengi aiseee...
 
ha hhah a chupi ni muhimu
 
mimi nakumbuka, niliota nipo chooni, naharisha balaa....otea nilipoamka asbh ilikuwaje....!
 
Hahaaaa hii imefanana na yangu
Tulikuwa tunafuata mikate ya shule, enzi hizo form one. Katikati ya safari tunaingia kichakani tunachokonoa mikate tunakula minofu ya ndani. Kesho yake wanakati wa breakfast watakaopewa hiyo iliyoliwa ndani shauri yao na hawalalamiki coz na wao ikifika zamu yao wanafanya hivyo hivyo, teh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…