Kituo cha umeme wa jua chajengwa wilayani Xinfeng mjini Ganzhou mkoani Jiangxi, China

Kituo cha umeme wa jua chajengwa wilayani Xinfeng mjini Ganzhou mkoani Jiangxi, China

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
Kampuni ya nishati mpya ya Ruixin iliyoko wilayani Xinfeng mjini Ganzhou mkoani Jiangxi, China imejenga kituo cha umeme wa jua chenye uwezo wa kuzalisha megawati 30 za umeme. Seti 28 za vifaa vya kuzalisha umeme zinaweza kusafirisha kwa wastani umeme kilowati saa milioni 30 kwa mwaka kwenye gridi ya taifa, hali ambayo inaweza kupunguza matumizi ya makaa ya mawe takriban tani milioni 97.5 kwa mwaka.
VCG111411290345.jpg

VCG111411290337.jpg

VCG111411290343.jpg
 
Anatokea jamaa sijui ana utahira gani, eti China kumejaa kila mahali mpaka mboga zinalimwa juu maghorofani, sasa hayo mashamba yaliyoweza kusanya hizo solar panels yametokea India?
 
Taifa la China limetawala duniani katika umeme usio chafua mazingira, kila uchwao linazidi kupiga hatua kwenye sekta hiyo.
Mkuu haya mambo yalifanyika Ujerumani miaka mingi kidogo na wako vizuri sana kwenye haya.
Hapa kwetu tunaweza kufanya uwekezaji huu sema hatuna sera nzuri kuhusiana na uwekezaji, kila kiongozi akiingia anaingia lake mradi tu avuruge sehemu aliyoacha mtangulizi wake.

Ebu fikiria Kikwete alivyotoka aliacha Mambo ya Gesi mtwara imepamba Moto pamoja na Bandari ya Bagakoyo, Magufuli alipoingia wawekezaji wa Gesi mtwara wakaanza kusaga lami kwenda Wizara ya nishati na madini bila kujua nini kinaendelea.

Samia ameingia nae anarudi kwenye Gesi na Bandari ya Bagakoyo ileile tulioambiwa ni mkataba wa kichaa ambae shetani pekee ndo anaweza kuikubali.

Fikiria: Je viongozi wa vizara hawajaiona hiyo mkataba?
Je usalama wa nchi ipo upande you kuhusiana na hiyo mkataba?
Je viongozi wa juu wa Chama hawajawahi kuiona hiyo mkataba?
Je wananchi wanamwamini Nani? Na wanataka kipi?

Mwisho, Wananchi Basi tujitambueni tunatia aibu sana.
 
Mkuu haya mambo yalifanyika Ujerumani miaka mingi kidogo na wako vizuri sana kwenye haya.
Hapa kwetu tunaweza kufanya uwekezaji huu sema hatuna sera nzuri kuhusiana na uwekezaji, kila kiongozi akiingia anaingia lake mradi tu avuruge sehemu aliyoacha mtangulizi wake.

Ebu fikiria Kikwete alivyotoka aliacha Mambo ya Gesi mtwara imepamba Moto pamoja na Bandari ya Bagakoyo, Magufuli alipoingia wawekezaji wa Gesi mtwara wakaanza kusaga lami kwenda Wizara ya nishati na madini bila kujua nini kinaendelea.

Samia ameingia nae anarudi kwenye Gesi na Bandari ya Bagakoyo ileile tulioambiwa ni mkataba wa kichaa ambae shetani pekee ndo anaweza kuikubali.

Fikiria: Je viongozi wa vizara hawajaiona hiyo mkataba?
Je usalama wa nchi ipo upande you kuhusiana na hiyo mkataba?
Je viongozi wa juu wa Chama hawajawahi kuiona hiyo mkataba?
Je wananchi wanamwamini Nani? Na wanataka kipi?

Mwisho, Wananchi Basi tujitambueni tunatia aibu sana.
Ni kweli ndugu uyasemayo,China wana utamaduni wa kujifunza maarifa kutoka jamii mbalimbali nao kuzileta katika jamii yao na kufanya kama walivyo fanya hizo jamii wao hujitahidi kufanya zaidi ya ile jamii waliyo jifunza mfano treni za mwendokasi za umeme hii teknolojia wamejifunza ujerumani na japan lakini wao kila uchwao uiboresha na kuifanya katika ubora zaidi ya Japan na Ujerumani.

