Kiukweli wazungu ni wabaguzi Sana!, Sio tuu wanawabagua wanawake, bali hata Afrika, Sijui Wanatuona Kama Manyani?

Binti wa Watu alipo Sema Wanatuona Nyani aliswekwa Lupango... Ila wewe kwa vile unawasema Mabeberu ni sawa tu. Hakuna neno.
Kama huwezi kujilisha mwenyewe na kutwa unaenda kuomba misaada nje na wakati una kila kitu ndani ya nchi yako wewe tofauti na nyani nini? Maendeleo Africa ni hisani ya Rais na siyo takwa la kikatiba
 
Duniani kote kwanzia magharibi hadi mashariki wanaelewa mwanamke hana uwezo wa kuongoza chochote! wala siyo ubaguzi wa kijinsia. Hata Samia amekuwa Rais si kwa uwezo wake, wala si kwa mapenzi ya Mungu wala ya wanadamu ila kifo cha ghafla cha JPM.
 
Ubaguzi kwa Waafrika si unafanywa tu na wazungu bali hata mataifa mengine dhidi yetu
 
Aliyetofautisha maumbile KE na ME alikuwa na maana yake ndio maana hakuna mfalme mwanamke na hakuna malikia wakiume,Rais mwanamke ni Rais lakini kwa kuwa siyo nafasi yake anaitwa mama tofauti na Rais wa kiume ambaye moja kwa anaitwa Rais na haitwi baba.
 
Duniani kote kwanzia magharibi hadi mashariki wanaelewa mwanamke hana uwezo wa kuongoza chochote! wala siyo ubaguzi wa kijinsia. Hata Samia amekuwa Rais si kwa uwezo wake, wala si kwa mapenzi ya Mungu wala ya wanadamu ila kifo cha ghafla cha JPM.
Tena hata Zanzibar tu hapo hawajawahi hata kuwa na Makamo wa Rais mwanamke lakini huwezi kusikia wazanzibar wanalalamika, angalia nchi zote za kiarabu hata kiongozi wa juu mwanamke hata kanisa katoliki au na penyewe hakuna wanawake? Paschal unazeeka vibaya sn jitafakari
 
Ni ujinga kuchagua mtu sababu ya jinsia ake badala ya uwezo wake.
 
Unataka kupoteza credibilty yako kwenye huu utitiri wa thread zako za leo.
 
Uchaguzi wao ni wao na wao ndio wameamua kwa matakwa yao
Trump mpaka Ulaya wanamuogopa kwa sababu anaangalia maslahi ya nchi yao
Kuhusu sisi hata usafiri wetu wenyewe tunauhujumu sasa kwanini wasituone hamnazo?

Umechanganya mambo mengi ila tujiandae kuambiwa ukweli na Trump maana hapepesi macho

Nimesikiliza sana waandishi wa habari wa huku nilipo wakiwa 🇺🇸 na kuwahoji wa Hispanic wengi wanamkibali Trump walipoulizwa amesema atafukuza wengi wenu
Wakajibu kuna wakati anasema vitu ambavyo hafanyi bali kuongea tu kwa mdomo bila vitendo

Ila kwa Ulaya anataka awanyooshe maana wengi wamepeleka viwanda vyao China kwenye cheap labour
 
Mkuu pascal Mayala hujawahi kuwaza kuwa labda nyani wana akili kuliko sisi waafrika? Fikiria nyani wanaishi maisha yao ya asili,na wanaishi vyema tu, wana amani,(where there is no black african) hawatekani wala kuuwana kwa upumbavu, hawaombiombi kama sisi, hawaibii nyani wenzao bali wana share kwa usawa kile kilichopatikana nk, afrka ni ushenzi mtupu, ukienda hospitali ya serikali dokta anakuona nyani, ukienda polisi polisi nao wanakuona nyani, ukienda mahakamani vile vile, viongozi tuliowachagua wakiboronga tukaongea wana tuteka na kutu ua, waliopewa madaraka ya kulinda rasilimali zetu ndiyo hao wanaozipora na kwenda kuzificha huko huko kwa wazungu, umewahi kusikia mzungu ameiba kwao na kuja kuficha afrika? Ni laana kuwa mtu mweusi!
 
Swali yeye anaheshimu ombaomba? anataka wazungu watuheshimu kwa kushinda kwao kuomba misaada? jitegemee kama unataka kuheshimika umepewa rasilimali zote na Mungu lakini kwa kukosa akili unashida unaomba misaada kwao badala ya kujitegemea tofauti yako na nyani ni nini?
 
Mrisho Mpoto alipokuwa UK alipromote lugha ya kiswahili Kwa niaba ya Kenya
Sababu ya kukosa akili, tuna mali zote lakini tumeshindwa kuzitumia matokeo yake tunauana wenyewe kwa wenyewe tofauti yetu na nyani ni nini? tena bora ya nyani wanapendana na kulindana sisi ni wajinga zaidi ya nyani kutwa tunatekana na kuuana
 
It's not fare au it's not fair

Kikubwa tumeelewa ulicholenga
 
Tangu Trump ashinde mbona unaweweseka ndugu Kuna nini nyuma???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…