Pre GE2025 Kiukweli 2025 simuoni Rais Samia akishinda kwenye Boksi la kura kama upinzani wakiweka mtu mahiri

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ila chaguzi zingine nilizówahi kushuhudia Marais kwa tiketi ya ccm walishinda vizuri tuu
Kuanzia uchaguzi wa 2010 mgombea wa ccm amekuwa akitangazwa mshindi kwa kura za mashaka. Uchaguzi wa 2020 ukageuka kuwa wa kihayawani sana.
 
Yaan mm Rais niliemchagua alikua Magufuli kipenzi cha watanzania...Apumzike kwa amani
 
Luhaga Joelson Mpina akimtimua CCM chadema anapata mgombea takayebwaingizia kura nyingi sana Kwa kutumia jina la magufuli. Kula za ngosha atazibeba
 
Sikuchangia kwa sababu najua Samia hatogombea 2025, siwezi kujadili yasiyokuwepo

Anaweza akagombea Mkuu.
Upinzani sioni wa kum-challenge.

Lisu sina hakika kama atapewa nafasi nyingine ya kupeperusha chama chake.

Pia Lisu sio chaguo la watanzania wengi. Siasa za Lisu sio pendwa kwa Watanzania wengi.
 
In DKT JK voice, labda mambo yak…. Hahha si unaona mwezi wa kwanza na mawe na habari maelezo walishamaliza kazi. Dkt Samia hakubaliki ndani ya nchi na nyanja za kimataifa (rejea ushahidi wa barua ya mabalozi kuonewa kodi na msababisha matatizo kujifanya ndiyo mtafuta njia). In short watamuambia tu wahuni ukigombea chama kitashindwa pumzika. Na walishamuandaa kisaikolojia kusema wabunge safari hii hakuna mbeleko na yeye akaishadadia hiyo kauli pasipokujua hata yeye Dkt Samia inamhusu maana yake mgombea wa CCM including kiti cha urais kama hakubaliki mfumo hautambeba na wakiona hizo dalili maana yake mgombea ataenguliwa ili asimame anayekubalika hahaha maana yake kwa sasa wahuni wanakusanya ushahidi tu na tutaona mpaka video za kumkataa Dkt Samia asigombee na hata uchomaji wa picha umeanza. Wahunis siyo watu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…