Jamii yetu imekosa huo utamaduni kama wakichina wa kujifunza mambo ya faida kutoka katika jamii zengine, tuna hitaji kutumia elimu kuingiza huu utamaduni katika vizazi vyetu.

Ukweli halisi serikali inajukumu laku boresha mfumo mzima wa elimu utakao saidia jamii kujifunza maarifa yaliyo bora kutoka katika jamii zengine na kuyaleta katika jamii yetu ili nasi tupate kuendelea kama mataifa mengine.

Mchango wako ndugu ni bora sana kwa mustakabali wa mabadiliko ya kimaendeleo katika jamii yetu ya kitanzania.
 
Ni kweli ndugu uyasemayo,China wana utamaduni wa kujifunza maarifa kutoka jamii mbalimbali nao kuzileta katika jamii yao na kufanya kama walivyo fanya hizo jamii wao hujitahidi kufanya zaidi ya ile jamii waliyo jifunza mfano treni za mwendokasi za umeme hii teknolojia wamejifunza ujerumani na japan lakini wao kila uchwao uiboresha na kuifanya katika ubora zaidi ya Japan na Ujerumani.

Jamii yetu imekosa huo utamaduni kama wakichina wa kujifunza mambo ya faida kutoka katika jamii zengine, tuna hitaji kutumia elimu kuingiza huu utamaduni katika vizazi vyetu.

Ukweli halisi serikali inajukumu laku boresha mfumo mzima wa elimu utakao saidia jamii kujifunza maarifa yaliyo bora kutoka katika jamii zengine na kuyaleta katika jamii yetu ili nasi tupate kuendelea kama mataifa mengine.

Mchango wako ndugu ni bora sana kwa mustakabali wa mabadiliko ya kimaendeleo katika jamii yetu ya kitanzania.
Nimefurahi kuona unaelezea China anacopy tec kutoka mataifa mengine. Na sio ujinga kuiga, ni mjinga tu ndie ataweza kumpuumzia China ktk hili kwenye kuiga.

Sisi tuna maeneo makubwa sana tena saaana, tunashindwa wapi kuwekeza namna hii, walau hata mkoa mmoja uwe unajitegemea wenyewe kuwa na umeme wa kutosha?
 
Nimefurahi kuona unaelezea China anacopy tec kutoka mataifa mengine. Na sio ujinga kuiga, ni mjinga tu ndie ataweza kumpuumzia China ktk hili kwenye kuiga.

Sisi tuna maeneo makubwa sana tena saaana, tunashindwa wapi kuwekeza namna hii, walau hata mkoa mmoja uwe unajitegemea wenyewe kuwa na umeme wa kutosha?
Hilo jambo ndugu pia mimi nimekwisha wahi kuliwaza, kuwa tuna hitaji umeme mbadala wa kukabiliana na jangamoto kubwa za umeme kama hivi sasa. tuna kila sababu ya kuwekeza kwenye umeme safi wa mazingira mfanano kama huo waliowekeza China.

Tunapaswa kutenga eneo kila mkoa/wilaya na kwa ajili ya shamba la kuvuna umeme jua utakao kuwa mbadala wa matatizo ya umeme katika hilo eneo husika na kama ikiwezekana kutengeneza umeme mkubwa zaidi kupitia hio teknolojia tuna kila sababu ya kuingiza huo umeme tutengenezao katika gridi kuu ya taifa.

Vipi kuhusu huu mpango ndugu, je utakuwa na tija kubwa kwa taifa ?
 
Hilo jambo ndugu pia mimi nimekwisha wahi kuliwaza, kuwa tuna hitaji umeme mbadala wa kukabiliana na jangamoto kubwa za umeme kama hivi sasa. tuna kila sababu ya kuwekeza kwenye umeme safi wa mazingira mfanano kama huo waliowekeza China.

Tunapaswa kutenga eneo kila mkoa/wilaya na kwa ajili ya shamba ya kuvuna umeme jua utakao kuwa mbadala wa matatizo ya umeme katika hilo eneo husika na kama ikiwezekana kutengeneza umeme mkubwa zaidi kupitia hio teknolojia tuna kila sababu ya kuingiza huo umeme tutengenezao katika gridi kuu ya taifa.

