Kituko kingine Wizara ya Afya, Waziri abariki uteuzi wa AMO kuwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu

tatizo letu watanzania tunapenda rahisisha mambo.mkuu jaribu kusoma ata vitabu uongeze maarifa yako.AMO hata siku moja hawezi kuwa na uwezo zaidi ya MD
 
define professionalism!

Zamani professionals walikuwa watu kama madaktari, wahandisi, wanasheria, n.k. Siku hizi professionals include manesi, accountants, walimu, wanasayasi, maafisa jamii na hata wafagiaji.

Lakini kwa kutojua bado kuna watu wanadhani professionals ni watu kama madaktari, wahandisi, wanasheria, n.k.

Ndiyo maana unakuta baadhi watu ambao bado wanaamini kwenye traditions (conservatives) kuwadharau watu wenye professions nyingine kwa msingi kuwa wao siyo professionals.

Na ndiyo maana huyo medical assistant anapigwa madongo eti hafai kuwa RMO kwa sababu siyo professional aka daktari.
 
Ki kanuni na taratibu, ni makosa AMO kuwa RMO. Lakini kuna shida pia ya taratibu hizi na hasa hapa nchini kwetu, LAZIMA DMO AU RMO AWE DAKTARI???? Its the wastage of human resources na ubinafsi tu, naamini kabisa nafasi za RMO na DMO zingeweza kuongozwa na hata na kada zingine ili mradi awe na package ya health management. Ni ubinafsi tu, maana hata wizara ya afya ati kurugenzi zote lazima uwe daktari, hawezi kuwa nurse, mfamasia, maabara?? na kwa sababu wizarani wakurugenzi ni madaktari hata maamuzi ndio kama haya ya DMO au RMO lazima awe daktari. Nchi za wenzetu, mfano zimbabwe, ile hospitali kubwa ya taifa inaongozwa na mtu si daktari na mambo safi kabisa. Kwa wasio fahamu, Amo, Clinical officers ni wataalamu wasiosajiliwa na baraza la madaktari, hawatambuliki kabisa, jamaa wanawabagua, na si hapa tu, hata kenya, uganda, japo sisi wanachi we salute them maana ndio tunaokutana nao hospitalini, for all those years.
 

aliyebadilisha hayo ya zamani kuwa ya sasa ni nani?
 
nijuavyo anayetibu clinically ni CO katika zahanati ya huko vijijini isiyokuwa na vifaa vya maabara na mara nyingi atatoa matibabu ya awali kabla ya kumrefer mgonjwa kwa hospital level.

Huwezi kuwa na Diagnosis bila investigations,usipotoshe unachokuwa nacho ni provisional Dx.hata magonjwa ya akili utahitaji kufanya investigations za rule out organic causes ili kufikia hitimisho.

Uwepo wa vyuo vya kata kama IMTU n.k umetuletea watu wa aina yako.
 
Mkuu sisemi daktari kuwa mtawala ni dhambi, hapana! Ninachosema mahali anapohitajika sana daktari ni pale alipo mgonjwa kuliko mahali pengine popote. Kazi ya utabibu haiwezi kufanywa na mtaaluma mwingine yeyote isipokuwa daktari, lakini kazi ya utawala inaweza kufanywa vizuri zaidi na watawala kuliko inavyoweza kufanywa na madaktari. If you are to choose between the two options at least on administration issues you have alternative. Unapomtoa Physician clinic kumpeleka kwenye cheo cha kisiasa ni matumizi mabaya ya Rasimali watu. Unamtoa professional kwenye taaluma ni sawa na kutumia gari kufugia kuku.
 


kuna cheo cha hapo hapo mkoani kinachoshabihiana na hiki,hebu tuangalie vigezo

The RHO shall have a University degree in Environmental Health or an advanced
Diploma in Environmental Health Science
. The RHO shall have working experience of at
least 5 years in a district in a similar position at that level.


tumejiwekea taratibu tusizikiuke na kama tunaona taratibu hizi zina mapungufu ni vyema zikarekebishwa.yaani nchi inaongozwa kwa hisia na utashi huku taratibu zikiwekwa kando.
 

Inaonekana umesoma UDOM chuo chenu cha kata we mama.
 
Naibu waziri wa Afya pia ni AMO pengine wameona since its just an administrative post it should just pass
 
Naibu waziri wa Afya pia ni AMO pengine wameona since its just an administrative post it should just pass
kigezo cha waziri wa afya ni tofauti na kigezo cha kuwa RMO na vyote vimeainishwa.
nchi hii haiongozwi kwa utashi!!ndio maana sekta ya elimu inakufa kwani kila waziri anakuja na utashi wake
 
the truth is wengi hampigi hesabu, hawa maRmo wote ni wakaa oficn 2,piga hesabu wako 26 na maDmo zaid ya mia,hawa wote wakiwa oficn hamuon km wanazidisha ugumu wa tiba kwa watanzania!
 
Mkuu msafi, nandhani utakuwa unakosea unaposema "wanabaguliwa"..jaribu kuangalia AMO amesoma nini na nini kwa miaka ile 3 na MD kasoma nini kwa miaka mitano!!Isiangalie wingi wa miaka(si hoja hapa)..Masomo is!

