Hivi unawajua wafanyabiashara wadogowadogo au unawasikia? Msiwababeshe lawama wasimamizi.nendeni Nyie wenyewe mkawapangie maeneo ya kufanyia biashara muweke na masharti mnawatafutia lawama wenzenu.Kama wanaosimamia wameshindwa kazi wapewe usaidizi. Tatizo sio wafanyabiashara wadogowadogo
Pambania haliyako mzee.Ondoa hiyo profile pic, huna hadhi hiyo, mtoto unaeishi kwa kula ya shemeji
Mtu akiuza nyanya zake barabarani wewe mpitaji unapungukiwa nini??Sio hapo kwenye stand tu maeneo mengi machinga wametandaza vitu mpaka wakafunga barabara tatizo Magu aliwapa uhuru sana machinga bila kujua anatengeneza tatizo
Sent using Jamii Forums mobile app
Unakubali kuwa kuna kutokuwajibika kwa viongozi katika suala la wamachinga kujaza barabara, hapo hapo unapinga wanaotoa hoja ya kurekebisha hiyo hali hawawapendi wamachinga sababu ya JPM🤣🤣.Ukiona wamachinga wanauza vitu barabarani katikati kuna watu wameshindwa kuwajibika.... kila kitu kinakua sawa kama utaratibu upo na unafuatwa
Labda uniambie shida yako ni kwamba hutaki kuwaona binadamu wanaoitwa wamachinga sababu walipewa kipaumbele na JPM
Maana binadamu hamkosi sababh
Akiuza nyanya bila kuzuia barabara nikiwa natembea kuelekea nyumbani au naendesha usafiri kupeleka mtu hospitali mfano hivi hakuna tatizo. Hapo ni sokoni, imagine sasa sehemu ambayo hakuna soko ila kuna hiyo hali na ww ni mtumiaji wa barabara hiyo.Mtu akiuza nyanya zake barabarani wewe mpitaji unapungukiwa nini??
Mbona ubungo wameondolewa wakati jiwe yupo?Na wakitolewa au kuguswa watasema mtetezi wao hayupo tena.
hebu jaribu kupita maeneo ya kariakoo halafu bahati mbaya ukanyage nyanya za mtu ambae amezitandaza barabarani uone watachokufanya. Halafu hapo utajua utapungukiwa nini.Mtu akiuza nyanya zake barabarani wewe mpitaji unapungukiwa nini??
Uchafu utajaa humu ndani Kwa walivyokuwa wengi. Humu ilistahili kuwe na mini shops , supermarket, migahawa ya kisasaNani sasa awaguse wakati mwendazake aliamuru wasiguswe waacheni tu mapaka watakapo oona kero ndio watawatfutia sehwmu nyingine....View attachment 1754433
Wahamishieni pale kwenye Uwanja wa ndege wakatandaze biashara zaoHakuna haja ya kuwagusa kama ina maana ya kuwaondoa
Ila ipo haja ya kutengeneza mfumo mzuri wa wao kuwepo kwa manufaa ya wote
Ni wazo zuri, lakini kuwaondoa si sahihi bali wawekewe utaribu mzuri ambao wao wataendelea kupata ridhiki zao bila kuwakwaza wapita njia.hebu jaribu kupita maeneo ya kariakoo halafu bahati mbaya ukanyage nyanya za mtu ambae amezitandaza barabarani uone wanatachokufanya. Halafu hapo utajua utapungukiwa nini.
Wamachinga kwa kuweka vitu barabarani wamejimilikisha barabara za halaiki na kujiona wapo sahihi. Hakuna mtu anaepinga uwepo wao maana wanasaidia katika kuuza bidhaa za muhimu, tatizo linakuja wanazingatia vipi mahitaji ya watumizi wengine wa maeneo wanayoweka biashara
Unakubali kuwa kuna kutokuwajibika kwa viongozi katika suala la wamachinga kujaza barabara, hapo hapo unapinga wanaotoa hoja ya kurekebisha hiyo hali hawawapendi wamachinga sababu ya JPM🤣🤣.
Wewe ni vuguvugu, unakaa hapo katikati, si moto si baridi.
Unaamini kuwa si sawa walivyojazana kila sehemu na kuna viongozi hawawajibiki ila wakati huo huo unapinga kurekebisha hilo sababu sijui JPM imekuwaje kulingana na akili yako.
Kufuata utaratibu si kurekebisha hili la wao kujazana sehemu wasizotakiwa kuwepo? Au unasimamia lipi wewe?
Wahamishieni pale kwenye Uwanja wa ndege wakatandaze biashara zao
Ww si mstaarabu sababu unatumia jina la JPM vibaya kuhalalisha hoja zako za uvuguvugu.Unapambana sana kuhamishia chuki za JPM kwa machingaz ila huwezi kufanikiwa
Una roho mbaya kiasi cha kutamani binadamu wenzio waondolewe wanakopatia riziki wafe njaa badala ya kujadili jinsi ya kuboresha utaratibu ili waendelee kufanya kazi kujipatia kipato
Kweli kila mtu ana ubongo ila matumizi ndio tofauti...... jitahidi kutumia ubongo wako kujenga zaidi ya kubomoa
Hapana nilikuwa nawashauri tu.Unawachukia eeeee
Kwani wamekunyima kupumua mkuu?
Kama wanaosimamia wameshindwa kazi wapewe usaidizi. Tatizo sio wafanyabiashara wadogowadogo.
Hakuna haja ya kuwagusa kama ina maana ya kuwaondoa
Ila ipo haja ya kutengeneza mfumo mzuri wa wao kuwepo kwa manufaa ya wote
Umeandika sanaaaaaaa kwanini hawa wamachinga wanakuumiza hivi?
Waache wenzio wapate rizki sababu nao wana mahitaji kama yako japo hawana kazi sawa na yako
@mama D utaacha lini unafiki?Tuacheni tutafte rizki jamani
Mbona mnaleta nongwa???
Mataga hao hawajielewi mkuu?Hakuna anaepinga kutafuta kwao rizki hivyo usipotoshe maudhui. Tatizo linakuja wanaitafuataje hiyo rizki. Ikiwa kila mmoja anatumia kigezo cha kutafuta rizki basi hata vibaka hawana makosa.
Kutafuta kwao rizki kusiwe kero kwa wengine, kama kuna sehemu maalum wanatengewa kufanya biashara na hawazitaki wanaishia kukimbilia pembezoni mwa barabara sasa hapo huoni kuwa wanakuwa wabinafsi kwa kuangalia matakwa yao tu kutokuzingatia mahitaji ya wengine.
Na siku nyingine ukiona mtu kaandika sana potezea mama, usisome kuepuka kukereka.