Vipi kuhusu huu mpango ndugu, je utakuwa na tija kubwa kwa taifa ?
Tatizo ni viongozi wetu....sijui kuna shida gani kwenye nyazifa za juu pale...watu wakizipata hakuna kinachofanyika, mfano tulipata shida sana ya umeme miaka kama kumi nyuma, huko..mpaka tukaingia kwenye kashfa za richmond, IPTL etc.....mvua za kutengeneza kutoka Malaysia etc...Cha ajabu kama taifa hatukujifunza kitu..leo hii...tumerudi tena kule kule..umeme wa mgao....hivi kweli jamani??

Magufuli alikuja na Bwawa lake la maji tena, hivi kweli kwa jinsi mabadiriko ya hali ya hewa duniani kuna uhalali wa kurisk kuwekeza kwenye umeme wa maji ya mvua kweli???

Binafsi kama taifa tungefanya tafuatayo:
1.Kutokuongeza ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme badala yake twende kwenye vyanzo mbadala.
2.Vyanzo mbadala kama Gas ( Mtwara), Upepo (Tanzania ya kati-Singida etc)

3.Umeme wa Jua (Tabora, Shinyanga, Singida huko).

4.Mabwawa yaliyoko sasa etc....

Tuunde kikosi mkakati chenye maslahi ya Taifa, cha vijana wenye akili, utashi, elimu, wapandikizwe kwenye mabalozi yetu nje huko, watutafutie elimu hizo, hata kama kwa kuiba teknologia....vyuo vyetu vitengeneze maabara ya utafiti zaidi, vijana wapelekwe kusoma kwa malengo maalumu warudi na taaluma ambazo tunazihitaji kwanza kwa vitu basic...sio lazima tutumie wawekezaji wa nje...sisi wenyewe tufanyekazi kama kitu kimoja......wengine wakete elimu, tuzifanyie utafiti sisi wenyewe..tuanze mdogo mdogo..baada ya miaka kumi....tuko mbali..

Tujikite katika matokeo kuliko maneno na siasa
 
Tatizo ni viongozi wetu....sijui kuna shida gani kwenye nyazifa za juu pale...watu wakizipata hakuna kinachofanyika, mfano tulipata shida sana ya umeme miaka kama kumi nyuma, huko..mpaka tukaingia kwenye kashfa za richmond, IPTL etc.....mvua za kutengeneza kutoka Malaysia etc...Cha ajabu kama taifa hatukujifunza kitu..leo hii...tumerudi tena kule kule..umeme wa mgao....hivi kweli jamani??

Magufuli alikuja na Bwawa lake la maji tena, hivi kweli kwa jinsi mabadiriko ya hali ya hewa duniani kuna uhalali wa kurisk kuwekeza kwenye umeme wa maji ya mvua kweli???

Binafsi kama taifa tungefanya tafuatayo:
1.Kutokuongeza ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme badala yake twende kwenye vyanzo mbadala.
2.Vyanzo mbadala kama Gas ( Mtwara), Upepo (Tanzania ya kati-Singida etc)

3.Umeme wa Jua (Tabora, Shinyanga, Singida huko).

4.Mabwawa yaliyoko sasa etc....

Tuunde kikosi mkakati chenye maslahi ya Taifa, cha vijana wenye akili, utashi, elimu, wapandikizwe kwenye mabalozi yetu nje huko, watutafutie elimu hizo, hata kama kwa kuiba teknologia....vyuo vyetu vitengeneze maabara ya utafiti zaidi, vijana wapelekwe kusoma kwa malengo maalumu warudi na taaluma ambazo tunazihitaji kwanza kwa vitu basic...sio lazima tutumie wawekezaji wa nje...sisi wenyewe tufanyekazi kama kitu kimoja......wengine wakete elimu, tuzifanyie utafiti sisi wenyewe..tuanze mdogo mdogo..baada ya miaka kumi....tuko mbali..

Tujikite katika matokeo kuliko maneno na siasa
Kuna muda unakuta hata mtoto wa kidato cha nne anaweza akawa na akili kuliko viongozi wetu pale juu. Kujadili kwa undani mambo ya nchi hii ni mtu kujitia hasira zaidi.

Kama unavyosema, tuna mito, maporomoko, gas, mikoa mikubwa yenye eneo kubwa la kuweka miradi kama ya umeme jua, upepo n.k sasa unakuta mtu badala ya kuendeleza kile kilichopo, anaenda kuanzisha kingine.