Pili ni vizuri ungejua hao AMO wako nchi ngapi duniani, na kwa nini walianzishwa hapa nchini, LENGO lilikuwa ni nini?

Ni kweli "wanapiga kazi" kama ulivyosema lakini bado madhara ya kiafya yanayotokana na wao(no offense) ni makubwa..though hii haimaanishi MDs huwa hakuna complications za management zao.

So, suala ut is not the matter of existence, but WHY do they exist,mkuu!
 
Wakuu, tatizo hapa ni jina la cheo,muundo na sifa zilizoainishwa kwenye hiyo nafasi ya uongozi.
Tunapaswa tujiulize RMO ana majukumu gani, je ni ya kiutawala au kitaaluma.
Kwa maoni yangu wataalamu wanapaswa kupewa nafasi za kazi zinazowapa fursa kutoa huduma kulingana na ujuzi wa kazi waliyoisomea. MDs na Specialist wangesaidia sana nchi hii iwapo wangehusika zaidi katika kutibu wagonjwa na kutoa ushauri kuliko kufanya kazi za kiutawala na kisera.
Uteuzi wa Professor wa mifupa kuwa waziri wa ulinzi ni matumizi mabaya ya taaluma, kwa maslahi ya aliyeteuliwa na sio watanzania.
Kwangu, mtawala kuwa AMO na kuwaacha ma MD na Ma'specialist mahospitalini ni sahihi na kitendo cha busara inayotumika. Kinachopaswa kubadilika ni maslahi. Daktari anayeona wagonjwa anapaswa kulipwa zaidi ya mtawala aliyeko ofisini kwa kazi ya uongozi.
Kinachosumbua hapa ni maslahi si cheo.
RMO akiwa AMO analipwa kama AMO, akiwa MD alipwe kama MD, tatizo halipo.
Vyeo hivi viwe na sifa tofauti za uongozi na si professional qualification.
 

tusichanganye mambo !!tukumbuke chini ya RMO kuna mtu anaitwa Regional health secretary huyu amesoma administration lakini kwa bahati mbaya hafahamu mambo ya tiba kwa sana.

ni misuse ya resources kwa kumtumia AMO ambaye purposely alitayarishwa kwa huduma ya kutibu(advanced diploma in clinical medicine) tena katika vituo vyetu vya afya(health centers) na badala yake tunampa madaraka ya ''kiutawala'' kama unavyosema
 
Ma MD wengi administration hawaziwezi. Nadhani ni wivu wa kike tu.
 
MD Degree courses

Anatomy
Biochemistry
Medical Ethics I
Basic Physiology
Behavioral Sciences
Development Studies
Microbiology & Immunology
Parasitology & Medical Entomology
Clinical Physiology
Development Studies
Introduction to Clinical Medicine
MUHIMBILI UNIVERSITY OF HEALTH AND ALLIED SCIENCES
36 MUHAS Prospectus 2011-2013
Pathology
Epidemiology & Research Methodology
Nutrition
Introduction to Clinical Medicine
Forensic Pathology
Clinical Pharmacology
Management of Diseases
Medical Ethics II
Medical Ethics III
Management of Disease s II
Community Medicine
Paediatrics and Child Health
Obstetrics Gynaecology
Elective Period
Surgery
Internal Medicine
Surgical Specialties
Orthopaedics and Traumatology
Psychiatry



COURSE ORGANIZATION FOR AMO'S TRAINING

BLOCK I 1st ACADEMIC YEAR


Introduction to clinical medicine
Internal Medicine
Surgery
Pediatrics and Child Health
Obstetrics/Gynecology

BLOCK 11 2nd ACADEMIC YEAR

Community Medicine
Surgery
Internal Medicine
Pediatrics and Child Health

Obstetrics /Gynecology
 

Dala dala nawachukia sana watu wa dala dala lakini kwa bandiko lako hili nimefurahi ingawa uwa sipendi kusikia kitu daladala baada ya mmoja wa madereva wao kunigonga. Lakini arrogance ya hawa wanaitwa MD ni kubwa na madhara yake ni mengi sana. Tuanzie babu, waganga uchwara mitaani n.k. Ukiangalia kwa umakini afya ya watanzania imo mikononi mwa AMO na wala si hawa MD km wanavyotaka kujulikana. Hawa watu ni waovyo (majority) na self centered. Kuna shirika moja lilitaka kusaidia kuanzisha mtaala wa degree kwa AMO, wahuni hawa walipinga kwa nguvu sana na kuweka hili kama mojawapo ya masharti eti AMO wasipewe degree ( kwa kupunguziwa baadhi ya masomo kufuatana na uzoefu wao, hii yafanyika sehemu nyingi eg. ACCA, NBAA, etc) kwani wanajua kuwa wao AMO ni more experienced than the MDs na hivyo kwa kupewa degree itapelekea wao kukosa soko. Kwa kweli tunahitaji mtu makini kuangalia sekta hii ya Afya
 

mkuu mbona AMO na COs wanapata degree!!cha muhimu wakubali kusoma 5 years tu !wapo wanaojiendeleza na kuwa MDs nenda bugando na KCMC,IMTU utawakuta wa kutosha.
tatizo mnataka madaktari wa vodafasta kama ilivyokuwa kwa walimu.

halafu kama hujui vitu ni bora ukakaa kimya au kuchangia kule chitchat na facebook
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…