Kivuli cha Hayati Magufuli kinataka kumtingisha Rais Samia

Kivuli cha Hayati Magufuli kinataka kumtingisha Rais Samia

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Ni lazima nikiri wazi kabisa, mimi nilikuwa ni mmoja wa wanaomuunga mkono JPM kwa muda wote aliokaa madarakani. Sikuficha kuunga kwangu mkono, nilisimama nae muda wote. Bahati mbaya Binadamu siku zake chini ya jua huwa zina mwisho hata afanye mema mengi kiasi gani.

Kipindi chote cha msiba wa JPM nilijawa na huzuni kuu, isiyoweza kuandikika. Lakini alipoapishwa Rais Samia kuwa wa sita tangu tupate uhuru sikuona sababu ya kutunza chuki kwake. Nilijua ni kudra ya mwenyezi Mungu anayemuandikia kila binadamu riziki yake na sikuwa nina wasiwasi na utendaji wake kwani alikuwa msaidizi mkuu wa hayati JPM kwa miaka yote ya urais wake.

Naona kama kivuli cha JPM kinataka kitumike kummaliza SSH. Ni wale wale waliokuwa wafuasi kindakindaki wa JPM ndio wanaogeuka maadui namba moja wa awamu ya sita!. Wanataka kumuona SSH akipita njia zile zile alizopita hayati ili wauone urais wake umekamilika.

Na hata akijaribu kurithi njia za kiuongozi za mtangulizi wake bado anacho kikwazo kingine kinachoangaliwa na hawa walioivaa roho mbaya awamu hii. Kigezo cha jinsia yake kudharaulika na kuonekana ni dhalili isiyo stahili kupewa nafasi ya juu ya uongozi. Akili zile zile duni za mfumo dume ndio zinazotawala baadhi ya vichwa.

JPM alikuwa na mfumo wake uliopambana sana kuhakikisha hakosolewi humu jukwaani na hata katika majukwaa mengine ya habari, hakupenda kukosolewa na huo ni udhaifu wake mkubwa.

Hakupenda kupokea ukosoaji kama changamoto ya mtu anayempenda bali alichukua kukosolewa kama ni uadui akiamini kwamba anajua kila kitu kinachoendelea duniani!. Huo ni udhaifu mkubwa sana na nadhani ni hulka aliyokuwa nayo tangu utotoni.

Akawa akitumia mbinu zile zile za ulaya mashariki za kuwa na wapelelezi wa chini kwa chini ili mradi tu Bwana Mkubwa asiguswe nafsi yake kitu ambacho kingemfanya akachukia. Hapa ndio naiona tofauti ya JPM na SSH.

JPM alitumia nguvu kubwa ili utendaji wake uonekane umekamilika kabisa (perfection) wakati SSH anafanya kazi na kuachia uhuru mpana wa maoni ya watu yakosoe kile ambacho wanaona hakiwafai. Wafuasi wa kudumu wa JPM sijui kama wanauona huo ufa wa awamu ya tano kwamba ni tatizo katika utendaji serikalini au upofu wa mahaba ni tatizo lao lisiloweza kutibika.

Naamini serikali ya awamu ya sita inaendeleza yale mema yaliyofanywa na awamu ya tano, kwani wote ni wale wale tu CCM. Na kwa wale wafuasi kindakindaki wa JPM kwao urais wa Samia utakuwa umekamilika iwapo atapita njia zile zile za mtangulizi wake.

Kwamba kama JPM aliwabagua na kuwaletea dharau jamii ya kimataifa na uwakilishi wao hapa nchini basi na SSH nae apite mule mule tu hata kama ni kwa madhara ya uchumi wetu kukosa kukua na kukosekana kwa harmony kwa maana ya uwepo wa uhusiano hasi wa TZ na jamii za nje.

Kwamba kama JPM alifukuza wakurugenzi na mawaziri kwa habari ambazo hakuwa na uhakika nazo basi na SSH nae apite mule mule tu, wawepo mawaziri na wateule wengi waliofukuzwa kazi huku wakiendelea kulipwa mshahara wa bure.

Kwamba kama JPM aliikuza chuki kati ya wanyonge na matajiri akiamini kuwa umaskini wa mnyonge chanzo chake ni utajiri wa tajiri basi na SSH aendeleze mateso kwa matajiri tena yale ya kihisia tu!.

