Kituko gani alikufanyia mtoto wa mwenyeji wako ulipokuwa ugenini huwezi kukisahau hadi leo hii?

Kituko gani alikufanyia mtoto wa mwenyeji wako ulipokuwa ugenini huwezi kukisahau hadi leo hii?

Tupo Sebuleni tunatizama Habari ITV namsikia kabisa kuwa Kajamba Yeye ila kwakuwa yuko Kwao akanisingizia Mimi na Mimi kwa Hasira sasa nikaamua Kuwajambia Mubashara ambapo Harufu ya Mjambo wangu ikaonekana ni tofauti na yake ndipo Baba yake akamkamata na Kumchapa sana Viboko na baadae Kuniomba Radhi pia.
Hahahahahah
 
Nilipata mfanyakazi wa stationery bana wakati anaanza kazi weekend alikuwa ana kuja na mtoto wa dada ake sasa kuna siku tuna mteja anasubri passport size dogo si akaanza kuropoka odo umejamba nilikaangalia kakaongeza sauti daaah alipoondoka mteja, nilimwamuru yule amrudishe dogo home na asije tena nae ofisini.
 
Wengine tukifika ugenini tunaogopwa mpaka na wazazi, tupo very strictly, Ukali upo usoni kabisa. Tunajitahidi kutabasamu kuuficha lakini watoto wanasaikolojia ya kumtazama macho na kumuelewa mtu ni wanamna gani
Naona tunafanana mi hata watu wazima hawanizoei kirahisi rahisi
 
Katoto kadogo darasa la awali namfundisha tuition hapa (do not comment [emoji1787]) jana tu alinisimulia jinsi bibi yake alivyochimba au tuseme alivyouza mchanga eneo la hifadhi akakamata.

Mtoto anamtaja hadi mtu aliyemfitini bibi yake.

Alimtaja hadi aliyemtolea bibi yake hela ya dhamana.

Akaniambia siku ya kesi ni tarehe 8, nimeona mtoto mdogo mwenye uwezo mkubwa wa uelewa.
Kuna watt wamejaliwa uelewa mapema sana sema familia zetu za kiafrika tunashindwa kugundua hilo mapema
 
Mtoto mkubwa wa sister ni mkubwa tuu 18 years now kamaliza form 4. kaja home. kufika kakuta wamepika makange akasema yeye hali makange. nkampa hela akaenda nunua chips. asubuh chai tukanunua mihogo kasema halagi mihogo anataka chapati za maji, akapewa. inshu ikaja kwenye kusaidia kazi. hakuna kazi anayoweza labda vyombo tuu kuosha na sio masufuria. kitu pekee anaweza pika ni chai. hata ugali wa mtu mmoja hawezi pika. nkamuuliza vizuri akasema yeye hata kwao wakipika ugali yeye hataki basi anapewa hela anaenda kula mgahawani.

nguo zake anafuliwa. na sio kwamba kwao ni matajiri hapana kipato chao ni cha chini sana.
Ndio unakutana na huyu binti unasema ni wife material oa sasa kimbembe chake [emoji3]
 
Dogo aling'ang'ania miwani Hadi akaivunja hakurizika akatoka nje viatu nilivulia mlangoni akavichukua akavikojolea dada wa kazi akampiga mama mtu akaja juu eti kwanini usingemwambia kwaustarabu maana mtoto hajui chochote niliaga hapo hapo na sijawahi Tena kukanyaga Ile familia
Duuh!hata mm sirudi aiseee
 
Aloooh!! Eti halagi nini? Na hela mnampa!!
Nilitembelea sister nikakuta binti eti hafanyi kazi yoyote nyumbani. Dada wa kazi anaamka yeye anaendelea kulala ataamka muda anaojisikia. Weeeh mbona nilimnyoosha. Hadi naondoka anafanya kila kazi. Huwa akiniona tu anajua hakuna ujinga.
Kuna watu wanawaharibu watt wao wenyewe kwa malezi ya hovyo
 
Mmenikumbusha enzi za utoto wangu .Chakula nilichokuwa napenda sana ni wali ndondo na lazima ndondo lipikwe daily kwa ajili yangu.Sasa ikafika kipindi no wali no ndondo.Sasa kwa kuwa nilikua sitaki ugali nikaamua kuunyea unga uliokuwa umehifadhiwa safi kabisa kwenye kilindo.Jiweke kwenye nafasi ya mzazi unatoka kwenye mihangaiko yako unakuta mwanao kanyea unga.Simu ni moja tu tukutane benki.
Hata hivyo tayari ww ulishaharibika,ungekuwa umelelewa malezi mazuri sidhan kama huo ujinga wa kunyea unga ungeufanya japo uliadhibiwa kwa kosa ulilofanya
 
Back
Top Bottom