Kituko cha utotoni ambacho sitakisahau



Hahaha....maza atakua alikua anakufuatilia sana kuanzia siku hiyo kumbikiri sister noma haha
 
Wakati niko form 1 shule fulani Arusha(bweni),nilitumiwa pesa ya matumizi kwa TMO,sh2,000. Zilkuwa za kutosha enzi hizo,wakati natoka kuzichukua posta,njiani nikakuta jamaa wanachezesha kamari ya karata,kikundu-keusi. Nikavutika,tamaa ikanijia,nikajaribu. Walikula zote,kasoro 200. Mama moja mpita njia aliniokoa,walitaka kuninyang'anya 200 iliyobaki. Toka siku hiyo sitaki kabisa michezo ya kubahatisha.
 
Hahaha....maza atakua alikua anakufuatilia sana kuanzia siku hiyo kumbikiri sister noma haha
Teh teh..Hawakuwa na wasiwasi kwa hilo..Walijua tu kijana hajui anachoongea..Sema waliamua kunipa kichapo ili niace kuokota maneno mtaani
 

Nyie kweli mlikuwa na akili za kitaahira
 

Ahaaaaaa,ndio maana mkuu stori zako ni za kuwangawanga kwa sana,kumbe tokea kitambk mtunduuu
 
Mi nilivyokuwa darasa la nne ripoti iitoka nimefeli kinyama,mwalimu akanipa kwwnye bahasha niipeleke home,mwanaume nikasema ngoja niifungue niicheki,kufungua tu daaaah,kitu nimekuwa wa 67 kati ya wanafunzi 77,nikaona huu ni msala nyumbani,basi nikaifuta ile sita kiustadi sana nikaonekana nimekuwa wa saba,home wakastukia mchezo kwani maksi zilikuwa mbovu halafu eti nimefaulu,weee,nilikula mbata,siwezi kuzisahau kamwe
 
Teh teh..Hawakuwa na wasiwasi kwa hilo..Walijua tu kijana hajui anachoongea..Sema waliamua kunipa kichapo ili niace kuokota maneno mtaani


Hahahah...na ilibidi uache tu hayo maneno mkuu!
 
Hey superman. Ukaogopa kwenda Zenj...ha ha ha
 
Mmmmh.... mie nilikua napenda sana kucheza mpira wa rede na mumy alikua hapendi, siku hiyo kuna wageni mamaa yupo busy nikakusanya soksi zangu nikatengeneza mpira wangu nikacheze nje.... kimbembe kikawa nitatokaje na mpira mama asijue...nikaweka tumboni tumbo linatuna ikanibidi niufiche kwenye chuppi nitoke nao....nikatoka kwa kujiamini sasa tembea yangu kama nimebakuliwa wananishangaa wewe unamatatizo gani mie kimyaaaa mwishowe mpira ukachoropoka papuchini puuu chin!! Nikikumbukaga nacheka sana
 
Ungemwambia mother nimezaa..!
 
ha ha haha ha utoto raha sana
 
kaolewana anagongwa na wengine ha ha ahhaha
 
Mwalimu kaingia darasani:

Wanafunzi wote tukasimama, na kutoka salam. Sasa sijui ilikuaje tu likaja wazo, nikaenda kutoa kiti cha mmoja wa jamaa alikua anajiona mjanja sana. Wakati mwalimu anasema 'Okay sit down' jamaa anakaa tu akaenda chini...dah class nzima wakaona na toka siku hiyo alikua mpole...utoto una raha yake
 
ha ha ha
 
ha ha aakili ya utoto bwana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…