SSH ameelewa umuhimu wa kujichanganya kimataifa, anajua ni kwa namna gani binadamu hajaumbwa aishi kama kisiwa hivyo amehakikisha sekta ya mahusiano na mataifa mengine inakuwa na watendaji nguli na wenye uzoefu nayo.

JPM alifanya mema lakini awamu yake isipewe sana utakatifu ambao haikuwa nao. Na SSH asipewe sana ushetani akionekana kama vile anakosea pale anapokwenda tofauti na mawazo au itikadi za mtangulizi wake.

Wote wawili kwa wakati wao wamebarikiwa kuwa marais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Ni lazima nikiri wazi kabisa, mimi nilikuwa ni mmoja wa wanaomuunga mkono JPM kwa muda wote aliokaa madarakani. Sikuficha kuunga kwangu mkono...
Kama haelewi Hilo watammaliza ila Kama anaelewa lazima ajipambanue kitofauti..

This time around Sukuma gang wameungana na Chadomo japo kwa maslahi tofauti..

Chadomo wanatafuta upenyo wa madaraka na Sukuma gang wanapigania Ligacy na Kutaka Mambo yaendelee Kama awali..

But Kama walishindwa mapema kabisa enzi za kina Jobo naona hiyo Ni nafasi ndogo kwao ila Chadomo ndio wanapuliza Sana..

Samia hawezi pita njia ya uovu maana kwa vigezo vyote iwe kwa namba au ufanisi Samia keshawafunika,Ni vile hapa Kuna Mambo ya dini,jinsia na Uzanzibari nothing else..

Kuliko Sukuma gang kurudi Madarakani Bora Nchi iende kwa Chadomo..

Sijawahi mkubali Mwendazake Wala siasa za CCM ila awamu hii Niko na SSH.
 
Watanzania ata kesho ukimuweka ‘Angela Kairuki’ kuwa raisi awatojali ili mradi maisha yawe na unafuu.

Wanajua uwezi watengenezea ajira wote, uwezi zuia mijizi yote serikalini na wala kutatua shida zao zote pamoja na kuwaondolea umaskini.

Watanzania wanataka kiongozi anaewajali, walau anaguswa na shida, mwenye huruma nao, na mwenye kujaribu kuzitatua changamoto zao hata kwa kupiga mikwara, wanataka waheshimiwe kwenye huduma za serikali na kupewa haki kwenye nchi yao.

Huko juu kwenye power struggle mkifungana na kutishana kama mnavyodai Magufuli ndivyo alivyokuwa anaongoza nchi au kuachiana majukwaa ya kutukanana sawa tu.

Tofauti ya Samia na Magufuli mmoja anapendwa na wanasiasa/vigogo serikalini na mwingine alikuwa anapendwa na wananchi aliokuwa anawaongoza.

Liko wazi raisi Samia hajali watanzania, yeye kajikita kufurahisha watu wenye nguvu ya kumlindia uraisi wake mpaka 2030 tu, hiyo ndio agenda yake; ila shida za watanzania sio zake.
 
Kama haelewi Hilo watammaliza ila Kama anaelewa lazima ajipambanue kitofauti..

This time around Sukuma gang wameungana na Chadomo japo kwa maslahi tofauti....
Wafuasi wa JPM hawajaungana na Chadema! Mmewavuruga wenyewe Chadema ambao waliweka silaha chini wakitegemea mageuzi ya demokrasia baada ya mbinyo wa JPM lakini wameshtuka wanaingia chaka!

Nasikia wametangaza kuanza mikutano ya hadhara mwezi December na sasa hivi kuna operations zinabadili upepo huko. Ndani ya CCM kuna minyukano ya kugombea ikulu! Chadema wameona wasisubiri haki yao kama kupewa peremende! Naona mnahaha sasa [emoji3]
 


Mlianzisha propaganda za kukauka kwa mto Ruvu na ukosefu wa maji chanzo ni kukatwa kwa miti ili kujenga bwawa la Nyerere

Baada ya video ya afande Sele kuwaeleza tatizo lilipo kwenye vyanzo sasa hivi serikali ndio imezinduka na maziara kila siku kukagua na kujionea uharibifu unao endelea kwenye vyanzo na njia za mito.

Ina maana bila ya video ya afande Sele kisingefanyika kitu au hao maafisa wa mabonde na NEMC walikuwa hawaoni huo uharibifu.

Hiyo kazi sio size yake Bi Tozo huo ndio ukweli, ni kuwapa watanzania shida tu kumlazimisha abaki.
 
