Kiukweli wazungu ni wabaguzi Sana!, Sio tuu wanawabagua wanawake, bali hata Afrika, Sijui Wanatuona Kama Manyani?

Siyo kweli Paskali. Ni mchanganyiko wa mambo mengi, yakiwemo na misimamo ya vyama viwili kuhusu abortion (pro-life vs non-pro-life), na watu wa jinsia moja, nk. Kuhusu ubaguzi, hata sisi wenyewe tunabaguana na tunawabagua wazungu pia. Kuna siku waandishi wa habari walimuuliza Papa Francis kwamba angetaka Wakatoliki wamchague nani, kati ya hao wagombea wawili. Yeye akasema wataamua wenyewe nani mwenye sera za kulinda uhai wa watu na mwingine ambaye uhai si kitu. Akasema wataona kati ya hao wagombea wawili "lesser evil" ni nani. Kuna siku moja nilipanda daladala, wazungu wawili, mtu na mkewe au na rafiki yake wa kike, walipanda hilo gari pia. Nauli ilikuwa kwa wakati huo Sh200 kwa route. Lakini konda alipofika kwa wazungu akawaambia elfu 10 kila mmoja na baadhi ya abiria waliguna, na konda akadai wasiingilie biashara yake, maana yuko kazini. Niliona aibu sana as if mimi ndiye niliyewaambia hiyo nauli, maana nimeshakuwa Ulaya pia, na sikuwahi kuambiwa nauli ya juu kwa vile tu ni Mwafrika. Baadaye nilifika kituoni, nikashuka. Sikujua kama walilipa au la, maana walimwambia kwa Kiswahili kwamba nauli wanayoijua ni Sh200 na si Sh10,000. Kwa hiyo, kuna madudu mengi pia tunayoyafanya, ikiwa ni pamoja na kuwabagua wanawake. Badala ya kusema wazungu, labda ungesema binadamu tuna tabia ya kubaguana, na ubaguzi mwingi nadhani uko kwetu, hasa tunawaona watu wenye mamlaka na fedha tofauti na wasio na mamlaka na fedha, na mara nyingi tunajikomba kwa hao wenye mamlaka na fedha dhidi ya wasio na mamlaka na fedha. Sisi pengine ni wabaya zaidi kuliko wazungu. Kaunda kwenye falsafa yake ya 'African humanism' anasema 'an African can easily live with contradictions - he/she can smile where he/she is grieving; he can say 'no' where he/she means 'yes'. Mwafrika anaweza kukuahidi "njoo kesho asubuhi" wakati anajua muda huo hatakuwepo au kama ukimwomba msaada anakupa matumaini, lakini siku aliyokuahidi umwone ukienda anaanza kukupa hadithi za kulipa ada za shule watoto na kwamba ametoka msibani muda si mrefu na hajui kama ana akiba yoyote.
 
Hatunaga misimamo tunaendeshea na njaa cc Mayala.
Pili tu wavivu acha tudharauliwe
 
Ni kweli kabisa, na mimi naona tuambiwe ukweli mpaka akili zikae sawa
Umasikini tulionao waafrika ni akili tu sio kingine
Huwezi kuwa na vitu vyote halafu hujui kuvitumia
Kuna nchi kama Thailand nimeona mito yao wanatumia kusafirisha matunda na mboga wanaita floating market upo Bangkok nimeenda na kushuhudia
Sisi wanakuambia usiisogelee maana mtaharibu
Hapo kama sio ng'ombe ni nani
Yaani unakatazwa ukiogopewa utaharibu wakati wengine wanafaidika navyo

Umasikini ni laana na itatutafuna haswa
 
Sababu tunaongozwa na wajinga zaidi
 
Kutengeneza vya kwenu hamuwezi, kazi kulialia vya wenzenu waweke contents zenu,
You are a hopoless race I have ever seen
 
Wazungu watakwambia download mziki kwenye simu yako hakuna atakae kuzuia kusikiliza.

TCAA hawana mamlaka ya kuwapangia watu business operation strategy zao, achilia Air Tanzania, let alone ndege za wazungu.

Ni fikra kama hizi ndio zinafanya nchi inasua-sua watu wa rika la Paschał ndio wapo kwenye maamuzi, kizuri ni kiłę wanachotafsiri wao tu na kila mtu akifuate.

Huu mtazamo ni shida na ndio viongozi wengi vijana wanarithishwa rejea mkuu wa wilaya alalamika polisi ajampigia salute, mwingine asusa mkutano japo kachelewa yeye halafu analalama kwanini mkutano uanze kabla yake.

Ndio una hoja, bargaining cheap ingekuwa kuhimiza watanzania wasipande ndege la hilo shirika kama umekerwa sana kushinikiza waweke hayo mambo unayotaka.

Lakini uwezi lazimisha watu wafanye mambo kwa ulazima wa sheria kama ilivyozoeleka Tanzania, wengine wana culture tofauti ya kubadili mambo.
 
DEMOCRATS CHAMA DUBWANA LILILOKUWA LIMEWAFUNGA MINYORORO WEUSI WA USA

Waswahili wa bara Afrika tunalilia sana kupendwa na watu wa Marekani ya Kaskazani, Ulaya, Mashariki ya Kati na Asia.

Hongera na kongole kwa weusi wa USA kujinasua kutoka minyororo mikongwe ya Democrats.

Kwa miaka mingi chama cha Democrats kilijiaminisha kuwa jamii ya yote ya weusi Marekani ni jimbo salama (safe constituency) la kujizolea kura kutoka kwa watu waliodhani wanaongozwa na roho ya mahaba iliyopelekea imani bila maswali kwa Democrats huku wakisahau kutumia uwezo wa kufikiri

Lakini sasa weusi wa Marekani wameonesha uwezo wa kufikiri badala ya kuongozwa na roho ya mahaba yaliyoweka imani potuvu vichwani mwao kuwa Democrats ni mwokozi wao aliye mithili ya chama cha Democrats kuwa makuhani wa kiimani wenye kuwaongoza ktk imani.

The Atlantic
www.theatlantic.com
Why Do Black People Vote for Democrats?

22 Oct 2024 — More and more college-educated voters are sorting into the Democratic Party, as many Hispanic and some Black voters shift toward the Republican...

The Washington Post
www.washingtonpost.com
Why are African-Americans such loyal Democrats when they are so ...

28 Sept 2016 — But should Donald Trump win the election, it's even safer to bet against his claim that he'll win 95 percent of the black vote in 2020. Such ...
 
Hao TCAA wapuuzi tu. Ni haohao vibaraka. Wanajua vizuri tu ila vibaraka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…