Kituko: Mbunge wa Arusha, Mrisho Gambo abanwa maswali na Mtangazaji wa StarTv na kushindwa kutetea Kauli zake, Wabunge wafundishwe kujenga Hoja..

Maswali mengi yalimlenga jiwe, yalikuwa juu ya uwezo wa Gambo so kwa kiasi kikubwa Gambo ameonewa hapo. Ila bado hili halimuondolei ukilaza wake. Kweli alitaitiwa
 
Wewe ulitaka afanye nini kama mbunge? Serikali ndiyo inayotoa fedha kugharimia shughuli za maendeleo tena siyo kupitia kwa mbunge hisipokuwa almashahuri. Wewe ni aina ya kina Mrisho Gambo msiojuwa wajibu na kazi ya mbunge.
1.Akwamishe bajeti ya serikali kwa kutoleta maendeleo jimboni kwake na huku serikaki/chama chake kilihaidi kufanya hivyo
2.Ajiuzuru ubunge.
3.Awambie wanajimbo wake wasilipe kodi kwa vile serikali imeshindwa kuwaletea maendeleo.
Akifanya hayo 3 au moja wapo maendeleo jimboni yatakuja tu.
 
1.Kukwamisha Au kutoridhia Bajeti ya Serikali Ni moja ya Sababu ambayo kikatiba inampa Nguvu Rais kuvunja Bunge na kuingia kwenye Uchaguzi Wa kuchagua wabunge wapya..

2.Kujiuzuru Ubunge sio suluhishi akijiuzuru atakuja mbunge mwingine na Yatakuwa yale yale..

3.Kuzuia Ulipaji wa Kodi au kushawishi kutolipa kodi ni kosa Kisheria la Uhujumu Uchumi na linaweza kupelekea kufungwa Jela kwa kuda mrefu tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…