Ni lazima nikiri wazi kabisa, mimi nilikuwa ni mmoja wa wanaomuunga mkono JPM kwa muda wote aliokaa madarakani. Sikuficha kuunga kwangu mkono, nilisimama nae muda wote. Bahati mbaya Binadamu siku zake chini ya jua huwa zina mwisho hata afanye mema mengi kiasi gani...
Hilo liko wazi, Kivuli cha JPM hakitawaacha salama waovu wote.

JPM siyo miaka Mitano Tu. Amekuwamo ndani ya mioyo ya watu tangu akiwa waziri.

Kwa hiyó legacy ni ya mda mrefu. Wanaopambana nayo wengi hawalijui hilo
 
Hiki kivuli Cha marehemu kama ni kweli lazima kitu kifanyike......!

Tumekuwa tukisikia Mambo mengi ambayo hayaendi vizuri kuwa tatizo ni marehemu kama vile;

Matatizo ya umeme ni marehemu,

Ukame ni marehemu,

Wanafunzi kukosa fedha toka bodi ya mikopo marehemu,

Ukosefu wa dawa mahospitalini ni marehemu,

Kukosa ajira kwa vijana ni marehemu,

Ajali barabarani ni marehemu,

Ukosefu wa maji ni marehemu,

Ukosefu wa chakula ni marehemu,

Ufisadi Serikalini ni marehemu,

Kumomonyoka kwa maadili marehemu,

Gharama za maisha kupanda ni marehemu.

Watu kubambikwa kesi ni marehemu,

Watu kutekwa ni marehemu,

N.k, n.k, n.k, n.k,

Hivi kwanini huyu marehemu asifukuliwe na maiti yake iwekwe hata pale uwanja wa mkapa ili Kila siku ichapwe viboko kumi asubuhi na viboko kumi jioni Hadi kipindi uchaguzi Mkuu mwingine utakapofanyika............!

Ni kwanini taifa lilimfanyia maziko na maombolezo ya kitaifa mtu katili kama huyu na kuongeza maumivu na mzigo kwa walipa Kodi.

Marehemu wengine wanapumzika lakini huyu wa kwetu Kila Leo anaamka na lake, marehemu gani msumbufu kiasi hiki.
 
Sjaelewa hata, ulichoandika, Sjui unataka useme nini hasa!

Wafuasi wa falsafa za JPM tunataka kuona Rais akimkemea waziri wake kama Makamba Kwa kukosa njia ya kutatua tatizo la umeme

Amkemee waziri wake wa maji Kwa nini maji ni shida ili hali kuna mafungu ya dhalula na maji kuchimbwa Kwa udhalula hapo kigamboni na kuingizwa kwenye sistimu ya Dawasiko Kwa udharula uleule

Tunataka kuona Mh wetu akiwa siriazi kwenye mambo yanayogusa maisha ya watu wake

Angelikuwa kaitisha vikao vya haraka kutaka kutafuta suruhisho la maji, umeme na kupanda Kwa gharama za maisha

Sasa Sjui unataka kusema nini mwandishi
 
Hizi nguvu za marehemu kama ni kweli lazima kitu kifanyike......!


Matatizo ya umeme ni marehemu,

Ukame ni marehemu,

Wanafunzi kukosa fedha toka bodi ya mikopo marehemu,

Ukosefu wa dawa mahospitalini ni marehemu,

Kukosa ajira kwa vijana ni marehemu,

Ajali barabarani ni marehemu,

Ukosefu wa maji ni marehemu,

Ukosefu wa chakula ni marehemu,

Ufisadi Serikalini ni marehemu,

Kumomonyoka kwa maadili marehemu,

Gharama za maisha kupanda ni marehemu.

Watu kubambikwa kesi ni marehemu,

Watu kutekwa ni marehemu,

N.k, n.k, n.k, n.k,

Hivi kwanini huyu marehemu asifukuliwe na maiti yake iwekwe hata pale uwanja wa mkapa ili Kila siku ichapwe viboko kumi asubuhi na viboko kumi jioni Hadi kipindi uchaguzi Mkuu mwingine utakapofanyika............!


Ni kwanini taifa lilimfanyia maziko na maombolezo ya kitaifa mtu katili kama huyu na kuongeza maumivu na mzigo kwa walipa Kodi..............!


Marehemu wengine wanapumzika lakini huyu wa kwetu Kila Leo anaamka na lake, marehemu gani msumbufu kiasi hiki.........!
Unamuuliza Nani sasa
 
Back
Top Bottom