Kituo cha umeme wa jua chajengwa wilayani Xinfeng mjini Ganzhou mkoani Jiangxi, China

Kituo cha umeme wa jua chajengwa wilayani Xinfeng mjini Ganzhou mkoani Jiangxi, China

Mkuu haya mambo yalifanyika Ujerumani miaka mingi kidogo na wako vizuri sana kwenye haya.
Hapa kwetu tunaweza kufanya uwekezaji huu sema hatuna sera nzuri kuhusiana na uwekezaji, kila kiongozi akiingia anaingia lake mradi tu avuruge sehemu aliyoacha mtangulizi wake.

Ebu fikiria Kikwete alivyotoka aliacha Mambo ya Gesi mtwara imepamba Moto pamoja na Bandari ya Bagakoyo, Magufuli alipoingia wawekezaji wa Gesi mtwara wakaanza kusaga lami kwenda Wizara ya nishati na madini bila kujua nini kinaendelea.

Samia ameingia nae anarudi kwenye Gesi na Bandari ya Bagakoyo ileile tulioambiwa ni mkataba wa kichaa ambae shetani pekee ndo anaweza kuikubali.

Fikiria: Je viongozi wa vizara hawajaiona hiyo mkataba?
Je usalama wa nchi ipo upande you kuhusiana na hiyo mkataba?
Je viongozi wa juu wa Chama hawajawahi kuiona hiyo mkataba?
Je wananchi wanamwamini Nani? Na wanataka kipi?

Mwisho, Wananchi Basi tujitambueni tunatia aibu sana.
Tatizo ni aina ya mikataba inayoingiwa. Simpaumu Magufuli, sioni sababu kwa nini mikataba inayohusu nchi isiwe wazi ijadiliwe na Bunge.
 
Back
Top Bottom