Nimegundua kuwa wanachukua maamuzi kama haya ili tu waibe, iptl, richmond hazikutokea kwa bahati mbaya, ni ili mtu aibe. Marehemu magufuli akaanzisha mradi stieglers ili apate pesa huko, kanunua mandege kwa maamuzi yake binafsi ili apate percentage huko. Kwahiyo hawatazami maslahi ya taifa ila familia zako zitaishije zaidi licha ya kuwekewa mazingira mazuri kabisa ya kula bata baada ya kustaff.

Viongoz wengi wa Afrika wana laana, hata sijui kwanini wakifa WANAPIGIWA MIZINGA NA KUPEWA HESHIMA ZA KIPUUZI NAMNA ILE.
 
Tatizo ni viongozi wetu....sijui kuna shida gani kwenye nyazifa za juu pale...watu wakizipata hakuna kinachofanyika, mfano tulipata shida sana ya umeme miaka kama kumi nyuma, huko..mpaka tukaingia kwenye kashfa za richmond, IPTL etc.....mvua za kutengeneza kutoka Malaysia etc...Cha ajabu kama taifa hatukujifunza kitu..leo hii...tumerudi tena kule kule..umeme wa mgao....hivi kweli jamani??

Magufuli alikuja na Bwawa lake la maji tena, hivi kweli kwa jinsi mabadiriko ya hali ya hewa duniani kuna uhalali wa kurisk kuwekeza kwenye umeme wa maji ya mvua kweli???

Binafsi kama taifa tungefanya tafuatayo:
1.Kutokuongeza ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme badala yake twende kwenye vyanzo mbadala.
2.Vyanzo mbadala kama Gas ( Mtwara), Upepo (Tanzania ya kati-Singida etc)

3.Umeme wa Jua (Tabora, Shinyanga, Singida huko).

4.Mabwawa yaliyoko sasa etc....

Tuunde kikosi mkakati chenye maslahi ya Taifa, cha vijana wenye akili, utashi, elimu, wapandikizwe kwenye mabalozi yetu nje huko, watutafutie elimu hizo, hata kama kwa kuiba teknologia....vyuo vyetu vitengeneze maabara ya utafiti zaidi, vijana wapelekwe kusoma kwa malengo maalumu warudi na taaluma ambazo tunazihitaji kwanza kwa vitu basic...sio lazima tutumie wawekezaji wa nje...sisi wenyewe tufanyekazi kama kitu kimoja......wengine wakete elimu, tuzifanyie utafiti sisi wenyewe..tuanze mdogo mdogo..baada ya miaka kumi....tuko mbali..

Tujikite katika matokeo kuliko maneno na siasa
Mapendekezo yako ndugu ni bora sana endapo yakitiliwa maanani na uongozi, yataleta matokeo yaliyo chanya.
 
Kampuni ya nishati mpya ya Ruixin iliyoko wilayani Xinfeng mjini Ganzhou mkoani Jiangxi, China imejenga kituo cha umeme wa jua chenye uwezo wa kuzalisha megawati 30 za umeme. Seti 28 za vifaa vya kuzalisha umeme zinaweza kusafirisha kwa wastani umeme kilowati saa milioni 30 kwa mwaka kwenye gridi ya taifa, hali ambayo inaweza kupunguza matumizi ya makaa ya mawe takriban tani milioni 97.5 kwa mwaka.
View attachment 2424622
View attachment 2424623
View attachment 2424624

Anapambana na mabadiliko ya tabia nchi kwa vitendo.
 
Anatokea jamaa sijui ana utahira gani, eti China kumejaa kila mahali mpaka mboga zinalimwa juu maghorofani, sasa hayo mashamba yaliyoweza kusanya hizo solar panels yametokea India?

Wakikaa vijiweni wanaanza kuambiana uongo ili kupitisha muda.
 
Halafu wana mipango madhubuti kwenye hilo.
Mipango yao uchina imenyooka sana katika hili Jambo, kwa miaka kumi iliyo pita na sasa kuna mabadiliko makubwa sana yanayo onesha ukuaji wa kasi katika teknolojia ya umeme ulio safi kwa mazingira.

Serikali yao inajitahidi kwa kadiri inavyo weza katika jambo hili, miaka thelathini ijayo watakuwa mbali sana.
 
Kwa jua linalowaka afrika mkoa wa Dodoma pekee unaweza iwasha Tanzania nzima kwa solar energy pekee
 
Sisi huku tuna waziri ambaye anachapa kazi kwa kunyoa kipara tu
 
Back
Top Bottom